Habari zenu ndugu zangu wana JF. Nilikaa kimya sana mdodosaji ila naamini ya kwamba kimya kingi kina mshindo mkuu. Jana nilikuwa ndani ya ofisi ya HESLB kuendelea kudodosa kulikoni sisi wa loan verification na wengine majina yetu yaliyopelekwa kusiko stahiki. Majibu niliyopewa ni kwamba toka jana majina yote ya wale ambao walifika pale ofisini na ku-verify majina yao basi waondoe shaka kwani majina yao yameshafika vyuoni toka jumatatu hii. Hivyo basi kama ulifika ofisi ya HESLB na ku-verify jina lako ondoa shaka mambo yapo safi kabisa tembelea website ya chuo ulichochaguliwa au nenda moja kwa moja hadi chuoni utakuta mkopo wako. asanteni. mjumbe hafungwi.