Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Nimeanagalia Taarifa ya habari saa 2:00 usiku na kushangazwa sana na kauli ya ERASTO TUMBO WA CHADEMA kwamba Mkuu wa mkoa wa Mbeya ABASS KANDORO hana sifa za kuwa Mkuu wa mkoa kwa sababu tu ya vurugu za wafanyabiashara ndogondogo, vurugu ambazo ni wazi kabisa zilichochewa na Mbunge wa Mbeya Mjini , SUGU pale alipowahutubia wananchi na kuwaambia wasitii amri ya POLISI.
Nina wasiwasi na kauli za baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakiwemo ERASTO, WILFRED LWAKATARE na SUGU kama zinakuwa ni kwa maslahi ya Taifa au wanakuwa na lengo la kumfurahisha mkuu wao ili kulinda ajira zao au ni kutaka umaarufu.
Najiuliza sana , hivi kwa nini Majimbo ya Chadema yenye vurugu ni Arusha, Mbeya na Mwanza? Je ni kwa sababu wabunge wake wana uchungu sana na watu wao kuliko wengine? au ni kwa sababu ya wabunge wao kuwa VILAZA na hiyo kuwa njia pekee ya kuwaaminisha viongozi wao kitaifa kuwa wanaweza? Mbona Ubungo, Rombo, Kawe, Kigoma Kaskazini na kwingine ni Wabunge wake wanatoka CDMA ila hakuna mambo hayo?
Bado nasisitiza , nina wasiwasi na uwezo wa LEMA, SUGU na WENJE. Lakini historia ya walikotoka na walichokuwa wakikifanya kabla hawajawa Waheshimiwa inawabeba na kuwahalalisha na vurugu za kijinga na kitoto.
Nina wasiwasi na kauli za baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakiwemo ERASTO, WILFRED LWAKATARE na SUGU kama zinakuwa ni kwa maslahi ya Taifa au wanakuwa na lengo la kumfurahisha mkuu wao ili kulinda ajira zao au ni kutaka umaarufu.
Najiuliza sana , hivi kwa nini Majimbo ya Chadema yenye vurugu ni Arusha, Mbeya na Mwanza? Je ni kwa sababu wabunge wake wana uchungu sana na watu wao kuliko wengine? au ni kwa sababu ya wabunge wao kuwa VILAZA na hiyo kuwa njia pekee ya kuwaaminisha viongozi wao kitaifa kuwa wanaweza? Mbona Ubungo, Rombo, Kawe, Kigoma Kaskazini na kwingine ni Wabunge wake wanatoka CDMA ila hakuna mambo hayo?
Bado nasisitiza , nina wasiwasi na uwezo wa LEMA, SUGU na WENJE. Lakini historia ya walikotoka na walichokuwa wakikifanya kabla hawajawa Waheshimiwa inawabeba na kuwahalalisha na vurugu za kijinga na kitoto.