Viongozi wa CCM waanza Kugeukana juu ya malipo ya Dowans

Si wameuona moto unawakaribia? wapuuzi kweli, yaani wanafanya watanzania wote ni mabwege, wajinga kabisa
 
Cheyo, Nape watupa kombora lao Dowans
Tuesday, 25 January 2011 00:05

cheyokichwachauma.jpg
Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo

Boniface Meena na Tausi Ally

MBUNGE wa Bariadi Mashariki, John Cheyo, amemtaka Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kuandaa maelezo ya kuwasilisha bungeni yatakayoonyesha wapi amepata Sh94 bilioni za kuilipa kampuni ya Dowans.

Cheyo alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili kwenye mkutano wa kujadili uwajibikaji wa pamoja katika matumizi ya fedha za wahisani, uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Alisema fedha hiyo haiwezi kulipwa kwa kuwa haiko kwenye bajeti ya Serikali iliyotengwa na Bunge mwaka jana na ili ilipwe lazima bunge liidhinishe.

"Sh94 bilioni zinatoka wapi? Nimechukizwa sana na hili. Wanasema walipe ina maana kama watalipa na sisi ndiyo tulipitisha bajeti inaonyesha kuwa bajeti hupitishwa kwenye makaratasi tu,"alisema Cheyo.

Cheyo alisema kuwa anashangaa kwa nini Serikali inaharakisha kuilipa Dowans badala ya kuangalia uwezekano wa kuepukana na deni hilo ambalo kimsingi ni mzigo kwa taifa.

Kwa mujibu wa Cheyo, pamoja na kuwa Serikali inaharakisha jambo hilo, lazima itoe taarifa kamili bungeni kueleza wapi itapata fedha hiyo na malipo hayo yatafanyikaje.

"Nimehuzunishwa sana na hilo kwa kuwa malipo hayo yanatokana na udhaifu mkubwa katika masuala ya mikataba unaofanywa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na wizara,"alisema Cheyo.

Kauli hiyo ya Cheyo ni mwendelezo wa wadau kupinga malipo hayo baada ya juzi Kambi ndogo ya Upinzani bungeni kuonya kuwa, kama Serikali ya CCM ikilipa fedha hizo, ijiandae kujiuzulu huku Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye, akisema tatizo ni jambo hilo, kutopitia kwenye Baraza la Mawaziri.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Nape Mnauye alisema kwamba haamini yale aliyoskia juu ya kuwalipa Dowans ni uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM anayoifahamu.

"Siamini kama yale niliyosikia juu ya kuwalipa Dowans ni uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM ninayoifahamu. Katika mazingira ambayo hukumu ile haijasajiliwa nchini, utata juu ya wamiliki na uhalali wa mikataba ya Richmond na baadaye Dowans,"alisema

Nape alisema kwamba chama chake , CCM hakiwezi kufanya maamuzi kama hayo wakati kuna asasi za kiraia zimefungua kesi kortini kupinga hatua ya Serikali kuwalipa Dowans. "Nina mashaka kama taarifa iliyotolewa na CCM ni ile iliyoamuliwa na Kamati Kuu," alisema Nape

Naye Mhadhiri Msaidizi wa Shule ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Onesmo Kyauke, ameitaka Serikali ilipe kwanza deni la mfanyabiashara mwenye asili ya Asia Devram Valambhia na Watanzania wote wanaoidai.

Kyauke ambaye pia ni wakili wa kujitegemea anaungana na wasomi, wanasiasa na watu wa kada mbalimbali ambao wanalaani hatua hiyo ya Serikali kutaka kuilipa Dowans.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Kyauke alisema haoni sababu ya Serikali kuwa na uharaka wa kuilipa Dowans wakati kuna Watanzania wengi wanaidai kwa kipindi kirefu na hawajalipwa.

Mwanasheria huyo alihoji kwa nini Serikali ikazanie kuilipa Dowans wakati kuna hukumu za nyuma za Watanzania ambazo hadi sasa bado hazijalipwa.

Valambhia anaidai Serikali kiasi hicho cha pesa yakiwa ni malipo ya magari kadhaa kutoka nchini Chechslovakia aliyoiuzia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa miaka ya 1980.

 
Jk acha unafiki kama kweli malipo hayo yankuuma sana kwa nini usiwajibike na kujiuzulu kwa kuliletea taifa hasara kubwa ambayo wewe uliipika baada ya kuingilia Bodi ya tanesco kwenye uteuzi wa Dr. Rashid ambaye hakuwa na sifa wala umri wa chini ya miaka 60 na wala hata kazi yenyewe hakuiomba......................


I can not trust these words at all. Nakumbuka Nyerere alisema baadhi ya watu unaweza kuwauliza swali, na akajibu kama mnavyotaka ajibu, lakini ukiangalia usoni unaona undani wake ni tofauti. JK has all the powers kikatiba nkumkamata Rostam na mafisadi wote, lakini hafanyi hivyo. Kinyume chake aliwasaidia kuwapiga kampeni kuwa wabunge, kuamua kuwapa Sitta na Mwakyembe uwaziri. Haya yote yanaonesha wazi kabisa kuwa hana nia na hana lengo. NI wananchi tu na wabunge wetu tunatakiwa kukomaa, otherwise tutaendelea na mgao wa umeme kwa miaka mingine mitano.
 

MBUNGE wa Bariadi Mashariki, John Cheyo, amemtaka Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kuandaa maelezo ya kuwasilisha bungeni yatakayoonyesha wapi amepata Sh94 bilioni za kuilipa kampuni ya Dowans.

Cheyo alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili kwenye mkutano wa kujadili uwajibikaji wa pamoja katika matumizi ya fedha za wahisani, uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Alisema fedha hiyo haiwezi kulipwa kwa kuwa haiko kwenye bajeti ya Serikali iliyotengwa na Bunge mwaka jana na ili ilipwe lazima bunge liidhinishe.

"Sh94 bilioni zinatoka wapi? Nimechukizwa sana na hili. Wanasema walipe ina maana kama watalipa na sisi ndiyo tulipitisha bajeti inaonyesha kuwa bajeti hupitishwa kwenye makaratasi tu,"alisema Cheyo.

Tatizo la Cheyo ni upeo finyu...............suala hapa siyo kama fedha zipo kwenye bajeti au la...............kwa sababu kama misingi ya kuilipa DOWANS ipo basi Bunge linaweza kupitisha muswada wa kurekebisha bajeti na kupitisha ulaji wa watu wachache kupitia malipo ya DOWANS......................

Suala ambalo wabunge wote wanatakiwa walifanyie utafiti ni je.....malipo ya TUZO ya DOWANS ni halali kulingana na sheria zetu................................................

Jibu kama ni hapana huo sasa unakuwa ni msingi wa kuishinikiza serikali au ijiuzulu kwa kuwajibika kwa kulitia taifa hasara hiyo na kutaka wote waliohusika kuwajibishwa chini ya makosa ya uhujumu uchumi.................................na kuiagiza serikali kupinga TUZO hiyo kwenye mahakama zetu..........................................

We need quality representation in the House not junkies....................................who are their to pick their pieces of silver................
 
Naye Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Nape Mnauye alisema kwamba haamini yale aliyoskia juu ya kuwalipa Dowans ni uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM anayoifahamu.

"Siamini kama yale niliyosikia juu ya kuwalipa Dowans ni uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM ninayoifahamu. Katika mazingira ambayo hukumu ile haijasajiliwa nchini, utata juu ya wamiliki na uhalali wa mikataba ya Richmond na baadaye Dowans,"alisema

Nape alisema kwamba chama chake , CCM hakiwezi kufanya maamuzi kama hayo wakati kuna asasi za kiraia zimefungua kesi kortini kupinga hatua ya Serikali kuwalipa Dowans. "Nina mashaka kama taarifa iliyotolewa na CCM ni ile iliyoamuliwa na Kamati Kuu," alisema Nape

Well, Nape grow up........................This is a new face of CCM................"official grand graft" is her middle name.......................
 
Wabunge wa CCM waigomea Dowans Tuesday, 25 January 2011 08:08

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameigomea Serikali wakitaka isilipe kabisa fidia ya Sh94 bilioni dhidi ya Kampuni ya Dowans, iliyorithi mkataba wa kifisadi wa Richmond au deni hilo lipunguzwe.

Tayari sakata hilo limekwishaitikisa Serikali ya CCM huku kukiwa na shinikizo kubwa la wanaharakati wa mashirika 11 ambao wamefungua kesi Mahakama Kuu kukata rufaa, kupinga malipo hayo.


"Serikali imekubali kamati ya wabunge wa CCM kuhusu Dowans kuona kama inaweza ama kupunguza au kuliondoa kabisa deni hili ili kupunguzia mzigo Watanzania," alifafanua Waziri Mkuu Pinda wakati akizungumza na waandishi wa habari.


Waziri Mkuu aliongeza kwamba, Dowans ina historia ndefu ambayo ni kuanzia Richmond na kuongeza kwamba, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inaweza kuzamia katika hilo kuona kama kuna mianya ya rushwa na kuongeza, "Ingawa hadi sasa sijapata taarifa zozote za namna hiyo."


Pinda aliongeza katika kulifanyia kazi vema sakata hilo, "'ndiyo maana kamati imeshauri Serikali isikilize ushauri wa kisheria na jaji atoe ushauri wake."

Kuhusu kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema kwamba fedha hizo lazima zilipwe na hakuna jinsi, Pinda alisema tatizo lililokuwepo awali ni kwamba kila mtu alipoulizwa na chombo cha habari aliweza kutoa kauli kwani kama asingesema vyombo vingeandika Serikali yagoma kuzungumzia Dowans.

Pinda akizungumzia mvutano wa hoja kati ya mawziri, alisema ndiyo maana imefanyika semina hiyo kwa lengo la kuondoa tofauti na kuwezesha mawaziri kuweza kuzungumza mambo bila kutofautiana.


Duru zaidi zilifafanua kwamba, hata Rais Kikwete alipozumgumzia suala hilo alitamka wazi kwamba linalomuumiza sana, huku akiweka bayana amekuwa akijadiliana na Waziri Mkuu kuona kama linaweza kuepukwa.

Taarifa hizo zilimnukuu Naibu Waziri Malima akiwaambia wabunge kwamba, fedha hizo ni nyingi, lakini wizara haikuwa na la kufanya kutokana na ushauri waliopewa na AG Werema kwamba hakuna jinsi wanavyoweza kukwepa kulipa.

Kauli hiyo ya Malima inatotafautiana na ile ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ambaye aliutangazia umma kwamba Serikali inajipanga kuilipa Dowans kiasi hicho cha fedha, hatua ambayo imekuwa ikipigiwa kelele na wananchi wengi.

Uchunguzi uliopendekezwa na wabunge ni ule unaohusu uhusiano baina ya kampuni ya awali ya Richmond na Dowans, pamoja na jinsi kampuni hizo mbili zilivyoingia mkataba wa kuzalisha umeme.


Awali, ilielezwa baada ya hoja za kisheria za Dk Mwakyembe alisimama mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrodi Mkono, aliyejitolea akisema ataisaidia Serikali kuhakikisha ama deni hilo linapunguzwa au halilipwi.

Naona kuna drama ilikuwa inachezwa au kiberiti kutingishwa sasa drama inabadilika tena..
Kwa taarifa hii,tunajifunza jinsi wengi wa viongozi wetu walivyo waongo,wafitini,wezi na wasivyojali wananchi wao.............

Pili, kuna kuzungumza ili mradi....Werema lazima tulipe,Ngeleja tuko njiani kuwalipa,Mkono nitaisaidia serikali(ulikuwa wapi siku zote)???Mi nafikiri whether DOWANS italipwa,kupunguziwa deni au kutolipwa Ngeleja na Werema na hata ikiwezekana Pinda wajiuzulu......Tumechoka kudanganywa,kudharauliwa na kukubali kuropokewa upuuzi pale tunapohoji mambo ya msingi na yenye maslahi kwetu....watu waliitwa mabata.....

Our leaders should be accountable and responsible of their actions and words that comes from their evil mouths, do they communicate in the first place?? mtu kama mwanasheria mkuu wa serikali kabla ya kusema zilipwe angeangalia options mbalimbali,ila alikuwa mwepesi sana wa kutamka na hili yapaswa limgharimu na wengine wajifunze.

Nafikiri pia huu waweza kuwa mchezo mchafu,wakatae kulilipa kwa wazi,lisahaulike,then walipane juu kwa juu kwa siri bila wananchi kujua,hakuna wema kutoka kwa watu hawa
 
Mizengo pinda aiagiza takukuru kuchunguza kama kulikuwepo rushwa kwenye mchakato wa zabuni ya richmond
maoni yangu:wazee wa kusafisha mafisadi si walishatoa ripoti yao na kusema mchakato ulikuwa safi,..hivi pinda ana ugonjwa wa kusahau au ndio anadhani watz ni wapuuzi kupindukia,..ajiuzulu!!halafu si walisema mjadala umefungwa??
 
Nape anaandaa mazingira ya kuchakachua ile taarifa ya CC, kwamba iliyotolewa sio sahihi! Jamani kuna mwenye taarifa ya CC in ful text amwage hapa!? hawa watu ni hatari sana!!
 
Rais hana nia ya dhati ya kutoilipa Dowans,ni hatua gani amechukua kwa watendaji kwa kuendelea kuiingiza nchi katika mizigo ya mikataba isiyo na maana kwa wananchi.? Hakuna... sasa hapo anasema kichwa kinamuuma kwa kuwaza hili jambo..?????? najaribu kuelewa falsafa ya uongozi wake naona chenga tupu..
 
Anachonikera Mtoto wa Mkulima wakati akiongea anaweka neno NADHANI/NAFIKIRI mara nyingi hadi nahisi labda ni mwoga ama hajui yeye ana mamlaka gani kama PM.
 
Sasa hivi kwa swala la Dowans hata kama source ni Rais mwenyewe huwezi kuamini anachokisema.

Hakuna credible source any more within the government and specifically CCM.
Kwenye magazeti leo wapo wamemnukuu JK kuwa "lazima kulipa" wakati wengine wanasema "wabunge ccm waigomea Dowans"!!

Just fed up with this rubbish!!!!!!! Aaghhhhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!!!
 
kama source ya taarifa ina uhakika bora EDWARD LOWASSA kuliko mizengo pinda.

Excuse me !! please tell us that you are just kidding!
EL ndo waanzilishi wa hili dude, how can he better kuliko Pinda? Unaelewa kweli unachokisema?
 
Wanaogopa kung'ang'ana na 'LAZIMA TULIPE' maana watu wamewashtukia sasa inabidi watulize kidogo kwa kujifanya na wao wamegundua kunaweza kua na tatizo!Au kila mmoja anajiongelea vile anavyoona ni sawa kadri ya upeo kitu ambacho kitawapeleka kubaya kwa kutokua kwenye ukurasa mmoja!
 
Janja yao wanataka kuitumia Tanesco ilippe,tena nje ya mahakama hivyo hakuna usajili wa mahakamani wala nini
ndio maana wamebariki Tanesco wapandishe tarrifs ili wadundulize wapate hiyo amount
 
Hi,

Mengi yamesemwa kuhusu Dowans. Kitakacho nisitikitisha zaidi ni kutochukua hatua za msingi ikiwa ni pamaja na kuwawajibisha wahusika ktk sakata hili. Kumbuka wahasisi wengi wa Taifa hili na watu wengi wenye heshima zao wameshangazwa sana na sintofahamu hii ya Dowans. Bahada ya kusikia kutoka vyombo vya habari kuwa hata 'Wabunge' wa CCM nao wamejiunga kama hilivyo kwa vijana wa chama hicho kuiomba serikali isilipe DOWANs-imenitia wasi wasi kuwa mjadala huu sasa unakaribia kuzimika-kuishia hewani. Ombi langu nikuwa tusibweteke na matamko yao maana waliisha zoea kuzima vuguvugu nyingi za jinsi hii kwa mtindo huu.

Tonapoendelea kusubili mahakama itoe hukumu ya kesi hii na hoja binafsi ya Mh Kafurila bungeni (ambayo haijawasilishwa kwa mjibu wa SPIKA), NIOMBE TUWEMAKINI na kufuatilia kila hatua inayopigwa. Tatizo sihamini sana Wabunge wa CCM na siamini sana Mahakama zetu (Mifano ninayo ya kutokuamini kwangu mihimili hii ya dola).
 
Si wameuona moto unawakaribia? wapuuzi kweli, yaani wanafanya watanzania wote ni mabwege, wajinga kabisa
Pinda hajui alifanyalo sasa anatapata baada ya kuona moto umewaka, yeye alikuja na kampuni yake ya kisheria bungeni 2008 na kuisifu kweli kweli, tanesco ikaingia mkenge..... Rex Anttoneys ikarudi tena na kushauri Dowans ilipwe.... Pinda kimya,sasa yanamtokea puani, anataka kujisafisha.... Leo hii ndiyo anaona umuhimu wa wanaharakati? Kweli za mwezi arobaini....
 
Back
Top Bottom