Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,897
- 941
Waziri Mhagama Ateta na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho ametembelea Ofisi za Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma na kukutana na Katibu wa Chama Mkoa Ndg. Mohamed ally.
Waziri amefanya ziara hiyo tarehe, 16/03/2024 ambapo aliambatana na Katibu wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea Vijijini Ndg. Juma Nambaila na kufanya mazungumzo mafupi katika Ofisi za Chama Mkoa wa Ruvuma.
Mhe. Mhagama amepata wasaa wa kuzungumza na Viongozi wa Chama juu ya uratibu wa shughuli mbalimbali akiwa katika ziara yake ya kuimarisha Chama katika Jimbo la Peramiho lilopo Halmashauri ya Songea Vijijini.