Vijana wa CHADEMA Tunduma wamechachamaa

Hiyo ni dalili ya wazi kuwa kundi kubwa la watawaliwa limechoshwa na hao wanaojiita watawala. Na mara zote kundi la watawaliwa "Lumpen" ndilo lilaloleta mabadiliko ya kweli, na hasa ikifika hatua ya kusema "We have nothing to lose, lets fight..."
 
heri kufa ukiamini katika fikra zinazoishi kuliko kuishi katika fikra zilizokufa. siku zote mapinduzi katika taifa lolote huletwa na watu wa chini na si wale wa tabaka la juu. Tunduma wanaishi katika fifra sahihi nawaunga mkono. Hizi sio enzi za zidumu fikra za mwenyekiti. PEOPLE ARE TIRED.

Uko sahihi mkuu sioni button ya like! Binafsi nimechoka na kz kubwa nnayoifanya ni kuzidi kumpa elimu ya uraia kila nnaeamini anastahili na amini usiamini watu wanabadilika.
 
hahaaaa tena huyu ndo anaiudhi mpaka basi..na kujifanya kuvaa miwani nyeusi kama mwanamuziki wa akudo..anajifanya NIGAZ 2 PUBLIC...
 
Mpaka muda huu Makamu wa rais hajafika na FFU wanalanda landa kila kona
Biashara zote zimesimama na watu kuingia mafichoni huku wakisoma upepo.
Kuna uwezekano makamu wa rais akalazimisha kukata utepe wa soko huku akishangiliwa na maFFU wananchi wametawanyika na hawapendi soko lifunguliwe kwani halijaisha na wamechukizwa na kitendo cha kushushiwa bendera ya chama chao kipendwa na askari.
 
Dr Bilal. rudi Magogoni watu hawakutaki huko, Soko wajengee Wananchi wewe ulazimishe kulifungua, hii imekaaje?
Arggghhh serikali hii :hatari:
 
leo hii tunduma, hapana usalama baada ya bendera ya chadema kushushwa kwa kukata mlingoti wake wa chuma huku ikidaiwa kwamba, wameukata hili kuondoa uchafu kwa mgeni ambaye ni makamu wa rais na akisha ondoka watauludisha. lakini wananchi wamegoma kwa hiyo hapa ffu nyomi kuhakikisha bilal anautubia na kufungua soko hilo jipya. wananchi wanasema lazima kieleweke bla hivyo hakuna kuutubia mtu pale

Je viongozi wa kitaifa wa cdm wanakubaliana na hiyo kama hawakubaliani nayo wamechukua hatua gani? Dr. Slaa na Mbowe tunataka majibu ya hili suala haraka iwezekanavyo
 
Kwani huyo bilal ameenda kufungua hilo soko kama mwakilishi wa CCM ama Serikali?

Tatizo la viongozi wa nchi ni kulewa madaraka kiasi kwamba wanashindwa kutofautisha shughuli ya serikali na shughuli ya chama. Ndiyo maana Tunduma wana wapopoa kwa mawe kwa sababu wanatumia raslimali za serikali kwa manufaa ya chama, kitu ambacho si sahihi hata kidogo. Waacheni wapigwe mawe tuu mpaka watakapojifunza.
 
Hiyo ndiyo kazi pekee polisisiemu wanayoweza kuifanya kwa umakini.

Chonde chonde ndugu zangu mjihadhari hao mapolisisiemu hawachelewi kuwalenga risasi za vifua na kusingizia kwamba mlikuwa mnataka kuvamia msafara wa dr. bilal, gari lao ama kituo cha polisi.

Watatutendea kila wawezalo ila siku ya mwisho kwa Mungu watalia na kusaga meno
 
Ama ni kwa makusudi au kutojua lakini naona kama polisi wanaihujumu CCM!
Mabomu na sakarakasi zao za 'kusafisha' mandhari zinawapa hasira wananchi na matekeo yake watu wanazidi kukichukia CCM.
 
Je viongozi wa kitaifa wa cdm wanakubaliana na hiyo kama hawakubaliani nayo wamechukua hatua gani? Dr. Slaa na Mbowe tunataka majibu ya hili suala haraka iwezekanavyo

jibu gani unataka? bendera za chadema wanazoshusha hao ffu zinawahusu nini?...kwa kifupi ni kwamba ccm wanalazimshwa kupendwa..katu hawapendeki..shombo walilonalo hata waoge vipi haliishi....
 
Mpaka muda huu Makamu wa rais hajafika na FFU wanalanda landa kila kona
Biashara zote zimesimama na watu kuingia mafichoni huku wakisoma upepo.
Kuna uwezekano makamu wa rais akalazimisha kukata utepe wa soko huku akishangiliwa na maFFU wananchi wametawanyika na hawapendi soko lifunguliwe kwani halijaisha na wamechukizwa na kitendo cha kushushiwa bendera ya chama chao kipendwa na askari.


Wajameni mimi mwenzenu hata sipati:photo::photo::photo:

Kwani kufungua Soko lazima aende kiongozi wa juu (Makamu Raisi wa Jamuhuri ya Muungano TZ)?????

Hivi kwani Katibu kata au mwenyekiti wa Serikali ya mtaa hawezi kufungua Soko hadi afunge safari kiongozi toka DSM kwa ajili ya kufungua Soko???


RIP REMI ONGALA = Aliimba katika wimbo wake "SAUTI YA MNYONGE"

"Wamepewa madaraka, wakalala usingizi, tembo wanateketea (jamani) uchumi wa taifa unatoweka............."


Sasa Serikali tumeipa madaraka inalala na kuzinduka kwenye kufungua masoko. Hivi hakuna mambo ya maana ya kufanya yenye tija kitaifa??, Songea kuna mgogoro kwa nini asiende huko ili kurudisha amani katika mji wa Songea?


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
hhahah..sipati picha huko aliko..atakuwa amekaa kama bagbo alivyokutwa hiko ivory coast.....mzee atakuwa anakenua meno kama pembe za ng'ombe...chezea tunduma!!!?!!
 
Sielewei kwa nini masela wanashindwa kukamata pumbafu moja waonyeshe mfano..........
kwanini wanakubali kuonewa kila siku?.........get one Maza Faka, send a message!!
 
Tatizo la viongozi wa nchi ni kulewa madaraka kiasi kwamba wanashindwa kutofautisha shughuli ya serikali na shughuli ya chama. Ndiyo maana Tunduma wana wapopoa kwa mawe kwa sababu wanatumia raslimali za serikali kwa manufaa ya chama, kitu ambacho si sahihi hata kidogo. Waacheni wapigwe mawe tuu mpaka watakapojifunza.

Kisha na huku Tunduma nakumbuka ndiko kuna msimamo mkali sana kuhusu viongozi kupigwa mawe hawa wanaotumia Magari ya Serikali kwa shughuli za Chama:-

(1) J. Kikwete
(2) S. V. Nahodha
(3)..................... (sitaji nisije ambiwa mmbea bure!!!!!!!!!!)



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Mkuu wa Kaya kashaliona hili ndo maana siku hizi anafungua bank dar na kambi za vijana huko kwao. mikoani kimeo

Weka picha ya police wakisusha bendera za CDM maana ni ushahidi tosha kuonyesha namna vyombo vya dola vinavyo jihusisha na siasa.NA HII picha itanisaidia kwenye album inayotungwa kuhusu police wa Tz walivyo mbumbumbu.
 
Hivi huyu Bilali hana shughuli nyingine zaidi ya "Uzinduzi?"
Halafu huko Tunduma kunani mbona wanapishana tu kila leo. Akitoka siju Nahodha, mara bilali mara sijui nani....!
Suala ni kutatua matatizo ya wananchi na siyo kuzurura nchi nzima kujitetea.

Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno.

chama kinachoelekea kufa hugeuka na kuwa chama cha uzinduzi
 
Back
Top Bottom