BabuK
JF-Expert Member
- Jul 30, 2008
- 1,845
- 329
Kwenu wana JF wenye mapenzi mema na falsafa ya Kuzungumza kwa uwazi na ukweli kwa manufaa ya jamii yetu. Nimesoma maelezo katika mtiririko wa mada ya huyu dada aliyepata kuimba wimbo wa "WANAWAKE NA MAENDELEO".
Ninahisi tunavuka mipaka tunaopoanza kuanika mambo binafsi ambayo yanamshushia utu na heshima muhusika isipokuwa pale mambo hayo yanapoonekana yanahujumu haki za wengine na yenye mueleko wa jinai na ufisadi.
Tutazame Forums/Blogs za wenzetu waliokomaa na kuendelea katika uhuru wa mtu kutoa mawazo yake na pia kwa kuzingatia utamaduni wa kitanzania ....sidhani kama kuna kujadili personal issue kama katembea na nani au anamtongoza nani kunaleta chachandu ya maendeleo au kukuza mawazo chanya ya kimaendeleo...
JF inasifika kwa kuwa na mawazo endelevu sasa hizi hoja zinazowapa watu mawazo ya pili ..regulators wasiziruhusu.
UHURU WA MWENZAKO UNAANZIA PALE UHURU WAKO UNAPOISHIA!
TUJADILIANE NA KUHABARISHANA KWA HESHIMA NA KUWEKA MBELE MAADILI YA KITANZANIA.
Ninahisi tunavuka mipaka tunaopoanza kuanika mambo binafsi ambayo yanamshushia utu na heshima muhusika isipokuwa pale mambo hayo yanapoonekana yanahujumu haki za wengine na yenye mueleko wa jinai na ufisadi.
Tutazame Forums/Blogs za wenzetu waliokomaa na kuendelea katika uhuru wa mtu kutoa mawazo yake na pia kwa kuzingatia utamaduni wa kitanzania ....sidhani kama kuna kujadili personal issue kama katembea na nani au anamtongoza nani kunaleta chachandu ya maendeleo au kukuza mawazo chanya ya kimaendeleo...
JF inasifika kwa kuwa na mawazo endelevu sasa hizi hoja zinazowapa watu mawazo ya pili ..regulators wasiziruhusu.
UHURU WA MWENZAKO UNAANZIA PALE UHURU WAKO UNAPOISHIA!
TUJADILIANE NA KUHABARISHANA KWA HESHIMA NA KUWEKA MBELE MAADILI YA KITANZANIA.
Last edited: