Uzito wa Zitto, Wepesi wa Hoja kwa Suala zito

Mimi naungana na EMT katika hoja yake ya kutanganza mtu mapema, vinginevyo kinafichwa nini? Hata wakati wa Mkapa uchaguzi 1995, kwa hoja ya EMT, ilimchukua Nyerere kazi kubwa sana kwenda kumuuza mgombea yule, na pamoja na hayo, akaambulia 60% tu ya kura; Ndio maana hata katika uchaguzi wa 2015, CCM haitaweka mtu mpya, ni hawa hawa tunaowasikia, watachukua mmoja wao, kwani haina muda wa kuanza kuuza mtu mpya;

Na mfano wa EMT kuhusu Obama na maandalizi ya muda mrefu, mfano huu ukusaidie kuelewa zaidi pia kwamba hata ndani ya vyama wagombea wana mitazamo tofauti - Obama, Clinton, Biden, etc, wote hawa walikuwa na mtazamo tofauti ndani ya itikadi moja; Sasa kusema Chadema kwa sasa waende kujiuza kwa wananchi, ni sawa, lakini kwa msimamo gani? Ina maana unataka wale wote watakaotia nia kugombea kupitia Chadema wawe na msimamo mmoja wakati wa kuchujwa na chama chao? Hii itakuwa na maana gani katika demokrasia?

Vema utaratibu huo ukawepo kama sheria za uchaguzi zitarekebishwa, maana mambo kama hayo si katiba ya nchi, ni sheria za ziada za uchaguzi ambazo huwa zinabadilikabadilika kutokana na sababu mbalimbali. Wakati walipoweka muda mfupi kulikuwa na sababu za wakati huo ambazo ziliridhisha. Lakini kama leo sababu hizo hazina uzito tena kwa sababu ya utambulisho wa mgombea kwa wananchi uongezewe muda, ni vema serikali, mbunge au mtu binafsi kama sheria zinaruhusu apeleke ajenda hiyo bungeni ijadiliwe na kuibadilisha sheria ya uchaguzi.
 


Kundi linalomkubali halina hoja za msingi ila tu kama mwenyewe alivyosema anataka nchi hii wagombea wale wa
kizazi cha baada ya uhuru, maana yake Zitto Kabwe ameshaweka ubaguzi katika kuongoza nchi kwamba waliozaliwa kabla ya uhuru wasipate nafasi. Je, kama wanafaa basi tuwaengue kwa hoja kwamba walizaliwa kabla ya uhuru?

Suala ambalo kama ilivyo kwa kigezo cha umri, basi kama hili nalo lina umuhimu kwa kizazi cha sasa, alipendekeze kwa wananchi ili wananchi watolee maoni suala hili mbele ya Tume ya KATIBA, ili limit ya umri na kizazi, linapokuja suala la kugombea urais, basi lipewe nguvu ya Kikatiba; Suala hili linaingiliana na Swali langu katika bandiko namba moja kwamba:


  • Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Katiba Mpya, hasa nini kiwemo na nini kisiwemo, pamoja na mkakati wake wa kusimamia na kuyalinda hayo?
cc: Dark City
 
Hata ulichokijadili hapo juu kwenye nukuu haikuwa nilicho maanisha; ukinisoma vizuri utanielewa; Kimsingi, hoja yako kwamba niweke kundi lingine linalo husiana na Zitto kuwa pandikizi la CCM, binafsi sikuona kama mjadala huo una nafasi humu, kwani mjadala wa namna hiyo umeegemea zaidi kwenye FITINA za siasa, suala ambalo lina nyuzi zake nyingi tu humu tayari kwa mtu huyu huyu - Zitto; Mimi nadhani haukunielewa, hivyo ukanitafsiri vibaya; Vinginevyo huwa nina thamini sana michango yako na pia nyuzi zako, lakini kama nimekukwaza kwa hili, naomba uniwie radhi, ila nina amini kwamba tutakutana tu kwenye mijadala mingine kama kawaida yetu, hasa iwapo uamuzi wako wa kusimamisha michango yako katika uzi huu, utasimama Per bandiko namba 34 la uzi huu;
Hujanikwaza kwa lolote mkuu,ungekuwa umefanya hivyo,ningekueleza wazi kwasababu mimi si mtu wa maneno mengi bali right on the money.Umezungumzia kuwa kuna watu wanasapoti na kuna wanaompinga ndani ya chadema.Hilo nakubaliana nalo.Lakini mimi binafsi ni mmojawapo wa wale ambao wako concerned kuhusu wanaomsapoti ambao hawako ndani ya chadema.So nimegunduwa kwamba thread hii hainihusu kwasababu najuwa kuna watakaochangia ambao wanamsapoti na wao si wa chadema kutoka kwenye hizo kambi mbili ulizozianisha.Again mkuu,mjadala mwema na usiwe na wasiwasi kuhusu kunikwaza.I'm fine.
 
Wewe ndiyo sijakuelewa kabisa,ni vyema urudi kwenye ile thread uliyoianzisha nikakuuliza swali na hadi sasa hujalijibu!Unaweza ukawa unajaribu kumsadia kujibu swali nililolielekeza kwake bila ya kutambua nilichomuuliza.

Samahani sani,ila nadhani umedandia treni kwa mbele.

Ameona maoni yako ana nafasi ya kuyajibu, na maoni yanayotundikwa hapa hayana pingamizi kwa mwingine kuyajibu. Tujitahidi kujenga uvumilivu na ustahimilivu katika kujadili mada huwa zinatujenga na kusaidia wengi.
 
Hapo kwenye red ndipo ilipo argument yangu kuwa wananchi wahusishwe both kwenye selection and election phases. Hii at least itapunguza hili tatizo and in the long run labda kulitokomeza kabisa. Lakini ume-argue kuwa mazingira bado hayaruhusu. Tuendelee tuu kuwazuia wananchi kutojihusisha kwenye selection process.


Kama ni kuwahusisha kwa jinsi unayoiongelea mkuu basi hiyo ni nadharia kwati mimi naongelea kile ambacho ama kinafanyika au kinaweza kufanyika kwa sasa.

Wewe unaona kuna chama kinafanya hayo unayoyasema au kina mpango wa kuyafanya?

CCM walivyoanzisha utaratibu wa kura za maoni kwa wagombea ubunge umewafikisha wapi?
 
Ameona maoni yako ana nafasi ya kuyajibu, na maoni yanayotundikwa hapa hayana pingamizi kwa mwingine kuyajibu. Tujitahidi kujenga uvumilivu na ustahimilivu katika kujadili mada huwa zinatujenga na kusaidia wengi.
Kitu gani kimeonyesha kwamba sina uvumilivu kwenye hoja hii?Kumwambia mjadala mwema ndiyo umetafsiri kwamba siyo uvumilivu?Vipi wewe?Umeshajibu ile hoja kwenye ile thread yako?Ama wewe ndo huna uvumilivu na unatafuta thread nyingine kujikakamua?
 
Hapa una entertain kambi mbili za tofauti kati ya viongozi wa chadema na mwasisi wao mzee Mtei.Goodluck!

Kwa sababu kusimamishwa kwa Zitto kutatokana na Kanuni na Katiba ya Chadema, sio ya Katiba ya CCM; Kwa maaana nyingine rahisi, yatasemwa mengi lakini ni chama kimoja tu kitakachoamua hatima ya Zitto na kugombea Urais, na chama hicho sio CCM au NCCR, bali Chadema; Kwa maana nyingine rahisi zaidi, Urais wa Zitto bila maamuzi ya wanachadema, hauwezekeani; Labda kama ataamua kuhamia vyama hivyo akishindwa kupata nafasi anayoitafuta;
 
Kwa sababu kusimamishwa kwa Zitto kutatokana na Kanuni na Katiba ya Chadema, sio ya Katiba ya CCM; Kwa maaana nyingine rahisi, yatasemwa mengi lakini ni chama kimoja tu kitakachoamua hatima ya Zitto na kugombea Urais, na chama hicho sio CCM au NCCR, bali Chadema; Kwa maana nyingine rahisi zaidi, Urais wa Zitto bila maamuzi ya wanachadema, hauwezekeani; Labda kama ataamua kuhamia vyama hivyo akishindwa kupata nafasi anayoitafuta;
Lakini kugombea kwake pia kutatokana na katiba iliyowekwa ya ccm kuhusiana na miaka 40,ama si kweli?
 
Kama ni kuwahusisha kwa jinsi unayoiongelea mkuu basi hiyo ni nadharia kwati mimi naongelea kile ambacho ama kinafanyika au kinaweza kufanyika kwa sasa.

Wewe unaona kuna chama kinafanya hayo unayoyasema au kina mpango wa kuyafanya?

CCM walivyoanzisha utaratibu wa kura za maoni kwa wagombea ubunge umewafikisha wapi?

Na chini ya utaratibu huu, hauruhusiwi kutanganza nia mapema kwani ni kinyume na taratibu ambazo ni unwritten, ambazo zinatawaliwa na utamaduni wa kulindana na kuchaguana kuliko demokrasia; Kwenye kura za maoni CCM, wajumbe wa mikutano hawaruhusiwi kuhoji utendaji wa mbunge aliyepo na pia wagombea wengine hawaruhusiwi kuhoja hilo, kwa madai kwamba kufanya hivyo kunatoa nyezo kwa wapinzani kukishambulia CCM kwenye uchaguzi mkuu; Mnacho ruhusiwa kufanya ni kujitambulisha wewe ni nani, mwanachama wa muda gani, una uzoefu gani wa uongozi, na UTATEKELEZA VIPI ILANI YA CCM, huku tayari mnaambiwa mbunge aliyepo msimshambulie kwani amekuwa anatekeleza ilani ya CCM ipasavyo; Humo humo chini kwa chini kunaendelea fitina dhidi ya wagombea, hasa juu ya Elimu zao kwamba ni za kuchachua, udini, ukabila na kwamba hana hela za kuwapa wajumbe na pia kuwaendeleza wana jimbo; Sidhani kama Chadema wapo tayari kwenda huko;
 
Lakini kugombea kwake pia kutatokana na katiba iliyowekwa ya ccm kuhusiana na miaka 40,ama si kweli?

Ni sahihi, lakini mbona hoja hii inapingana na hoja ya awali kwamba Zitto ni pandikizi la CCM hivyo tumjadili kwa mtazamo wa kundi hili pia? Kwani kama CCM inataka ku maintain (KIKATIBA) kiwango cha umri wa mgombea - minimum kiwe miaka 40, basi chama hiki cha CCM hakiwezi kuwa ndio kile kile hicho kinachotafuta candidacy ya Zitto 2015, mwaka ambao Zitto atakuwa hajafikisha miaka 40 per requirement ya Katiba ambayo inaungwa mkono na CCM;

cc: Dark City
 
Lakini kugombea kwake pia kutatokana na katiba iliyowekwa ya ccm kuhusiana na miaka 40,ama si kweli?
Hata mimi nimesema huko nyuma kwamba, kwa mujibu wa katiba ya nchi ya sasa, Zitto hawezi kugombea urais. Na kama hivyo ndivyo kujadili kanuni za CHADEMA haina mshiko. Suala la msingi ni kwamba mfumo wa sasa wa chaguzi ni wa kisanii na mapendekezo yoyote ya ku-superimpose maboresho ya aina yoyote juu yake hayawezi kuleta tija.
 
Suala ambalo kama ilivyo kwa kigezo cha umri, basi kama hili nalo lina umuhimu kwa kizazi cha sasa, alipendekeze kwa wananchi ili wananchi watolee maoni suala hili mbele ya Tume ya KATIBA, ili limit ya umri na kizazi, linapokuja suala la kugombea urais, basi lipewe nguvu ya Kikatiba; Suala hili linaingiliana na Swali langu katika bandiko namba moja kwamba:


  • Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Katiba Mpya, hasa nini kiwemo na nini kisiwemo, pamoja na mkakati wake wa kusimamia na kuyalinda hayo?

Tatizo moja ambalo naliona vijana wengi huwa hatuko tayari kuona mambo kwa mapana na marefu na inapotokea kuonyesha madhaifu ya vijana ndipo inapotokea vijana kujenga hoja kwamba mtu unapinga vijana kugombea madaraka ya juu kuongoza nchi.

Katika mada ambayo imesomwa na watu wengi hivi karibuni jukwaa la siasa niliweka yenye kichwa cha habari
[h=1]Wasiomjua Dr. Slaa soma mada hii, kabla ya uanasiasa na baada[/h]
Hitimisho la habari hiyo nilitoa tahadhari kwa vijana tabia ambazo kwa sababu ya kukosekana ukomavu, uzoefu na ustahimilivu huweza kutokea katika historia ya vijana wenye umri ndogo kuongoza nchi kama ifuatavyo:

Kuongoza nchi hakuna shule wala kitabu cha kusomea au chuo. Hekima na busara ya mtu ndio kielelezo cha fanaka katika kuongoza nchi.

  • Vijana wana papara,
  • wanataka njia ya mkato,
  • pagumu wanataka kulazimisha bila busara wala kutumia akili
  • Vijana wanalipuka kama moto wa gas
  • mambo yakigeuka magumu ni mabavu hutumika.
Ukweli unauma lakini hali halisi ndiyo hiyo. Hata hivyo si vijana wote wanaoweza kuwa hali kama hiyo. Malikia wa Uingereza ameanza kushika nchi akiwa na umri nadhani chini ya 35 na leo amefikisha kukalia kiti kile kwa miaka 60. Mwenye ukomavu ushauri anaopewa Zitto angekuwa mwelevu wa kuelewa, lakini dalili ya kutosikia na kudharau ushauri hata pale katiba inapoonekana kutomruhusu na kubaki kung'ang'ania niseme wazi anakwaza jamii ya vijana na kuja kueleweka kama ni ving'ang'anizi.

Kikwete ni mfano dhahiri wa yanayomkua Zitto. Nyerere alikuwa mmojawapo aliyemshauri kuvuta subira kwa vile umri wake bado unadai na nihazina ya Chama sikuzijazo, alivumilia huyo sasa yupo Ikulu. Vwai naye kutoka kule Zenj aliambiwa vivyo hivyo uchaguzi mkuu uliopita, ametulia, ipo siku mambo yatamnyookea tu. Hii ya kushindana kwa nguvu zote wakati katiba haimpi nafasi kuna kitu cha kujiuliza ambacho kipo ndani ya moyo wake.
 
Kwa sababu kusimamishwa kwa Zitto kutatokana na Kanuni na Katiba ya Chadema, sio ya Katiba ya CCM; Kwa maaana nyingine rahisi, yatasemwa mengi lakini ni chama kimoja tu kitakachoamua hatima ya Zitto na kugombea Urais, na chama hicho sio CCM au NCCR, bali Chadema; Kwa maana nyingine rahisi zaidi, Urais wa Zitto bila maamuzi ya wanachadema, hauwezekeani; Labda kama ataamua kuhamia vyama hivyo akishindwa kupata nafasi anayoitafuta;

Jambo hili kama Dark City alivyotolea ufafanuzi na hata mie nilishalijadili hakuna haja ya kujadili hoja ya Zitto kugombea Urais kama katiba ya chama chake inamruhusu au la, sababu kifungu cha katiba ya nchi ni kitanzi kinachomfunga, hata arukie chama gani atakutana nacho.

Bora tujadili mambo mengine lakini hili la Zitto akishafikisha umri wa miaka 40 yuko huru kugombea tutamjadili au kifungu cha Katiba kikiratibiwa na kuteremshwa umri wa kugombea tutajadili. Kwa sasa hatuna sababu ya kujadili kitu ambacho kikatiba hakimpi nafasi.
 
Na chini ya utaratibu huu, hauruhusiwi kutanganza nia mapema kwani ni kinyume na taratibu ambazo ni unwritten, ambazo zinatawaliwa na utamaduni wa kulindana na kuchaguana kuliko demokrasia; Kwenye kura za maoni CCM, wajumbe wa mikutano hawaruhusiwi kuhoji utendaji wa mbunge aliyepo na pia wagombea wengine hawaruhusiwi kuhoja hilo, kwa madai kwamba kufanya hivyo kunatoa nyezo kwa wapinzani kukishambulia CCM kwenye uchaguzi mkuu; Mnacho ruhusiwa kufanya ni kujitambulisha wewe ni nani, mwanachama wa muda gani, una uzoefu gani wa uongozi, na UTATEKELEZA VIPI ILANI YA CCM, huku tayari mnaambiwa mbunge aliyepo msimshambulie kwani amekuwa anatekeleza ilani ya CCM ipasavyo; Humo humo chini kwa chini kunaendelea fitina dhidi ya wagombea, hasa juu ya Elimu zao kwamba ni za kuchachua, udini, ukabila na kwamba hana hela za kuwapa wajumbe na pia kuwaendeleza wana jimbo; Sidhani kama Chadema wapo tayari kwenda huko;
Anatangaza nia ya nini wakati haruhusiwi kugombea? Ndo tunamshangaa na kushangaa mjadala wowote ambao unajadili jambo nyeti kama hili la kutangaza nia mapema ila katika context ya Zitto. Huo utaratibu Wa CCM umeshindwa kutekezeka kwa kuwa chaguzi zetu ni za kisanii zaidi. CHADEMA au chama kingine wanatakiwa kuandaa umma kama ilivyokuwa wakati wa kudai uhuru. Wakishapewa ridhaa ya kutuongoza wabadili mfumo wa uchaguzi. Kw sasa ni ngumu sana kwani tunachagua wafanyabiashara/walanguzi badala ya viongozi.
 
Jambo hili kama Dark City alivyotolea ufafanuzi na hata mie nilishalijadili hakuna haja ya kujadili hoja ya Zitto kugombea Urais kama katiba ya chama chake inamruhusu au la, sababu kifungu cha katiba ya nchi ni kitanzi kinachomfunga, hata arukie chama gani atakutana nacho.

Bora tujadili mambo mengine lakini hili la Zitto akishafikisha umri wa miaka 40 yuko huru kugombea tutamjadili au kifungu cha Katiba kikiratibiwa na kuteremshwa umri wa kugombea tutajadili. Kwa sasa hatuna sababu ya kujadili kitu ambacho kikatiba hakimpi nafasi.

Kwa hoja hii, nadhani wengi tunakubaliana kwamba ni hoja nzito, sio nyepesi; Kwahiyo mjadala wa candidacy ya Zitto Per KATIBA JMT (1977) hauna maana tena, na inatakiwa hata wanaompinga ndani ya Chama chake cha Chadema watumie hoja kama hii kwa lugha nyepesi tu na ya kumpa moyo kwamba asubirie kwanza mabadiliko hayo iwapo yatakuja, na kauli hii itoke kwenye vikao, sio vibarazani au barabarani ambapo hoja nyepesi za kumpinga zitto hujitokeza;

Lakini katika kipindi hiki, Zitto asife moyo, aendelee tu na azima yake hii, lakini ajikite hasa katika swali langu la TANO, bandiko la kwanza la uzi huu, nililoelekeza kwa kambi inayomuunga mkono:


  • Zitto Anasimamia Wapi Kuhusu Katiba Mpya, hasa nini kiwemo na nini kisiwemo, pamoja na mkakati wake wa kusimamia na kuyalinda hayo?
Akijipanga sawa na hoja yake kuhusu umri wa kugombea na aina cha kizazi cha kugombea, huku yeye na timu yake wakihamasisha vijana watoe maoni hayo katika mchakato wa katiba mpya, pengine itamsaidia zaidi;
 
Kama ni kuwahusisha kwa jinsi unayoiongelea mkuu basi hiyo ni nadharia kwati mimi naongelea kile ambacho ama kinafanyika au kinaweza kufanyika kwa sasa.

Wewe unaona kuna chama kinafanya hayo unayoyasema au kina mpango wa kuyafanya?

CCM walivyoanzisha utaratibu wa kura za maoni kwa wagombea ubunge umewafikisha wapi?

Mkuu the fact kuwa hakuna chama kinachofanya hivyo au kina mpango wa kuyafanya hivyo, haina maana kuwa viendelee kufanya wanayofanya sasa. Otherwise, tutakuwa tunalalamika tuu halafu wakti huo huo tunajustify wanayofanya sasa. Kwa mfano utaratibu wa CCM, nafasi ya mwenyekiti na makamu wake hazigombewi, bali hutokana na uteuzi wa Kamati Kuu na majina kuthibitishwa na Halmashauri Kuu (Nec), ambapo chini ya utaratibu wa sasa, Rais ndiye anayekuwa mwenyekiti wa chama taifa. Kimsingi huu si utaratibu mzuri. Lakini pia haiwezekani uachwe kwa sababu tuu mazingira hayaruhusu. Kuwepo kwa mabadiliko ya kuchagua mtu makini mwenye viwango vya kuwa Rais kutalazimisha kuwepo mabadiliko kwenye vyama pia.
 
Anatangaza nia ya nini wakati haruhusiwi kugombea? Ndo tunamshangaa na kushangaa mjadala wowote ambao unajadili jambo nyeti kama hili la kutangaza nia mapema ila katika context ya Zitto. Huo utaratibu Wa CCM umeshindwa kutekezeka kwa kuwa chaguzi zetu ni za kisanii zaidi. CHADEMA au chama kingine wanatakiwa kuandaa umma kama ilivyokuwa wakati wa kudai uhuru. Wakishapewa ridhaa ya kutuongoza wabadili mfumo wa uchaguzi. Kw sasa ni ngumu sana kwani tunachagua wafanyabiashara/walanguzi badala ya viongozi.

Kimsingi nakubaliana na hoja yako; Ningependa pia kusikia mawazo yako kuhusiana na majibu yangu kwa jmushi1 kwenye bandiko namba 50 la uzi huu, bandiko ambalo pia nilikutumia copy;
 
Ni sahihi, lakini mbona hoja hii inapingana na hoja ya awali kwamba Zitto ni pandikizi la CCM hivyo tumjadili kwa mtazamo wa kundi hili pia? Kwani kama CCM inataka ku maintain (KIKATIBA) kiwango cha umri wa mgombea - minimum kiwe miaka 40, basi chama hiki cha CCM hakiwezi kuwa ndio kile kile hicho kinachotafuta candidacy ya Zitto 2015, mwaka ambao Zitto atakuwa hajafikisha miaka 40 per requirement ya Katiba ambayo inaungwa mkono na CCM;

cc: Dark City

Wengi wetu tumezoea majibu ya mkato na pengine kutoruhusu ubongo ufanye kazi yake ipasavyo. Mara kadhaa nimeangalisha vyombo vya habari badala ya kuhabarisha, kuelimisha, kudadisi na kufafanua kwa manufaa ya jamii vimejikita kwenye ushabiki na hivyo uchaguzi unapokaribia utakuwa vyombo vya habari vinaendeshwa na vyama kwa misingi ya kiitikadi badala ya kujenga taswira ya kuwasaidia wapiga kura kuwaelewa wapiga kura.

Tanzania tuna kazi ya kuondokana na utamaduni wa kuchagua chama badala ya mtu. Sasa hivi utasikia mimi nataka CCM na Mwingine nataka Chadema na kule watakuambia mimi yangu CUF. Hao wagombea wanafaa au la haina maana kwao zaidi ya rangi ya chama.

Ningeweza kuja na wazo kwamba mfumo wa vyama vya siasa kujijenga kwa misingi ya matawi na kupeperushwa bendera imepitwa na wakati na ndicho kinachotuharibia kupata watu makini. Pamoja na kwamba copy and paste tusiiruhusu sana, lakini mfumo huo ambao Marekani hutumika naona unafaa kwani hakuna mambo ya matawi mitaani, wanachama wanaojiunga wengi ni kwa sababu ya kutafuta nafasi za uongozi, kwani watu wasio na malengo ya kisiasa hawahangaiki na mambo ya vyama ila wakati wa uchaguzi ukiwadia nani mwenye sera nzuri ndiye anayechaguliwa.
 
Mkuu the fact kuwa hakuna chama kinachofanya hivyo au kina mpango wa kuyafanya hivyo, haina maana kuwa viendelee kufanya wanayofanya sasa. Otherwise, tutakuwa tunalalamika tuu halafu wakti huo huo tunajustify wanayofanya sasa. Kwa mfano utaratibu wa CCM, nafasi ya mwenyekiti na makamu wake hazigombewi, bali hutokana na uteuzi wa Kamati Kuu na majina kuthibitishwa na Halmashauri Kuu (Nec), ambapo chini ya utaratibu wa sasa, Rais ndiye anayekuwa mwenyekiti wa chama taifa. Kimsingi huu si utaratibu mzuri. Lakini pia haiwezekani uachwe kwa sababu tuu mazingira hayaruhusu. Kuwepo kwa mabadiliko ya kuchagua mtu makini mwenye viwango vya kuwa Rais kutalazimisha kuwepo mabadiliko kwenye vyama pia.

Inashangaza kuona vyama vingi vya siasa including Chadema, wameiga mfumo wa CCM hata kioganaizesheni; Je hii ina maana kwamba, tukiachana na udhaifu mwingine wa CCM kama vile ufisadi, Chadema iliona mfumo huu ni more effective au ilitokana na ukosefu wa ubunifu?

Chadema wanasahau kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Muungano wa TANU na ASP, na chama kiliposhika hatamu mwaka 1977, ndio kikaja na mfumo wake ulioendelea mpaka pale vyama vingi vya siasa ulipoingia, ambapo ilbidi ubadilishwe kidogo na kuendelea mpaka hivi sasa; Chadema inaonekana wanacheza ngoma ile ile, sasa sielewi kama ni mfumo effective? Ukosefu wa ubunifu? ni matakwa chini ya sheria ya msajili wa vyama vya siasa?

cc: candid scope
 
Hujanikwaza kwa lolote mkuu,ungekuwa umefanya hivyo,ningekueleza wazi kwasababu mimi si mtu wa maneno mengi bali right on the money. Umezungumzia kuwa kuna watu wanasapoti na kuna wanaompinga ndani ya chadema.Hilo nakubaliana nalo.Lakini mimi binafsi ni mmojawapo wa wale ambao wako concerned kuhusu wanaomsapoti ambao hawako ndani ya chadema.So nimegunduwa kwamba thread hii hainihusu kwasababu najuwa kuna watakaochangia ambao wanamsapoti na wao si wa chadema kutoka kwenye hizo kambi mbili ulizozianisha.Again mkuu,mjadala mwema na usiwe na wasiwasi kuhusu kunikwaza.I'm fine.

Mkuu hapo kwenye red sidhani kama mleta mada amesema hiyo. Nilivyomwelewa mleta mada amesema kuwa "Suala la Zitto kutangaza nia yake kuwania Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema Uchaguzi Mkuu Ujao wa mwaka 2015, limepokewa kwa hisia na tafsiri mbalimbali ndani ya Jamii [emphasis added in red]. Alikuwa na maana gani aliposema "Jamii"?

Akaendelea kusema kuwa "Pamoja na mgawanyiko huu wa hisia na tafsiri, mgawanyiko mkubwa upo katika kambi kuu mbili; Kambi ya Kwanza ni ile inayo muunga Mkono Zitto kwa uamuzi huu, wakiwepo viongozi kadhaa ndani ya Chadema; Kambi ya Pili ni ile inayo mpinga Zitto kwa uamuzi huu, akiwemo Mwasisi wa Chadema, Mzee Edwin Mtei."

Mimi nilidhani hapo kwenye "wakiwepo viongozi kadhaa ndani ya Chadema" na "akiwemo Mwasisi wa Chadema, Mzee Edwin Mtei", ni moja ya watu walio kwenye hizo kambi kuu mbili. Hapo naweza ku-interpret hao aliowataja kama ni mifano ya watu walio kwenye hizo kambi. Nadhani "Kambi ya Kwanza ni ile inayo muunga Mkono Zitto kwa uamuzi huu" na "Kambi ya Pili ni ile inayompinga Zitto" regardless of whether wapo ndani au nje ya Chadema

Kama kuna kambi ya tatu inayomuunga mkono lakini hawako ndani ya Chadema, then it is possible pia kuwepo kwa kambi ya nne ambayo haimuungi mkono na iko nje ya Chadema? Hii nayo tuijadili?

Hata hivyo, it sounds odd kwa kambi inayomuunga mkono Zitto whether ndani au nje ya Chadema kama kisheria this president wannabe hataweza kuwa certified na mamlaka husika kwa sababu ya kutotimiza vigezo vyote vya kisheria vya kuchaguliwa kama Rais wa nchi hii.
 
Back
Top Bottom