Uzito wa Zitto, Wepesi wa Hoja kwa Suala zito

Niseme tu kwamba mimi sina ufahamu iwapo katika demokrasia ya kiliberali ambayo ndio tunaifuata, suala la timing katika suala tunalojadili, linakuwa treated vipi, hasa ikizingatiwa kwamba hakuna a universal approach katika suala hili, hata katika mfumo unwritten...; ndio maana narudi kwenye Kanuni;


Kama ukiamua kunisoma vizuri, mada yangu hailengi kumjadili MTU kwa Kumfananisha na MTU, bali MTU na Masuala, kwanza ya ndani KIKANUNI na KIKATIBA na vile vile kwa nje, Msimamo wake dhidi ya MASUALA ambayo yanazunguka maisha ya wananchi wa leo;

Vinginevyo Siasa za timing katika ugombea Urais, zilizaliwa CCM, na inanishangaza kwanini Chadema wanaiga utamaduni huu na sina uhakika kama una manufaa; Ningeomba unielimishe zaidi juu ya hili;

Kwa vile wewe ni mwana CCM (naamini sijakosea) ungetumia muda wako kidogo kujielimisha kwa nini CCM iliasisi mfumo huo wa timing na kuzuia watu kugombea endapo kuwa Rais anayetaka kumalizia muhula wa pili.

Pia kwa vile tuko katika siasa zinazotawaliwa na CCM kwa kiasi kikubwa, ungejaribu pia kujielimisha kwa nini CCM inaongoza kwa mbinu chafu ikiwemo fitna, rushwa na hata kuondoa uhai wa watu ili mradi ibaki madarakani.

Sasa, mtu yeyote makini, atajuaje kama si mbinu za CCM kujaribu kupunguza idadi ya watu wa kushughulikia kabla ya 2015?

Nadhani ni vigumu kujadili hoja yako bila kuielewa Tanzania yetu na TANU hadi CCM!!
 
Mchambuzi,Tutamjadili Zitto Kabwe kugombea urais wa Tanzania atakapofikisha umri ambao kikatiba unamruhusu, kwa sasa katiba haimruhusu Zitto Kabwe kugombea urais kwa vile yuko chini ya umri wa miaka 40. Hata 2015 kama kifungu cha katiba kuhusu umri wa kugombea urais Tanzania usipofanyiwa marekebisho bado hatakuwa na nafasi hiyo.

Bora Zitto na wanamwunga mkono wangehangaikia Katiba mpya kufanyiwa marekebisha badala ya kuhangaikia kitu ambacho kikatiba ni ukiukwaji.

Hiyo ni hoja nzito ambayo inagusa Katiba ya nchi kuhusu umri wa mgombea Urais

Na hiyo pia ndiyo hoja inayowafanya watu wengine washindwe kujua kinachomnyima Zitto uvumilivu hadi aanze kufikiria kitu ambacho hakipo kikatiba....!!

Hata kama tutahitaji kubadilisha umri, ni kwa sababu ya Zitto au matakwa ya jamii pana na nyakati zetu?

Hii issue inazua maswali mengi ambayo kwa bahati mbaya (kwa maoni yangu) yanamweka Zitto katika mazingira magumu sasa na huko mbele ya safari!!
 
Upo sahihi, hii ni hoja nzito, sio hoja nyepesi; Pengine ana matarajio kwamba kigezo hiki kitatenguliwa ndani ya katiba mpya, lakini kama ulivyosema, hadi ifikie huko, as we stand, Zitto hawezi kuwa Rais wa Tanzania kwa vile Katiba haimruhusu kutokana na suala la ugombea; Lakini swali langu linalofuata kwako ni je, pingamizi ndani ya chama chake zinatokana na Chadema pia kuheshimu kigezo kilichopo ndani ya katiba ya nchi? Au kuna lingine Kikanuni na Kikatiba?

Sasa kama anazuiliwa na Katiba ya nchi, kwa nini tena tuongelee mambo ya chama ambayo hayawezi kuja juu ya Katiba ya nchi?

Na kwa vile katiba haijabadilishwa, kitu gani kinamnyima Zitto uvumilivu hadi atangaze nia katika kitu ambacho kisheria hakiwezi kuwepo?

Kwa nini asingekaa kimya ila akawekeza nguvu zake kwenye mabadiliko ya katiba ili baadaye ndiyo akunjue makucha?
 
Kwa kuliangalia hili suala kwa mapana zaidi nafikiri linapokuja suala na nani agombee urais either Chadema, CCM au chama kingine wapiga kura wanakuwa hawajui ni akina nani watagombea urais mpaka dakika za mwisho kabla ya uchaguzi kufanyika.

Kwa mfano, kwenye uchaguzi uliopita Chadema walimtangza Dkt. Slaa kuwa mgombea wa Urais nafikiri miezi mitatu or so kabla ya uchaguzi kufanyika. Nafikiri hili ni tatizo. Kwanza, kunakuwa hakuna muda ya kutosha kumnadi mgombea hasa kama alikuwa hajulikani sana. Mfano tuu, watu wengi walipokea habari ya Dkt. Slaa kugombea Urais kwa mshutuko kidogo.

Wapo wanaosema kuwa Dkt. Slaa angepata kura nyingi zaidi au hata kushinda ule uchaguzi kama alikuwa amejulikana mapema zaidi kuwa atagombea Urais. Huwezi kumnadi mgombea Urais hasa wa chama cha upinzani ndani ya miezi mitatu na kutegemea kuwa atashinda huo uchaguzi. Unafikiri kama akina Obama au David Cameron wangetangazwa miezi mitatu kabla ya uchaguzi kuwa watagombea, wangeshinda?

Pili, kunakuwa hakuna muda wa kutosha kwa wapiga kura ku-scrutinise hao wagombea kama wanafaa kuwa Rais wa nchi. Simaanishi kuwa wagombea Urais watangazwe mapema kabisa kabla ya tarehe ya uchaguzi, bali angalao kila chama kiweke mazingira ambayo yatawaonyesha wapiga kura kuwa huyu ndiye mtu tunayemwandaa ili aje kugombea Urais kwenye uchaguzi ujao. This will enable the whole party to rally behind him/her.

Nafikiri hapa pia linakuja suala la kutenganisha nafasi ya Rais wa nchi na mwenyekiti wa chama tawala. Kuwe na system ambayo inamtayarisha mtu mapema kabisa kama mgombea Urais kwa kumpa majukumu ya kukiongoza chama kama mwenyekiti ili wapiga waone kama kweli anaweza kuongoza. Siyo mtu anaibuka dakika za mwisho na kuchukua fomu eti naye anataka kugombea Urais. How do you expect a voter to scrutinise you?

Tukija kwa Chadema bado hakuna anayejua ni nani anayeandaliwa na chama kuwa mgombea wa Urais 2015. Hata kwa CCM, hakuna anayejua. Wakiulizwa wanasema bado ni mapema mno. Kwa mara nyingine tena wapiga kura wanaachwa kwenye mataa mpaka dakika za mwisho. Wapiga wanatakiwa kujua ni nani atagombea Urais ili waweze kumchambua kwa kina kama kweli anafaa kupigiwa kura. Pia hii inakisaidia chama kumnadi huyo potential candidate kwa wananchi.

For the political parties, the preparation for the election is longer especially for opposition parties such as Chadema. The quality and focus of preparations for the 2010 elections, and how Chadema handled the election, should provide valuable and timely lessons to them. Unfortunately, I can't see this happening kwa sababu ya system iliyoko sasa.

Matokeo ya kutokuwepo kwa system ya hii ndiyo unakuta watu wanaamka asubuhi na kutangaza kuwa watagombea Urais huku wengine wakisubiri kuoteshwa kwanza ili watangaze rasmi kuogombea. Wengine wanatangaza kugombea Urais wakati wanajua wazi watakuwa hata hawa-qualify kisheria kugombea huo urais in the first place.
 
Kwa kuliangalia hili suala kwa mapana zaidi nafikiri linapokuja suala na nani agombee urais either Chadema, CCM au chama kingine wapiga kura wanakuwa hawajui ni akina nani watagombea urais mpaka dakika za mwisho kabla ya uchaguzi kufanyika.

Kwa mfano, kwenye uchaguzi uliopita Chadema walimtangza Dkt. Slaa kuwa mgombea wa Urais nafikiri miezi mitatu or so kabla ya uchaguzi kufanyika. Nafikiri hili ni tatizo. Kwanza, kunakuwa hakuna muda ya kutosha kumnadi mgombea hasa kama alikuwa hajulikani sana. Mfano tuu, watu wengi walipokea habari ya Dkt. Slaa kugombea Urais kwa mshutuko kidogo.

Wapo wanaosema kuwa Dkt. Slaa angepata kura nyingi zaidi au hata kushinda ule uchaguzi kama alikuwa amejulikana mapema zaidi kuwa atagombea Urais. Huwezi kumnadi mgombea Urais hasa wa chama cha upinzani ndani ya miezi mitatu na kutegemea kuwa atashinda huo uchaguzi. Unafikiri kama akina Obama au David Cameron wangetangazwa miezi mitatu kabla ya uchaguzi kuwa watagombea, wangeshinda?

Pili, kunakuwa hakuna muda wa kutosha kwa wapiga kura ku-scrutinise hao wagombea kama wanafaa kuwa Rais wa nchi. Simaanishi kuwa wagombea Urais watangazwe mapema kabisa kabla ya tarehe ya uchaguzi, bali angalao kila chama kiweke mazingira ambayo yatawaonyesha wapiga kura kuwa huyu ndiye mtu tunayemwandaa ili aje kugombea Urais kwenye uchaguzi ujao. This will enable the whole party to rally behind him/her.

Nafikiri hapa pia linakuja suala la kutenganisha nafasi ya Rais wa nchi na mwenyekiti wa chama tawala. Kuwe na system ambayo inamtayarisha mtu mapema kabisa kama mgombea Urais kwa kumpa majukumu ya kukiongoza chama kama mwenyekiti ili wapiga waone kama kweli anaweza kuongoza. Siyo mtu anaibuka dakika za mwisho na kuchukua fomu eti naye anataka kugombea Urais. How do you expect a voter to scrutinise you?

Tukija kwa Chadema bado hakuna anayejua ni nani anayeandaliwa na chama kuwa mgombea wa Urais 2015. Hata kwa CCM, hakuna anayejua. Wakiulizwa wanasema bado ni mapema mno. Kwa mara nyingine tena wapiga kura wanaachwa kwenye mataa mpaka dakika za mwisho. Wapiga wanatakiwa kujua ni nani atagombea Urais ili waweze kumchambua kwa kina kama kweli anafaa kupigiwa kura. Pia hii inakisaidia chama kumnadi huyo potential candidate kwa wananchi.

For the political parties, the preparation for the election is longer especially for opposition parties such as Chadema. The quality and focus of preparations for the 2010 elections, and how Chadema handled the election, should provide valuable and timely lessons to them. Unfortunately, I can't see this happening kwa sababu ya system iliyoko sasa.

Matokeo ya kutokuwepo kwa system ya hii ndiyo unakuta watu wanaamka asubuhi na kutangaza kuwa watagombea Urais huku wengine wakisubiri kuoteshwa kwanza ili watangaze rasmi kuogombea. Wengine wanatangaza kugombea Urais wakati wanajua wazi watakuwa hata hawa-qualify kisheria kugombea huo urais in the first place.

Unayoongea mkuu ningeyakubali kama mpiga kura wa Tanzania angekuwa na madhara makubwa katika kuamua nani awe Rais wa nchi.

Kwa vile mfumo mzima wa uchanguzi wetu umekaa kimagumashi, basi kwa sasa tujipange kwa mambo ambayo yanachangia zaidi. Kwa mtazamo wangu, CHADEMA tayari wanafanya kazi muhimu ya kupeleka chama kwa wananchi ili hata wakitangaza mgombea, kila mtu kutoka pembe ya nchi hii awe anakijua chama tofauti na huko nyuma.

System za Ulaya Magharibi na Marekani haziakisi ukweli halisi katika mazingira yetu!
 
Unayoongea mkuu ningeyakubali kama mpiga kura wa Tanzania angekuwa na madhara makubwa katika kuamua nani awe Rais wa nchi.

Kwa vile mfumo mzima wa uchanguzi wetu umekaa kimagumashi, basi kwa sasa tujipange kwa mambo ambayo yanachangia zaidi. Kwa mtazamo wangu, CHADEMA tayari wanafanya kazi muhimu ya kupeleka chama kwa wananchi ili hata wakitangaza mgombea, kila mtu kutoka pembe ya nchi hii awe anakijua chama tofauti na huko nyuma.

System za Ulaya Magharibi na Marekani haziakisi ukweli halisi katika mazingira yetu!

Asante sana Mkubwa,
Kucopy na kupaste kila kitu kutoka Magharibi ndivyo vinavyotuchanganya, tatizo letu kubwa tunashindwa kutumia elimu za darasani na hali halisi, vitabu vimeandikwa na watu baada ya kuakisi hali halisi kutokana na mazingira, wakati matukio. Swala la kuanza kampeni miaka mitatu, minne au mitano Tanzania kiukweli ni fujo.

Chama kama chadema achilia mbali kukampeni leo kuingia ikulu kwa mtu mmoja kinahitajika kujengwa kwanza ni sawa na kung'ang'ania sahani wakati hata jiko haliko. Hii ni tamaa tu na kutaka kuwahi kitanda wakati hata fedha za kununulia kitanda hazipo.

Nafikiri tungekuwa na team work ya chama yenye malengo ya kwenda ikulu kutatua matatizo halisi ya Mtanzania na lazima mgombea huyu abebe ujumbe, sera, na matarajio ya wananchi lazima chama kiamue kama chama nani atafaa wakati ukifoka.

Leo tujikite kujenga chama, siasa za Tanzania ni siasa za chama hakuna atakayekwenda Ikulu na sera zake au mipango yake huo ni uongo labda awe mgombea binafsi, Chama legelege kitatuletea Raisi Legelege, kama CCM ingekuwa imara leo Raisi asingekuwa legelege. Kiongozi anayetokana na chama cha siasa lazima akubaliane na chama husika au kutofautiana kisera na kiutendaji na ajitoe kwenye chama husika.

Mfumo wetu wa demokrasia bado haujakuwa na hatuwezi kulazimisha kukomaa leo wakati mfumo uko kwenye stage ya mtoto wa miaka kumi. Tutafika mahala ambapo uraisi utakuwa ni wa taasisi ya mtu ila huko bado.

Hata mgombea binafsi kushinda kwenye mazingira ya Tanzania ni ngumu sana labda mtu auze nchi kwa mafisadi na wa ndani na nje ili wamchangie fedha nyingi ili aweze kuingia ikulu.

Tujenge dempkrasia ya kweli sio demokrasia madaraka.
 
Hoja ya kumpinga mgombea wa chama chochote kutangaza nia itakuwa ni hoja nzito iwapo tu ni suala la KIKANUNI/KATIBA; Hoja ya kumuunga mgombea itakuwa ni hoja nzito iwapo tu inahusisha msimamo wake vis a vis matarajio na matumaini ya wananchi walio wengi; Nje ha hapo, mjadala huu utaenda kinyume na kilichokusudiwa, na isitoshe, uliyoyazungumza yameshajadiliwa sana elsewhere;
Humu JF kuna wanachama zaidi ya wale wa chadema,kama unamaanisha mjadala huu ni wa wana chadema peke yake,then i'm sorry!

Naomba uwazuie wanachama wote wasiokuwa wa chadema kuchangia mjadala huu.
 
Asante sana Mkubwa,
Kucopy na kupaste kila kitu kutoka Magharibi ndivyo vinavyotuchanganya, tatizo letu kubwa tunashindwa kutumia elimu za darasani na hali halisi, vitabu vimeandikwa na watu baada ya kuakisi hali halisi kutokana na mazingira, wakati matukio. Swala la kuanza kampeni miaka mitatu, minne au mitano Tanzania kiukweli ni fujo.

Chama kama chadema achilia mbali kukampeni leo kuingia ikulu kwa mtu mmoja kinahitajika kujengwa kwanza ni sawa na kung'ang'ania sahani wakati hata jiko haliko. Hii ni tamaa tu na kutaka kuwahi kitanda wakati hata fedha za kununulia kitanda hazipo.

Nafikiri tungekuwa na team work ya chama yenye malengo ya kwenda ikulu kutatua matatizo halisi ya Mtanzania na lazima mgombea huyu abebe ujumbe, sera, na matarajio ya wananchi lazima chama kiamue kama chama nani atafaa wakati ukifoka.

Leo tujikite kujenga chama, siasa za Tanzania ni siasa za chama hakuna atakayekwenda Ikulu na sera zake au mipango yake huo ni uongo labda awe mgombea binafsi, Chama legelege kitatuletea Raisi Legelege, kama CCM ingekuwa imara leo Raisi asingekuwa legelege. Kiongozi anayetokana na chama cha siasa lazima akubaliane na chama husika au kutofautiana kisera na kiutendaji na ajitoe kwenye chama husika.

Mfumo wetu wa demokrasia bado haujakuwa na hatuwezi kulazimisha kukomaa leo wakati mfumo uko kwenye stage ya mtoto wa miaka kumi. Tutafika mahala ambapo uraisi utakuwa ni wa taasisi ya mtu ila huko bado.

Hata mgombea binafsi kushinda kwenye mazingira ya Tanzania ni ngumu sana labda mtu auze nchi kwa mafisadi na wa ndani na nje ili wamchangie fedha nyingi ili aweze kuingia ikulu.

Tujenge dempkrasia ya kweli sio demokrasia madaraka.

Hayo ndiyo tunayoyasema,

Yaani watu wameshaona makosa ya CCM na jinsi yanavyotugharimu kama taifa halafu wanataka turudie hayo hayo...Hili tunatakiwa kulipinga kwa nguvu zote. Upuuzi wa kutumia mitandao na familia kuingia ikulu bila ajenda ya chama ndiyo umetusababishia matatizo haya tutayokabiliana nayo sasa na madhara yake yatatuchukua miaka mingi sana kuyasafisha. Na tukirogwa tukampa Lowasa urais, tutakuwa tunaendelea kuongeza gharama ya upuuzi wetu.

Kwa watu wenye akili, waunde chama imara chenye timu imara na itakayoweza kupambana na uchafu kwanza ndani ya chama chenyewe, kwenye serikali na jamii nzima kwa ujumla.

Kinyuma cha hayo tujiandae kwa miaka mingine 10 ya mizaha na upuuzi/usanii!!
 
Upo sahihi, hii ni hoja nzito, sio hoja nyepesi; Pengine ana matarajio kwamba kigezo hiki kitatenguliwa ndani ya katiba mpya, lakini kama ulivyosema, hadi ifikie huko, as we stand, Zitto hawezi kuwa Rais wa Tanzania kwa vile Katiba haimruhusu kutokana na suala la ugombea; Lakini swali langu linalofuata kwako ni je, pingamizi ndani ya chama chake zinatokana na Chadema pia kuheshimu kigezo kilichopo ndani ya katiba ya nchi? Au kuna lingine Kikanuni na Kikatiba?

Vyama vyote vya siasa nchini katiba zao haziwezi kupingana na Katiba ya nchi kwa vile vinafanya siasa ndani ya nchi hii yenye katiba yake inayoongoza nchi. Hivyo kipengere cha kwamba Zitto anakiuka katiba ya Chadema au la ni kile kile ambacho katiba ya nchi inamkaba.

Kama katiba ya nchi ingekuwa inampa nafasi, basi tungekuwa na wasaa wa kuangali je katiba ya Chadema inasemaje, kwa sasa hoja ya katiba ya nchi inamfunga pingu, basi hatuna haja ya kuhangaikia Katiba ya Chadema kwa vile sheria mama ndio kigezo cha kwanza kwa raia wa nchi hii kufuatwa.
 
Kwa vile wewe ni mwana CCM (naamini sijakosea) ungetumia muda wako kidogo kujielimisha kwa nini CCM iliasisi mfumo huo wa timing na kuzuia watu kugombea endapo kuwa Rais anayetaka kumalizia muhula wa pili.

Pia kwa vile tuko katika siasa zinazotawaliwa na CCM kwa kiasi kikubwa, ungejaribu pia kujielimisha kwa nini CCM inaongoza kwa mbinu chafu ikiwemo fitna, rushwa na hata kuondoa uhai wa watu ili mradi ibaki madarakani.

Sasa, mtu yeyote makini, atajuaje kama si mbinu za CCM kujaribu kupunguza idadi ya watu wa kushughulikia kabla ya 2015?

Nadhani ni vigumu kujadili hoja yako bila kuielewa Tanzania yetu na TANU hadi CCM!!

Nimeheshimu maoni yako, lakini ninaweza kutofautiana nawe kwa hoja kwamba kama unaona kuna hitaji la kujadili kuhusu ajenda ya CCM kama ulivyodokeza, bora ungeanzisha mada hiyo kwa muda muafaka ili nayo tuijadili. Hapa tukijenga mtazamo wa nani kaleta mada kwa misingi ya itikadi za kichama tutafanya wengine wasikia kinyongo au kupata kinyaa cha kujadili mada zinazoletwa na watu wa itikadi tofauti.

Tuelewe kwamba kuna baadhi ya watu licha ya kutofautiana kitikadi za kisiasa kwa misingi ya vyama vya siasa, lakini wako very open kwa kuona kila upande nini bora kingefaa badala ya kuegemea upande mmoja tu kama alivyo mleta mada hii Bwana Mchambuzi. Binafsi ningekushauri tuijadili mada kama ilivyo ina manufaa kwa watanzania wote.

 
Sasa kama anazuiliwa na Katiba ya nchi, kwa nini tena tuongelee mambo ya chama ambayo hayawezi kuja juu ya Katiba ya nchi?

Na kwa vile katiba haijabadilishwa, kitu gani kinamnyima Zitto uvumilivu hadi atangaze nia katika kitu ambacho kisheria hakiwezi kuwepo?

Kwa nini asingekaa kimya ila akawekeza nguvu zake kwenye mabadiliko ya katiba ili baadaye ndiyo akunjue makucha?


Hilo ndilo jambo la msingi ambalo alitakiwa kulifanya, lakini wakati akijua katiba haimruhusu lakini amekaza mishipa usoni lazima agombee kana kwamba hana akili timamu wakati ni mbunge aliye kwenye baraza la kutunga sheria za nchi na ambao wanasimamia katiba isikiukwe. Hapa inaleta shaka kama ulivyosema nini anachokitaka Zitto kabwe.
 
Humu JF kuna wanachama zaidi ya wale wa chadema,kama unamaanisha mjadala huu ni wa wana chadema peke yake,then i'm sorry!

Naomba uwazuie wanachama wote wasiokuwa wa chadema kuchangia mjadala huu.

Una spin suala lililo mbele yetu visivyo jmushi1, mimi sijasema kwamba wanachama wengine hawana nafasi katika mjadala huu, ukinisoma vizuri utaelewa nina lenga nini hasa; vinginevyo ni mtazamo wangu tu, lakini kama kawaida, Chadema mkiona uzi wowote juu ya chama chenu, hata kama uzi huo unalenga maslahi ya taifa, mnakuwa very defensive;

Endelea tu na hoja zako mkuu hata za kumjadili Zitto Ki-CCM kama unavyo shauri, na kama wapo wa kuchangia mawazo yako, watachangia tu; Vinginevyo, again, ule ulikuwa ni mtazamo wangu tu;
 
Asante sana Mkubwa,
Kucopy na kupaste kila kitu kutoka Magharibi ndivyo vinavyotuchanganya, tatizo letu kubwa tunashindwa kutumia elimu za darasani na hali halisi, vitabu vimeandikwa na watu baada ya kuakisi hali halisi kutokana na mazingira, wakati matukio. Swala la kuanza kampeni miaka mitatu, minne au mitano Tanzania kiukweli ni fujo.

Chama kama chadema achilia mbali kukampeni leo kuingia ikulu kwa mtu mmoja kinahitajika kujengwa kwanza ni sawa na kung'ang'ania sahani wakati hata jiko haliko. Hii ni tamaa tu na kutaka kuwahi kitanda wakati hata fedha za kununulia kitanda hazipo.

Nafikiri tungekuwa na team work ya chama yenye malengo ya kwenda ikulu kutatua matatizo halisi ya Mtanzania na lazima mgombea huyu abebe ujumbe, sera, na matarajio ya wananchi lazima chama kiamue kama chama nani atafaa wakati ukifoka.

Leo tujikite kujenga chama, siasa za Tanzania ni siasa za chama hakuna atakayekwenda Ikulu na sera zake au mipango yake huo ni uongo labda awe mgombea binafsi, Chama legelege kitatuletea Raisi Legelege, kama CCM ingekuwa imara leo Raisi asingekuwa legelege. Kiongozi anayetokana na chama cha siasa lazima akubaliane na chama husika au kutofautiana kisera na kiutendaji na ajitoe kwenye chama husika.

Mfumo wetu wa demokrasia bado haujakuwa na hatuwezi kulazimisha kukomaa leo wakati mfumo uko kwenye stage ya mtoto wa miaka kumi. Tutafika mahala ambapo uraisi utakuwa ni wa taasisi ya mtu ila huko bado.

Hata mgombea binafsi kushinda kwenye mazingira ya Tanzania ni ngumu sana labda mtu auze nchi kwa mafisadi na wa ndani na nje ili wamchangie fedha nyingi ili aweze kuingia ikulu.

Tujenge dempkrasia ya kweli sio demokrasia madaraka.

Maoni yako yana uzito wa kushawishi, tatizo ambalo tunatakiwa kuangalia katika maoni yako ni mfumo wa nchi.

Marekani ulikotolea mfano sheria zao za uchaguzi zinaruhusu mchujo wa wagombea kuanza mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu kutokana na ukubwa wa nchi, wingi wa states ambazo zina sheria tofauti pengine nyingine zinazopingana na sheria mama kwa vile kila state inajiona kama huru katika kuendesha serikali yake na sheria zinazoridhiwa na bunge na senetor ya state.

Tanzania kuna sheria ya uchaguzi ambayo inakataza kufanya kampeni kabla ya muda unaotangazwa, na kama itatokea mmoja kufanya hivyo maana yake ataondolewa katika orodha ya wagombea kwa vile amekiuka sheria ya uchaguzi.

Binafsi siona sababu ya kuogopa muda uliopo kama chama cha siasa kimejitanua vya kutosha na kufungua matawi nchini. Katika uchaguzi mkuu uliopita Chadema hakikuwa chama chenye ukubwa na mvuto kama wa leo. Sitegemea Chadema ya leo ishindwe kusimamisha mgombea au ipate kigugumizi cha kusimamisha mgombea kwa vile vifaa wanavyo, wapiga kura wanao.

Kulinganisha mfumo wa uchaguzi wa Marekani na Tanzania ni sawa na kufananisha uwezo wa simba na paka. Hao wamarekani wamekamilika katika mengi, watu wako wa daraja ya juu, wanachambua mambo na kuwa na uelewa wa hali ya juu kiwango ambacho Tanzania tuko nyuma. Tanzania ukianza mambo kama ya Marekani ndio kuanza kuweka nyufa ndani ya chama kama tunavyoshuhudia. Marekani wanapima hoja na uwezo wa mtu lakini Tanzania bado tuko katika daraja ya kupima rangi ya chama kama upenzi wa timu ya mpira vile.

Uchaguzi Mkuu wa Marekani utakaofanyika Mwezi Ujao, tayari wapiga kura kila kaya wameshatumiwa makarabasha ya kuonyesha wagombea katika ngazi zote na maelekezo namna ya kupiga kura kwa walio raia wenye haki ya kupiga kura. Je uwezo huo tunao? Hapana, ni mapema mno, tunahitaji kuvuta subira huku tukiendelea kuboresha hatua kwa hatua hadi kufikia huko waliko wenzetu.

Kwa taarifa tu Uchaguzi Mkuu Marekani kura zinaanza katikati ya mwezi huu Oktoba wakati uchaguzi mkuu kilele chake ni Mwezi November. Tanzania tunaweza kutunza masanduku ya kura kwa usalama kwa majuma matatu wakati masaa pungufu ya 24 yanatushinda na kulalamikia kuibiwa kura?

Kwa sasa mfumo uliopo unafaa mpaka hapo wengi tutakapopanda ngazi ya juu zaidi katika ufahamu, upambanuzi, ustahimilivu, uwazi na uelewa.
 
Una spin suala lililo mbele yetu visivyo jmushi1, mimi sijasema kwamba wanachama wengine hawana nafasi katika mjadala huu, ukinisoma vizuri utaelewa nina lenga nini hasa; vinginevyo ni mtazamo wangu tu, lakini kama kawaida, Chadema mkiona uzi wowote juu ya chama chenu, hata kama uzi huo unalenga maslahi ya taifa, mnakuwa very defensive;

Endelea tu na hoja zako mkuu hata za kumjadili Zitto Ki-CCM kama unavyo shauri, na kama wapo wa kuchangia mawazo yako, watachangia tu; Vinginevyo, again, ule ulikuwa ni mtazamo wangu tu;
Siwezi kuendelea kuchangia kwasababu sitaki kuharibu thread yako.Umeshaweka misingi miwili ya criticism,kwamba kuna pande mbili zinazompinga na zinazomsapoti,na zote ziko ndani ya chama cha chadema.Sasa mimi si mtu wa aina hiyo,nilitaka upanue mjadala kwa kuwashirikisha na wale wenye kumsapoti ambao si wa chadema,kama ume assume kuwa nina kadi ya chadema(licha ya kwamba i wish that i had it),basi mjadala mwema.
Mchambuzi said:
Kambi ya Kwanza ni ile inayo muunga Mkono Zitto kwa uamuzi huu, wakiwepo viongozi kadhaa ndani ya Chadema; Kambi ya Pili ni ile inayo mpinga Zitto kwa uamuzi huu, akiwemo Mwasisi wa Chadema, Mzee Edwin Mtei;
Hapa una entertain kambi mbili za tofauti kati ya viongozi wa chadema na mwasisi wao mzee Mtei.Goodluck!
 
Unayoongea mkuu ningeyakubali kama mpiga kura wa Tanzania angekuwa na madhara makubwa katika kuamua nani awe Rais wa nchi.

Kwa vile mfumo mzima wa uchanguzi wetu umekaa kimagumashi, basi kwa sasa tujipange kwa mambo ambayo yanachangia zaidi. Kwa mtazamo wangu, CHADEMA tayari wanafanya kazi muhimu ya kupeleka chama kwa wananchi ili hata wakitangaza mgombea, kila mtu kutoka pembe ya nchi hii awe anakijua chama tofauti na huko nyuma.

System za Ulaya Magharibi na Marekani haziakisi ukweli halisi katika mazingira yetu!

Mimi naungana na EMT katika hoja yake ya kutanganza mtu mapema, vinginevyo kinafichwa nini? Hata wakati wa Mkapa uchaguzi 1995, kwa hoja ya EMT, ilimchukua Nyerere kazi kubwa sana kwenda kumuuza mgombea yule, na pamoja na hayo, akaambulia 60% tu ya kura; Ndio maana hata katika uchaguzi wa 2015, CCM haitaweka mtu mpya, ni hawa hawa tunaowasikia, watachukua mmoja wao, kwani haina muda wa kuanza kuuza mtu mpya;

Na mfano wa EMT kuhusu Obama na maandalizi ya muda mrefu, mfano huu ukusaidie kuelewa zaidi pia kwamba hata ndani ya vyama wagombea wana mitazamo tofauti - Obama, Clinton, Biden, etc, wote hawa walikuwa na mtazamo tofauti ndani ya itikadi moja; Sasa kusema Chadema kwa sasa waende kujiuza kwa wananchi, ni sawa, lakini kwa msimamo gani? Ina maana unataka wale wote watakaotia nia kugombea kupitia Chadema wawe na msimamo mmoja wakati wa kuchujwa na chama chao? Hii itakuwa na maana gani katika demokrasia?
 
Dark City and Mkwawa nilichokuwa najaribu kueleza ni wananchi wenyewe kujihusisha moja kwa moja kwenye selection ya wagombea. Kwenye siasa kuna phases mbili za ku-recruit wanasiasa. Phase ya kwanza ni selection na ya pili ni election ya hao wanasiasa. Kwa hali iliyo sasa wananchi wanahusishwa tuu kwenye process ya ku-elect candidates lakini sio kwenye process ya ku-select candidates. Kwa hiyo, mna-ague kuwa hakuna haja ya wananchi kuhusishwa kwenye phase ya ku-select candidates kwa sababu mazingira hayaruhusu?

Nadhani the way candidates are selected ina-affect siasa za vyama, demokrasia kwa ujumla na legitimacy ya hao wagombea. Selection of candidates inasaidia sana kuchanganua quality za viongozi wanaokuwa elected and how these candidates behave in office. Otherwise, tutaendelea kuletewa watu bomu, tutaambiwa kuwa ndiyo wanafaa, tunawa-elect baada ya mwaka tuu tunaanza kujutia huku tukisema hakuna haja ya kuwa involved kwenye selection process kwa kuwa mazingira bado hayaruhusu.

Siamini kupractice secret garden of politics kwa kigezo kuwa kutofanya hivyo tutakuwa tuna-copy and kupaste kwenye mazingira ambayo hayaruhusu. Openness and inclusive ni muhimu sana kwenye jamii yoyote regardless of the environment. In deed, process tunayotumia sasa ni kwa ajili ya kuwapata wagombea ubunge lakini siyo presidential wannabes.
 
Siwezi kuendelea kuchangia kwasababu sitaki kuharibu thread yako.Umeshaweka misingi miwili ya criticism,kwamba kuna pande mbili zinazompinga na zinazomsapoti,na zote ziko ndanio ya chama.Sasa mimi si mtu wa aina hiyo,nilitaka upoanue mjadaka kwa kuwashirikisha na wale wenye kumsapoti ambao si wa chadema.Mjadala mwema.

Hata ulichokijadili hapo juu kwenye nukuu haikuwa nilicho maanisha; ukinisoma vizuri utanielewa; Kimsingi, hoja yako kwamba niweke kundi lingine linalo husiana na Zitto kuwa pandikizi la CCM, binafsi sikuona kama mjadala huo una nafasi humu, kwani mjadala wa namna hiyo umeegemea zaidi kwenye FITINA za siasa, suala ambalo lina nyuzi zake nyingi tu humu tayari kwa mtu huyu huyu - Zitto; Mimi nadhani haukunielewa, hivyo ukanitafsiri vibaya; Vinginevyo huwa nina thamini sana michango yako na pia nyuzi zako, lakini kama nimekukwaza kwa hili, naomba uniwie radhi, ila nina amini kwamba tutakutana tu kwenye mijadala mingine kama kawaida yetu, hasa iwapo uamuzi wako wa kusimamisha michango yako katika uzi huu, utasimama Per bandiko namba 34 la uzi huu;
 
Siwezi kuendelea kuchangia kwasababu sitaki kuharibu thread yako.Umeshaweka misingi miwili ya criticism,kwamba kuna pande mbili zinazompinga na zinazomsapoti,na zote ziko ndani ya chama cha chadema.Sasa mimi si mtu wa aina hiyo,nilitaka upanue mjadala kwa kuwashirikisha na wale wenye kumsapoti ambao si wa chadema,kama ume assume kuwa nina kadi ya chadema(licha ya kwamba i wish that u had it),basi mjadala mwema.

Bwana jmushi1 mambo hayaendi hivyo, tujitahidi kujenga uvumilivu kwani hata mimi nilishtuka aliposema kuna migawanyiko ya makundi mawili, lakini mimi sikuona kama hilo ni tatizo la kujadili mada kwani huu ni mtazamo wake. Labda ungemwuliza afafanue ndicho kinachotakiwa katika mdahalo, kwani lugha nazo huwa zinatatiza pengine huhitaji kufafanuliwa au mkalimani atolee ufafanuzi. Lakini kwamba kuna wanaokubali na wasiokubali juu ya hilo ni jambo linaweza tafsirika kwamba kuna makundi mawili yanayomkataa na kumkubali.

Kundi linalomkubali halina hoja za msingi ila tu kama mwenyewe alivyosema anataka nchi hii wagombea wale wa kizazi cha baada ya uhuru, maana yake Zitto Kabwe ameshaweka ubaguzi katika kuongoza nchi kwamba waliozaliwa kabla ya uhuru wasipate nafasi. Je, kama wanafaa basi tuwaengue kwa hoja kwamba walizaliwa kabla ya uhuru?
 
Hayo ndiyo tunayoyasema,

Yaani watu wameshaona makosa ya CCM na jinsi yanavyotugharimu kama taifa halafu wanataka turudie hayo hayo...Hili tunatakiwa kulipinga kwa nguvu zote. Upuuzi wa kutumia mitandao na familia kuingia ikulu bila ajenda ya chama ndiyo umetusababishia matatizo haya tutayokabiliana nayo sasa na madhara yake yatatuchukua miaka mingi sana kuyasafisha. Na tukirogwa tukampa Lowasa urais, tutakuwa tunaendelea kuongeza gharama ya upuuzi wetu.

Kwa watu wenye akili, waunde chama imara chenye timu imara na itakayoweza kupambana na uchafu kwanza ndani ya chama chenyewe, kwenye serikali na jamii nzima kwa ujumla.

Kinyuma cha hayo tujiandae kwa miaka mingine 10 ya mizaha na upuuzi/usanii!!

Hapo kwenye red ndipo ilipo argument yangu kuwa wananchi wahusishwe both kwenye selection and election phases. Hii at least itapunguza hili tatizo and in the long run labda kulitokomeza kabisa. Lakini ume-argue kuwa mazingira bado hayaruhusu. Tuendelee tuu kuwazuia wananchi kutojihusisha kwenye selection process mpaka mazingira yatakaporuhusu?
 
Bwana jmushi1 mambo hayaendi hivyo, tujitahidi kujenga uvumilivu kwani hata mimi nilishtuka aliposema kuna migawanyiko ya makundi mawili, lakini mimi sikuona kama hilo ni tatizo la kujadili mada kwani huu ni mtazamo wake. Labda ungemwuliza afafanue ndicho kinachotakiwa katika mdahalo, kwani lugha nazo huwa zinatatiza pengine huhitaji kufafanuliwa au mkalimani atolee ufafanuzi. Lakini kwamba kuna wanaokubali na wasiokubali juu ya hilo ni jambo linaweza tafsirika kwamba kuna makundi mawili yanayomkataa na kumkubali.

Kundi linalomkubali halina hoja za msingi ila tu kama mwenyewe alivyosema anataka nchi hii wagombea wale wa kizazi cha baada ya uhuru, maana yake Zitto Kabwe ameshaweka ubaguzi katika kuongoza nchi kwamba waliozaliwa kabla ya uhuru wasipate nafasi. Je, kama wanafaa basi tuwaengue kwa hoja kwamba walizaliwa kabla ya uhuru?
Wewe ndiyo sijakuelewa kabisa,ni vyema urudi kwenye ile thread uliyoianzisha nikakuuliza swali na hadi sasa hujalijibu!Unaweza ukawa unajaribu kumsadia kujibu swali nililolielekeza kwake bila ya kutambua nilichomuuliza.

Samahani sani,ila nadhani umedandia treni kwa mbele.
 
Back
Top Bottom