Ciril
JF-Expert Member
- Jan 10, 2011
- 8,558
- 7,156
Mwenyekiti wa NCCR James Mbatia amesema ameteuliwa kuwa mbunge na Rais kwa sababu chama chake hakiamini katika vurugu na kumwaga damu kama baadhi ya vyama vinavyofanya.
Mbatia amesema hiyo ndiyo sababu pekee iliyosababisha Rais kukipa heshima chama chake na wala sio kulipwa fadhila kama baadhi ya watu wanavyosema
Source: Mwananchi Jumamosi
Chama chake hakiamini katika vurugu kama vyama vingine?Kwa sheria za jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaruhusu/ama kusajili vyama vyenye vurugu?Huyu Mbatia analo lake jambo hawezi kutoa sababu ya kijinga namna hii kuwa ndio imemmfanya raisi kumchagua yeye na chama chake.