Hiki kinachotokea kwa viongozi wakuu wa CWT (M/Kiti na Katibu wake) ni UONEVU wa waziwazi

Burkinabe

JF-Expert Member
Feb 12, 2023
1,900
3,206
Siwafahamu kiundani,.lakini nina uhakika vyombo vya dola vinawafahamu vizuri zaidi na ndio maana vikapeleka majina yao kwa Mh. Rais kwa nafasi za Ukuu wa Wilaya.

Sasa kinachoonekana kwa sasa ni kwamba, hawa viongozi wa walimu, wanaandamwa kwa sababu ya kugomea uteuzi wa Mh. Rais!

Kama kweli walikuwa na kashifa za ufisadi, mbona hawakushughulikiwa hapo kabla?

Ina maana kukataa uteuzi wa Mh. Rais ni kosa?!

Nimejisikia kuongelea hilo kwa maana kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na changamoto sana kwa wale wanaoonekana kutokubaliana na Mh. Rais, kuibuliwa kwa vikwazo vingi.

Hili la viongozi wa CWT, nalifananisha na kile kilichotokea kwa kiongozi wa chama cha NCCR-Mageuzi, Mh. James Mbatia, ambaye baada ya kugoma kuitikia wito wa Mh. Rais wa kwenda Ikulu kufanya maridhiano, vikwazo vikaanza kuibuka kwa viongozi wenzake waandamizi!

Kama Mtanzania, nimeona niliongelee hili, maana kinachotokea kwa viongozi wa walimu, binafsi naona ni kwa sababu ya "kukataa" uteuzi na wala si vinginevyo.

Asalaam Aleykum.
 
Hawakuwa na busara unakataaje kazi unayotumwa na Mkuu wa nchi.Inabidi wajitathmini ikiwezekana wawapishe viongozi wengine waongoze hiyo Taasisi yao maana wao imewashinda.
 
Hao Cwt lazima waandamane kwa sababu wameonesha dharau kubwa kwa mh Rais .Mama alipanga kusolve mgogoro wao unaotokana na kugombea fedha za walimu Kiutu uzima lakini wao wakakomaza mafuvu kugomea teuzi za Udc hiyo ni dharau kubwa kwa mama.Kwa ushauri Serikali isiishie hapo tu kwa kuliacha hili suala la kudharau mamlaka ya uteuzi lipite ila waende mbele zaidi kwa kukifuta hicho kikundi cha wasaka ngawila kwa migongo ya vyama vya wafanyakazi
 
Kwakweli kugomea uteuzi wa Rais haipendezi kabisa na Kama kuwatumikia waalimu si hata huko walipoteuliwa Kuna walimu kwanini wasingeenda kuwatumikia?
 
Mama Samia alionesha ule umama haswa kwa kuwateua DC ili kuondoa mvutano uliokuwepo.
Kugomea maana yake walimpa ujumbe kwamba awaache waendelee kuharibu CWT, kwa maoni yangu hili limechelewa
 
Kama hawana hatia kwanini waandamwe?
Unakula Tsh 15-58 elfu ya mwalimu,
Kila mwezi halafu unampa tisheti ya buku 5 na kofia kwa mwaka,
Usipoandamwa na serikali hata ndoto mbaya na majinamizi yatakuandama tuuu...
Shenz kabisa viongozi Wa CWT
Pole mwl
 
Jamani acheni tu kwenye vyama vya wafanyakazi hawa viongozi wakubwa ni kama miungu watu.... pesa wanayopata huko ni kufuru tupu... walikuwa sahihi kugomea uteuzi ili kufanikisha malengo yaovya ngawila...
 
Siwafahamu kiundani,.lakini nina uhakika vyombo vya dola vinawafahamu vizuri zaidi na ndio maana vikapeleka majina yao kwa Mh. Rais kwa nafasi za Ukuu wa Wilaya.

Sasa kinachoonekana kwa sasa ni kwamba, hawa viongozi wa walimu, wanaandamwa kwa sababu ya kugomea uteuzi wa Mh. Rais!

Kama kweli walikuwa na kashifa za ufisadi, mbona hawakushughulikiwa hapo kabla?

Ina maana kukataa uteuzi wa Mh. Rais ni kosa?!

Nimejisikia kuongelea hilo kwa maana kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na changamoto sana kwa wale wanaoonekana kutokubaliana na Mh. Rais, kuibuliwa kwa vikwazo vingi.

Hili la viongozi wa CWT, nalifananisha na kile kilichotokea kwa kiongozi wa chama cha NCCR-Mageuzi, Mh. James Mbatia, ambaye baada ya kugoma kuitikia wito wa Mh. Rais wa kwenda Ikulu kufanya maridhiano, vikwazo vikaanza kuibuka kwa viongozi wenzake waandamizi!

Kama Mtanzania, nimeona niliongelee hili, maana kinachotokea kwa viongozi wa walimu, binafsi naona ni kwa sababu ya "kukataa" uteuzi na wala si vinginevyo.

Asalaam Aleykum.
Wangekuwa mafisadi, wasingeteuliwa. Nadhani wameonyesha kujiamini na kutoshobokea rushwa ya vyeo na mizengwe ya kuwaondoa CWT ili wawekwe chawa wa Samira
 
Jamani acheni tu kwenye vyama vya wafanyakazi hawa viongozi wakubwa ni kama miungu watu.... pesa wanayopata huko ni kufuru tupu... walikuwa sahihi kugomea uteuzi ili kufanikisha malengo yaovya ngawila...
Sina uhakika, lakini nafikiri hawa ndugu wanaonewa. Ni figisu figisu wanafanyiwa kwa sababu ya kuonekana kama "wamemdharirisha" Mh. Rais kwa kugomea uteuzi wake. Sasa sijui kwa nini wasiambiwe tu ukweli kuliko kuzunguka zunguka na sababu zisizo na kichwa wala miguu?!

Binafsi ni mwathirika wa uonevu, hivyo huwa najisikia vibaya sana nikiona binadamu mwenzangu anaonewa pasipo sababu ya msingi.

HAKI NI MSINGI WA AMANI NA UTULIVU.
 
Ningefurahi sana siku moja serikali ingemtuma CAG akakague mapato na matumizi ya hao Cwt kama serikali ilivyofanya mwaka 2018
 
Back
Top Bottom