WanaJF
Gazeti la RAI linalomilikiwa na kampuni ya Habari Cooperation limeubuka na kile kinachodai ni kura ya maoni ya nani atachaguliwa kuwa mbunge wa Arumeru Mashariki
Katika kile wanachodai ni utafiti wao katika kata 17 ni kwamba mgombea wa CCM Siyoi Sumari anatarajiwa kupata ushindi mkubwa wa asilimia 61% huku mgombea wa CDM Joshua Nassari akitarajiwa kuambulia asilimia 38.5%. RAI wanadai Siyoi Sumari anaungwa mkono na makundi yote ya wananchi jimboni humo na pia ndiye anaonekana kuwa kivutio kikubwa kwa wananchi
My take:Nadhani ufike wakati vyombo vya habari viache propaganda chafu kwa ajili ya kukatisha wananchi tamaa.Bado hatujasahau gazeti hilihili lilitoa tathmini kama hii wakati wa uchaguzi mdogo jimbo la Igunga ambapo walidai katika utafiti wao mgombea wa CCM angepata ushindi wa asilimia 70%.Lakini nadhani wote tunayajua matokeo ya Igunga yalivyokuwa.Pia tafiti za kipropaganda kama hizi zimekuwa zikitumiwa na maafisa wa tume ya uchaguzi wasio waaminifu kuchakachua matokeo.
Gazeti la RAI linalomilikiwa na kampuni ya Habari Cooperation limeubuka na kile kinachodai ni kura ya maoni ya nani atachaguliwa kuwa mbunge wa Arumeru Mashariki
Katika kile wanachodai ni utafiti wao katika kata 17 ni kwamba mgombea wa CCM Siyoi Sumari anatarajiwa kupata ushindi mkubwa wa asilimia 61% huku mgombea wa CDM Joshua Nassari akitarajiwa kuambulia asilimia 38.5%. RAI wanadai Siyoi Sumari anaungwa mkono na makundi yote ya wananchi jimboni humo na pia ndiye anaonekana kuwa kivutio kikubwa kwa wananchi
My take:Nadhani ufike wakati vyombo vya habari viache propaganda chafu kwa ajili ya kukatisha wananchi tamaa.Bado hatujasahau gazeti hilihili lilitoa tathmini kama hii wakati wa uchaguzi mdogo jimbo la Igunga ambapo walidai katika utafiti wao mgombea wa CCM angepata ushindi wa asilimia 70%.Lakini nadhani wote tunayajua matokeo ya Igunga yalivyokuwa.Pia tafiti za kipropaganda kama hizi zimekuwa zikitumiwa na maafisa wa tume ya uchaguzi wasio waaminifu kuchakachua matokeo.