Utabiri: Mkapa alimwandaa JK, Je JK anamwandaa nani kuwa commander in chief?

Hivi kama Membe vile ndiyo last card yake....Naona kama vile maandalizi yote kwa sasa yapo kwa mtindo huo....Ni mawazo tu bw not real what do you think?

Lakini mm mpaka mafuta nawaambia piga ua garagaza Rais hatoki nje ya north iwe CCM ama CDM!
 
Mkapa alikuwa mwelevu sana wala asingemuandalia mazingira ya kuingia Ikulu huyu bwana ambaye ni BAD NEWS kwa mtz wa kawaida. Well, Kikwete anakiandalia chama cha upinzani kuchukua mamlaka ya kuunda serikali!
 
kumbe kichwa cha mada kakileta kiujanjajanja na hana suala aliloleta?kalete suala ndugu hapo umeleta majina ya watu na sisi wengine kumjadili mtu huwa taabu hasa akiwa hajajileta peke yake.
 
2015 Pakiwa na free and fair election kwa mara ya kwanza RAIS Tz atatoka chama cha upinzani! nimutazamo tu.
sasa nani aliyekwambia 2015 ccm itafanya free and fair elections. africa nchi zenye free and fair elections ni ghana, botswana na zambia.
 
Sikuwahi kujua kuwa nawe huwa una mawazo ya kihafidhina. Pole WildCard. Kuundoa utawala mbovu kama wa CCM hauhitaji katiba mpya. Hata kwa katiba iliyopo CCM wanaweza kuondoka. Hivyo vyombo vya dola unavyovizungumzia ni vipi? Watawala waliondolewa sehemu zingine haikuhitaji katiba mpya. Inahitajika mikakati endelevu, sera imara na mbadala, kukubalika kwa watu, basi. The rest will have to follow...si suala la kumsubiri Said Mwema au wenzake...
Waitara,
Kwa namna vyombo vya DOLA vilivyo hakuna namna upinzani utatangazwa kuwa umeshinda hata kama utakuwa umeshinda kweli. Chukua mfano mdogo tu wa uchaguzi wa Urais wa Zanzibar. Kule CCM haijashinda tangu mwaka 1995 na haitashinda hata kwa chaguzi nyingine tano zijazo. Tunataka KATIBA MPYA itusaidie kunyoosha baadhi ya mambo yafuatayo:-
-Ituwekee taasisi zenye nguvu na huru kabisa katika UTENDAJI na MAAMUZI yake kama vile TUME YA UCHAGUZI;
-Iweke wazi mgawanyo wa madaraka wa MIHIMILI mitatu ya DOLA;
-Iweke mifumo mizuri ya kuwapata wagombea kuanzia ndani ya vyama;
Kimsingi chaguzi tulizofanya tangu mwaka 1995 ni maigizo tu. Uhalisia wa kuchaguana haupo. Kwa kuwa wewe umeamua kujiajiri kwenye SIASA unajua taabu mnayoipata hata kuupata UDIWANI tu kwa mfumo katili wa sasa.
 
Waitara,
Kwa namna vyombo vya DOLA vilivyo hakuna namna upinzani utatangazwa kuwa umeshinda hata kama utakuwa umeshinda kweli. Chukua mfano mdogo tu wa uchaguzi wa Urais wa Zanzibar. Kule CCM haijashinda tangu mwaka 1995 na haitashinda hata kwa chaguzi nyingine tano zijazo. Tunataka KATIBA MPYA itusaidie kunyoosha baadhi ya mambo yafuatayo:-
-Ituwekee taasisi zenye nguvu na huru kabisa katika UTENDAJI na MAAMUZI yake kama vile TUME YA UCHAGUZI;
-Iweke wazi mgawanyo wa madaraka wa MIHIMILI mitatu ya DOLA;
-Iweke mifumo mizuri ya kuwapata wagombea kuanzia ndani ya vyama;
Kimsingi chaguzi tulizofanya tangu mwaka 1995 ni maigizo tu. Uhalisia wa kuchaguana haupo. Kwa kuwa wewe umeamua kujiajiri kwenye SIASA unajua taabu mnayoipata hata kuupata UDIWANI tu kwa mfumo katili wa sasa.
kaka nipo na wewe bega kwa bega lakini je hiyo katiba itapatikana?na isipopatikana unahisi nini kitatokea,kwa sababu watanzania ni waoga lakini sio kama zamani huoni dalili za nchi kuvurugika ziko wazi sana.nasema hivi kwa sababu hakuna nchi ambayo wananchi wake walizaliwa wanapenda fujo ila udhalimu ndio ulisababisha.usishangae siku moja tz ikalipuka niamini aka dalili zinaonekana wazi.sio kwa upinzani tu kuichafua nchi hata chama tawala peke yake mwenendo wake ni wa kuichafua nchi hatupo salama sisi kama taifa.historia ni mama wa yote.siku njema.
 
Kikwete hakuandaliwa na Mkapa, wacha kupotosha watu. Kama ulikuwa bado u mdogo na hujui yaliyojiri ni bora uulize kuliko kujaza watu ujinga.
 
kaka nipo na wewe bega kwa bega lakini je hiyo katiba itapatikana?na isipopatikana unahisi nini kitatokea,kwa sababu watanzania ni waoga lakini sio kama zamani huoni dalili za nchi kuvurugika ziko wazi sana.nasema hivi kwa sababu hakuna nchi ambayo wananchi wake walizaliwa wanapenda fujo ila udhalimu ndio ulisababisha.usishangae siku moja tz ikalipuka niamini aka dalili zinaonekana wazi.sio kwa upinzani tu kuichafua nchi hata chama tawala peke yake mwenendo wake ni wa kuichafua nchi hatupo salama sisi kama taifa.historia ni mama wa yote.siku njema.
Busara iliyotumika kuamua tuingie kwenye mfumo wa vyama vingi itatumika pia kutupatia KATIBA MPYA kama ile ya jirani zetu KENYA. Hili hata Kikwete mwenyewe litamjengea heshima ya aina yake baada ya kuvurunda sana kwenye URAIS wenyewe.
 
hatuwezi kuacha kumchagua mtu kwa sababu eti ndugu yake ni kiongozi wa ngazi ya juu ili mradi tu anasifa za kuchaguliwa. Kuwa mke wa rais ama mtoto wa rais siyo kikwazo, lakini isizidi kama ambavyo cdm wamezoea.

ila kwa cdm ni kosa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom