Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Wanajamii;
Kwa wafuatiliaji wa habari bila ya shaka watakua wamegundua kuwa Makamu Wa Rais Mh. Dk Bilali kwa kipindi kirefu sasa amekuwa katika ziara za kikazi mikoani na wilayani na kupewa kipau mbele katika media za Tanzania. Ziara hizi kwa mtazamo wa haraka japokuwa ni za kikazi lakini zimekuwa ni nyingi sana zaidi ya kiongozi mwingine yoyote wa Kisiasa.
Ikumbukwe kuwa Dr. Bilali ni Makamu wa Rais na anafanya zile kazi ambazo Rais amemwagiza au yuko aware nazo.
Yawezekana kabisa kuwa Rais Kikwete ameamua kuchukua uamuzi huo wa kumuandaa na kumtangaza Bilali awe mgombea Urais wa CCM 2015 ili kukinusuru chama chake CCM kutokana na makundi ambayo itake isitake 2015 yatakimega CCM kabisa kwa asilia 100%. Huenda akawa na sababu nyingi lakini chache ni zifuatazo:
Ni nini maoni yako binafsi kuhusu Dk. Bilali na harakati zake za kuzunguka mikoani na wilayani in connection na mbio za Urais 2015? Je yawezekana akawa ni Chaguo la JK?
Nawasilisha.
Kwa wafuatiliaji wa habari bila ya shaka watakua wamegundua kuwa Makamu Wa Rais Mh. Dk Bilali kwa kipindi kirefu sasa amekuwa katika ziara za kikazi mikoani na wilayani na kupewa kipau mbele katika media za Tanzania. Ziara hizi kwa mtazamo wa haraka japokuwa ni za kikazi lakini zimekuwa ni nyingi sana zaidi ya kiongozi mwingine yoyote wa Kisiasa.
Ikumbukwe kuwa Dr. Bilali ni Makamu wa Rais na anafanya zile kazi ambazo Rais amemwagiza au yuko aware nazo.
Yawezekana kabisa kuwa Rais Kikwete ameamua kuchukua uamuzi huo wa kumuandaa na kumtangaza Bilali awe mgombea Urais wa CCM 2015 ili kukinusuru chama chake CCM kutokana na makundi ambayo itake isitake 2015 yatakimega CCM kabisa kwa asilia 100%. Huenda akawa na sababu nyingi lakini chache ni zifuatazo:
- Safari hii ni zamu ya Wazanzibar kutoa Rais. Kumbuka hii ni hoja rahisi kama walivyoamua kuwa safari hii Spika ni Mwanamke na hivyo kumweka Sita pembeni. K
- Dk. Bilali hana Makundi na amekuwepo katika siasa za Bara na Visiwani na anakubalika (Of course ziara za sasa zimam-promote)
- Dk. Bilali amekuwa Makamu wa Rais na anakubalika kama Presidential Material
- Ili kuzima chokochoko za Wazanzibari kuua Muungano dawa ni kumweka Mzanzibar. JK hawezi kuruhusu Zanzibar iwe Nchi au Dola (Historically na Kikatiba).
- JK hataki aonekane kaivuruga Nchi ndo maana kwa mambo yote makubwa nchi hii kaamua bora tu akae kimya kuliko kusema. La kuhusu katiba ameona bora atofautiane na Chama chake ili kuacha Lergacy na kuleta utengamao katika Nchi.
Ni nini maoni yako binafsi kuhusu Dk. Bilali na harakati zake za kuzunguka mikoani na wilayani in connection na mbio za Urais 2015? Je yawezekana akawa ni Chaguo la JK?
Nawasilisha.