Abraham Lincon
Member
- Oct 22, 2010
- 78
- 0
Linapokuja suala la kujihusisha na mapenzi katika umri mdogo (ama hata mambo mengine yenye matokeo hasi kwa watoto) wazazi wengi huwa hawawi wazi kwa watoto wao kiasi cha kutosha kuwaonesha wazi wazi madhara ya kujihusisha na ngono katika umri mdogo. Wanasema tu, 'usifanye hivi, usifanye vile' nk. Watoto wengi, kwa udadisi wa kutaka kujua ubaya ama uzuri wa kufanya ama kutofanya walichokatazwa kufanya na wazazi wao wameishia kuharikiwa na kupoteza ndoto za muda mrefu za maisha yao lakini yote ni sababu wazazi hawakuwa wazi kiasi cha kutosha kuwapa msimamo thabiti katika kujenga maisha yao. Mara nyingi watoto hufanya kile walichokatazwa kufanya iwapo sababu za kufanya ama kuto fanya hazikuwekwa wazi. Tujitahidi sana kutoa sababu za msingi tunapokataza watoto kufanya kitu fulani chenye matokeo hasi ili kuwaepusha na matatizo yanayoweza kuwapata pindi wanapoamua kujitafutia sababu za kwa nini wafanye ama wasifanye walichoambiwa wasifanye. Tena tufanye hivyo at the right time! Waharifu wa kwanza wa mtoto ni wazazi! Unadhani kuna sababu ya msingi kuwaficha watoto ukweli wa mambo kwa dunia ya leo? Kumbuka, asiyefunzwa na mamaye, ulimwengu utamfunza!