Urais wa Zitto 2015 ni kwa tiketi ya CHADEMA - Habib Mchange

Labda urais wa TFF. CDM ni wakati muafaka wa kung'oa magugu maji ambayo ni Mzito kabwela! rose nusu! shibuda! na huyo habib mchanga.
 
Wanaodhani wengine tunaipenda tu Chadema (kama makada wa CCM walivyo) wanakosea sana,akina Habib Mchange ni mmojawapo wa watu wanaodhani Chadema imefika hapo pa kupendwa tu.

Sina muda wa kujadili hoja zake dhaifu lakini namtahadharisha kuwa Watanzania tunataka mabadiliko kwa namna yeyote,Watanzania watampa nafasi yule waliyenae mtaani kila siku akiwatetea kwa moyo mmoja bila hila,Watanzania wanataka mtu safi na kiongozi aliyekomaa kwelikweli na amedhihirisha hivyo kwa vitendo na si kwa simulizi zake kutuambia aliyofanya kama vile sisi ni vipofu!

Hawa akina Mchange wasameheni tu ni vijana wadogo wanaodhani wameshakomaa kisiasa na sifa zinawaharibu sana.Someni makala hiyo muone kama kuna kijana aliyeiva hapo!!!

mkuu umenena vema sana! Wananchi wanahitaji rais mkomavu na mwenye kuleta mabadiliko ktk uchumi wa nchi
 
Wewe wawapi usiyejua kwamba mgombea urais atapatikana baada ya mchakato ndani ya chama,cdm ni chama kikubwa kuliko unavyoweza kufikiri na kwamba hakiwezi kuongozwa na kauli nyepesi zinazotoka kwenye akili ndogo kama yako.upatu unaoufanya haukijengi chama,kina heche wanazunguka kukijenga chama wewe umekaa kibaha ukiendelea kupiga ramli.Akili ndogo haiwezi kuiongoza akili kubwa kamwe ndani ya cdm.


John Heche anawapagawisha kwa jinsi anavyokubalika vijijini.Yule ni habari ingine,hawa wapika majungu wamebaki tu kutukana kupitia Facebook
 
Kuna kitu kinapikwa toka magambaz na hawa "pimbi" wanatekeleza! utapogundua wana njama ya kuua Chama Wajiandae kukabili hasira zetu kwa vitendo!
 
Nitoe ushauri wangu kwa watu wa chadema. Huwezi kufikia malengo unayoyataka ktk chama kwa kukiponda chama chako. Kupuuza m4c ni kupuuza chama chako. M4C ni moja ya program ya cdm iliyoleta mafanikio makubwa sana. Ni m4c ndio inawanyima ccm usingizi hadi wanatumia jeshi la polisi kuizima. Swali: kama wewe ni mwanachadema, kwa nini uipuuze na kuibeza m4c? Je tukisema unatumiwa na ccm, tutakuwa tumekosea? Kama kweli ni mwanachadema, mchange angeitumia m4c kujiimarisha kisiasa. M4C haitaishia kuiondoa ccm tu, bali na wanachadema wanaoibeza na kuipuuza. Note my words
 
John Heche anawapagawisha kwa jinsi anavyokubalika vijijini.Yule ni habari ingine,hawa wapika majungu wamebaki tu kutukana kupitia Facebook

Watu wengine bana nani anayemjua Heche zaidi ya nyie wafuasi wa Dr Slaa na Mbowe.
 
Nitajaribu kujibu baadhi ya hoja za Habibu Machange.

*Zitto Kabwe anakosa sifa ya msingi ya kuwa mgombea Urais 2015, umri wake utakuwa chini ya miaka 40

*Chadema ni chama, hivyo mafanikio ya Chadema kisiasa ni zaidi ya mchango wa mtu mmoja.

*Pamoja na mchango wa Zitto Kabwe katika kuijenga chadema kisiasa lakini pia anamchango mkubwa katika kuibomoa na kuipasua(mfano Chaguzi za ndani eg.Bavicha na uchaguzi mkuu 2010 eg.Kigoma)

*Zitto ni mtu hatari sana kwa Chadema kwa sasa, kwa sababu ya tabia yake ya kutoa siri za ndani za chama na kuzipeleka kwa watawala na CCM.

*Zitto hana mchango wowote mkubwa kwa sasa kwa Chadema katika ujenzi wake(eg. uduni wake katika ushiriki wa M4C)

*Zitto ni mtu asiyeaminika kabisa kwa wanaCHADEMA na kwa watanzania kutokana na kuwa na sura mbilimbili za kisiasa.
 
Kamanda Mchange, Kamanda, Matata, Kamada Zitto, Kamanda Chagulani, Kamanda Shibuda, Makamanda Madiwani wa Arusha, fungukeni watanzania wapo nyuma yenu.
 
John Heche anawapagawisha kwa jinsi anavyokubalika vijijini.Yule ni habari ingine,hawa wapika majungu wamebaki tu kutukana kupitia Facebook

John ni mtu wa kazi. Kweli jamaa halali. Vijana mmepata mtu sahihi kwa kazi sahihi. Nina uhakika wanaopiga kelele dhidi ya John wasingeweza kufanya kazi kama anayoifanya.
 
mchange 2lia ndugu yangu, tulia ukue, ujifunze siasa kwanza. Acha kujitutumua, ni mapema mno!, utachuja kabla ya kua maarufu!
 
Wewe ni mnafiki KAMA ZITTO mwenyewe! Alishindwaje kuwapigia kampeni wabunge wa jimboni kwake, akawapigie wa mwanza na mbeya? Huoni haya wala aibu? Kampeni yako imeshindwa 100% unasababisha ZITTO achukiwe kama kinyesi kipya cha mharo, shauri yako.
 
Kamanda Mchange, Kamanda, Matata, Kamada Zitto, Kamanda Chagulani, Kamanda Shibuda, Makamanda Madiwani wa Arusha, fungukeni watanzania wapo nyuma yenu.

Sema ccm iko nyuma yenu, si watanzania.
 
I guess what, baada ya kuona vijana wengi wameonesha umahiri ndani ya CDM(eg;-Wenje,Msigwa,Lema,Mnyika,Lusinde) huyu dogo ZZK anajiona kuShare umaarufu alioupata hapo kabla ambao angependa ubaki kuwa faida yake pekeyake.So,anajaribu kujionesha kwamba IQ yake iko superior kuliko wenzake.Ila atambue CDM ni zaidi ya mnara wa baberi.
 
Kila mtu atapewa kwa kiwango kile kile anachotoa. Ukifanya mambo makubwa haina haja ya kuwaambia watu kwa kuwa kama ni makubwa kama unavyodhani watakuwa wameyaona hamna haja ya kurudia rudia kuwaambia.

Ninachotaka kusema ni kuwa KAMA KUNA MTU ANATAKA URAIS AACHE KUPIGA MAYOWE ATUACHE TUONE WENYEWE
 
Zitto celibate man tumweke ikulu ikulu sio ya wahuni, bado anahitaji kwenda club bado anatafuta mchumba. Afanye kwanza hayo na aacha undumila kuwili he will be considered not now!
By ze wei Lile hammer na Vogue kayatoa wapi vile?

mbona aliyeko huko ni celebrity man?au wewe hujui?
 
Naona maisha ya siasa ndani ya CHADEMA kwa upande wa rafiki yangu Mchange, sijui Machange yanaelekea ukingoni kama ilivyo kwa bosi wake Zitto. Hii tabia ya mwanachama mmoja kujiona bora kuliko chama ni sera ya chama kilichonyauka ambacho ni CCM. CHADEMA ni chama kinachokua na kupendeza; hivyo hawa wanaonyauka ndani yake watabaki pembeni mwa barabara ya kuelekea ukombozi halisi wa nchi hii.

Sijui ni Mtanzania gani mwenye falsafa halisi ya CHADEMA atawaunga mkono mamluki kama Mchange na wenzake; na sidhani kama harakati zao zitapunguza kasi ya chama hiki makini. Kama hawaelewi tukisemacho, wajifunze kwa rafiki yao Shibuda.
 
Hapo kuna hoja ya tani moja japokuwa si Zitto peke yake anayefanya vizuri bungeni kupitia CDM lakini kama wabunge wote watafanya vizuri bungeni basi huo ni mtaji wa kisiasa tosha kwa CDM. Nadhani jamaa huenda alikuwa anataka kukumbusha jinsi ambavyo wabunge wa CDM walivyomtupa mkono Zitto kwenye hoja yake ya kupinga posho za vikao!
Nashindwa kumuelewa mwandishi wa makala hiyo hapo kwenye wino mwekundu.Tunauelewa mchango wa Zitto na wabunge wengine wa CHADEMA katika bunge,hapa mwadishi anajaribu kutushawishi ya kua M4C haina umuhimu au kuna mgawanyiko ndani ya CHADEMA kuhusiana na M4C.

Na uhakika kama wabunge wote wa CHADEMA kama watashiriki vyema katika zoezi hili M4C kutaiweka CHADEMA katika mazingira mazuri ya kuchukua dola bila kujali nani atapeperusha bendera Zitto,Mbowe,Dr.Slaa n.k.

M4C NI MLINGOTI NA ILI BENDERA IPEPEE MLINGOTI NI LAZIMA KWA KAULI ZA ZITTO KAISHA SHONA BENDERA ANASAHAU YA KUA ILI BENDERA IPEPE MLINGOTI NI LAZIMA.
 
Mkuu hujui kuna mchakato wa kuandika katiba upya na vijana wanataka umri wa kugombea urais uwe kuanzia miaka 40? Hujui kwamba ahadi ya Rais JK ni kwamba katiba mpya itapatikana kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015? Ikiwa hivyo na bahati nzuri umri ukapunguzwa hadi miaka 40 basi Zitto atakuwa ndani ya wigo.
Hivi unakijua unachoandika kweli? Mwaka 2015 Zitto atakuwa na miaka 39, na katiba ya sasa inasema mgombea urais awe na umri wa kuanzia miaka 40. Labda uniambie katiba ijayo itaruhusu mgombea wa miaka 35, jambo ambalo mimi siliungi mkono. Umri wa kugombea urais ubaki huo huo wa miaka 40. Habari za kutuwekea watu wa kwenda kufanya utoto Ikulu hatutaki. Hiyo akili ya Zitto yenyewe haitoshei hata kuwa waziri mkuu, halafu anatafuta urais. Dogo aache kujikweza huyu, awe na subira. Tumpe Slaa miaka mitano arekebishe mambo, baada ya hapo Zitto aingie. Hivi hakuna watu wenye hekima wa kumwelekeza huyu dogo apunguze uroho wa madaraka?
 
It is too early to start these kind of threads unless you are someone who doesn't like CDM successes. CDM has a lot of things to put in order before 2014. For us who are working hand in hand change lovers, we are facing a lot of challenges to to put our party ready for 2014 election, and there after 2015. I dont think CDM has a problem in getting a presidential candidate in a right time, there are many candidates capable of going to state house and not the few you are thinking and trying to put us in a Pandora box. If you think by bringing this topic you are going to take CDM off road, you are cheating yourself, CDM is not a batch of foools, there are brains in there.

For example; who knew that, Dr. Slaa was going to contest in 2010? Are you a GT? then think.
 
Kamanda Mchange, Kamanda, Matata, Kamada Zitto, Kamanda Chagulani, Kamanda Shibuda, Makamanda Madiwani wa Arusha, fungukeni watanzania wapo nyuma yenu.

Lini uliitisha hicho kikao na kuchukua sensa ya wanaowaunga mkono hao unaowaita makamanda?
 
Back
Top Bottom