Urais wa Zitto 2015 ni kwa tiketi ya CHADEMA - Habib Mchange

Nasema ILIBIDI kwa kuwa sina uhakika kama hili litatokea kutokana na sababu kadhaa ambazo tayari wananchi tunazijua. najaribu kuiona Tanzania baada ya 2015 na ninaona picha ambayo si njema sana kwa upanzani. CCM iko katika mikakati mingi sana ya kujipanga. Toka leo hadi 2015 si muda mwingi lakini kisiasa si muda mchache hata kidogo. CCM ina nafasi na faida kubwa ya kushika tena Dola pindi ikiamua kuweka japo 1/3 ya kasoro zake kando, na kwa akili za watanzania ni wazi kuwa njia yao itakuwa nyeupe.

CCM inahitaji mpinzani madhubuti ifikapo 2015. Kiukweli inahitaji damu changa ambayo itaongozwa na mawazo ya wazee wa chama. Na viongozi wa chama waanze kujipanga tangu sasa kumuandaa huyo damu changa tangu sasa kwa kuwa katika hali halisi ukimuacha Dk Slaa, ni Zitto pekee anayekubalika kitaifa japo yuko upinzani. Zitto simjui na kwa maana hiyo hanijui.

Jambo la kufanya sasa hivi ni kuona kuwa maoni ya kutosha yanapatikana katika kipengele cha kupunguza umri wa kugombea nafasi ya Urais. Nasema naiona Tanzania baada ya 2015 na karata za upinzani zisipopangwa vyema ni wazi kuwa upinzani utapoteza tena. Mbaya zaidi upinzani ukipoteza hapo 2015 ni vigumu kuendelea kuwa na nguvu ya kipinzani iliyoko sasa, toka kwa wananchi pamoja na upinzani wenyewe.

Katika kuona pia kuwa mgombea anaandaliwa kuanzia sasa, itampa huyu mgombea ari na shauku na moyo wa kujipanga katika kufikia lengp la chama na Taifa kwa ujumla. Kama lengo si kushika Dola basi Zitto asiteuliwe, ila kama lengo ni kushika Dola basi ateuliwe, japo ccm wanaweza kutumia mbinu chafu kama walizotumia 2010.

Katika uchaguzi wa 2015, Zitto atakuwa na nguvu za kiushawishi kama alizokuwa nazo Dk Slaa kipindi kilichopita. Kama itajulikana kuwa umri utarekebishwa katika kipengele cha urais basi cdm isisite kufanya haya maamuzi mazito kwa mustakabali wa chama na Taifa. Viongozi wa cdm watazame huu ujumbe kwa mtazamo tofauti kidogo maana baada ya uchaguzi mkuu unazi utawasuta kama hawatataka kubadilika.

Kadhalika pale ambapo patahitaji muungano wa vyama katika kukipiku ccm, basi vyama visisite kufanya hivyo.
Mkuu wangu kwanza shukran sana kwa kutoa tahadhali iliyopo mbele ya chama. Nachoweza kuongezea tu leo hii ni kwamba swala la UMRI kupunguzwa tayari limekwisha pitishwa ni swala kusubiri lini itatangazwa kuwa sheria.. Na hii imetokana pia kuwa moja ya silaha ya CCM kuitumia dhidi ya CDM baada a kugundua kutaleta mgogoro mkubwa kwao ktk uchaguzi ujao.

Hivyo wana CDM jiandaeni mapema na swala hili maana Zitto lazima agombee na mkianza kuparuzana leo hii sijui itakuwaje Mwaka 2015 maana makundi yenu ndani ya chama tayari yamewapa CCM mwanya wa kuwalisha chambo..Kubadilisha kwa miaka (kushushwa) hakutakuwa na madhara kwa CCM maana wao tayari wameisha jipanga vizuri..
 
Tunahitaji mtu mwenye uchu wa uraisi kuliko yule anaejidai wazee wamenituma nigombee. Msijidanganye cdm baada ya kukataliwa dk Slaa 2010 mtupekee aliyebaki ni Zitto . Mkilazimisha dk Slaa 2015 tutamkataa tena.

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk 2
Nimekupa like ila hapo wenye bold umepitiliza. DK ana heshima yake na wala watanzania hawakumkataa bali mfumo wa Dola ulirubuniwa
 
Tunahitaji mtu mwenye uchu wa uraisi kuliko yule anaejidai wazee wamenituma nigombee. Msijidanganye cdm baada ya kukataliwa dk Slaa 2010 mtupekee aliyebaki ni Zitto . Mkilazimisha dk Slaa 2015 tutamkataa tena.

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk 2

Mkuu mimi siyo Mfuasi wa Zitto wala Dr. Silaa.
Kimsingi Zitto sina pingamizi la Zitto kuwa Rais, ila apunguze kukurupuka na ajishughulishe kuimarisha Chama, in so doing atakuwa anajiimarisha na yeye pia. Yeye kuanza kujitangaza kuwa atagombea Urais ilhali Chama bado hakijajiimarisha vya kutosha nchini ni Ujinga...
 
Mkuu wangu kwanza shukran sana kwa kutoa tahadhali iliyopo mbele ya chama. Nachoweza kuongezea tu leo hii ni kwamba swala la UMRI kupunguzwa tayari limekwisha pitishwa ni swala kusubiri lini itatangazwa kuwa sheria.. Na hii imetokana pia kuwa moja ya silaha ya CCM kuitumia dhidi ya CDM baada a kugundua kutaleta mgogoro mkubwa kwao ktk uchaguzi ujao.

Hivyo wana CDM jiandaeni mapema na swala hili maana Zitto lazima agombee na mkianza kuparuzana leo hii sijui itakuwaje Mwaka 2015 maana makundi yenu ndani ya chama tayari yamewapa CCM mwanya wa kuwalisha chambo..Kubadilisha kwa miaka (kushushwa) hakutakuwa na madhara kwa CCM maana wao tayari wameisha jipanga vizuri..
Hata mimi mawazoni niliamini kuwa kwa makusudi watawala watashusha umri wa kugombea ili kuleta mtafaruku cdm. Ni jambo jema sana maana siasa ni kama Draft. Siamini kama cdm itashindwa kupanga vyema kete zake maana tumeshuhudia mara kadhaa cdm wakitumia makosa ya ccm hadi wakafika hapo. Hata kama ccm wameshajipanga, na hata kama cdm hawatashinda uchaguzi ujao ni vyema wakamsimamisha huyu kijana kwani kwa kupitia yeye cdm itakua zaidi. They should take it from us
 
Mkuu mimi siyo Mfuasi wa Zitto wala Dr. Silaa.
Kimsingi Zitto sina pingamizi la Zitto kuwa Rais, ila apunguze kukurupuka na ajishughulishe kuimarisha Chama, in so doing atakuwa anajiimarisha na yeye pia. Yeye kuanza kujitangaza kuwa atagombea Urais ilhali Chama bado hakijajiimarisha vya kutosha nchini ni Ujinga..
Hapana sio Ujinga bali hakutumia busara..
 
Hata mimi mawazoni niliamini kuwa kwa makusudi watawala watashusha umri wa kugombea ili kuleta mtafaruku cdm. Ni jambo jema sana maana siasa ni kama Draft. Siamini kama cdm itashindwa kupanga vyema kete zake maana tumeshuhudia mara kadhaa cdm wakitumia makosa ya ccm hadi wakafika hapo. Hata kama ccm wameshajipanga, na hata kama cdm hawatashinda uchaguzi ujao ni vyema wakamsimamisha huyu kijana kwani kwa kupitia yeye cdm itakua zaidi. They should take it from us
Binafsi sidhani kama ZZK anaelewa siasa. Pengine TZ hatuhitaji mtu anayeelewa siasa (Itikadi) bali Uzalendo tu. Hadi sasa hivi Zitto ana mapungufu mengi sana ya kisiasa na hivyo anaweza kuwa mzuri sana ama hatari sana.
 
Hivi kuna uwezekano wa kujadili masuala ya Zitto (kwa wale mnaopenda) bila kuwashambulia viongozi na makada wengine wa Chadema kama Slaa, Mbowe, n.k.? Labda nithibitishiwe kuwa viongozi wa Chadema wanampiga vita Zitto katika harakati zake za kisiasa ikiwa pamoja na kuutaka urais - kitu ambacho sijakisikia rasmi. Sijamsikia Mbowe au Slaa wakimkosoa Zitto kwa hilo. Dr. Kitilla aliandika makala nzuri kuhusu haki ya Zitto kutangaza nia yake na akatoa angalizo muhimu kwa Chadema kuweka utaratibu wa kidemokrasia wa kupata wagombea tofauti na ule wa CCM unaodumaza haki ya wanachama kugombea na kuchagua viongozi. Imekuwa kama vile ushabiki ndani ya JF ndio kauli rasmi za Chadema; kama vile chama kimeshasema kina wagombea wawili tu wasiogusika - wapi hii ilisemwa?
 
Mwalimu nyerere aliwahi kuonya kuwa ikulu ni mahali patakatifu zaidi ni pagumu.alisema kuwa unapokuwa ikulu huku kuna watu wanakufa nja na wengine wanakufa kwa magonjwa hakika ni hali inayoumiza sana kwa wale wenye dhamiri hai.siku za karibuni kumeibuka kimbunga cha wanasiaa na hasa zitto kabwe(aliyetangaza waziwazi)kulilia kuwa marais wa nchi hii.maswali ya kujiuliza hapa ni mengi sana.itoshe kwa mimi kuuliza yafuatayo kwa zitto na wengine wote wenye nia na mawazo kama zitto;pia wana jamvi tunaweza kuongeza mengine ili kupanua mjadala na hatimaye wagombea feki wote wajichuje kama sio kuchujwa na wapiga kura;
1. Hivi ni kweli kuwa wanayaelewa matatizo ya tanzania na watu wake?
2.hivi ni kweli kuwa yanawagusa sana kuliko watu wengine?
3.hivi ni kweli kuwa wanasukumwa na matatizo haya kuingia ikulu?
4.hivi ni kweli kuwa kwa sifa zao kama viongozi kwa nafasi walizo nazo au walizowahi kuwa nazo wana sifa ya kuwa marais wa tanzania?
5.hivi kweli watu hawa wana uadilifu unaotosha kuingia ikulu?
6.hivi ji kweli kuwa nchi hii itakufa kama wao hawatakuwa marais?
7. Hivi ni kweli kuwa wamewajibika vya kutosha kwa nafasi walizo nazo sasa n kwamba wapo tayari kupokea majukumu makubwa zaidi?
Naomba kuwasilisha
8.
 
Tafadhalini sana, mijitu ya CCM msituchonganishe. CDM NI CHAMA KIMOJA CHA WATU WENYE UMOja
 
No hapa huajajibu hoja haata kama ni mwa cdm ni lazima awe na hoja za mcngi za kugombea.urais sio buia unayoweza kumpa kila mtu
 
bora anayesema wazi wazi, kuliko wanafiki kama membe wanajifanya hawataki, kumbe nyuma ya pazia wanafanya kampeni
 
Back
Top Bottom