Watanzania tuna matatizo sugu. Badala ya kufanya kazi za kujenga nchi tumekalia kujadili watu. Subirini kampeni zikianza mtafanya kazi hiyo tena kwa mapana na marefu. Jamani mpaka lini ujinga huu?
Kwanza napenda kukupongeza kwa uchambuzi huu ambao ni yakinifu halafu una mafundisho mengi sana.
1. Kwanza CDM ni chama chenye vision
2. CDM ina falsafa inayoeleweka, sio unafiki
3. CDM ina kanuni zinazotekelezeka, yaani kupitia katiba na miongozo yake
4. CDM katika mzingira haya yanadumisha nidhamu ya hali ya juu ndani ya chama kwa kuzingatia demokrasia
5. Inafanya kila kiongo kujua wajibu na nafasi yake ndani ya CDM
6. Inaondoa dhana ya chama mtu, na hivyo kila kiongozi anajua kuwa uongozi ni dhamana
7. CDM inahaha kudumisha nguvu ya umma kwa kila mbinu, chama cha wanachama kwa niaba ya umma.
Yapo mengi mengine yanayofanya CDM iwe na mshikamano wa hali ya juu.
Huu uzi umenikonga roho.
Hongera Dk Silah na Mk Mbowe.
Umesahau kuorodhesha fanikio moja ambalo hawa wawili wanalo nalo ni mafundi wa kuiba viburudisho vya watu
Umesmtua na Faizafoxy kuja kuongezea nguvu?Ndugu siasa sio kama mchezo wa kiduku ukichuchumaa watu wanashangilia.
Kwa hiyo msipakane mafuta kwa mgongo wa chupa, sifa mnazowamwagia hawa jamaa ni sifa za kienyeji zaidi.
Mwisho wa siku mtasema Mbowe na DK Slaa, wanamzidi Obama, kwa siasa.
Wewe unasumbuliwa na na usemi wa Bendera hufuata upepo na wala huna data zozote. Ni wasomi wangapi wanaunga mkono CHADEMA? Unajua undani wa CHADEMA mpaka useme viongozi wake hawana migogoro? Slaa ni BMOWE ni kama X na Y kwa watu wa hesabu wanajua , mlinganyi kama Y =2x, Y inatemegea sana X ,Wale jama wanajuana na wanajua wanavyoitafuna CHADEMA. SLAA anaishi kwa fedha za CHADEMA, Mbowe anaidai Chadema madeni kibao na ni kama Mzabuni wa CHADEMA, sasa atawezaje kumkoromea Slaa ambaye ni mtendaji wa Chama? Hebu jikumbushe episodi ya ZITTO na Mbowe katika kugombea ukuu wa Chama hicho. Unajua chanzo cha kifo cha Chacha Wangwe?. Mimi usiniambie kabisa kuhusu hao Mabwanyeye. Ni kweli kwamba wamefanikiwa kufanya harakati mbalimbali kama Migomo vyuoni, migomo ya wafanyakazi n.k. Hivi siku wakifanikiwa kushika hatamu watajidai kwamba walikuwa wapiganaji au wachochezi? Uliza fukuto la upendeleo wa uongozi kwa wanawake katika Chama hicho. Unajua chizi anaweza kujifanya anajua sana mbele ya watu wenye akili zao akadhani yeye ndo basi kumbe wanamsanifu tu. Hakuna wasomi wanaokiunga mkono Chadema bali wanakiona kama kikundi fulani cha wasanii, si unajua wasanii wanavyoweza kushangiliwa kwenye majukwaa lakini siku ya siku JINA WASANII linatawafanya waendelee kuonekana wasanii tu.
Suala la Udini na Ukaskazini wamelishughulikia vipi?
Tukumbuke kabla ya hawa watu hawajaingia madarakani, siasa za Tanzania hazikuwa na chembe ya udini, hata kama hii dhana ilikuwepo, ilikuwa kwa kiwango cha chini sana.
kila nikisoma post zenu nazidi kuichukia saccoss ya wachaga
Namsikitikia sana Zitto, nadhani anajuta lakini afanye nini.
upuuzi mtupu hapo hakuna chochote cha maana alichochambua,eti nafasi ya mboe na slaa isiguswe au ndio namna ya uteteaji wa mfumo kristo ndio maana hutaki watoke kwy nafasi zao?