Unazuia sherehe za Uhuru, unaadhimisha birthday ya CCM

Ni utaratibu usio sawa. Lakini umehalalishwa na serikali za CCM. Magari ya serikali kutumika katika shughuli binafsi haswa kwa viongozi waandamizi (mawaziri, wakuu wa wilaya na mkoa, DEDs, DASs, RASs, makatibu wakuu, wakurugenzi, makamishina, majaji n.k) ni matumizi mabaya ya mali za umma.

Siwezi kuongelea juu ya viongozi wakuu wa dola: Rais, Spika, Jaji Mkuu na Waziri Mkuu. Hawa wanastahili hiyo 'favour' ingawa ni vyema nao kuongozwa na sheria za namna ya kutumia mali za umma kwa mambo binafsi. Hapa mambo binafsi hayuhusiana na wao kuhudhuria sherehe za chama. Hili si sawa. Lakini wengine wote hawastahili kutumia mali za umma kwa matumizi binafsi.

Watu wa CCM uwa wanapenda sana kutoa mifano ya nchi zingine pale wanapohalalisha jambo lililo upande wao. Lakini ung'aka pale watu wanapotoa mifano ya nchi zingine kwa mambo wasiyoyataka. Utawasikia, "kila nchi inaamua mambo yake". Kwenye hili la matumizi ya mali za umma, serikali ya CCM ijifunze kwa nchi nyingine kama, Uingereza, Uswisi na nchi za Scandanavia.

NB: si Magufuli alisema ataachana na 'mashangingi'? Mbona bado yanatawala fleet ya serikali?!
Mkuu huo ni usanii kama kina joti
 
Pesa zilihamishiwa kwenye ujenzi wa barabara ya Morocco to Mwenge. Je barabara haikuanzwa kufanyiwa kazi immediately baada ya tamko lake?
Ccm wanafanikiwa sana kwa kuwafunika watu na maguo ya kijani.....kama ingekuwa kweli kwanini Magufuli alijiliza pale kwenye Siku ya sheria kuwa kakuta Hazina Nyeupe hakuna hata mishara wee na Magufuli tumuamini nani
 
Wanabodi
Salaam;

Serikali ya awamu ya 5 inajinasibu kubana matumizi na kufuta baadhi ya sherehe za kitaifa kwa lengo hilo la kuzuia matumizi yasiyo ya lazima.

Kichekesho kimeonekana leo baada ya serikali nzima kuhamia singinda kwenye sherehe za birthday ya ccm ya kutimiza miaka 39.

Huko nyuma tulishuhudia sherehe za uhuru zikipigwa kumbo,sherehe za wabunge zikapigwa ban,baadae tbc nayo ikapigwa ban kwa lengo hilo hilo la kubana matumizi. Cha kushangaza Rais na serikali nzima walikuwa kwenye birthday hiyo ya ccm kwa ajili ya kutoa hotuba za mipasho!!

Kweli hii nchi ngumu sana aisee!
Mkuu chama kina uongoz na vipaumbele vyake na serikali ina uongoz wake na vipaumbele pia...Yanayofanyika serikalini si lazima yafanyike kwenye chama
 
Can you prove that?!? Yaani magari ya viongozi wa serikali, polisi, hata ya viongozi wastaafu yaliwekewa mafuta na CCM? Na walinzi na security details wa viongozi walilipwa na CCM?

Ndiyo... Ujue pia kuna mfuko wa Rais ambao unaweza kufanya hizo shughuli..
 
Rais na wenzie wanahaki ya kusherehekea birthday ya chama chao, to the full extent, ndo mzazi wao, ni chama ndo kimewaweka madarakani.
Mfano wangekuwa ACT wangeshinda? Ni sawa kusherehekea birthday ya chama chao..
 
Ndiyo... Ujue pia kuna mfuko wa Rais ambao unaweza kufanya hizo shughuli..
Mfuko wa Rais unaochangiwa na CCM?! Kwa hiyo huo mfuko upo kwa ajili ya kugharamia matumizi ya Rais na viongozi waandamizi wa serikali na wastaafu wakati wa sherehe za CCM?
 
Mshana jr mtendee haki mtoa mada, usiendelee kumjaza ujinga. Ninafahamu wewe una uelewa zaidi kuhusu tofauti ya sherehe za vyama na serikali.

Waziri Mkuu alipoenda Arusha kwenye sherehe ya kusimikwa Askofu Mkuu KKKT Frederick Shoo unadhani kanisa la KKKT lilimlipia pesa za mafuta ya magari na walinzi wake?

Nimekuambia nenda shule ukajifunze civics!
Mimi naelewa tofauti ya sherehe za chama na za kiserikali. Lakini pia naamini msafara wa kiongozi wa kitaifa utagharamiwa na serikali hata kama amealikwa kuzindua kanisa au msikiti au hoteli au night club au hata kilabu cha kilaji!

Swali la msingi ni Je, kama Rais anaamini katika kubana matumizi na ana uchungu na pesa za walipa kodi, kwa nini asiikatae mialiko kama hiyo ISIYO YA KITAIFA inayosababisha atumie PESA ZA WALIPA KODI ambazo zingeelekezwa kwenye huduma za jamii?

Hapo ndipo penye hekima na busara, na uache kuwashambulia wenzio kwamba hawajasoma wakati wewe mwenyewe na 'usomi' wako umeshindwa kupambanua jambo dogo kama hili kwa sababu tu ya ushabiki na mahaba ya kichama.
 
Mfuko wa Rais unaochangiwa na CCM?! Kwa hiyo huo mfuko upo kwa ajili ya kugharamia matumizi ya Rais na viongozi waandamizi wa serikali na wastaafu wakati wa sherehe za CCM?
Mfuko wa Rais hakuna wa kuuhoji matumizi yake... Ni Rais mwenyewe ndiyo huupangia utaratibu mzuri wa matumizi...

Kuwa kwenye system ndiyo utaelewa zaidi..
 
Hivi huyo jamaa alisema hivyo kwa hisia tu ama kuna nadharia katika sayansi ya siasa inayosema hivyo? Kama ipo unaweza kunitajia ili nijifunze.

Mi nadhali lina ukweli fulani.

Wote tunafahamu CCM haijawahi kushinda uchaguzi Zenj na sasa kimegeuka kuwa chama cha kigaidi huko Zenj.

Naamini Lusinde alikuwa ananyoshea kidole wenzake akasahau vidole vinne vinamsonta yeye na chama chake.
 
Mimi naelewa tofauti ya sherehe za chama na za kiserikali. Lakini pia naamini msafara wa kiongozi wa kitaifa utagharamiwa na serikali hata kama amealikwa kuzindua kanisa au msikiti au hoteli au night club au hata kilabu cha kilaji!

Swali la msingi ni Je, kama Rais anaamini katika kubana matumizi na ana uchungu na pesa za walipa kodi, kwa nini asiikatae mialiko kama hiyo ISIYO YA KITAIFA inayosababisha atumie PESA ZA WALIPA KODI ambazo zingeelekezwa kwenye huduma za jamii?

Hapo ndipo penye hekima na busara, na uache kuwashambulia wenzio kwamba hawajasoma wakati wewe mwenyewe na 'usomi' wako umeshindwa kupambanua jambo dogo kama hili kwa sababu tu ya ushabiki na mahaba ya kichama.
Asante sana mkuu kwa kuwa mkweli ktk jambo muhimu
 
Hili suala wachieni viongozi wa UKAWA walifuatie na walizungumzie, wao wanamadaraka ya kufuatia kila jambo ili kuhakikisha mali ya umma untumika ipasavyo. Sana sana sasa hivi tuna tumia enegy nyingi tu ya kutoa maini na matusi wakati wakina LOWASA wamekaa kimyaa
 
Irrelevant post, Magufuli sio mwenyekiti wa chama useme anayo mandate ya kupiga marufuku shughuli za chama kama alivyofanya kwa serikali acha kwanza muda wake ukifika umpime kwa maamuzi yake.
 
Kurusha Birthday ya ccm Live Azam Tv siyo gali lakini kuonyesha Bunge lenye maslai mapana na nchi tena kwenye chombo chenyekutumia kodi za haohao wananchi ni gali sana
 
Back
Top Bottom