Unavyofikiri Tanzania itajengwa na CHADEMA peke yake?

Mtoa thread kauliza swali la msingi sana. Nahakuna mchangiaji aliyetoa jibu lenye maana.
Sera ya CDM inaelekea ni kuipinga CCM , sera ambayo naona si mbaya ila haina filosofia ya kule wanakoelekea wana CDM.
Kwa post kama hii ndio unaona jisi CDM vipofu wanavoongoza vipofu wenzao.
Zaidi ya ufisadi,suala linaloweza kudfanywa vizuri tu ma wanaharakati, CDM haina muono wala sera ya muelekeo kifilosofia.
Kama ni mafisadi CDM wako tele na wanafahamika.
Ni vyema tukaelewa kuwa kama CDM ikikamata nchi uchumi utakuwaje,siasa ya ukulima itakuwaje, wafanyakazi wattendewa vipi. Nasuala la uwekezaji umekaa vipi kulingana na rasilmali za waTanzania.
Nina uhakika watakachokuja nacho ni kama chama tawala tu maana CDM haina jipya zaidi ya kuingia madarakani.

Lole acha kukurupuka: Je unajua kwamba Chadema ni chama kinachoamini katika mrengo wa wakati na falsafa ya umma? Au ni uvivu wa kusoma?chadema inaamini katika kujenga tabaka la kati la wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara.

Chini hapa ni extract kutoka official website ya Chadema kuhusu itikadi na mwelekeo!

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama mbadala kinachokua na kinachoongozwa kwa Falsafa ya “Nguvu ya Umma” na kuamini katika itikadi ya “Mrengo wa Kati”. CHADEMA inawataka watanzania kuelewa kwamba mabadiliko ya kweli yataletwa na kubadilisha mfumo wa utawala. Maendeleo ya kweli hayawezi kuletwa na mafisadi walewale wa chama kile kile chenye uoza ule ule wakiendeleza yale yale kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. CHADEMA inatambua kwamba kwa falsafa ya Chukua Chako Mapema (CCM), Tanzania yenye neema kamwe haitawezekana. Lengo la CHADEMA ni kusimamia mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli ili kuunda Taifa la watu walio huru na lenye kuzingatia misingi ya utawala bora na linalotoa fursa kwa wananchi wake kushiriki katika kuboresha maisha yao. Tanzania endelevu, yenye haki na isiyovumilia ukandamizaji wa aina yeyote kwa wananchi wake-ndiyo nchi tunayoitaka. CHADEMA inafanya kazi kuhakikisha kuwa vyombo vya utawala na viongozi wanafanya maamuzi ya busara na makini yanayowaletea wananchi nafuu ya maisha na kuwapa matumaini ya kuendelea kupiga hatua za kimaisha katika nyanja zote za maendeleo.
 
mimi nimemuelewa mtoa mada,nadhani uwezo wangu wa kusoma falsafa ya dini,unaniwezesha kuyajua mawazo ya mtu ambaye ameshindwa kuyafafanua....hapa amemaanisha;- tupo watu humu ndani tunaodhani kuwa Chadema ndio kila kitu,nadhani amerejea baadhi ya watu wa humu ndani wanavyowashambuli watu wengine wanaojaribu kuikosoa chadema,chadema ni chama cha siasa,hivyo usiamin kwamba kitakuwa sahihi kwa kila jambo,naamini humo ndani wamo wenye malengo binafsi,pia wapo wenye upendo na uchungu wa kweli kwa nchi,hatuwapimi watu kwa kuwaona majukwaani wanavyoweza kukosoa serikali tu,pia tunawahitaji tuwatambue hata kwa maisha yao na majirani zao,hivyo sio kwamba kila jambo la chadema ni bora na sio kwamba chadema bila changamoto na wakosoaji itaweza kusonga na ikatuvusha..msiwe bendera tafakari na uwe mdadisi sio tu unashangiria bila sababu ya maana,plz naomba muwe great thinkerz sio washabiki jamani,mm ni mwanachadema ila sipendi kutohoji 'be a man of critical thinking and aguments'
 
mimi nimemuelewa mtoa mada,nadhani uwezo wangu wa kusoma falsafa ya dini,unaniwezesha kuyajua mawazo ya mtu ambaye ameshindwa kuyafafanua....hapa amemaanisha;- tupo watu humu ndani tunaodhani kuwa Chadema ndio kila kitu,nadhani amerejea baadhi ya watu wa humu ndani wanavyowashambuli watu wengine wanaojaribu kuikosoa chadema,chadema ni chama cha siasa,hivyo usiamin kwamba kitakuwa sahihi kwa kila jambo,naamini humo ndani wamo wenye malengo binafsi,pia wapo wenye upendo na uchungu wa kweli kwa nchi,hatuwapimi watu kwa kuwaona majukwaani wanavyoweza kukosoa serikali tu,pia tunawahitaji tuwatambue hata kwa maisha yao na majirani zao,hivyo sio kwamba kila jambo la chadema ni bora na sio kwamba chadema bila changamoto na wakosoaji itaweza kusonga na ikatuvusha..msiwe bendera tafakari na uwe mdadisi sio tu unashangiria bila sababu ya maana,plz naomba muwe great thinkerz sio washabiki jamani,mm ni mwanachadema ila sipendi kutohoji 'be a man of critical thinking and aguments'

ndugu umeongea kweli na nimependa mawazo yako. ndugu zanguni mimi ninichoomba ni kwamba kampeni ziwepo wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi tofauti zetu tuziweke pembeni tufanye kazi hakuna chama wala mtu yyte ambaye yuko perfect. malumbuno ya wanasiasa yaishie bungeni baada ya nje tunachotaka lao liwe moja ni kutuongoza sisi kufikia malengo yetu na si vinginevyo.
 
CDM ni chama cha siasa kilichosajiriwa na lengo kuu ni kuongoza serikali katika kulisaidia taifa letu kuendelea na kutoka kwenye umasikini uliokithiri chini ya ubabaishaji wa magamba

sasa sijuhi ni kwa nini umeuliza swali potofu kiasi hiki,kwanza waangalie viongozi wake,pili uitizame ilani yake mpaka CCM wanalazimika kuimplement bila kupenda,tatu fuatilia historia ya chama kama kinashuka,kinadumaa ama kinazidi kushika kasi

mwisho nataka tu uelewe kwamba CDM kipo ili kuomba ridhaa ya kuongoza nchi,siyo chama kinachosubiri kuungana na chama kingime kwa maana kila chama kina ilani yake na ndo maana kikaomba usajiri

kama hutu tuvyama twingine tunasubiri kuungana tuungane twenyewe na kama hatuwezi mbio hizi ni bora tujivunje twende penye nguvu,siyo lazima tuwe na vyama lukuki visivyoweza hata kukaza,kwani walilazimishwa kuundwa vyama???

huu nao ni uchizi mwingine,hivi kwa nini Afrika mnapenda sana serikali za umoja? tatizo hapa ni uroho wa madaraka,kulazimisha ushindi na ulaghai wa kidemokrasia
 
Wewe unavyofikiri Tanzania itajengwa na ccm pekeyake?,...pengine mimi ndo sijui...hivi ccm saizi inashirkiana na chama gani? hadi uituhumu cdm kuwa unahisi haitakuwa na ushirikiano na vyama vingine? :help:
 
Wewe unavyofikiri Tanzania itajengwa na ccm pekeyake?,...pengine mimi ndo sijui...hivi ccm saizi inashirkiana na chama gani? hadi uituhumu cdm kuwa unahisi haitakuwa na ushirikiano na vyama vingine? :help:

ndio maana hatuna maendeleo, kwasababu ccm haiwapi ushirikiano vyama vyengine so hofu yangu chadema nayo isije ikafanya makosa haya. na mwelekeo wa chadema NDIO UNANITISHA ZAIDI BAADA YA KUGOMA KUSHIRIKIANA NA VYAMA VINGINE VYA UPINZANI SO HII IMEPUNGUZA NGUVU YA VYAMA VYA UPINZANI BUNGENI.
 
Back
Top Bottom