Nimesoma maoni ya Chadema kuhusu miswada mitatu; Je, huu uchambuzi umefanywa na wasomi wa Tanzania au wa Havard University?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,106
Kama tunasoma vyuo vilevile bila kujali vyama vya siasa tunavyotoka, kwanini CHADEMA wawe na timu inayoweza kufanya uchambuzi wa kina na usio na upendeleo (biasness) kwa kiwango hiki?

Kwa uchambuzi huu waliofanya, naamini hakuna maoni yaliyochambuliwa kama ya hawa watu. Taasisi na mashirika mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa wamewasilisha maoni. Tofauti ya maoni ya makundi mengine ni kwamba hawa wenzetu walikaa wakachambua nakuandika kitaalamu na kwa lugha ambayo kila mtu akisoma anapata mantiki na anaona vision yao kuhusu mfumo wa uchaguzi nchini

Sina uhakika kama waajiriwa wa CHADEMA wanalipwa kiasi gani ila naamini wanalipwa kidogo kulinganisha na chama tawala.

Je, wanapata wapi wasomi wazuri kiasi hiki wasiopenda maslahi makubwa bali wanapenda itikadi yao? Wanawezaje kusajili watu wenye akili timamu kwa miaka zaidi ya 30 mfululizo?

Viongozi wengi wazuri ndani ya chama cha mapinduzi na wanaokubali mjadala japo kwa kiasi kidogo waliwahi kuwa chadema , viongozi wa vyama vya upinzani karibia wote waliwahi kuwa chadema. Lakini hakuna mwana CCM mwenye nafasi ya uongozi chadema kwa maana hiyo chadema imeweza sana kuwaandaa watu makini na wenye akili timamu ikilinganishwa na taasisi nyingine.

Swali la nyongeza, ni kweli kwamba haya maoni yameandikwa na wana chadema au wamelipwa washauri kutoka Mataifa na vyuo vikubwa Duniani? Kama wameandika wenzetu watanzania ; tunaweza kufahamu majina yao? Itatusaidia sana kuwapa mchongo wa kazi za uandishi lakini pia hata waliopo madarakani wanaweza wakawa chukua kuwasaidia kazi.

Huu uchambuzi unanipa moyo kwamba hatuna umuhimu wakutumia makampuni ya kigeni kwenye kesi zetu; tuandae watanzania na kwa kuanza tujifunze kutoka mfumo wa chadema.

Hongereni kwa hatua hii, niwaombe na taasisi nyingine vikiwemo vyama vya siasa waweke wazi maoni yao waliyowasilisha kwa maandishi jamii ione. Tusiwe kama Joseph Selasini ajaandika chochote cha taasisi anakwenda kutoa maoni binafsi kwa niaba ya NCCR.
 
Kama tunasoma vyuo vilevile bila kujali vyama vya siasa tunavyotoka, kwanini CHADEMA wawe na timu inayoweza kufanya uchambuzi wa kina na usio na upendeleo (biasness) kwa kiwango hiki?

Kwa uchambuzi huu waliofanya, naamini hakuna maoni yaliyochambuliwa kama ya hawa watu. Taasisi na mashirika mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa wamewasilisha maoni. Tofauti ya maoni ya makundi mengine ni kwamba hawa wenzetu walikaa wakachambua nakuandika kitaalamu na kwa lugha ambayo kila mtu akisoma anapata mantiki na anaona vision yao kuhusu mfumo wa uchaguzi nchini

Sina uhakika kama waajiriwa wa CHADEMA wanalipwa kiasi gani ila naamini wanalipwa kidogo kulinganisha na chama tawala.

Je, wanapata wapi wasomi wazuri kiasi hiki wasiopenda maslahi makubwa bali wanapenda itikadi yao? Wanawezaje kusajili watu wenye akili timamu kwa miaka zaidi ya 30 mfululizo?

Viongozi wengi wazuri ndani ya chama cha mapinduzi na wanaokubali mjadala japo kwa kiasi kidogo waliwahi kuwa chadema , viongozi wa vyama vya upinzani karibia wote waliwahi kuwa chadema. Lakini hakuna mwana CCM mwenye nafasi ya uongozi chadema kwa maana hiyo chadema imeweza sana kuwaandaa watu makini na wenye akili timamu ikilinganishwa na taasisi nyingine.

Swali la nyongeza, ni kweli kwamba haya maoni yameandikwa na wana chadema au wamelipwa washauri kutoka Mataifa na vyuo vikubwa Duniani? Kama wameandika wenzetu watanzania ; tunaweza kufahamu majina yao? Itatusaidia sana kuwapa mchongo wa kazi za uandishi lakini pia hata waliopo madarakani wanaweza wakawa chukua kuwasaidia kazi.

Huu uchambuzi unanipa moyo kwamba hatuna umuhimu wakutumia makampuni ya kigeni kwenye kesi zetu; tuandae watanzania na kwa kuanza tujifunze kutoka mfumo wa chadema.

Hongereni kwa hatua hii, niwaombe na taasisi nyingine vikiwemo vyama vya siasa waweke wazi maoni yao waliyowasilisha kwa maandishi jamii ione. Tusiwe kama Joseph Selasini ajaandika chochote cha taasisi anakwenda kutoa maoni binafsi kwa niaba ya NCCR.
Hiyo ni kazi binafsi ya JJ. Mnyika with few imputs from the rest. JJMnyika is dam good, tatizo lake ni moja, hana a good team to play with.

Ni kweli kati ya vyama vyote na maoni ya taasisi zote, maoni ya Chadema ni funga kazi. Big up sana Chadema for that!.

Sii kweli kuwa CCM haijatoa viongozi wazuri Chadema, kwani unajua Dr. Slaa alitokea wapi?, na wakati akiwa Chadema, kadi yake ya uanachama huko alikotokea ilikuwa wapi na ilikuwa imelipiwa miaka mingapi?.

P
 
kwanini CHADEMA wawe na timu inayoweza kufanya uchambuzi wa kina na usio na upendeleo (biasness) kwa kiwango hiki?

Chama makini kinaangalia mustakabali wa nchi miaka 200 mbele, kuwa sheria nzuri na katiba sahihi itazuia viraka vingi kuwekwa ktk katiba siku za mbeleni wananchi wakiwa wanachagua vyama mbadala.

CCM hawaangalii mustakabali wa nchi, kwao chama ndiyo kikubwa kuliko nchi wakati siyo kweli.

Kuna kipindi chama tawala chocolate kinaweza kukosa mvuto, ushawishi au sera nzuri na chama kingine kikaingia kama chama tawala. Hii inathibitisha kuwa umma na nchi ni vitu viwili vikubwa kuliko chama chochote cha kisiasa. Hilo chama kongwe dola CCM kimeshindwa kubaini.

Kutokana na wasilisho hilo, inatakiwa CHADEMA na wadau wote wenye mapenzi mema na nchi yetu Tanzania waendelee mfululizo kurudia kwa kina maoni hayo ktk media zote, mitandao na majukwaa ya kijamii ili elimu ya uraia iwafikie umma mpana na wote ikiwemo wabunge na viongozi wa CCM hadi ikifika tarehe 30 January 2024 wawe wameelimika kuuondoa miswada hii mibovu.
 
Uchambuzi wenyewe upo wapi mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app


View: https://m.youtube.com/watch?v=bKf7xpsl0VI
Source:
 
Uchambuzi wenyewe upo wapi mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app



Na pia msikilize kamanda Benson Kigaila:

𝗕𝗲𝗻𝘀𝗼𝗻 𝗞𝗶𝗴𝗮𝗶𝗹𝗮 𝗡𝗮𝗶𝗯𝘂 𝗞𝗮𝘁𝗶𝗯𝘂 𝗠𝗸𝘂𝘂 𝗕𝗮𝗿𝗮 𝟬𝟰/𝟬𝟭/𝟮𝟬𝟮𝟰
Hii Tume ya Uchaguzi tuliyonayo leo ukiitaka kuiita kwa jina sahihi ni 𝗖𝗛𝗢𝗠𝗕𝗢 𝗖𝗛𝗔 𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗖𝗛𝗔 𝗞𝗨𝗥𝗔𝗧𝗜𝗕𝗨, 𝗞𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘𝗦𝗛𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗨𝗦𝗜𝗠𝗔𝗠𝗜𝗔 𝗨𝗖𝗛𝗔𝗚𝗨𝗭𝗜, pia ambayo inapendekezwa jina inayostahili ni hilo hilo kwa sababu Kamati ya Usahili ni Kamati ya Rais, hatuwezi kusema kuna nafuu.Tunachokosea kuhusu kutunga Sheria zetu tunataka kumfanya Rais kama Mungu, Rais ni mtu na ni mgombea wa uchaguzi wa Chama, kwa nini tunampa mamlaka ya kuunda vyombo vya kusimamia uchaguzi?.𝗠𝗵𝗲.

View: https://m.youtube.com/watch?v=fl3EE2ZLPjk
 
Kwa uchambuzi huu waliofanya, naamini hakuna maoni yaliyochambuliwa kama ya hawa watu.

Katika hotuba moja ya mheshimiwa Rais Dr. Samia Suluhu Hassan alifunguka kutoka moyoni jinsi anavyokubali hoja kutoka upinzani.

Ni matumaini yetu makubwa mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mwenyekiti wa CCM Taifa, mawasilisho haya ya CHADEMA mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge atayafanyia kazi kubadilisha miswada hii. Kwani wasilisho la CHADEMA linakwenda sawia na zile 4R , sheria za haki na katiba mpya inayokubalika kuwa ni ya usawa kwa wote bila kujali vyama.

Toka Maktaba :

17 Feb 2020
Samia Suluhu : "Napenda mawazo ya wapinzani, huwa wanajenga hoja vizuri, walini 'inspire' niingie siasa"



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amefunguka kuhusiana na historia ya maisha yake ambapo ameeleza siri ya mafanikio na chanzo kilichomvutia kuingia kwenye siasa. Samia Suluhu anaona hoja za upinzani ni moto, zimejaa mantiki kuliko za mawaziri wa serikali ya CCM , hivyo walinivutia / inspire, mimi ni activist ... kuingia siasani baada ya kuona majibu na hoja za upande wetu (CCM) hazina uhalisia na hazijibu maswali ya wananchi ....


View: https://m.youtube.com/watch?v=gb3MPZNXdt4
Video toka maktaba, Mh. makamu wa Rais na mwanachama wa CCM Dr. Samia Hassan akionesha kuwakubali wapinzani wenye hoja.
 
10 January 2024
Dodoma, Tanzania

Kamati ya Kudumu ya Bunge yapewa elimu ya uraia

Mbunge wa jimbo la Nkasi kamanda Mh. Aida Kenani aelezea umuhimu wa katiba, mara baada ya CHADEMA kufanya wasilisho mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge. Mbunge huyo wa CHADEMA anashauri Kamati ya Bunge .....


View: https://m.youtube.com/watch?v=Pn86StKAfho
 
10 January 2024
Dodoma, Tanzania

GASTON GARUBINDI : WANANCHI WAPITIE MAONI YA CHADEMA KWA KINA, MAANA MWENENDO WA TUME YA KUDUMU YA BUNGE UNATIA SHAKA


View: https://m.youtube.com/watch?v=JyNY75jex-8
Maoni hayo yametolewa leo jijini Dodoma na mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya magharibi pia mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA kamanda wakili msomi Gaston Shundo Garubindi akielezea masikitiko yake juu ya kamati ya kudumu ya bunge .....
 
Hiyo ni kazi binafsi ya JJ. Mnyika with few imputs from the rest. JJMnyika is dam good, tatizo lake ni moja, hana a good team to play with.

Ni kweli kati ya vyama vyote na maoni ya taasisi zote, maoni ya Chadema ni funga kazi. Big up sana Chadema for that!.

Sii kweli kuwa CCM haijatoa viongozi wazuri Chadema, kwani unajua Dr. Slaa alitokea wapi?, na wakati akiwa Chadema, kadi yake ya uanachama huko alikotokea ilikuwa wapi na ilikuwa imelipiwa miaka mingapi?.

P
Siyo kazi binafsi ya JJ.Mnyika. Chadema ni Taasisi kubwa Myika kafanya mawasilisho ya mapendekezo.

Maoni yamekusanywa kutoka kwa wengi, na majumuishi yamefanywa na chama, JJ Mnyika kayawasilisha mbele ya kamati.

Kipe chama credit siyo mtu. Yale hayakuwa maoni ya JJ .Mnyika bali ya chama cha demokrasia na maendeleo.
 
Back
Top Bottom