WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Maisha ya mwanadamu hayazidi miaka 70 wachache kuenda hadi 100 kwa wale waliojaaliwa kuishi umri mkubwa, achilia mbali life expectancy ambayo kwa Watanzania kufuatia UKIMWI kuwa tishio na magonjwa mengine kama shinikizo la damu, cancer etc,hayazidi miaka 50.
Chukulia kuwa toka kuzaliwa hadi uweze kusimama kwa miguu yako mwenyewe kimaisha, ukijumlisha na miaka ya kusoma hadi chuo ni miaka 25. Halafu ongezea miaka mingine kama 15 ya kujijenga kimaisha ( kuanzisha familia yako na kujiweka sawa kiuchumi) kwa walio wengi ukiondoa wachache wenye kukuta wazazi wamewawekea kila kitu au labda waliorithi, au kubahatisha kupata mali upesi kwa njia halali au labda zisizohalali! Hapo tayari ni miaka 40. Ongezea hapo miaka mingine 20 ya consolidation na kustaafu = 60.
Baada ya hapo ni mtu kupumzika na ama kula jasho lake au kuanza msoto mkali wa kutafuta riziki baada ya kustaafu, ilhali mwili na hata akili vimeanza kuchoka kwa miaka 10 = 70 ambapo ndio umri mrefu wa wastani wa binadamu kuishi.
Huwa najiuliza, hivi binadamu tuna raha gani ya maisha? Je wewe mwenzangu huwa unajiuliza maswali gani ya kifilosofia juu ya maisha?
Chukulia kuwa toka kuzaliwa hadi uweze kusimama kwa miguu yako mwenyewe kimaisha, ukijumlisha na miaka ya kusoma hadi chuo ni miaka 25. Halafu ongezea miaka mingine kama 15 ya kujijenga kimaisha ( kuanzisha familia yako na kujiweka sawa kiuchumi) kwa walio wengi ukiondoa wachache wenye kukuta wazazi wamewawekea kila kitu au labda waliorithi, au kubahatisha kupata mali upesi kwa njia halali au labda zisizohalali! Hapo tayari ni miaka 40. Ongezea hapo miaka mingine 20 ya consolidation na kustaafu = 60.
Baada ya hapo ni mtu kupumzika na ama kula jasho lake au kuanza msoto mkali wa kutafuta riziki baada ya kustaafu, ilhali mwili na hata akili vimeanza kuchoka kwa miaka 10 = 70 ambapo ndio umri mrefu wa wastani wa binadamu kuishi.
Huwa najiuliza, hivi binadamu tuna raha gani ya maisha? Je wewe mwenzangu huwa unajiuliza maswali gani ya kifilosofia juu ya maisha?