Umaarufu wa Kikwete upo juu

Unajua,ivi vitu tuacha tu,kikwete amejalibu lakini jamani wakati mwingine watu wa wakalibu nae wanamuangusha otherwise so far so good
 
Jamani tuacheni propaganda. Si kubaliani na yeyote anayesema kuwa viongozi wote ni mafisadi. Kwani hawa viongozi ni akina nani. Si ni baba zetu, wajomba zetu, mama zetu, kaka zetu n.k. Mimi ninaamini kuwa tatizo lilopo Tanzania si la viongozi tu, bali ni la watanzania wote. Na tukisimama kuwasaidia viongozi wazuri waliopo madarakani waraka wenye maslahi ya Taifa.

Kama Mwenye uwezo wa kuwachukulia hatua mafisadi anawatetea kuwa "Hawakuwa makini"- Refer Richmond saga, wakati UFISADI/ RUSHWA unaonekana kwenye mkataba huo wa kitapeli unataka tumuiteje? Chama ni watu na hivyo kama Chen - Ge yumo kwenye kamati ya Maadili ya Sisiemu, unategemea CCM iwe chama safi?

Kuwasaidia viongozi walioko madarakani ni kuwaweka benchi ili waangalie watanzania wengine wakiongoza jahazi.
 
Pili ndio kuwaelimisha wananchi jinsi ya kuwangoa mafisadi. Nilichokigundua mimi kuwa rythm tunayoipiga bado aslimia 70 ya wananchi hawawezi kucheza. Mpaka huo ndio ukweli tutalalama sana na wapinzani tukidhani tunaonewa.

.
Zawadi ,
Nafikiri hapo nakuelewa.We need to know the truth in order to win the battle.Kweli wananchi wengi bado hawajaelewa nini kinachoendelea katika serikali na maneno matamu yamewalevya kiasi kwamba hawajui lipi jema.Kama mafisadi wakienda kwa wapiga kura wao wanashangiliwa kama mfalme na mashujaa,unafikiri hii inaashiria nini?Bado uelewa mdogo na watu wanaridhika na vitu vidogo vidogo hawaangalii future hasa vijijini na mikoani ukiondoa Dar.
 
"Sema ukweli, propaganda zisikupofue macho. Ulitembelea vijiji gani Tabora? Tazengwa, Lusu, Uyumbu, Kazaroho, , Uyowa au Izimbiri? Hali halisi ya Wakulima wa Tumbaku ninaijua manake Familia yetu ni wakulima wa Tumbaku. Please tell the truth and shame the devil. Ukweli ni kwamba Muungwana ameona umaarufu wake unashuka kwa style ya Free-fall ndiyo maana amekuja na style ya kuongea na wananchi kwa njia ya TV(ambayo nadhani haikuwa na mafanikio) na sasa anawatumia makada wake kwa nguvu kumuuza kwa Watanzania".
"

Longo longo. Dola inayumba hiyo inaeleweka. Maisha ni utatuzi wa matatizo.
 
Last edited:
Ndugu Zawadi, Waingereza wanasema "Dont re-invent the wheeel". Yaani gurudumu lilishagunduliwa zamani kwa nini kama unataka kutengeneza gari model yako uanze tena kugundua gurudumu lingine? Kuna kampuni zamani ilijulikana kama Steadman(sasa hivi imenunuliwa na kubadili jina) imekuwa ikifanya utafiti mara kwa mara na juzi juzi imetoa matokeo yanayoonyesha kwamba ingawa Kikwete bado ana mvuto kwa wapiga kura Tanzania lakini mvuto huo umeshuka chini kulinganisha na mwaka 2005 na sababu za kupungua zimetolewa.

"Steadman" wana utaalam wa hali ya juu kuliko JF na Magazeti ambayo unataka wafanye utafiti yaani "they should re-invent the wheel!" kama Zawadi alivyofanya ingawa hana utaalam katika mambo ya research. Tena kumbuka kwamba katika kutafiti kuna kitu kinaitwa "incumbency factor" kinachangia sana katika kuongeza mvuto wa Rais aliye madarakani kwa wakati huo. Hata Idd Amini kule Uganda alikuwa na mvuto kwa Waganda akiwa madarakani lakini JWTZ walipomtimua toka Kampala wananchi walikesha wakisherekea kwa kucheza ngoma!
 
Ndugu Zawadi, Waingereza wanasema "Dont re-invent the wheeel". Yaani gurudumu lilishagunduliwa zamani kwa nini kama unataka kutengeneza gari model yako uanze tena kugundua gurudumu lingine? Kuna kampuni zamani ilijulikana kama Steadman(sasa hivi imenunuliwa na kubadili jina) imekuwa ikifanya utafiti mara kwa mara na juzi juzi imetoa matokeo yanayoonyesha kwamba ingawa Kikwete bado ana mvuto kwa wapiga kura Tanzania lakini mvuto huo umeshuka chini kulinganisha na mwaka 2005 na sababu za kupungua zimetolewa.

"Steadman" wana utaalam wa hali ya juu kuliko JF na Magazeti ambayo unataka wafanye utafiti yaani "they should re-invent the wheel!" kama Zawadi alivyofanya ingawa hana utaalam katika mambo ya research. Tena kumbuka kwamba katika kutafiti kuna kitu kinaitwa "incumbency factor" kinachangia sana katika kuongeza mvuto wa Rais aliye madarakani kwa wakati huo. Hata Idd Amini kule Uganda alikuwa na mvuto kwa Waganda akiwa madarakani lakini JWTZ walipomtimua toka Kampala wananchi walikesha wakisherekea kwa kucheza ngoma!
Nashukuru kwa maelezo yako. Lakini upungufu mkubwa katika habari yako ni kutotoa namba. Kwa sababu hata kutoka 80% mpaka 75% bado ni kushuka lakini vilevile nibado juu. Kwasababu rais ana hitaji 51% tu ya kura. Si unakumbuka Mkapa alipita kwa 52%.

Hivyo jaribu kuwa specific, hasa ukizingatia kuwa shirika lilotoa hizo habari kama ulivyoeleza lina uzoefu. Tupe hizo kwanza ili tulinganishe na zile nyingine tulizonazo.
 
Zawadi Ngoda, molimoli mkwamisi: Nakumbuka hoja yako ya jana, naona umeachana nayo kabisa leo. Hata hivyo nimekupata vizuri, bila shaka unatokea kitengo cha Tabwe Hiza pale Lumumba. Mkuu njaa njaa ziangalie sana, zitatupeleka pabaya.
Kazi kwelikweli. Tujifunze kujiamini na kusema ukweli bila woga. Maisha yetu hayamilikiwi na mtu awaye yote. Kujipiga bei chee kwa mtu kama ndo njia ya kutokea, sio tu ni kujidharirisha, bali pia ni kupoteza thamani yetu bila sababu. Utawala huu, kama tawala nyingine zote, utakuja na kwenda na watakaobaki salama ni wale waliosimamia ukweli bila kujiingiza kwenye siasa za kuendekeza njaa. Na kubwa kuliko yote, hii ni nchi yetu. Tukiibomoa, tunajibomoa wenyewe.
 
Zawadi,

Mimi nataka kukuuliza kwenye mambo ya takwimu. Sijui hizi takwimu umechukuliaje,
- Kwenye hizi chaguzi bado watu wanaoishi vijijini wenywewe wanapiga kura tuu ilimradi mtu amepata khanga, au sukari kwa umaskini au kudanganywa na ahadi - hii yote ni kukosekana kwa Elimu ya Uraia.

- Katiba, kwenye hili nikuwa hapa kuna vitu vingi, kutangaza mshindi ambapo unakutana na wizi wa kura ilimradi Serikali inayotawala ikitaka atangazwe anatangazwa tena kwa ulinzi mkali hata muda mwingine kura zikiwa zinakusanywa vituoni.

Kama nchi yetu tungekuwa na uwanja wa Demokrasia bila hivi vitu vya vurugu hapo ndo ungesema kuwa takwimu ni sahihi zinazotangazwa, vinginevyo kama Katiba haitabadilishwa, na Elimu ya Uraia kutolewa hakuna Demokrasia na takwimu zitakuwa ni kupaka poda mshindi.
 
Ukweli ni kwamba JMK hapingiki wala hatetereki uchaguzi ujao, Rais, kama atakuwa hai, na InshaAllah atakuwa hai na Mwenyeezi Mungu ampe maisha marefu. Amin.

Hakuna Rais yeyote katika Tanzania aliyepita kabla ya JMK, aliyefanya mambo anayoyafanya JMK. Kwa hilo nampa pongezi.

Hata humu ndani ya ukumbi kila anaempinga JMK analeta upupu tu na hana kamili la kumponda. Mimi nna challenge aanzishe mtu mada ya kusema hili JMK hakulifanya inavyotakiwa na anioneshe Rais gani wa Tanzania kabla yake kalifanya! Nakuhakikishieni hakuna anaeweza kuja na hata moja, labda upupu tu.

Ahsante JMK, wenye macho na masikio, tunaona na tunasikia unavyopambana na adui Ujinga, Maradhi, Umaskini, Ubadhirifu, na mengine mengi. Heko na shukrani zangu za dhati kwako.
 
Ukweli ni kwamba JMK hapingiki wala hatetereki uchaguzi ujao, Rais, kama atakuwa hai, na InshaAllah atakuwa hai na Mwenyeezi Mungu ampe maisha marefu. Amin.

Hakuna Rais yeyote katika Tanzania aliyepita kabla ya JMK, aliyefanya mambo anayoyafanya JMK. Kwa hilo nampa pongezi.

Hata humu ndani ya ukumbi kila anaempinga JMK analeta upupu tu na hana kamili la kumponda. Mimi nna challenge aanzishe mtu mada ya kusema hili JMK hakulifanya inavyotakiwa na anioneshe Rais gani wa Tanzania kabla yake kalifanya! Nakuhakikishieni hakuna anaeweza kuja na hata moja, labda upupu tu.

Ahsante JMK, wenye macho na masikio, tunaona na tunasikia unavyopambana na adui Ujinga, Maradhi, Umaskini, Ubadhirifu, na mengine mengi. Heko na shukrani zangu za dhati kwako.

Kweli tabasamu la JK limewapofusha watu! Usemi pekee wa JK kwamba anashindwa kuelewa kwa nini TZ ni maskini inatosha kum-disqualify, tukiacha ahadi zake nyingi hewa na mbwembwe zake za "maisha bora kwa kila mtz"! Angejuaje wakati yuko busy na safari za majuu! Kasi yake mpya ya kupambana na ufisadi imeishia pale alipodai kuwa mzee BWM "aachwe apumzike" kwa kazi nzito ya kufanya biashara ikulu!
 
Zawadi,

Mimi nataka kukuuliza kwenye mambo ya takwimu. Sijui hizi takwimu umechukuliaje,
- Kwenye hizi chaguzi bado watu wanaoishi vijijini wenywewe wanapiga kura tuu ilimradi mtu amepata khanga, au sukari kwa umaskini au kudanganywa na ahadi - hii yote ni kukosekana kwa Elimu ya Uraia.

- Katiba, kwenye hili nikuwa hapa kuna vitu vingi, kutangaza mshindi ambapo unakutana na wizi wa kura ilimradi Serikali inayotawala ikitaka atangazwe anatangazwa tena kwa ulinzi mkali hata muda mwingine kura zikiwa zinakusanywa vituoni.

Kama nchi yetu tungekuwa na uwanja wa Demokrasia bila hivi vitu vya vurugu hapo ndo ungesema kuwa takwimu ni sahihi zinazotangazwa, vinginevyo kama Katiba haitabadilishwa, na Elimu ya Uraia kutolewa hakuna Demokrasia na takwimu zitakuwa ni kupaka poda mshindi.
Ndugu zanguni, msione vyaelea, vimeundwa. Wengi wanapozungumzia Demokrasia, picha zao zipo ulaya nchi ambazo zimechukua miaka zaidi ya 300 kujenga Demokrasia ukilinganisha na ya kwetu miaka 15. Jamani ujenzi wa Demokrasia ni mgumu kuliko kitu chochote kile.

Hao watu wa vijijini unaowasema wanahaki haki ya kupiga kura kama wewe. Kama ni kanga au sukari mimi sijui, lakini mbona wenzetu wa Pemba pamoja na sukari bado wanachagua kilicho moyoni mwao. Uchaguzi wenyewe ni wasiri, inamzuia nini mtu kuchukua kanga na kuchagua CUF au CHADEMA? Kwa maoni yangu hao watu hayajawafika shingoni, au hawaoni kuwa wanateseka kama unavyowaona wewe. Inawezekana vile vile kuwa hawana uchaguzi mwingine, kwa sababu ukienda vijiji vingi hata hivyo vyama maarufu vya upinzani kama CUF na CHADEMA hawavijui kabisa. Ukiacha huko kaskazini, maeneo mengi ya kati na kusini (vijijini) CCM iligombea viti vya wabunge na madiwani bila kuwa na mgombea wa upinzani. Ndugu zanguni tuangalieni vigezo vyote kabla hatukilalamikia chama tawala. Kama hatukukubali mapungufu ya vyama vya upinzani basi kamwe hatutaweza kuvisaidia, na vinaweza kufa kitu ambacho ni hatari sana.

Niandikieni nchi kumi za Afrika, (toka Misri mpaka Naijeria, Ethiopia mpaka Zambia, Aljeria mpaka Ghana, Msumbiji mpaka Gambia n.k) ambazo zilifanya uchaguzi bila kulalamikia matokeo kuwa mshindi ni mwizi wa kura. Jamani tusidanganyane, hakuna. Na hapo ndipo utapokubaliana nami kuwa ujenzi wa Demokrasia ni safari ndefu ya machozi na uvumilivu mkubwa.

Katiba ni mbovu, lakini tunahitaji wabunge wengi wa upinzani. Tunarudi katika square 0.
 
Unaweza ukajitahidi kum-bomoa mtu kumbe ndio unajenga na kumpandisha chati...!

Uhuru huu haukuwepo enzi zile za Musa (Julius) na che Mkapa, thanx God... watu wanazungumza sasa.
 
Kweli tabasamu la JK limewapofusha watu! Usemi pekee wa JK kwamba anashindwa kuelewa kwa nini TZ ni maskini inatosha kum-disqualify, tukiacha ahadi zake nyingi hewa na mbwembwe zake za "maisha bora kwa kila mtz"! Angejuaje wakati yuko busy na safari za majuu! Kasi yake mpya ya kupambana na ufisadi imeishia pale alipodai kuwa mzee BWM "aachwe apumzike" kwa kazi nzito ya kufanya biashara ikulu!
Ndugu yangu mkono mtupu haulambwi! Tabasam peke yake bila vitendo halisaidii hata kidogo. Tuacheni uongo Rais Kikwete kafanya kazi. Nitakuorodheshea baadhi ya matatizo sugu yaliyokera sana wananchi katika maeneo mbalimbali.

Ujambazi ni tatizo lililokuwa linatukosesha usingizi kabisa hasa sisi wakazi wa Dar. Sijui mwenzangu unaishi wapi, lakini wakati alipoipokea nchi toka kwa Mkapa hali ilikuwa mbaya sana. Maana ule ulikuwa sio ujambazi bali ni vita, maana wakikuingilia wewe ni kukaa tu na kuwaachia wachuke vitu vyao. Ukweli tulikuwa hatulali. Hilo amefanikiwa sana na akipewa miaka mingine 5 nfikiri atalitokomeza kabisa.

Ajali za barabarani zimepungua sana, na zinaendelea kupungua siku hata siku. Unaweza kufikiri hili ni dogo, lakini pale unapoondokewa na mke wako, wazazi wako ndio utaelewa nini maana ya kupunguza ajali za barabarani.

Parking za magari zimeimarishwa, hata kuzunguka soko la Kariakoo wamachinga wote wamefukuzwa na tumepata Parking.

Wamachinga kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu, kwa kujengewa masoko nje ya kongo na kariakoo. Na si kujengewa tu bali vile vile kuwahamasisha kuhamia huko. Kwa tulioshuhudia tuliona kuwa kazi haikuwa rahisi, maana ilikuwa ni vita.

Halmashauri za miji kuthibitiwa ipasavyo katika matumizi na mapato. Na kwa uhakika ukusanyaji wa mapato ya kodi yameongezeka karibu kwa kila Halmashauri.

Ununuzi wa mazao ya hifadhi ya taifa umeongezeka kwa mara tatu. Hii ni muhimu sana, ili tupatapo matatizo ya njaa tuache kukimbila Marekani na Ulaya.

Uhuru wa vyombo vya habari. Hapa sina haja ya kufafanua maana nyie wenyewe ndio matunda yake mnayaona. Na kwa kuongeza tu, mwaka jana alipongezwa na mabalozi wa nchi za nje akiwemo balozi wa Marekani na Ujerumani kwa kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari. Kazi hii ilimshinda Mkapa.

SACCOS zimeimarika na zinawanachama wengi sana kwa kipindi kifupi. Sasa hivi kila pembe utayopita ni SACCOS, na huku ndiko kushirikisha wananchi katika uchumi

Hayo ni machache tu kuyataja na bado sijaingia upande wa kilimo.

N.B Muundo wowote wa uchumi usioshirikisha wananchi hautafanikiwa. Na hapo ndipo Kikwete anapojitahidi kupafikia, Njia yake si rahisi lakini tutafika tu.
 
Ndugu yangu mkono mtupu haulambwi! Tabasam peke yake bila vitendo halisaidii hata kidogo. Tuacheni uongo Rais Kikwete kafanya kazi. Nitakuorodheshea baadhi ya matatizo sugu yaliyokera sana wananchi katika maeneo mbalimbali.

.......

N.B Muundo wowote wa uchumi usioshirikisha wananchi hautafanikiwa. Na hapo ndipo Kikwete anapojitahidi kupafikia, Njia yake si rahisi lakini tutafika tu.

Hayo ya kutaka kuibadili Tanzania kuwa nchi ya kiislam tu ndiyo yanakufanya upaaze sauti hapa na kuimba ngonjera za kumpongeza Kikwete.
 
Unaweza ukajitahidi kum-bomoa mtu kumbe ndio unajenga na kumpandisha chati...!

Uhuru huu haukuwepo enzi zile za Musa (Julius) na che Mkapa, thanx God... watu wanazungumza sasa.

Naona kwa makusudi umemvuka mzee mwinyi ambaye wakati wake kina Stan Katabalo walikufa kwa vifo vya kutatanisha...

mkemia mkuu wa serikali na wenzake waliofuatilia ile skendo ya vyakula vibovu vilivyoletwa nchini na ............. jina unalifahamu vyema.
 
Ukweli ni kwamba JMK hapingiki wala hatetereki uchaguzi ujao, Rais, kama atakuwa hai, na InshaAllah atakuwa hai na Mwenyeezi Mungu ampe maisha marefu. Amin.

Hakuna Rais yeyote katika Tanzania aliyepita kabla ya JMK, aliyefanya mambo anayoyafanya JMK. Kwa hilo nampa pongezi.

Kweli kabisa, hakuna raisi anayekumbatia mafisadi kama Kikwete. Pongezi zako naona zinatokana na uamuzi wa Kikwete wa kutaka kuiingiza nchi ya Tanzania kwenye jumuiya ya kiislam mara baada ya uchaguzi mkuu.

Hata humu ndani ya ukumbi kila anaempinga JMK analeta upupu tu na hana kamili la kumponda. Mimi nna challenge aanzishe mtu mada ya kusema hili JMK hakulifanya inavyotakiwa na anioneshe Rais gani wa Tanzania kabla yake kalifanya! Nakuhakikishieni hakuna anaeweza kuja na hata moja, labda upupu tu.

Ahsante JMK, wenye macho na masikio, tunaona na tunasikia unavyopambana na adui Ujinga, Maradhi, Umaskini, Ubadhirifu, na mengine mengi. Heko na shukrani zangu za dhati kwako.

Upupu ni wako wa kutosoma yote yaliyoandikwa kuhusu Kikwete hapa.
 
Shukran kwa maoni yako. Lakini ni vyema kama ungeiangalia shilingi kwa pande zote mbili, na si kwa mapenzi ya moyo kama ushabiki wa mpira.

Ukweli ni kwamba, wananchi si kama wanamuona Kikwete kama Raisi aliyewatimizia yote, bali wananchi hawawaamini wanasiasa. Na kwa maana hii, hawana imani kuwa kama watambadili na kuuweka upinzani ndio mambo yao yatakuwa mazuri. Maana Zimwi likujualo halikuli likakwisha.

CHADEMA ni moja kati ya vyama vilivyopata heshima sana nchini Tanzania. Lakini tukio la hivi karibuni la kumtoa katika kinyanganyiro cha uenyekiti, mbunge maarufu Zitto Kabwe kimeishushia hadi sana chama hicho. Na wananchi wanajiuliza hivi tukiwapa Urais watawezaje kugawana post za Uwaziri na nyinginezo. Hivi hawa wapo pamoja au wanatuhadaa tu.


Watanzania mpaka leo si watu wa kuchukua Risk kubwa kiasi hicho. Kwa hili wengi tutakubaliana.

Katika utafiti wangu nilioufanya safari hii wananchii hawakubaliani na zimwi likujualo ,ndio maana umethibitisha mwenyewe nini kimewatokea viongozi wa CCM kwenye maeneo ambayo chaguzi zilikofanyika,uthubutu wao wa kukemea na kuzomea na hata kuhoji huwezi kuniambia kwamba watakubaliana na ujinga wa zimwi likujualo ukweli ni kwamba sasa hivi wako kwenye pilikapilika za kuhakikisha kwamba kanga na fulana zitakazoletwa na ccm zitatutumika kama vitanzi kuhakikisha wanawanyonga CCM wataki tena mashara,ya kuwawapa wachumia tumbo wanaoneemesha mmatumbo yao ya ndigu zao na watoto wao,

Angalia vilio vya vijana waliomaliza vyuo wengine digrii moja wengine mbili hakuna kazi na hakuna juhudi zozote za makusudi kuhakikisha hali hiyo haitokei,angalia miji inavyojaa maji ,uchafu,na hata umaskini uliotukuka hata hapa Dar es Salaam munaposema wanakusanya asilimia 70 ya pato la taifa
Hakika propaganda zako haziwezi tena kupenya kwa wananchi si ni hao wananchi wanaokataa kuridhika na serikali ya CCM kipimo halisi ni vipindi vinavyorusha na TBC radio na TBC1 television utaona walivyoamuka nina uhakika safari hii hawatachagua mafisadi

Tunakwambia mwambie rafiki yako Mheshimiwa Raisi Jakaya kachemsha au amefulia watu walimuamini sana na kwa uzoefu wa kukaa serikalini miaka alfulela na ulela hakika alikuwa ni jibu lakini kawavunja moyo wananchi wa vijijini hastaili kabisa kupewa kipindi cha pili acha tumpate mwingine naye ajaribu
Matukio katika chaguzi ya vyama huwa yanatokea katika vyama vyote na ndio maana CCM wakimaliza vituko vyao kwenye chaguzi na manyanyaso wanayopeana huwa wanaombana na radhi na kushawishiana kuvunja makundi ya Chadema kwa maoni yangu ilikuwa danganya toto ukilinganisha na ya CCM uchaguzi wa vijana,wanawake,wazazi,na sasa kimbuka kinachotimuka kwenye CC
Kama ulivyosema hapo juu Watanzania wa leo sio wa jana subiri utaona
 
Jamani jamani hivi tatizo liko wapi?..
Zawadi kafanya uchunguzi wake na katuletea hapa matokeo imekuwa nongwa kwa baadhi ya watu kwa sababu tu Zawadi kazungunmzia waraka wa kanisa!..

yaani hapa JF imekuwa kijiwe cha udini mtupu kila anayeandika kitu huchunguzwa kwanza dini yake... Na yaonyesha wazi kwamba kuna chuki kubwa sana kwa JK kwa sababu tu ni Muislaam wla sii swala la uongozi wake tena. Hitimisho hili litatugawa hata hapa JF, nimeambiwa siku nyingi sana kuhusu hali halisi ya JF sikutaka kuamini lakini sasa imefikia wakati nikubali ukweli... ama kweli Miafrika Ndivyo Tulivyo..
 
"

Ongezeko la tumbaku: RUVUMA, toka tani milioni 1.5 mwaka 2007 hadi tani milioni 3 mwaka 2008. Tabora ongezeko la asilmia 40 toka mwaka 2007 hadi 2008. Tazama shirika la takwimu au TAT. Sina maelezo zaidi. Tafadhali nipe takwimu zako, tuache hizi longo longo.

Longo longo. Dola inayumba hiyo inaeleweka. Maisha i utatuzi wa matatizo.

Kuongezeka uzalishaji wa Tumbaku hakuna maana kuongezeka kwa kipato cha watu. Nitakupa mfano rahisi, Tanzania sasa hivi ni nchi ya tatu kwa uzalishaji wa dhahabu Africa lakini bado madini yanachangia less tahn 3% kwenye uchumi wa Taifa. Madini yanazidiwa na Pombe ambayo inachangia around 4.6% kwenye GDP. Wakulima vijijini wako desperate na wakati mwingine hawajui kukokotoa faida halisi ya ukulima wao.

Mwaka 2008, nilifanya kazi kubwa sana kumzuia mama yangu asiendelee kulima Tumbaku. Nilifanikiwa tu pale nilipompigia hesabu kuonyesha net profit ni Tsh, 29,000 kwa mwaka mzima ndipo alipokubaliana na mimi. Wakulima wanaibiwa kwenye madeni, tumbaku yao huchelewa kununua mpaka ipoteze ile moisture content inayotakiwa na kuwa nyepesi kama karatasi. Kisha hao Matajiri wakienda kuiprocess Morogoro wanaihifadhi na ku-replenish moisture iliyopotea. Vilevile wakulima hukopeshwa magunia kwa gharama ileile kila mwaka hata kama magunia hayo ni makuu kuu. Kwenye upande wa Tumbaku bado mambo si mazuri kabisa. Hapo bado sijazungumzia mambo ya madaraja. Mtafute Classifier mmoja umdadisi atakueleza kinachoendelea katika mambo ya ununuzi wa Tumbaku.

Kwa hiyo suala siyo Takwimu ya kinachozalishwa bali ni nini mkulima anapata.
Dola inayumba kwa sababu hatuna sera za kuiendeleza nchi. kutatua tatizo ni kuondoa mzizi wa tatizo na siyo kukata matawi. na hapa mzizi wa matatizo ya nchi yetu ni sera za sisiemu.
 
Ukisoma JF na magazeti mengine unaweza kudhani kwamba, mwaka 2010 Kikwete hawezi kuambulia hata 20% ya kura za watanzania. Lakini hali halisi nchini ni nyingine kabisa. Nimetembelea Mwanza, Lindi,Tabora, Ruvuma, Dodoma, Dar es Salaam na baadhi ya vijiji na kupata picha halisi.

Nimetembelea vijiji sita, na nikajaribu kueleza jinsi Kikwete alivyowaangusha wakulima kwa ahadi hewa. Vijiji vya Tabora na Ruvuma, walinieleza kuwa wao ni wakulima wa Tumbaku na toka Kikwete aingie madarakani wamesikilizwa sana kwa kuwabana wawekezaji katika eneo hilo. Aidha wale wa Ruvuma walifurahia kuona mwaka jana zao hilo liliongezeka mara mbili, na kila mmoja alihisi tofauti katika mfuko wake. Hali kama hiyo nilielezwa na wananchi wa Tabora. Kifupi katika mikoa yote nilipata majibu ya kuonyesha wanaimani na Rais Kikwete.

.

Zawadi soma sehemu ya article iliyokuwa presented kwenye panel ya WHO-Durban, the devil is in the red font:-

African farmers turn backs on tobacco Kerry Cullinan
November 21 2008 at 09:55AM
Most African farmers grow tobacco because they are poor and lack alternative ways to earn a living, but with encouragement, many Tanzanian farmers are giving the killer crop the cold-shoulder.

This is according to Lutgard Kagaruki, from the Tanzania Tobacco Control Forum, who addressed a panel at the World Health Organisation's tobacco control conference in Durban this week.

Tanzania is the second biggest grower of tobacco in Africa after Malawi, but many tobacco farmers were "enslaved in permanent debt to the tobacco companies" and wanted to get out, said Kagaruki.

"The tobacco companies give subsidies and loans for them to buy fertiliser, chemicals (pesticides) and seed.

"But then they under-grade the crops and set low prices. The farmers can't repay the loans and find themselves enslaved in permanent debt bondage," said Kagaruki.

The 80 000 tobacco farmers in Tanzania earned an estimated US$1 (R10) a day, she added.

In addition, three-quarters of the farmers smoked and suffered from the respiratory sicknesses and cancer associated with smoking.

The TTCF started to organise among tobacco farmers in the Namtambo district, encouraging them rather to grow food by pointing out that at least they could eat their crops when they faced hard times.

"In October 2006 there were 22 300 tobacco farmers in the district, but a year later there were only 6 333," said Kagaruki.

"They have started growing simsim (sesame seeds) and sunflowers and groundnuts, and they are very happy. They call me on my cellphone and tell me how well they are doing," she added.

While tobacco is Tanzania's second biggest foreign exchange earner, bringing about $55,5-million into the country in 2003/4, one of the country's cancer institutes, the Ocean Road Cancer Institute, reported spending $30-million treating smoking-related cancers during the same period.

("This article was originally published on page 5 of The Star on November 21, 2008 ")


Zawadi, ukitaka kujua usanii wa JK na serikali yake soma paragraph hii hapa chini ambayo nimeitoa kwenye Daily News ya 16 Sept 2009 ikielezea kauli ya Mkuu wa wilaya ya Serengeti:

"He described the report as misleading, calling farmers to continue co-operating with the Morogoro-based tobacco firm, in developing tobacco growing in the district. He warned farmers against smuggling tobacco to the neighbouring Kenya via 'panya' routes, saying that those who would be caught doing so will be taken to task"

Unafikiri kwanini Wakulima wanauza Tumbaku yao Kenya?? Au wakulima wa Kahawa Kalinzi wanauza Kahawa yao Burundi hata kama serikali inakataza? Au Karafuu inauzwa Kenya kinyemela??


My take: 2010 Campaign zimeanza rasmi lakini zamu hii muungwana atakuwa na hali ngumu sana labda kitakachomsaidia ni TUME YA UCHAGUZI kwa kuwa ni yake na Dola (polisi). Kinachowatesa wakulima wengi ni ukosefu wa elimu hivyo wanaangalia gross income badala ya net profit.
 
Back
Top Bottom