Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,783
- 1,822
Ukisoma JF na magazeti mengine unaweza kudhani kwamba, mwaka 2010 Kikwete hawezi kuambulia hata 20% ya kura za watanzania. Lakini hali halisi nchini ni nyingine kabisa. Nimetembelea Mwanza, Lindi,Tabora, Ruvuma, Dodoma, Dar es Salaam na baadhi ya vijiji na kupata picha halisi.
Nimetembelea vijiji sita, na nikajaribu kueleza jinsi Kikwete alivyowaangusha wakulima kwa ahadi hewa. Vijiji vya Tabora na Ruvuma, walinieleza kuwa wao ni wakulima wa Tumbaku na toka Kikwete aingie madarakani wamesikilizwa sana kwa kuwabana wawekezaji katika eneo hilo. Aidha wale wa Ruvuma walifurahia kuona mwaka jana zao hilo liliongezeka mara mbili, na kila mmoja alihisi tofauti katika mfuko wake. Hali kama hiyo nilielezwa na wananchi wa Tabora. Kifupi katika mikoa yote nilipata majibu ya kuonyesha wanaimani na Rais Kikwete.
Maeneo ya mijini kulikuwa na majibu mchanganyiko. Kuna ambao hawakujali ni nini amefanya, wao cha muhimu ni chama wanachokishabikia.Kundi hili lilifanya kama asilimia 30. Kuna wengine ambao ni zaidi ya 40% ambao wao hawakufikiria kuwa kubadili chama ni jibu. Wakitoa mfano wa Kenya, Zambia na Malawi na kusema wanamarafiki wengi wanatoka huko na kueleza hakuna mabadiliko yeyote yale kwa mwananchi wa kawaida kiuchumi. Wakithibitisha hayo na kusema, ona wakenya wanakimbilia nchi yetu kama sisi tutakavyo kwenda Ulaya. Mmoja wao alisema "Braza si unasikia kila siku polisi wanakamata Waithiopia, wasomali na wanaijeria". Kama hapa pabaya kwanini waje, Kikwete wetu ni mtoto wa mjini. Katufungulia wamachinga masoko." Hapo sikuwa na neno.
Huwezi kuamini Kule kijijini nilipoendelea kuleta longo longo kidogo nipigwe, ilibidi nikubaliane nao. Na nilipojaribu kuwauliza kama wanafikiriaje ule waraka wa Kanisa katoliki? Ukweli hawajapata kusikia kitu kama hicho. Nilikuwa nao mkononi waraka huo, na nilijaribu kuwasomea. Hata pragraf moja sikumaliza, kabla sijanyamazishwa na mmoja na kuungwa mkono na wote. "Unajua hayo mambo ya kwenye makaratasi sasa hivi sisi hatuangalii, tunachoangalia ni kama tunapata fedha ya kusomeshea wanetu na pesa kidogo kidogo ya kununu dawa. Haya mambo ya Ufisadi tumeyasikia toka enzi ya fagio la chuma, sijui nani alikuwa Rais." Walinijibu hivyo, na nilikuwa mtiifu nikijua kuwa niliepuka mkong'oto dakika chache zilizopita. Mara moja nikaukunja waraka wa Pengo na kuuweka mfukoni kwa haraka sana.
Nikiwa hapo Magomeni nilipozungumzia waraka wa Kichungaji kuelekea uchaguzi 2010, nao walinibeza na kusema du hata kanisa nalo linataka kura ill lile. Hapa nikafahamu kuwa waraka unaweza kumpa umaarufu zaidi Kikwete kuliko walivyodhania. Sikuweza kuamini vipi anaweza kuwa maarufu licha ya kutolewa mabomu mengi ya ufisadi. Ni nini hasa mwananchi wa kawaida anapima uongozi bora. Hivi magazeti na JF yawezekana kuwa hawajui wananchi watakacho? Nikapigwa na Bumbuwazi!
Amini usiamini umaarufu wa Kikwete upo juu sana kuliko aonekanavyo magazetini na katika JF. Ningeviomba vyombo vya habari (magazeti na jf) kuchukua statistic angalau kwa watu laki moja na kuhakikisha haya nisemayo. Cha kuzingatia ni kutochukua hiko kipima joto katika mtandao, badala yake waende kwa wananchi, wapiga kura. Nasema hivi kwasababu kwenye mtandao wengi wapo ughaibuni, hivyo si wapiga kura active.
Nimetembelea vijiji sita, na nikajaribu kueleza jinsi Kikwete alivyowaangusha wakulima kwa ahadi hewa. Vijiji vya Tabora na Ruvuma, walinieleza kuwa wao ni wakulima wa Tumbaku na toka Kikwete aingie madarakani wamesikilizwa sana kwa kuwabana wawekezaji katika eneo hilo. Aidha wale wa Ruvuma walifurahia kuona mwaka jana zao hilo liliongezeka mara mbili, na kila mmoja alihisi tofauti katika mfuko wake. Hali kama hiyo nilielezwa na wananchi wa Tabora. Kifupi katika mikoa yote nilipata majibu ya kuonyesha wanaimani na Rais Kikwete.
Maeneo ya mijini kulikuwa na majibu mchanganyiko. Kuna ambao hawakujali ni nini amefanya, wao cha muhimu ni chama wanachokishabikia.Kundi hili lilifanya kama asilimia 30. Kuna wengine ambao ni zaidi ya 40% ambao wao hawakufikiria kuwa kubadili chama ni jibu. Wakitoa mfano wa Kenya, Zambia na Malawi na kusema wanamarafiki wengi wanatoka huko na kueleza hakuna mabadiliko yeyote yale kwa mwananchi wa kawaida kiuchumi. Wakithibitisha hayo na kusema, ona wakenya wanakimbilia nchi yetu kama sisi tutakavyo kwenda Ulaya. Mmoja wao alisema "Braza si unasikia kila siku polisi wanakamata Waithiopia, wasomali na wanaijeria". Kama hapa pabaya kwanini waje, Kikwete wetu ni mtoto wa mjini. Katufungulia wamachinga masoko." Hapo sikuwa na neno.
Huwezi kuamini Kule kijijini nilipoendelea kuleta longo longo kidogo nipigwe, ilibidi nikubaliane nao. Na nilipojaribu kuwauliza kama wanafikiriaje ule waraka wa Kanisa katoliki? Ukweli hawajapata kusikia kitu kama hicho. Nilikuwa nao mkononi waraka huo, na nilijaribu kuwasomea. Hata pragraf moja sikumaliza, kabla sijanyamazishwa na mmoja na kuungwa mkono na wote. "Unajua hayo mambo ya kwenye makaratasi sasa hivi sisi hatuangalii, tunachoangalia ni kama tunapata fedha ya kusomeshea wanetu na pesa kidogo kidogo ya kununu dawa. Haya mambo ya Ufisadi tumeyasikia toka enzi ya fagio la chuma, sijui nani alikuwa Rais." Walinijibu hivyo, na nilikuwa mtiifu nikijua kuwa niliepuka mkong'oto dakika chache zilizopita. Mara moja nikaukunja waraka wa Pengo na kuuweka mfukoni kwa haraka sana.
Nikiwa hapo Magomeni nilipozungumzia waraka wa Kichungaji kuelekea uchaguzi 2010, nao walinibeza na kusema du hata kanisa nalo linataka kura ill lile. Hapa nikafahamu kuwa waraka unaweza kumpa umaarufu zaidi Kikwete kuliko walivyodhania. Sikuweza kuamini vipi anaweza kuwa maarufu licha ya kutolewa mabomu mengi ya ufisadi. Ni nini hasa mwananchi wa kawaida anapima uongozi bora. Hivi magazeti na JF yawezekana kuwa hawajui wananchi watakacho? Nikapigwa na Bumbuwazi!
Amini usiamini umaarufu wa Kikwete upo juu sana kuliko aonekanavyo magazetini na katika JF. Ningeviomba vyombo vya habari (magazeti na jf) kuchukua statistic angalau kwa watu laki moja na kuhakikisha haya nisemayo. Cha kuzingatia ni kutochukua hiko kipima joto katika mtandao, badala yake waende kwa wananchi, wapiga kura. Nasema hivi kwasababu kwenye mtandao wengi wapo ughaibuni, hivyo si wapiga kura active.