Ukimya wangu!

Weeeeee.....

JF hatupo doro,tunang'aa kama mji wa moro
Kwa sauti nyororo,za wadada waso na vihoro
Unahitaji supu ya kongoro,uchangamke usiwe sharobaroTumkaribishe zinduna,Kwa matarumbeta na vicheko.

hahahahahaa! umeniacha hoi
 
Wallahi wanikumbusha, nyanya yangu kijakazi
alikuwa na maneno matamu, hakuna mfanowe
kama utamu wa halua, achia mbali wa tende
tenda wema wende zako, usingoje shukurani

Sublaheri Bwana!

Mbona unatutomasa, unatutia hamasa
kwa mambo haya ya sasa, shairi tulishasusa
kisa cha wewe kukosa, kimegeuka mkasa,
umefungua kurasa, kwa shairi bila visa,
Lugha yako ya msasa, imefungua vitasa,
Nakupongeza!
 
Back
Top Bottom