Baada ya kufukuzwa kazi kaka yagu alitembea na mke wangu mpaka kumzalisha

george aloyce

JF-Expert Member
Aug 22, 2017
1,177
1,823
Na. Mwanaume Story

Wakati naoa, nilikuwa na kazi yangu nzuri tu lakini kama unavyojua maisha yalinipiga, nikaondoka kipindi cha vyeti feki. Katika kuhangaika, niliamua kuhamia kwa kaka yangu, akanipa chumba cha nje nyumbani kwake, lakini karibu kila kitu mimi na mke wangu tulikuwa tunafanyia kwa kaka, yeye pia kaoa mke wake alikuwa ni mtu mzuri tu.

Anajali, hana ile manyanyaso ya shemeji, nilijipanga nikapata pesa ya chumba lakini kila nikitaka kuondoka mke wangu ananiambia kwa nini tusikae hapa mpaka kujipanga vizuri, kwa nini tusikee hapa sijui mpaka vipi. Kushangaa ana mimba ndiyo nikaona kweli bora kukaa kwa kaka sababu sijajiandaa vizuri, lakini katika kujifungua kaka alimhudumia sana mke wangu.

Ila kuna kitu nilishangaa mtoto alifanana sana na kaka kiasi kwamba nilikuwa na wasiwasi, lakini kwa sababu ni ndugu ingawa hatujafanana nilikaa kimya nakujipa moto hakuna kitu. Siku moja nashika simu ya mke wangu SMS inaingia, kwa kawaida sipendi kusoma SMS zake, ila hiyo ilinivutia imeandikwa, ‘Nimekuambia hicho cheti kingine choma moto mume wako akijua mimi nawafukuza wote.

Nikalazimika kuingia kuangalia, ndipo nakuta mke wangu wanagombana na kaka yangu baada ya mke kumuambia ana vyeti viwili vya kliniki. Kumbe alikuwa na mahusiano na kaka yangu na ndiyo kambembelesha mimba, nilipomuuliza aliniomba msamaha lakini nilishindwa nifanye nini?

Kuongea na kaka alinijibu kwa dharau, unakula na kunywa kwangu ulitegemea nini? Hakuna kitu cha bure mke wako kalipia au ulitaka ulipie wewe!” Sikujibu kitu niliondoka na kumuacha mke wangu pale huu ni mwaka wa 8 sijarudi tena nyumbani kila mtu anajua nimetelekeza familia lakini kila nikiwaza kuhusu kurudi nyumbani nashindwa.

Mama yangu alifariki dunia mwaka jana, nilishindwa hata kumzika, niko mjini napambana sijajipata. Huwezi amini mke wangu bado anaishi kwa kaka na kikubwa kaka anadai kuwa anamsaidia kwa sababu mimi nimetelekeza ila ukweli ni mke wake na mimi nipo tu nahangaika na maisha!

1702437943612.jpg
 
Ndugu kama ni huyo hameni hapo upesi sana mje mkae kwangu nitawapa nyumba ya vyumba viwili na usijali kuhusu kazi nitakutafutia kazi uwe usafiri na magari yangu mikoani kama Manager.

Mkuu msiendelee kukaa hapo kwa huyo dhalimu mkuu nikucheki inbox kwa mawasiliano ya karibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom