Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,802
- 71,229
Hakuna majibu bora kama haya. Lakini kwa vile wapo watu hawatumii akili zao Bali ushabiki wataendelea kuzoza.Safi sana nilijua ni lazima Lowassa atajwe na waabudu mizimu. Hivi wewe na wenzako mje mtuambie Lowassa alipata faida kiasi gani kwa sakata la Richmond na ama alilipwa kiasi gani au washirika wake walilipwa kiasi gani? Halafu huu umajunun wa kuugeuzia ukweli mgongo mtaacha lini?
Mitambo ya Richmond iko Pale Ubungo inatumiwa na Symbion kuiuzia Tanesco umeme, sasa tatizo la Lowassa na Richmond ni nini? Kama uharamu ni mitambo mbona mnaitumia, kama tatizo ni Lowassa mbona hamsemi msimamo wa aliyekuwa bosi wake, yaani Kikwete ulikuwa nini? Hivi Richmond na Escrow-Tegeta, Aggreko na mauza uza mengine kipi hasa kina ushahidi ulio wazi?
Hao hao Stanbic waliikopesha serikali ilipe hela za Escrow na zile hela kuna ushahidi wa wazi kabisa kwamba ziliibwa kimfumo, leo kufikishwa kwa mkwe wa Lowassa imekuwa nongwa, kwamba hapo Lowassa anahusika. Mbona Mwanaisha alipofeli hamkusema kama baba yake anahusika?
Pale Morogoro Lissu alipotamka hadharani kuwa mwenye Richmond ni JK (na alisema hayo JK akiwa bado Rais) wenye akili tulijua mchezo umefika mwisho, kwamba kama Lissu anaropoka basi kwa vile serikali inaujua ukweli Lowasa amekwisha. Lakini kama Lissu alisemalo ni kweli basi yatakayofuata ni maigizo tuu.
Na kweli, JK akiwa Mwanza kufunga kampeni akajibu kwa utani jambo kubwa kama hilo eti Richmond ni ya huyo anayetembea na Lissu. Hapo kila mtu akaelewa kumbe ya Lissu yana ukweli