Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

May be those who blames the teacher were not attending or they came late!
So you be first when the papers will be given tommorrow!
the national cake is for all and dont ever cry while it is too early!
 
At least hao wote ni Watanzania!

Wait until July 01st 2010 when 'Soko la Pamoja' la EAC litakapoanza... ndipo itakapojulikana kwamba huo ni mbuyu au ubuyu...

For now kwenye mashirika na taasisi 'that matter' watu wa HR wengi wao wanatoka nji fudodo...

What will happen when they are allowed to employ their kith and kins?

I'd bet my life that this discussion will be different this time next year, only that it will have little bearing in changing the reality on the ground.

Mlenge
 
mi naona katika hayo makabila wengi wao wamesoma ndio maana unawaona wako wengi maofisini. so solution elimu sawa kwa wote ndio iwe kampeni
 
najua hii topiki haitokuwa poplar na baadhi ya watu humu ndani na hata wenye website lakini potelea mbali

je ni kweli wizara hizo zimejaa makabila ya wachagga,wanyakyusa na wahaya?

Mimi nilikuwa siamini mpaka pale nilipo ambiwa kuwa kuna ukabila wa hali ya juuu kule ikulu na vile vile namba mbili kwa ukabila ni tra je kuna ukweli katika haya?

Japo kuna watu wanasema kuwa ni udini lakini sumu ambayo hatuko tayari hata kuijadili ni hii ya ukabila na ndio inayoturudisha nyuma je mnakubaliana nayo?




-jambo forums where we dare talk openly


umesahau watu wa kanda ya ziwa pale ikulu wajita,sukuma, haya, kurya na zanaki ila ikulu wajita ndo kibao almost 78%
 
umesahau - usalama wa taifa na tume ya taifa ya mawasiliano - wakulya kibao....
 
.sijawahi kusikia kibaka mchagga ingawa najua wapo...
Wapo kibao best ila si unajua wakikamatwa tu wenzao wanawawahisha kwao Moshi. Nenda gereza kuu la Karanga -Moshi ndo utaamini wengi walikamatwa Dar au Mz na A-town na ni juzi tu hapa Nairobi jamaa wawili wakenya walikamatwa kwa wizi wa gari wakamtaja mwenzao aliyekimbia kwa jina la Chuwa nadhani kinaChuwa mnjua watokeako. Anyways back tu the main topic kuhusu makabila ikulu sina uhakika na kwa mawaziri naona namba yao kidogo ni kubwa ila tukubali kanda ya ziwa ina majimbo mengi ya uchaguzi ila sikatai hilo. Kuhusu askari ni kweli kina Mura ni weengi ila kama ujuavyo shule si saaaaana ndo maana wengi wanastaafu before 45.
Kuhusu dini km wengine walivyochangia nadhani huyu jamaa alipokuwa anaingia madarakani alitaka kufanya hivyo lakini kama mnavyojua usalama wa taifa nadhani walimshauri.

Ila kuhusu TRA na Benki nyingine best kina Massawe ni wengi lakini tuangalie kama kweli wamezisomea kazi hizo na kama wamezisomea basi wanastahili. Nadhani hata ndugu zetu wakina IWE wa kanyigo wengi ni waalimu wa shule za msingi so mazingira yanachangia sana!
 
Kwa Namna fulani kuna Ukweli katika hili. Mimi ninaomfano Mzuri wa mtu aliyesoma kisha akapata wadhifa serikalini lakini akapigwa majungu bila sababu ya msingi akaachishwa kazi.
 
Tunaweza kucheza na maneno tunavyotaka,hata tukasema ukabila hauko kwa sababu alizotoa hapo juu. Tanaweza kuona hata yeye anakubali kwamba ukabila upo ila, anasema umehalalishwa na historia!
Ebu tuone mwanakijiji anasema historia imejenga ukabila,kwa hiyo ni sawa.
Anasema ukichukua hatua za kupinga au kusahihisha mabaya ya historia utajenga ubaguzi! Lo, mwanakijiji kweli,lakini historia ilituletea ukoloni wa wazungu na walikuwa wamesoma sana,Tuliwakataa tukajaza nafasi zao hata kwa watu wasioukuwa wamesoma kiasi cha kufaa kuchukuwa nafasi zao.kwa maana moja tu kwamba tulikuwa tunaondoa mabaya ya historia.
Hata ndani ya taifa letu historia ilitengeneza mabaya,nayo ni kuwanyima waandali ,wanyaturu,wamakonde elimu hivyo kuwafanya kutoweza kushirika katika uongozi na hata uchumi wa Taifa lao kama wengine.

Nakumbuka wakati Mwalimu alipoliona hilo alichukuwa kwa makusudi hatua za kurekebisha hali hiyo.kwa mfano kwenye miaka ya sitini marks za kujiunga na shule za sekondari zilitofautiana toka mkoa hadi mkoa ili kumwezesha kijana wa kimasai aliyepata marks 60 kupata nafasi na hata kumwacha mjita aliyepata marks 70.Kwa mantiki ya mwana kijiji huu ulikuwa ubaguzi mbaya sana.
Lakini nia ya mwalimu ilikuwa kujenga utaifa ili wote tujione ni wamoja.Angeweza kuendelea kuwatumia tu wachaga ,wanyakyusa, wahaya nk kwa sababu walitosha kushika utawala na uongozi wa nchi kwa sababu walisoma.Wakati huo hata mwananchi asiyekuwa na elimu hata ya darasa la saba aliruhusiwa kuwa mbunge,na sio sasa. Kwa nini na wasomi walikuwepo!

Mwanakiji wakati mwingine unazungumza kisomi na nadharia za kisomi hata unashindwa kuona mambo mdogo.
pAMOJA NA USOMI WAKO NATAKA NIKUAMBIE HIVI,bado tuajenga kitaifa hiki kichanga,hiki unachokiita taifa ni mrundikano tu wa vikabila,tuahitaji hekima na busara kuviunganisha vikabila 127 ili viwe nation.Jinsi tunavyo fikiri ndicho kitu muhimu. Huwezi kusema hakuna haja ya mwaandali kufanya kazi ikulu kwa sababu kuna wanyakyusa wamesom wanatosha.Ni kwamba waandali wanataka kujisikia na kujiona ni sehemu ya uongozi na utawala wa nchi na watajiona tu kama watawaona waandali nao wako hizo sehemu.

Ebu tutoe mfano hata kama kabila x wamependelewa na historia na wamesoma saana kwa hali ya leo itakuwa ni ubaguzi tu utakaosababisha kabila x wawe 35 kati ya nafasi 40 maana yake ni kwamba kabila moja kati ya makabila 127 wana ajira 35 kati ya 40, mwanakiji anasema tukisema huu ni ukabila anasema tuna ubaguzi.
Tuwe wakweli tujenge taifa kwa utaifa,siyo kwa historia maana hata katika historia sisi si Taifa,kabila langu lililokuwa chini ya Chifu wetu Mirambo ndilo lililokuwa taifa langu!! True history of our nations,sasa Tujenge taifa toka hapo.
Wakabila wameshangilia sana lakini, hii mada si dili chochote ni too defensive.
Mwenye akili yeyote hawezi kusimamaq kwenye jukwaa akatetea kifua mbele hali hii. Please makabila 124 ni wengi mno kuliko makabila 3 nk.
Tujenge Taifa.
 
unajua mtu usipojua historia yako.. kuna hatari ya kujaribu kuiandika upya! Ili kuelewa hapa tulipo sometimes we have to look back where we are coming from. Historia yetu haikuanza jana au juzi (kama baadhi wanavyotaka tuamini) matatizo tuliyonayo leo hayakuanza jana (isipokuwa haya ya kina Richmonduli!) lakini mengi yana msingi toka huko nyuma. Binafsi, nitashtuka zaidi kama kwenye nafasi fulani kwenye taasisi kumejaa Wakerewe, Wanyali, au Watindiga.. kwa sababu hakuna jibu zuri la kihistoria linaloweza kuonesha kujaa huko!!

La maana ni kuongeza jitihada ili baadaye hali ielekee uwiano kwani Waha na Wamang'ati na wenyewe watakuwa na shule nyingi na wanapata nafasi nyingi za kusoma.. kwani hata hivi sasa bado Uchagani, Mbeya n.k wanaendelea kuwa na shule nyingi na zenye kutoa wanafunzi wengi (angalia matokeo ya hivi karibuni!)..

Do we need some kind of affirmative action which would not be translated as reverse discrimination?
Asante san kwa michango yako yote na siku zote huwa naomba Mungu Akusaidie na akupe Uzima Daima Asante sana juu ya yote
 
Elimu inaweza kuwa kigezo lakini sidhani kama ni wao pekee waliosoma hivyo mpaka wakawa wengi na kwa nini wawe kundi moja mahali pamoja yaani wachaga TRA etc
 
tuipendenchiyetu, karibu na tunafurahi kuwa umeweza hatimaye kuamua kuchangia badala ya kuwa mtazamaji tu.

a. Katika maendeleo yote ya elimu hadi hivi sasa, Makabila hayo yamerudi nyuma au yameendelea mbele?

b. Ili kuweza kufikia uwiano, je tuamue kuyafunga breki, kwa mfano kusitisha kwa miaka mitano kuchukua wanafunzi wa elimu ya juu toka makabila hayo?

c. Tukiamua kufanya hivyo, tuhakikishe kuwa hawaendi kusoma nje ya nchi pia kwa muda huo?

d. Je, tunapopokea CV ya mtu au kumchagua mtu tukiona jina la "Kagaruki", "Mwakipesile" au "Lyimo" tuwaengue moja kwa moja?

e. Kwenye ofisi ambazo zimejaa watu wa makabila hayo tuzipangue na kuwaaingiza watu wa makabila mengine ilimradi isionekane wamejaa watu wa kabila moja?

f. Tukishaanza kufanya hivyo na tukagundua kuwa watu warefu ndio wengi zaidi, tuanze kuhakikisha watu wafupi nao wanaingizwa? tukifanya hivyo tukagundua kuwa wengi wanaofanya kazi maofisini wanatumia mikono ya kulia, tuanze kutafuta watumiaji wa mikono ya kushoto? na tukimaliza hivyo na kugundua kuwa wengi waliojariwa ni wanaume, tuwapunguze ili tuongeze wanawake? Tukishamaliza hivyo na kugundua kuwa wanawake wengi waliojariwa ni waislamu, tuwaombe wastaafu ili wawapishe wakristu? tukifanya hivyo na kugundua kuwa wakristo hao wengi ni wakatoliki tuwatake wawamegee nafasi hizo waprotestanti?.. ni jinsi gani tutasitisha zoezi hilo la kibaguzi?

Mkuu dhambi ya ubaguzi ni kama moto wa kiangazi, huanza na jani moja kavu then utaendelea na kumaliza hekari nyingi za misitu.
 
Swala hapa linalojadiliwa ni fulani kapata fulani kakosa, aliyekosa ndo anaanza kutafuta sababu za kwanini huyu apate na mimi nikose. Kuna vijana wangu kibao ninaowajua wapo TRA na wote ni makabila tofauti, tulipomaliza chuo wao waliomba na kupata na mimi nilikosa.
Baadae nilipata BoT bila ya kupitia mtu yeyote, nimefika nikakuta Kabila langu wapo hapa na kwa bahati nzuri au mbaya hamna ninayefahamiana naye, tumekuja kujuana hapa hapa. Ila kwa sababu tupo wengi utaambiwa UKABILA. jamani mnataka upewe kazi hata bila kuomba? Nafasi zikitangazwa msisite kutuma maombi yenu kwa kuogopa ukabila.
 
Nadhani suala kupata taarifa ndio la msingi.Wanasema "information is Power". Sasa kwa kuwa hayo makabila yapo kule kwa sababu za kihistoria, jamaa zao wanawahi kupata taarifamapema za nafasi za kazi hivyo kuwa na nafasi nzuri ya kushiriki katika kinyang'anyiro.

Huo si ukabila ila ni advantage.
 
kilichochangia mpaka haya makabila matatu yawe niyawasomi ni kwa sababu yawaingereza waliwatawala na kuanzisha shule na nakufunguwa makanisa ndiyo maana haya makabila unakuta wengi niwakristo ,alafu mikowa yao inashule nyingi .kwa hiyo usishangae kuwakuta sekta kama hizo
 
Kwa kawaida ukishakuwa na Umri Mkubwa unakuwa umeona mambo mengi sana.
Mimi nina Umri wa kutosha sasa.
Naomba ni kanushe kuwa maeneo yote yaliyotajwa hayana Ukabila.
Wafanyakazi walioko pale wako kwa ajili ya elimu zao.
Kama umesoma na unafiti kwenye Fani lazima utapewa kazi.
Ukiuliza hapo utaambiwa wachaga wengi wako Ikulu, TRA, BOT n.k
Wote hao wamesoma Shule ndiyo Maana wako pale.
Watu wanaolalamikia Ukabila ni wale ambao hawakusoma na kama wamesoma sehemu kubwa wametawaliwa na majungu.
Kabila la Wahaya lilikuwa likisakamwa kwa kuwa na ukabila lakini si kweli, Wahaya ni watu wanaopenda sana kusoma na kujiendeleza Ndiyo maana Wanakuwa sehemu muhimu za kazi kwa ajili ya Uwezo walio nao.
Ukabila tanzania hauko kabisa.
Mzee Varisanga uko sahihi kabisa! wakati mwingine woga tu unamkosesha mtu ajira kwa kuogopa kuomba kazi mahali fulani akiamini kuwa kwa vile yeye si wa kabila fulani basi hawezi kupata kazi.
 
unajua mtu usipojua historia yako.. kuna hatari ya kujaribu kuiandika upya! Ili kuelewa hapa tulipo sometimes we have to look back where we are coming from. Historia yetu haikuanza jana au juzi (kama baadhi wanavyotaka tuamini) matatizo tuliyonayo leo hayakuanza jana (isipokuwa haya ya kina Richmonduli!) lakini mengi yana msingi toka huko nyuma. Binafsi, nitashtuka zaidi kama kwenye nafasi fulani kwenye taasisi kumejaa Wakerewe, Wanyali, au Watindiga.. kwa sababu hakuna jibu zuri la kihistoria linaloweza kuonesha kujaa huko!!

La maana ni kuongeza jitihada ili baadaye hali ielekee uwiano kwani Waha na Wamang'ati na wenyewe watakuwa na shule nyingi na wanapata nafasi nyingi za kusoma.. kwani hata hivi sasa bado Uchagani, Mbeya n.k wanaendelea kuwa na shule nyingi na zenye kutoa wanafunzi wengi (angalia matokeo ya hivi karibuni!)..

Do we need some kind of affirmative action which would not be translated as reverse discrimination?

Kwanza nitakugongea THANKS mara baada ya kuandika vijisentensi viwili vitatu hapa.Majibu uliyoyatoa kwa kweli ni ya msingi sana na kwa kuwa ndugu yetu hameshindwa kutoa uthibitisho juu ya madai yake basi suala zima linakuwa kama ni uzushi!

Ombi langu mimi ni moja tu,yaani watu wanapoleta hoja kama hizi za ukabila na nini au hoja yoyote ile,tusiwakatishe tamaa kwa kuwaambia kuwa haina maana au hakuna jipya hapo.Dawa yake ni kama ulofanya Mwanakijiji...unasumbuka kidogo halafu unamwaga maukweli basi inakuwa mwanzo na mwisho.Ikiwezakana ku-quote some old posts well and good...kama ni kumwandikia tena hoja za msingi aendelee kuzichambua na iwe mwanzo na mwisho wa kuleta madai mepesi mepesi.

Mwanakijiji wewe ni mkali sana....THANKS!
 
Sijui kama ni bwana au bibie lakini mwana JF Samvulachole naamini utakuwa umeenda shule na kama umeenda shule unaweza ukawa historia ya mwenendo mzima wa elimu hapa. Namaanisha kuwa unajua elimu imeanzia wapi na ni sehemu gani watu wamesoma kwa wingi kiasi ambacho mtu anaona aibu kwa sasa hivi mtoto wake akiishia darasa la saba. Vile vile unajua ni wapi watu hawajali elimu bali wanajali kuozesha watoto wao mapema kwa ajili ya mahari na wengine wakachunge mifugo yao. Kwa kifupi mahali utakapoona kuna makabila matatu uliyotaja hapo juu yanaongoza kwa namba ya wafanyakazi ujue ni elimu imewapeleka hapo. Hata kama kutakuwepo na kaupendeleo naamini huyo mtu atakuwa ankiji haja zote za kuwa kwenye position aliyo nayo. Unataka tule usawa wa makabila kazini bila kuangalia kiwango cha elimu. Kama hivyo wachukuliwe hata wagema mnazi. TULIA wacha mapepe.
 
Wanajamii, kukataa kuwa hayo maeneo yaliyotajwa hayana ukabila ni sawa na kukataa kuwa Tanzania kuna rushwa na ufisadi, pengine turekebishe kidogo hiyo kauli kwa kuwa inaonekana kuwakera baadhi ya watu ambao aidha makabila yao ndiyo yapo maeneo hayo au na wao ndugu zao wapo huko. Nadhani kwa faida ya kupunguza jazba tuseme kuwa maeneo yale kazi zinapatikana kwa kujuana sana kuliko 'merit'. Yaani kujuana ni 'added advantage' unapokuwa na 'merit'. Haiwezekani hao watu wawe wamesoma kuliko kabila jingine 'NJI' hii, haya makabila madogo pia yanao watu ambao wamesoma vizuri lakini kwapo maeneo hayo mara nyingi ni kwa bahati mbaya tu. Yaani hawa unakuta wamesoma hadi unaona haya kuwakosesha ajira.

Tusikatae ukweli. Kwa taarifa zenu mnaobisha haya ni matunda ya mfumo ambao tumeuzaa na kuulea, hii ndiyo reflection ya jamii tuliyonayo. Sasa hivi si serikalini wala private sector kote ngoma droo, nenda Vodacom ukajionee standard seven na form four wanalivyopewa rungu kuwaongoza magraduates wenye uwezo. Vodacom nimechukulia kama mfano lakini kote hali ndivyo ilivyo. "Let us call a spade a spade and not a spoon"
 
Back
Top Bottom