singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,484
- 8,343
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO CHAKE
MWANDISHI: SINGANOJR
GENRE: FICTION (KUBUNI )
........................….........................................
UTANGULIZI
.....................................................
Damiani mhitimu wa chuo kikuu cha uhasibu , anahitimu masomo yake na kurudi kijijini kwao kwa ajili ya kusubiria upepo wa ajira lakini katika hali ya kutokutegemea mama yake kipenzi anapigwa risasi mbili za kifuani na kufa hapo hapo na hio inatokana na kumpatia msaada mwanaume ambae hamfahamu mwenye asili ya ulaya (mzungu ) ambae na yeye alikuwa kwenye hatua ya mwisho ya kupoteza uhai wake kwani alikuwa na jeraha la risasi tumboni ,lakini mzungu huyo kabla ya kupoteza maisha anamkabidhi damiani nyaraka bila kumpa maelekezo ya aina yoyote ile .
Damiani anajikuta anajenga chuki na kisasi kwa watu waliohusika na mauaji ya mama yake , anajiapiza kuwatafuta mahali popote pale na kulipiza kisasi , katika harakati za kuwatafuta wabaya wake anajikuta akifahamu siri nzito iliokuwa nyuma ya kifo cha ghafla cha raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , anapata waraka ulioachwa na raisi huyo uliopewa jina la KAULI YA MWISHO YA RAIS KABLA YA KIFO CHAKE .
JE UNAFIKIRI ATAFANIKIWA KULIPIZA KISASI CHAKE ?
JE NI KAULI GANI YA MWISHO ALIO ACHA MHESHIMIWA RAISII KABLA YA KIFO CHAKE ?.
.
Damiani ni kijana wa miaka ishirini na mbili mhitimu wa chuo kikuu cha TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) akiwa amechukua kozi ya Finance and accounting in public sector(kozi inayohusu maswala ya uhasibu) , mara baada ya damiani kumaliza masomo yake hakutaka kubaki ndani ya jiji la dar es salaam , kwani hakuwa na kazi maalumu ambayo ingemuwezesha kujiingizia kipato ndani ya jiji hilo , pia maisha ndani ya jiji hilo yalikuwa ni ghali sana na yalikuwa yakihitaji pesa ili kuweza kuishi .
Hivyo mara baada tu ya kumaliza masomo yake aliamua kurudi nyumbni kwao kijijini mkoani Tanga kwa ajili ya kusikilizia upepo wa ajira kwani mwaka ambao alikuwa amemaliza haikuwa kama miaka ya nyuma kwamba ukimaliza tu unasubiria matokeo na kupata ajira , kinyume chake ni kwamba utasubiria matokeo yatoke na kuomba ajira kwa makampuni ambayo yatakuwa na uhitaji ama serikari pale itakapo tangaza nafasi za ajira na kuomba , na kwakuwa kipindi hicho kulikuwa na wimbi kubwa la vijana ambao walikuwa ni wahitimu na hawakuwa na ajira mtaani hivyo ilikuwa ni ngumu sana kupata ajira , ilikuwa ni kama kubahatisha tu pale nafasi zinapo toka kwani wengi waombaji wana sifa zinazofanana .
Mkuzi ndio kijijini kwa kijana damiani , kijiji hiki kilikuwa ndani ya wilaya lushoto kilomita kadhaa kutoka lushoto mjini , yaani kama utasafiri kwa gari ni muda wa dakika therathini mpaka arobaimi kufika ndani ya kijiji hichi , ni moja ya vijiji ambavyo vilikuwa vimezungukwa na misitu na kuwa na mazingira ya kuvutia sana , na yalikuwa ni moja ya mazingira ambayo watalii wengi wa mataifa ya nje na hata watalii wa ndani pia walikuwa wakipenda kutembelea na hio yote ni kutokana na hali yake ya hewa ilivyokuwa safi na ya kuvutia .
Basi kijana damiani ndani ya kijiji cha mkuzi ndio alikulia na kujipatia elimu yake ya msingi na sekondary .
Damiani alikuwa ni kijana mpole mcheshi mrefu maji ya kunde mwenye sura yake ya kuchongoka lakini ilioumbwa vizuri , alikuwa ni moja ya vijana walio kuwa na miili mikubwa ya wastani , Damiani alikuwa akiishi na mama yake tu kwani baba yake alikuwa amekwisha kufariki miaka mingi nyuma kipindi akiwa tu na umri wa miaka kumi .
Kurudi kwa damiani kijijini baada ya kumaliza masomo ilikuwa ni moja ya furaha kubwa sana kwa mama yake kumuona mwanae kurudi ndani ya kijiji hicho , kwani mama huyo alikuwa akimpenda sana mwanae .
" karibu sana mwanangu " mama alifurahia sana kwa mwanae kumaliza masomo yake ya ngazi ya juu , na kujihisi kuwa mwanamke aliefanikiwa kulea kwani watoto wengi ndani ya kijiji hicho hawakufanikiwa kufika ngazi ya juu ya kielimu kama ilivyokuwa kwa damiani .
" Asante mama , hatimae nimemaliza chuo na nimerudi rasmi " aliongea damiani huku akiachia tabasamu huku nje watoto wengi walikuwa wakimwangalia na kumshangaa , hio ilikuwa ni kawaida sana kwa vijiji kushangaa watu walio tokea mjini na hata kwa wageni pia .
Basi damiani alikaribishwa vizuri na mama yake katika nyumba yao hio ya vyumba vitatu ilio ezekwa kwa samora , na kwakuwa damiani alikuwa na chumba chake tokea akiwa shuleni ndiko mama yake alipeleka begi lake na kukifanyia usafi .
Maisha ya kijana damiani yanaanza rasmi ndani ya kijiji cha mkuzi , licha ya damiani kuwepo ndani ya kijiji hicho lakini alikuwa na mipango mikubwa sana ya maisha yake hapo mbeleni , kwani alihitaji kuja kuwa mfanya biashara mkubwa sana katika maisha yake na hio ilikuwa ndio moja ya ndoto yake kubwa, japo alikuwa amesoma na alikuwa akitarajia kuwajiriwa lakini ajira kwake haikuwa kipaumbele , ila kipaumbele kwake ikikuwa nikupata mtaji utakoa mwezesha kuanzisha biashara , hakika alikuwa na safari ndefu sana na hata kwa yeye pia alilijua hilo na hivyo kwa umri aliokuwa nao hakuwa na sababu ya kukatishwa tamaa na mazingira aliokuwemo na aliokulia , kwani alichokuwa akikiamiani katika maisha yake ni juu ya uchapaji kazi kwa bidiii na kutokukata tamaa na kuwa na malengo ndio nguzo kubwa sana ya kuja kufanikiwa , hakutaka kabisa kukatishwa tamaa na hali ya maisha yao ya umasikini yaliopo hapo nyumbani , ila aliamini katika mawazo chanya tu .
Basi hatimae wiki ,mwezi na hata miezi ilikatika na matokeo yake yalikuwa yamekwisha kutoka na akiwa amefaulu kwa ufaulu wa daraja la kwanza , kwake na kwa mama yake ilikuwa ni furaha na faraja kubwa sana , kwani aliamini kupitia ufaululu mkubwa basi angeweza kumrahisishia kupata kazi kwa wepesi zaidi .
Hakutaka kusafiri mpaka dar es salaam kwa ajili ya kuomba kazi ilihali kulikuwa na njia rahisi , alichokifanya yeye ni kutuma maombi kwa kila kampuni ambayo iljkuwa ikitangaza nafasi za ajira kwa njia ya mtandao .
Mwezi wa kwanza uliisha kijana damiani akiwa amekosa kabisa uelekeo wa ajira kwani ni makampuni zaidi ya matatu ambayo alikuwa ameomba kwa ajili ya kupata ajira lakini amekosa hata wito wa interview( mahojiano ya kiufanisi ) , zikiwa zimepita siku kadhaa za kijana damiani kukata tamaa hatimae kwenye moja ya kampuni ambayo haikuwa imetoa majibu ilirudisha jibu kwa kijana damiani kwa ajili ya kuhudhuria interview .
ilikuwa ji moja ya kampuni ilio kuwa ikipatikana ndani ya jiji la dar es salaam ,kampuni moja ya usafirishaji iliokuwa na makao yake makuu ndani ya posta , kwake damiani alifurahia kwani aliona tumaini la kupata ajira linaridhisha zaidi , alimwambia mama yake juu ya taarifa hio na mama yake pia alifurahia na kumpa baraka zote mwanae kwa ajili ya kuhudhuria interview hio.
Ilikuwa ni siku ya jumatatu ndio siku ambayo kijana damiani alikuwa ndani ya basi akielekea jijini dar kwa ajili ya kuhudhiria interview ,alifanya maombi juu ya safari yake hio na kusudio lake analoliendea kulifanyia kazi.
Kutoka lushoto mpaka ndani ya jiji la dar ni umbali wa masaa sita mpaka saba , hivyo damiani alikuja kufika ndani ya jiji hilo kwenye muda wa saa nane kamili mchana ,siku hio alipanga akifika ndani ya jiji hilo kwakuwa hakuwa na ndugu wa kufikia , alipanga kwenda kwa rafiki yake mmoja aliekuwa amemuacha ndani ya chuo akiendelea na masomo kwa ajili ya kumuhifadhi mpaka siku inayofuata afanye interview na kisha ageuze kurudi nyumbani .
Basi baada tu ya kushuka ndani ya basi akijisogeza mpaka kwenye daladala zinazoelekea mbagala na kisha alipanda huku malengo yake aje ashukie mtongani kwa azizi ally kwani hapo ndio rafiki yake huyo alipokuwa akipatikana kwa kuishi , barabara haikuwa na foleni sana hivyo hawakuchukua masaa mengi kufika sehemu aliokuwa amekusudia .
Mara baada tu ya kushushwa hatimae alinyoosha moja kwa moja upande wa kushoto wa barabara , huku akipita vichochoro viwili vitatu na kuja kutokelezea mbele ya nyumba moja kubwa iliokuwa na ukuta, Hatimae alisimama nje ya geti la nyumba hio huku nikama ni mtu aliekuwa akijishauri agonge ama asigonge , ila kwakuwa kilichomleta hapo ni kuonana na rafiki yake na rafiki yake alikuwa akiishi ndani ya nyumba hio basi hakuwa na budi ya kugonga geti hilo.
Haikuchukua muda mrefu hatimae alikuwa amefunguliwa na msichana mmoja aliekuwa amejifunga khanga moja , na alionekana alikuwa akifua kwani alikuwa na mapovu mikononi .
" Karibu " sauti hio nyororo ilimkaribisha ndani huku.dada huyo akitangulia mbele na kumuacha kijana damiani kumsanifu mdada huyo kwa nyuma , alikuwa ni mlimbwende kweli aliekuwa amejaliwa umbo zuri haswa la kumvutia kila mwanaume atakae mtia machoni , alikuwa mrefu wa wastani mwenye rangi yake ya chocolate , alibarikiwa uso wa duara na kwa tathimini za haraka haraka mdada huyo alionekana umri wake haukuwa si chini ya miaka ishirini kwenda juu.
" nimemkuta elvisi ??"
" katoka sema anakuja muda si mrefu , wewe ndio Damiani ??"
" Ndio ni mimi "
" " Okey ! Alinipa maelekezo yako kwamba ukifika nikukaribishe ndani " aliongea msichana huyo huku akimkaribisha damiani ndani kwani muda wote huo alikuwa amesimama , Damiani alijua lazima huyo bidada atakuwa hawara(mwanamke anaeishi na mwanaume pasipo kuolewa au mpenzi ) wake elvis maana alimjua mngoni huyo songea kwa kupenda warembo hakuwa nyuma na ndio maana kabla ya kutoka nyumbani alimtaarifu kuwa atakuja kulala kwake .
Basi bidada huyo alimuongoza damiani ndani ya nyumba hio iliokuwa imepakwa rangi nyeupe mpaka kwenye chumba cha katikati upande kushoto na kisha alimkaribisha ndani , kilikuwa ni chumba kimoja kikubwa saizi ya kati kilichokuwa kimejaa makorokocho mengi , Damiani alikuwa akikijua chumba hichi sana kwani hata kwa baadhi ya vitu hivyo villkuwa vyake na ni baada ya yeye kumaliza masomo alimuuzia rafiki yake huyo .
Basi baada ya kukaribishwa dada yule alitoka nje na kuendelea na shughuri yake ya ufuaji huku akimwacha damiani akimsubiri rafiki yake , na haikuchukuwa hata dakika isbirini rafiki yake elvisi aliingia ndani ya nyumba hio , elvisi alifurahia sana kumuona damiani na hata kwa damiani ilikuwa ni hivyo hivyo , wote walifurahia kuonana kwa mara nyingine .
" karibu sana HB asietaka warembo " aliongea elvis akionesha kumtania mwenzie na kwa damiani kwakuwa alikuwa ashamzoea rafiki yake huyo kwa matani basi na yeye alicheka .
" mzee wa totozi , naona shemeji yangu wa awamu hii ni shida "
" Yaani acha tu mzee toto la toto na isitoshe limedata na ndio limenifanya nihangaike siku ya leo "
" Unahangaishwa na nini sasa?? "
" hahaha lazima kuhangaika , unajua jana ulivyonicheki unakuja ilikuwa ghafra sana na sikutaka kukwambia naishi na mtoto wa kike, kwa hio unavyoniona hapa kuna msela nimetoka kumpanga ili ukale mbonji kwake ukamilishe mambo yako maana hapa sikuwa na jinsi "
" Daah ! hapo ndio maana nakukubali mshikaji wangu "
" hahaha .. usijali mzee si unajua hata wewe umenisaidia mara kibao , hata mavitu haya ni kama ulinipa tu kutokana na bei ile "
Basi damiani walichukuana na rafiki yake na kutoka eneo hilo kuelekea barabarani na kupanda magari ya kuelekea Rangi tatu , walivyo fika mbagala zakhemu walishuka na kuchukua upande wa kushoto barabara , umbali wa mita kadhaa hatimae waliingia chochoro ambayo walikuja kuibukia mbele mtaa mwingine , na wakaja kutokea mbele ya kanisa la KKKT na hapo walipinda kushoto tena na kukuta nyumba moja kubwa iliokuwa na geti na kwa nje ilisomeka kwa maandishi ya lodge , elvis alisukuma mlango na kisha aliingia ndani , kwa damiani yeye alikuwa akifatisha tu kuona mwisho wake kwani kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kaletwa lodge
" Oya mshikaji anakaa hapa , sio lodge hapa tena japo ilikuwa lodge , mwenye nyumba kaamua kuifanya nyumba ya kupangisha " aliongea elvis na kumfanya Damiani aelewe , walipita kwenye vyumba kadhaa na hatimae walisimama nje ya mlango na elvisi aligonga na nusu dakika mlango ilifunguliwa na jamaa mmoja wa makamo mfupi mwenye mwili mkubwa wa kibonge .
" Karibuni "
Waliingia ndani ya chumba hicho , kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri sana , na pia hata kitanda na samani(furniture) zilizokuwemo humo ndani zilionesha jamaa anaeishi humo ndani hakuwa mnyonge kipesa .
" oyaa huyu ni joshua rafiki yangu sana mwaka wa kwanza hivyo ndio utachili hapa kwake mpaka utakapo kamilisha mambo yako " aliongea elvis na joshua alimkaribisha Damiani na elvisi aliaga akaondoka .
Basi siku nyingine iliingia ambayo ni siku Damiani alikuwa akielekea mtaa wa posta kwa ajili ya kufanya interview , alikuwa amevaa akapendeza maana kwenye nguo alikuwa nazo na mkopo ulimsaidia sana kipindi akiwa chuo .
Alijisogeza mpaka barabarani ili kusubiria gari ya kwenda stesheni posta apande , ila mara baada ya kufika tu kwenye barabara nje kabisa ya supermarkert iliosomeka kwa jina la Kivoni , ilisimama gari moja aina ya vanguard nyeusi na kioo kilishushwa na akaonekana bwana mmoja wa makamo , makadirio ya miaka 30 kuendelea mweusi alivalia shati jeupe na koti akiwa na miwani , Damiani wakati huo gari hio ikisimama alikuwa akiiangalia na hata jamaa huyo alivyoshusha kioo alikuwa pia akimwangalia , Damiani alijikuta akijishtukia na hio ni mara baada ya jamaa huyo kumuonesha ishara ya kumuita , alijihakikishia kama ndio yeye aliekuwa akiitwa na hapo ndipo alipo piga hatua kulisogelea gari hilo
INAENDELEA HIVI PUNDE ........
SEHEMU YA 02.
INAENDELEA
“Vipi wapi unaelekea ?”. aliuliza mwanaume yule
" Naelekea posta "
" Okey ingia twende , naelekea upande huo , nina baadhi ya maswal nataka nikuulize " aliongea jamaa yule na kumfanya hata damiani ashangae inakuwaje mtu asie mjua awe na maswali ya kuulizwa na yeye ,jambo hilo lilimpa mashaka mengi juu ya mtu huyo .
" fanya haraka , ingia acha uoga asubuhi yote hii unawaza mambo mabaya " aliongea yule jamaa na ni kama alijua ni kitu gani alikuwa akimaanisha na Damiani kwa mashaka mengi alijiingiza kwenye gari hilo na kisha likawashwa na kuondoshwa eneo hilo .
" Unaenda kufanya interview ?" aliuliza yule bwana na kumfanya damiani ashangae Zaidi ni kivipi kajua anaenda kufanya interview .
" usiwe na wasiwasi mimi nimeishi miaka mingi na najua hulka ya vijana wengi hasa wanaoenda kuomba kazi na wewe kwa uvaaji wako unaonekana kabisa unaenda kufanya interview kama sio kuomba kazi .”
" Yeah! naenda kufanya interview " alijibu
" umesomea kozi gani na elimu yako ni kiwango gani ?? "
" Degree of finance and accounting in public sector"
" okey safi na hongera , unapaswa kujiamini tu na maswali ya kawaida sana wanauliza , unaweza ulizwa elfu kumi ina mnyama gani na ukakuta swali lina maksi nyingi "
Aliongea yule bwana huku akiongeza umakini katika barabara hio iliokuwa na magari mengi asubuhi hio .
Hawakuchukua muda mrefu walikuwa posta , na gari ilisimamishwa kwenye jengo la waterfront na Damiani akashuka , huku bado akiwa na dukuduku la maswali mengi kichwani mwake kwa jamaa yule kwa jinsi alivyomwambia wakati wa kumpandisha kwenye gari kwamba alikuwa na maswali ya kumuuliza , lakini cha kushangaza hata hayo maswali yenyewe hakuulizwa , ila hakutaka kufikiria sana na aliona ni labda jamaa huyo hakuwa na nia ya kumuuliza maswali ila alikuwa akitaka tu kumsaidia kwa kumpa lift na kama alivyosema alijua kuwa alikuwa akielekea kwenye interview .
Basi wakati akiwa anatembnea kuelekea upande wa samora alijikuta akikumbuka yale maneno ya kwamba anaweza kuulizwa maswali ya kawaida sana hata elfu kumi ina mnyama gani , na hapo ni kama amekumbuka kitu , alianza kujiuliza elfu kumi ina mnyama gani lakini hakuweza kabisa kupatia alijaribu kuchekescha akili yake ili kupata jibu la elfu kumi ina mnyama gani lakini alijikuta akikosa jibu kabisa , aliinua mkono wake wenye saa na kuona bado alikuwa na muda wa kutosha kabla ya interview kuanza .
Basi kijana damiani alijiamulia kusogelea duka moja lililokuwa na tigo pesa kwa ajili ya kutoa kiasi kidogo cha pesa ambacho kitamsaidia katika mahitaji yake ya siku hio na pia kilichokuwa kingebaki angefanya nauli ya kurudi nyumbani kwao lushoto.
“ kumbe tembo daah ! upuuzi kabisa yaani siku zote naishika hii hela nimeshindwa kujua kuwa mnyama ni tembo haha .. “ aliongea huku akivuka barabara na kutembea hatua chache tu aliona jengo alilokuwa akilitafuta mita kadhaa kwani ndipo kampuni ya usafirishaji aliokuwa akiitafuta na kwenda kufanya interview ndio ilikuwa ikipatikana katika eneo hilo .
Alijikuta akipigwa na mshangao mara baada ya kufika ndani ya eneo hilo maana kulikuwa na watu kibao waliokuwepo ndani ya eneo hilo na wote hao walionekana walikuwa wameitwa kwa jili ya kufanya interview .
“ hapa kweli kuna kupata ajira kweli?? “ alijiongelesha huku akiingia ndani kabisa ya jengo hilo na kwenda mpaka eneo la mapokezi na aliambiwa kuwa utaratibu ni kusubiri kwani interview itaanza muda sio mrefu .
Basi alijiunga na wenzie kwa ajili ya kusubiri na hakutaka kukata tamaa kirahisi kwani alikuwa amejiandaa vya kutosha na siku zote aliamini kwamba kwenye nafasi ya watu kuchaguliwa na wakawa na nafasi sawa basi hakuna kukata tamaa na hata yeye anayo nafassi ya kushinda na kupata ajira hivyo alizidi kujipa moyo na kujiandaa na interview , ni baada ya kama dakika arobaini hivi ndio watu wote waliitwa kwa kuanza interview, ilikuwa ni written interview(mahojiano ya kuandika ) katika nafasi ya finance manager( msimamizi wa fedha ) .
Basi mameneja rasilimali watu waliokuwa wakisimamia interview hio walitoa taratibu na maelekzo ya kila namna na hatimae interview ilianza , ajabu kwa damiani ni kwamba jambo lile aliloambiwa kule na yule mtu aliempa lift likuwa ni vile vile na hata yeye alijikuta akishangaa sana ilikuwaje jamaa yule akajua kwamba ataulizwa swali la kwamba elfu kumi ilikuwa na mnyama gani ilikuwa ajabu ilio jaa bahati .
Basi interview ile ilienda vizuri kwa upande wake huku akiamini kabisa amefanya vizuri na kilichofata hapo ilikuwa ni matokeo tu ya interview hio , japo mtu yule wa asubuhi alikuwa na mashaka nae ila alijikuta akiona kwamba mtu yuke alikuwa kama malaika kwake alietumwa na mungu . .
*****
Upande mwingine ndani ya jengo la LPPF tower lililokuwa likipatioana ndani ya mikocheni sayansi kuna gari moja nyeusi aina ya range rover sport ilisimama asubuhi hio ndani ya eneo la kupark magari na alishuka mwanaume mmoja mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi aliekuwa amevalia suti yake nadhifu kabisa iliomkaa vizuri , alikuwa na mwili mkubwa kidogo na alionesha hali yake ya kiafya sio mbaya , alikuwa ametangulizana na bwana mmoja hivi aliekuwa amevalia miwani na bila shaka alikuwa ni mlinzi wake kama sio msaidizi .
Basi alitembea kuingia ndani ya jengo hilo huku mkononi alikiwa ameshikilia miwani yake ya jua na yule msaidizi wake akiwa ameshikilia briefcase nyeusi ,walifatana mpaka kwenye lift na kisha walibofya kitufe cha namba kumi na sita kuashiria ndio floor waliokuwa wakielekea , haikuwachukua muda mrefu walikuwa ndani ya korido ndefu kidogo iliokuwa na mandhari ya kuvutia huku kwa mbele kabisa kulikuwa na maandishi yameandikwa KIMBONA INTERNATIONAL LINK AND COMPANY (KILAC)
Mzee huyo alitembea kwa mwendo wake wa taratibu lakini wenye afya na kufika eneo la mapokezi na alikutana na dada .mmoja alievalia nadhifu kabisa eneo la mapokezi na baada ya kumuona mzee huyo alisimama haraka na kusalimia, alikuwa ni secretary .
" shikamoo boss ,karibu kazini " aliongea dada huyo kwa heshima kubwa sana na mzee huyo aliitika huku akiwa sio mwenye kujali sana na akapita kuelekea ofisi moja iliokuwa ikisomeka jina la mkurugenzi , aliingia ofisini humo na kisha yule mlinzi aliweka ile briefcase juu ya meza
Ni moja ya ofisi iliokuwa ikivutia sana iliokuwa imenakishiwa vyema huku samani zilizokuwemo humo ndani zilionesha kuwa zillikuwa ni za bei ya juu sana lakini bei hio iliendana na ofisi kwani ziliipendezesha kwa ujumla wake .
"okey derick tutaonana baadae na hakikisha unafatilia lile.swala kwa umakini mkubwa maana baadae nina kikao na nataka kuwa kwenye nafasi nzuri kwemye kikao hicho "
" Sawa boss " aliongea kijana huyo kwa sauti ya kikakamavu kabisa na kisha aligeuka na kutoka ndani ya ofisi hio .
Hazikupita dakika kumi simu ilipigwa na ilitoka kwa sekretary na alimjulisha bossi wake huyo kuwa kuna mgeni wake na bwana huyo aliruhusu mgeni huyo kuingia .
" mister kimbona!. "
" Samueli! hahha ..Umefika lini Tanzania? " aliongea mister kimbona kwa bashasha sana huku akimlaki mwanaume huyo aliekuwepo mbele yake , alikuwa ni mwanaume wa saizi yake sio mrefu sana umri ulikuwa ni miaka arobaini hivi kupanda kimakadirio, akiwa amevalia suti yake ya gharama ya rangi ya blue .
" Nimefika juzi mara baada tu ya kupata taarifa za kunifurahisha moyo wangu ".
" hahaha karibu sana , unipe hizo taarifa , huenda na kwangu pia zikawa zakufurahisha .
" wewe ushazisikia sana na kama ni zakufurahisha basi zishakufurahisha mpaka zikachuja .
" hahahahaha... hahahaha... ni kweli kabisa usemayo na najua ni kipi una maanisha hahhaha.. , karibu sana Tanzania kwa mara nyingine kwenye nchi yako .
Basi walionekana kuwa maswahiba wakubwa sana hawa watu kwani walionesha furaha sana kwenye nyuso zao na walionekana kufurahia jambo .
" Nimekuja Tanzania kwa kazi maalumu , naamini unaelewa biashara zetu hizi zilivyoyumba ndani ya utawala wa mwendazake , sasa baada ya kusikia taarifa ya kwamba keshatutangulia mbele za haki , kwangu ilikuwa njema sana na niliona ni wakati mwingine tena wa kufufua biashara zetu .
" ni kweli usemayo , lakini sidhani kama itakuwa ni rahisi na jambo la kufanyika haraka haraka maana linahitaji connection na unajua nchi yetu imeimarika ki ulinzi kwa sasa .
" Ndio hilo nalifahamu fika , na ndio maana nikasema nimekuja kwa kazi hio na mtu ambae naamini atanisaidia kwenye mpango huo ni wewe , we have to establish our destroyed system once again."
"Nimekusikia na ninaelewa shauku na mipango yako , lakini mimi nakusaidiaje katika hilo ?."
" Nafikiri unaelewa mister bruno ndio alikuwa chanzo kwa sysytrm yetu kufa hapa nchini mara baada ya mwendazake kuchukua madaraka "
" Ndio nalielewa fika swala hilo "
"Sasa hapo ndio pa kuanzia "
" Kivipi sam??? "
" come on! Kimbona usiniambie siku hizi umekuwa mlokole kiasi cha kupelekea akili yako kushindwa kung'amua swala dogo kama hilo ."
" haha….you meaan to kill him?? "
" correct , na naamini hilo ni swala unalo liweza sana na lipo ndani ya uwezo wako , naujua upande wako mwingine , na ukiutumia vyema tutafanikiwa katika hili , na nakwambia mtu wa kwanza kupata faida sio mimi tu ni wewe pia maana utakuwa pia kwenye system " aliongea mwanaume huyu anaejulikana kwa jina la samueli kwa lugha yake iliojaa tamathali za nchi za nje .
Bwana kimbona alijikuta akiwaza na kukuna kichwa na akainua uso wake akamwangalia sam usoni na kisha aliachia tabasamu .
"Assume its dome from now on , We are back my friend " aliongea huku akimfanya sam kufurahia sana na kisha walipeana mikono na kutakiana siku njema na kisha wkaagana huku sam akimsisitizia kuwa swala hilo lifanyike mapema .
*******
Katika watu waliotoka na sura zilizojaa tabasamu alikuwa ni kijana Damiani , huku wenzake wengi wakitoka na nyuso za kuonesha kukata tamaa kwa kile walichokutana nacho .
" Daah ! nakutumia kwangu kote pesa eti leo nimeshindwa kung'amua elfu kumi ina mnyama gani , hata hawa HR wenyewe wanazingua " aliongea kijana mmoja aliekuwa na marafiki zake hapo akionesha kulalamika kwa kukutana na swali kama lile kwani lilikuwa ni swali ambalo halikuwa la kawaida na la kutegemea hasa kwa nafasi kama hio ya finance manager (usimamizi wa pesa ).,hakuwa kijana mmoja tu aliekuwa akilalamika ila wengi walionyesha kuchukizwa na aina hio ya swali na kilichowakasirisha ni kwamba maswali yale magumu yaliwekewa maksi chache . .
" Mambo ! " Ilisikika sauti moja nyororo sana ya kuamsha hisia kwenye ngoma za masikio ya Damiani na kumfanya ainuke kwani wakati huo alikuwa ameegamia uzio kuangalia upande wa barabarani magari yaliokuwa yakipita na watu waliokuwa kwenye hekaheka za siku hio .
Alikuwa ni msichana mrembo kweli kweli , alikuwa mrefu saizi ya kati , aliekuwa na rangi flani hivi ambayo kwa haraka haraka ungejua kabisa mlimbwende huyu alikuwa ni mchanganyiko wa mataifa mawili ,kama sio wa muhindi basi ni mzungu na mwafrika , huku baba yake akiwa ni mzungu kamili ama mhindi , alikuwa anavutia kwakweli na hasa tabasamu alilokuwa ameachia usoni mwake lilimfanya vishimo vyake kwenye mashavu vizidi kuupamba uso wake na kumfanya kijana damiani abung'ae .
" poa mambo " alijikuta akiitikia ki uoga uoga
" Naitwa merina wewe je ??"
" Damiani " .
" Ohoo ! Na wewe upo kwenye interview?! "
" Ndio " .
" Hata mimi pia , nafrah kukufahamu Damiani " Aliongea msichana huyo na alionekana kuwa mchangamfu kwani ndio aliekuwa ametawala maongezi hayo .
" by the way how is written ?" aliongea mwanadada huyo kumuuliza swali hilo na kumfanya Damiani atabasamu kidogo na kisha alijibu .
" Nashukuru mungu , ilikuwa safi , and you ??? "
" Me pia " jibu hilo lilimfanya Damiani awaze na kuona kati ya watu waliokuwa wamefanikiwa kujua elfu kumi ina mnyama gani basi hata huyo mlimbwende atakuwa amepatia , sasa swala hilo kidogo lilimnyima raha maana aliona kuwa nafasi yake inakuwa ndogo ya kuchaguliwa ila hakutaka kuonyesha hilo na kukata tamaa ,
" Umetokea chuo gani?"
" Harvard " jibu hilo lilimfanya Damiani ashangae kwani alijua duniani chuo kinachotamkika kwa jina hilo kilikuwa ni chuo kikubwa duniani na kilikuwa hakipo tanzania bali kilikuwepo ndani ya nchi kubwa duniani yaani Marekani .
" You mean USA ??"
" Yeah !." Hapo Damiani ndio alipochoka maana alijua kama mwanadada huyo alikuwa amepatia maswali yote ya written basi hata kama yeye atapita na kwenda oral interview basi asingefua dafu mbele ya bidada huyo man a kwanza chuo tu kingembeba .
" congratulation (hongera ) "
"Thanks!, And you? "
" TIA "
" ooh! Kipo wapi? "
" Tanzania institute of accountancy kipo njia ya mbagala " aliongea Damiani huku akionekana hata mood ya kuongea na mwanamke huyo ikipotea ghafra kwani aliamini kwa nafasi hio moja iliokuwa ikipiganiwa na mamia ya wahitimu asingepata kitu kabisa , kiufupi alinyong'onyea .
Basi damiani aliachana na mlimbwende yule na hio ni mara baada ya kutangaziwa kuwa majibu yatatoka kesho na kwa wale ambao wamepita kwa hatua inayofata basi watajulishwa na ukiona wewe mpaka saa nne asubuhi hujapata ujumbe wowote ama simu kutoka kwetu basi jua hujapita na tunakushukuru sana kwa kushiriki .
Kwa damiani alikosa Tumaini kabisa na aliona ni kama alipoteza hela zake tu za kuja jijini dar ,alitamani kuondoka siku hio hio kurudi lushoto kwao lakini hakutaka kuondoka siku hio hio , aliona ngoja asubiri akapambane na mwanadada yule , kwani aliamini pia kumaliza kwenye chuo kikubwa sio tija, tija ni kuwa competent(uwezo) kwa kile unachokijua .
Alirudi zake mbagala huku akiwasiliana na mama yake juu ya siku yake ilivyo enda , huku mama yake akiendelea kumpa nguvu ya kutokata tamaa bali azidi kujipanga , alirudi mpaka zakhem mbagala bahati nzuri au mbaya hakumkuta yule joshua ila kwakua alikuwa amepewa ufunguo aliingia na kujipumzisha huku akianza kufikiria matukio yote ya siku hio ,kuanzia asubuhi mpaka muda huo , alijikuta akitabasamu na kuna jambo lilimpa nguvu zaidi na kuona kama mungu alikuwa na makusudi ya kupata ajira kwa wiki hio atapata kwa hio hakutaka kukata tamaa , kwani alivyokumbuka mtu yule wa asubuhi alivyomuambia kuhusu elfu kumi ina mnyama gani na kweli swali hilo likawepo kwenye interview basi aliona ni mungu ndie aliemua kujidhihilisha kwake kupitia mtu yule , kwa hio hakuona kuna haja ya kukata tamaa .
Siku nyingine iliwadia na kwa damiani alikuwa na furaha sana kwani alikuwa tayari amekwisha kupokea ujumbe kuwa amepita kwenda kwenye oral interview , kwake ilikuwa jambo la baraka sana na alimshukuru mungu na alijipanga haswa kwa ajili ya lililoko mbele yake .
Aliagana na joshua huku akimtakia mafanikio mema na pia alimpigia mama yake kipenzi kwa hatua alio fikia na mama yake alimuambia anamuombea , alifika barabarani na alibahatika kupata gari baada ya kufika tu lililokuwa likielekea stesheni na alipanda , ndani ya madakika machache alikuwa chini ya jengo la kampuni hio .
Alitembea kwenye ukingo wa barabara na kisha alikunja kushoto na kuingia eneo hilo na wakati huo huo anaingia gari aina ya Audi new model rangi nyeupe ilisimama na alishuka yule dada wajana Merina na alionyesha alikuwa akiendesha yeye mwenyewe , alimuoa a Damiani na mdada ndio wa kwanza kuita jina la damiani kwani Damiani wala hakuwa hata na habari nae .
" Mambo "
" Poa , za toka jana?. "
" Safi , hongera " aliongea merina na kutabasamu huku akionekana hakuwa na wasiwasi wowote kabisa hali iliomfanya Damiani kuamini kwamba mdada huyo alikiwa na uhakika wa kupata nafasi hio .
Waliongozana na kupewa utaratibu na muda kidogo alianza merina ,siku hio walikuwa wa nne ndani hapo , aliingia merina na ndani ya dakika kumi na tano alitoka , na aliingia mwingine na kisha aliingja Damiani , aliulizwa maswali kadhaa na akajibu ki ufasaha kwa kadri anavyojua na kisha alimaliza interview yake.
UNAFIKIRI NI BIASHARA GANI ,
.................SEHEMU YA TATU..............
.
ILIPOISHIA
Siku nyingine iliwadia na kwa damiani alikuwa na furaha sana kwani alikuwa tayari amekwisha kupokea ujumbe kuwa amepita kwenda kwenye oral interview , kwake ilikuwa jambo la baraka sana na alimshukuru mungu na alijipanga haswa kwa ajili ya lililoko mbele yake .
Aliagana na joshua huku akimtakia mafanikio mema na pia alimpigia mama yake kipenzi kwa hatua alio fikia na mama yake alimuambia anamuombea , alifika barabarani na alibahatika kupata gari baada ya kufika tu lililokuwa likielekea stesheni na alipanda , ndani ya madakika machache alikuwa chini ya jengo la kampuni hio .
Alitembea kwenye ukingo wa barabara na kisha alikunja kushoto na kuingia eneo hilo na wakati huo huo anaingia gari aina ya Audi new model rangi nyeupe ilisimama na alishuka yule dada wajana Merina na alionyesha alikuwa akiendesha yeye mwenyewe , alimuoa a Damiani na mdada ndio wa kwanza kuita jina la damiani kwani Damiani wala hakuwa hata na habari nae .
" Mambo "
" Poa , za toka jana?. "
" Safi , hongera " aliongea merina na kutabasamu huku akionekana hakuwa na wasiwasi wowote kabisa hali iliomfanya Damiani kuamini kwamba mdada huyo alikiwa na uhakika wa kupata nafasi hio .
Waliongozana na kupewa utaratibu na muda kidogo alianza merina ,siku hio walikuwa wa nne ndani hapo , aliingia merina na ndani ya dakika kumi na tano alitoka , na aliingia mwingine na kisha aliingja Damiani , aliulizwa maswali kadhaa na akajibu ki ufasaha kwa kadri anavyojua na kisha alimaliza interview yake
INAENDELEA ……….
Basi baada ya damiani kumaliza interview ,alitoka huku akiwa amepewa maelekezo kwamba majibu yatatoka siku kumi zijazo kama amepata kazi au hajapata . .
Alitoka na moja kwa moja na kuondoka eneo hilo na alipanga siku hio hio kuondoka kuelekea Tanga maana muda ulikuwa ukirihusu .
Saa sita kamili alikuwa ndani ya basi la mining nice akielekea lushoto , alikuwa na nusu tumaini la kupata ajira , kwani kila akikumbuka bidada yule aliona kabisa kumshinda mtu alietoka katika moja ya chuo kikubwa duniani ni vigumu na ndio maana alikuwa na nusu tumaini na hilo lilikuwa ni kutokana na kwamba alikuwa amejibu vyema maswali alioulizwa , lakini alijua mfumo wa Tanzania ulikuwa ukiangalia sana nani katoka chuo gani .
Basi saa moja kamili ndio muda aliokuwa akiingia lushoto mjini , alishuka na nakisha alisogelea mpaka moja ya noah zilizokuwa zikielekea kijijini kwao na kisha bahati nzuri zilikuwepo , alipanda na kisha alisubiria baadhi ya abiria wajae na hatimae walifanikiwa kuondoka eneo hilo kuelekea kijijini kwao mkuzi .
Japo alikuwa na mawazo ila picha ya yule mwanadada ilikuwa muda mwingine ilikuwa ikimjia , kuna muda alijisema kama ingekuwa ni rafiki yake elvis mpenda warembo basi hata interview asingejali na angejali kumtongoza yule mwanamke , maana kila akimkumbuka aliishia kutabsamu na kukiri kwamba alikuwa mrembo haswa ambae hakuwa level yake .
Alikuja kushituka kwenye mawazo mara baada ya kufika mkuzi na konda kumshitua, aliangalia nje kama ndio sehemu aliokuwa akishukia , ila aliona anashukia kituo cha mbele yake kwa hio alimtaaarfiu kabisa konda na mara baada ya kufika eneo husika alishushwa na kuanza kuporomoka kwenye kijimlima kuelekea kijijini kwao , kijiji cha mkuzi kilikuwa na umeme kila kona , na pia kilikuwa kimechangamka na hata baada tu ya yeye kushuka alionekana na baadhi ya watu waliuokuwa wakimfahamu na walimsalimia na watoto walimpokea na kupeleka mizigo kwao .
********
Ilikuwa ni siku kadhaa tokea raisi wa tanzania apoteze maisha , raia wengi wa tanziania walikuwa kwenye maombolezo ya siku ishirini na moja , japo kiongozi huyo alikuwa amezikwa lakini watanziania wengi waliokuwa wakimpenda walikuwa wakimlilia na hio ni kutokana na raisi huyo kupendwa sana , .
Naam ! bendera onyango ni raisi wa awamu ya nane ndani ya taifa la Tanzania , ni moja ya maraisi waliokuwa na msimamo sana katika uongozi wake , na kupita hilo alitokea kupendwa sana na kundi kubwa la watanzania huku kundi lingine likuwa halimpendi na hio nikawaida sana katika siasa , licha ya raisi huyu kutopendwa na kundi dogo la watu ni raisi aliekuwa akijitahidi sana kutekeleza majukumu yake ya kazi , hususani yale ambayo alikuwa ameyaahidi katika kampeni zake , huku chini yake akiwa na makamu wake bwana henri mushi .
Hakika bwana onyango alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana katika kuhakikisha yale yote aliyo yaahidi kuyatimiza na hayo ni hususani katika maswala ya miundombinu , msimamo wake katika kusimamia kodi za raia ulimpa wafuasi wengi sana , lakini hata hivyo kuna waliokuwa hawampendi kwasababu zao ama ziwe za msingi ama sio za kimsingi ilihali binadamu hakuwa amekamilika na alikuwa na madhaifu yake basi hawezi kuwa sawa katika kila Nyanja za kiuongozi na hivyo hata bwana bendera alikuwa moja ya binadamu hao ambao hawakuwa wamekamilika .
Katika mambo ambayo bwana onyango alifanikiwa kuyakomesha ndani ya utawala wake moja wapo lilikuwa ni swala la madawa ya kulevya nchini , kwani alijitahidi kwa kushirikiana na wasaidizi wake na polisi kuhakikisha anaziba njia zote za uingizwaji wa madawa ya kulevya hapa nchini, na vile vile madawa kupitishwa nchini, na kwa asilimia kubwa hilo lilifanikiwa , lakini mwanzo wa kufanikiwa kwa jambo hilo ndio mwanzo wa kutengeneza maadui na wafanya biashara hao wa madawa , lakini kwakuwa kazi hio hakuwa akifanya mwenyewe, bali alikuwa akishirikiana na watu wengine na hao walikuwa ni mawaziri na wafanya biashara hao hao wa madawa ya kulevya , na moja ya wafanya biashara hao alikuwa ni bwana Bruno lamberk , huyu bwana alikuwa ni mzungu na alikuwa ndani ya nchi ya Tanzania kwa muda wa miaka ishirini na alikuwa ni moja ya wawekezaji wakongwe ndani ya tafia la Tanzania , bwana huyu alikuwa ni nmoja ya matajiri wakubwa sana waliotajirika wakiwa ndani ya taifa hili , lakini licha ya biashara zake za halali , pia alikuwa ni muuza ngada ndani ya ukanda wa afrika mashariki na kwa kifupi yeye ndie aliekuwa doni ndani ya ukanda wa afrika mashariki yote ,.
Bwana huyu haikujulikana kama alikuwa na familia au lah , kwani kwenye maisha yake hakuwahi kuishi na mwanamke zaidi ya wale wanawake wa kuja kufanya starehe na kuondoka , basi bwana huyu mara baada ya raisi bendera kuingia madarakani , haikujulikana raisi huyo alitumia mbinu gani kumnasa bwana huyo mpaka kupelekea bwana Bruno kutoa ushirikiano na kuwasaliti wauza madawa wenzake, na kupelekea biashara hio kwa Tanzania kufungiwa kabisa na haikuweza kufanyika ,na wauza madawa maarufu kukimbilia nje ya nchi , na moja ya watu waliokuwa wamekimbilia nje ya nchi alikuwa ni bwana Samuel saitoto(rich sam) , huyu alikuwa ni muuza madawa mkubwa sana ndani ya mtandao wa bwana bruno na baada ya kusalitiwa na rafiki yake ndipo alipo amua kukimbilia mexico pamoja na familia yake
Basi habari ya kifo cha raisi bendera kwa bwana Bruno ilikuwa ni pigo kubwa sana , kwani raisi huyo ndie aliekuwa akimpa ulinzi mkubwa sana zidi ya maadui zake , ni siku ya ishirini sasa tokea kuzikwa kwa raisi bendera ndani ya nchi ya Tanzania, bwana Bruno alikuwa amejificha ndani ya jiji la Tanga wilayani lushoto.
“ mkuu nimefanikiwa kuongea nae , anaoneakna ni kijana shupavu kama atakuwa na mafunzo maalumu atafaa kabisa “ aliongea bwana mmoja ambae tulimuona ndani ya jiji la dar es salaam , aliempa lift kijana Damiani . na siku hio bwana huyo alikuwa ndani ya wilaya hio na walioneakana walikuwa na mambo kadha wa kadha walikuwa wakiuongea .
“ Good nimempenda yule kijana na piga ua piga chini lazima tumuingize kwenye system , kwa hio endelea kumwangalia , maana muda si mrefu tutaexcute the plan , my enemies are looking for me , bendera is dead , no one can protect me now “ aliongea huku akiamaanisha kwamba muda mchache ujao wataendelea na mpango wao kwani bendera amekufa na hakuna mtu yoyte anaeweza kumlinda .
“Inabidi uondoke ndani ya nchi hii “
“ siwezi danny nitafia hapa hapa Tanzania “
“ but its too dangerous “{ lakini ni hatari sana )
“ najua na ndio maana nakwambia endelea kumtrack Damiani we need to prepare him ( akimaanisha aendelee kumchunguza damiani kwani wanatakiwa kumuandaa mapema .
*******
Kimbona kama alivyokuwa ameahidiana na samu juu ya kumtafuta bruno na kumpotezea mbali mzungu huyo , hakutaka kabisa swala hilo lifeli , na alikuwa na mood kweli ya kulifanya swala hilo , hasa kila alipokuwa akikumbuka ni kiasi gani alikipoteza mara baada ya Bruno lamberk kuwasaliti kwenye mtandao wao , kilimuuma sana , hela zake zilimpa nguvu ya kukamilisha mauaji hayo .
Haikumuia vigumu ,kwani ni kama alikuwa amepumzika katika biashara hio, kwani watu wake (gang) walikuwepo ndani ya nchi hio na alikuwa akiwalipa kisiri siri kwani alikuwa akiamini siku moja atarudi ulingoni na kuendelea na biashara hio, kwake baada ya kifo cha ghafra cha raisi bendera aliiona hio kama fursa nyingine ya kurudi kwa kishindo katika biashara hio ya uuzaji wa madawa ya kulevya .
“ Derick hakikisha unawapanga vijana mkao wa kazi , taarifa zilizopo kwa sasa kutoka kwa shushu wetu ndani ya TISS ni kwamba bwana Bruno kajificha ndani ya wilaya ya lushoto mambo view hotel.
“sawa mkuu vijana kwa sasa wako tayari na wanasubiria maelekezo yako tu “
“ basi safi , pumzika kwa leo na kesho nitakuambia nini cha kufanya , hakikisha swala hili linafanyika kwa weledi mkubwa , hakuna kufeli “
“ sawa boss “ huku akitoka
“ hahahahaha… hahaha… hii ni fursa nyingine kabisa kwangu naenda kurudi ulingoni muda si mrefu , Bruno …. Brunooooo …. Ama zako ama zangu “ aliongea tajiri kimbona kwa kicheko cha kifedhuli huku akigugumia wine yake aina ya black and white .
Siku ilio fuata derick alipokea simu kutoka kwa boss wake na kumtaarifu kufika kwenye kampuni yake ndani ya jengo la LAPF tower , kampuni iliokuwa ikjjulikna kwa jina la KILAC (KIMBONA INTERNATIONAL LINK AND COMPANIES }.
Derick haikumchukua muda mrefu kufika ndani ya jengo hilo la LAPF, alifika moja kwa moja na aliripoti kwa secretary na aliruhusiwa kuingia moja kwa moja na alisalimiana na boss wake huyo na kisha alipewa ramani nzima ya kufanya tukio hilo .
“ kuweni makini na Danny huyu ni jasusi wa kimataifa na ana mbinu nyingi za kuwazidi , lakini na nyie pia mna mbinu nyingi za kumzidi akili , narudia swala hili halina kufeli hakikisheni mnalimaliza baada ya siku kumi zijazo.
“ sawa boss “
Derick alitoka ofisini hapo na kisha hakutaka kuchelewa aliwashitua genge lake la kimafia na kuwapa ramani wapi wakutane kuelekea lushoto .
********
Ni baada ya siku kumi kupita kijana damiani bila kupokea ujumbe wowote kutoka kwa kampuni ambayo amekwisha kufanya interview , japo mama yake alimtia moyo wa kutokata tamaa ila kwake yeye ukiunganisha na yale anayo yajua mwenyewe hakuona nafasi kabisa ya kushinda kazi ile , alimwangalia mama yake aliekuwa amevaa nguo zilizoochanika na zisizokuwa zikivutia , alimuonea hruma sana , alitamani amtoe mama yake katika lindi hilo la umasikini kadri ya uwezo wake , kiufupi alikuwa akimpenda mama yake sana , kila akikumbuka misoto mama yake aliopitia kwa ajili ya kuhakikisha anasoma ,ilizidi kuumia mno aliilaumu serikali sana kwa kutokuwa na mfumo mzuri wa kutoa ajira kwa wanafunzi , kwani wahitimu walikuwa wakijitahidi kusoma sana kwa bidiii na pia wazazi wanawasomesha watoto wao kwa juhudi zote, lakini mwisho wa siku wanamaliza hakuna ajira , ilikuwa ni swala la kukatisha tamaa sana wazazi pia na wahtimu wenyewe .
Siku hio damiani aliamua kushinda na mama yake tu nyumbani hawakwenda popote , maana hata mama yake siku hio alikuwa kichwa kinamsumbua hivyo hakuweza kabisa kwenda kwenye vibarua vyake ambavyo vilikuwa vikimuwezesha kuleta nyumbani na kupata chochote tumboni .
Basi siku hio damiani alikuwa akitengeneza banda lao la mbuzi hapo uwani huku muda mwingi aliangalia emaili yake ama simu ikiita , kwani alikuwa na shauku kubwa ya kujua kama amepita ama hajapita , lisaa la kwanza likapita , la pili nalo likapita , la tatu hatimae la nne , mpaka saa kumi na moja hakukuwa na jumbe wala simu yoyote , aliweka simu chini huku akiona kabisa hakukuwa na tumaini lingine lililobaki la kupata ajira , hakuona sababu ya kukaa nyumbani hapo alimuaga mama yake kwa kumwabia anarudi muda si mrefu anaenda kwenye shanba lao la miti kwa ajili ya kuchukua miti kidogo aje amalizie banda lao la mbuzi , maana hakupenda kabisa kulala na mbuzi hao nyumba moja kwani mikojo yao ilikuwa na harufu kali .
Alitembea kwa muda wa kama nusu saa na hatimae alipita kijijini kwao , siku hio watu wengi walionekana kuwa barabarani kwani siku hio kulikuwa na sherehe iliokuwa ikifanyika kwenye kanisa moja la roman kwa hio watoto watoto alikuwepo huko na hata baadhi ya wamama pia , ni mama yake pekeee na baadhi ya wanakijiji waliokuwa wapo majumbani hasa wale wazee waliokuwa hawawezi kutembea , alitembea huku akiwa anakula apple kwani kijiji chao hicho kilikuwa na kilimo cha matunda aina ya apple , matunda damu na peasi na hata mananasi.
Basi baada ya dakika kama arobaini na tano hivi ndio muda alioingia kwenye shamba lao kubwa la miti ya biashara , hakutaka kuchelewa maana baada ya kufika tu alianza kazi ya kutafuta mikalitusi ilio nyooka na kisha kuikata , lakini wakati akiendelea na kazi hio simu yake ilitoa mlio kwamba kuna ujumbe umeingia , aliendelea kukata miti kwanza kama ishirini na aliridhika kwamba hio inatosha , ndipo alipo toa simu yake kuangalia ni ujumbe gani umeingia .
“ HONGERA BWANA DAMIANI RABANI UMEFANIKIWA KUPITA KWENYE INTERVIEW YAKO ULIO FANYA TAHEHE HIO , UNAPASWA KURIPOTI KAZINI MAPEMA KABLA YA TAREHE HIO”
Ulikuwa ni ujumbe uliomtoa machozi bwana damiani , yes yalikuwa ni machozi ya furaha alijikjuta akiruka ruka kwa furaha sana , hata ile kazi ya kukata miti iliishia hapo na jambo alilolifikiria kwa kwakati huo ni kurudi nyumbani na kwenda kumuonesha mama yake ili wafurahie pamoja , muda ulikuwa umeenda na kagiza kameanza kuingia alifunga miti yake haraka haraka huku akipiga mluzi wa furaha hata haikueleweka ni wimbo gani ulikuwa ukiimbwa .
Lakini wakati hayo yakiendelea mara alisikia kitu kilicho mfanya kunyanyuka haraka na kuangalia upande wa kushoto kwani kilikuwa ni kishindo kikubwa cha kitu kudondoka , lahaula ! ilikuwa mtu bwana kadondoka tena mwenye ngozi nyeupe huku akioneakana kuvuja damu nyingi usoni na ubavuni , damiani alipatwa na woga na akili yake yote iliwaza kukimbia kwa wakti huo , lakini alishuhudia mtu yule akimpungia mkono kwa shida kama anaomba msaada , ilibidi damiani aangalie kulia na kushoto kuona kama kuna mtu anakuja , maana akili yake ilicheza na kufanya kazi kama mashine kwa wakati huo na alijua mtu yule lazima atakuwa anawindwa kama sio kukimbizwa , alimsogelea kwa tahadhari .
“ help me to get out here wataniuu ..wa tafadhari nisaidie “ aliongea na kweli alikuwa mzungu kama damiani hisia zake zilivyokuwa zikimwambia , hakutaka sana kujishauri maana kweli aliona mtu huyo alikuwa akihitaji msaada , lakini alifikiria ni msaada gani anatakiwa kumpa , alichokifanya ni kurudi pale alpoacha miti yake na kisha aliichukua na kuisukumizia kichakani na haikueleka alikuwa na maana gani , kisha alimrudia yule mtu na kumuweka begani huku mzungu yule akiinua uso wake.
“shika hii just in case tusipofanikiwa , kimbia uniache.” Ilikuwa ni bahasha iliojaradiwa kwa mfuko wa plastic.
Damiani alivipokea huku akiwa hajui mzee yule alikuwa akimaanisha nini , ila kwakuwa wakati huo alichokuwa akiamini ni kumuokoa tu basi alijitahidi kadri ya uwezo wake kumtoa msituni hapo na kumfikisha nyumbani kwao kwani aliamini ndio ingekuwa sehemu salama , na angejua angefanya nini baada ya hapo
Uzuri ni kwamba giza lilikuwa limetamalaki hivyo kwa kupitia njia za vichaka aliweza kupita bila kuonekana kwa urahisi lakini pia kwakuwa watu walikuwa kwenye sherehe , alitembea na kufanikiwa kutoka kwenye msitu na hatimae aliingia ndani ya kijiji chao, alionekana na mbibi mmoja tu aliekuewa hawezi kutembea vizuri na kuongea pia kwani alikuwa amepinda mdomo , na kwa fununu ni kwamba ni adhabu alio pata katika shughuli ya ulozi wake .
Alimpitisha mpaka kwao na mama yake alipigwa na mshangao nusu apige kelele, lakini damiani alimzuia na kumwambia huyo mtu anataka msaada kamuokota huko msituni , mama yake alifungua mlango na walimpitisha kisha walimlaza kwenye kipande cha mketa , na wakati huo mzungu huyo hakuwa na fahamu , nadhani ni kutokana na kupoteza damu nyingi .
“ mama inabidi tumuite mzee kivinje anaweza kumsaidia nikifanya taratibu za kupata usafiri wa kumpeka hospitalini “( mzee kivinje alikuwa ni mganga kutumia mitishamba )
“ kwanini usimpeleke moja kwa moja akitufia hapa si itakuwa kesi “
“ hapana mama hali yake hio inaonesha anawindwa na inatupasa kumsaidia kwanza na kufanya mambo kwa umakini “ aliongea damiani kwa ujasiri mkubwa sana na kisha alitoka na kwenda kwa kivinje daktri wa mitishanmba lakini pia alikuwa mganga wa kienyeji .
Hapakuwa mbali sana , kutokana na mwendo wake alifanikiwa na bahati nzuri aliweza kumkuta bwana kivinje akiwa nje kashikiria kikombe na alionekana alikuwa akinywa maziwa ya mbuzi , damiani alieleza shida yake na kumstua sana kivinje na hakutaka kupoteza muda aliingia ndani na kutoka na dhana zake za kazi na kuongozana na damiani .
Haikuwchukua muda , walifika na kivinje alihitaji damiani amuoneshe mgonjwa alipo lakini hapo ndipo damiani aliposhuhudia kitu ambacho hakukitarajia kabisa .
Alimuona mama yake akiwa kwenye dimbwi la damu , huku mwili wa yule mzungu na wenyewe ukiwa kwenye dimbwi la damu , aliishia kutamka neno mama lakini sauti haikutoka.
INAENDELEA
INAENDELEA SEHEMU YA NNE
Damiani alijikuta akijikaza na kumkimbilia mama yake pale alipo na wala hakujali zile damu maana alimuinua mama yake huku akilia
“ mamaaa, mamama , amka mama nini kimetokea mama yangu … mamaaaa… mama amka “ mama yake damiani alikuwa akitapatapa na aliishia kunyosha mkono kuelekea mlangoni na hapo hapo akakata roho , ilikuwa ni huzuni kwake kwani alilia na kuutingisha mwili wa mama yake japo aamke , lakini haikuwezekana kabisa na kivinje ndio alimsogelea na kumshikilia asiendelee kufanya anacho kifanya
“ mama mama wee ,, mama amka mimi mwanao unaniacha na nani , mama yangu , bado sijapata nafasi ya kukutoa kwenye umasikini mama yangu wee …. Amka mamama nimefanikiwa kupata ajira sijakuambia bado mma amka mama weeee…..” ilikuwa ni huzuni na kama haukuwa na moyo basi ungelia ,maana mama yake alikuwa ameuwawa kikatili sana , watu tayari walikuw wamejaa kwani walisikia vilio hivyo , kila alieambiwa na kivinje kwamba mama damiani kafariki ilikuwa ni kilio kikubwa mno kwa kila aliekuwa akimjua mama huyo .
Watu waliendelea kulia ,damiani alikuwa amezimia wakati huo ,chopa ilisikika ikitua eneo la karibu ndani ya kijiji hicho na mwili wa yule Bruno ukichukuliwa na kupelekwa upande chopa ilipokuwepo , huku polisi nao wakiwa eneo la tukio , ilikuwa ni tukio la kusikitisha na kila mtu alikuwa akiongea lake , na wakati huo hayo yanaendelea vijana wa kimbona walionekana hapo na derick mwenyewe akiwa wamesimama upande wa juu hivi kuepuka watu kuwaona na mara baada ya kuona mwili wa Bruno ukitolewa na wao waliondoka eneo hilo .
*******
“Hahaha… hahahah…. Safi sana derick , kazi nzuri vijana wangu “ aliongea kimbona huku akionekana kuwa katika uso uliojawa na furaha ya ushindi baada ya kusikia kuwa bruno kazichapwa risasi na amekwisha kufa.
Hakutaka kuchelewa aliinua mkonga wake na kumpigia sam na kumpa tarifa hizo ambazo kwa sam alizipokea kwa furaha kubwa mno , na kumshukuru sana kimbona huku akimualika kuwa siku hio aende serena hoteli kuna watu anataka kuwakutanisha nao muda was aa nne usiku .
Na bila hiyana mzee huyo aliitikia wito huo kama atakuwepo eneo hilo bila kukosa , ilikuwa ni furaha sana kwa kimbona katika moja ya hatua ya kurudi kwenye biashara yake aliiona kabisa kwa mafanikio makubwa inakwenda kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana .
Ilivyofika muda wa saa nne usiku kimbona alimuaga mkewe na familia yake kwa ujumla na kisha alitoka na mlinzi wake kuelekea kwenye miadi yake kama alivyokuwa ameelekezwa na Samuel , kwakuwa ni usiku gari haikukawia kufika ndani ya hoteli hio ya hadhi ya juu sana ndani ya jiji la dar es salaam .
Alifika mpaka mapokezi na kujitambulisha hapo na kisha ni kama ujio wake ulikuwa umetegemewa kwani aliongozwa mpaka kwenye lift na mdada mmoja mrembo sana aliefika eneo hilo kumchukua , lift ilipanda mpaka kwenye floor ambayo ilikuwa na vyumba vya VVIP yaani kwamba hapo walikuwa wakiingia watu wa hadhi ya juu sana ndani ya jiji hilo , alitabasamu maana ilikuwa ni muda kidogo kuingia sehemu zilizokuwa zina ulinzi mkali kama aliouona ndani hapo .
Mdada yule mrefu mrembo alievalia suti yake ya zambarau na viatu vya high heels alitembea mpaka kufika kwenye moja ya chumba na kisha alifungua mlango na kumkaribisha bwana kimbona , kimbona alijikuta akiwa kwenye mshangao kwani watu waliokuwepo hapo ndani hakuwatarajia kabisa .
“ mheshimiwa , alijikuta kimbona akiongea kwa kupaniki kwani aliekuwa mbele yake alikuwa ni rais mstaafu wa awamu ya saba bwana Athumani ndalu , upande wa kulia alikuwepo waziri wa mambo ya ndani bwana musiba , mbele yake alikuwepo samueli , kulikuwa na jumla ya watu wanne ukimjulisha na yeye pia lakini kuna kiti kilionekana hakikuwa na mtu ..
“ hongeera sana bwana kimbona kwa ushindi wa leo “ aliongea raisi mstaafu .
“ asante sana mheshimiwa , unajua ni mara yangu ya kwanza kuonana na wewe laivu , ni heshima kubwa sana “
“ hahahaha.. kimbona huu ni mwanzo tu , na sasa unakwenda kukutana na mtu mkubwa Zaidi na penginepo wakubwa Zaidi karibu kwenye U-97( UNITY 97) aliongea sam kwa sauti ya majisifu
“U-97?” aliongea kimbona akimwangalia sam lakini hapo hapo mlango ulifunguliwa na hapo ndipo bwana kimbona aliposhangaa zidi kwani mtu aliekuwepo mahali hapo hakumtegemea kabisa.
“ Mheshimiwa raisi!!!”””” alijikuta akijisemea moyoni kwa mshangao
*******
Watu walikuwa wakizungumza hili na lile ndani ya kijiji hicho na habari zilitapakaa kila kona , kila mtu alikuwa akiongelea swala la mama damiani kupigwa risasi na watu wasiojulikana , pia mzungu kupigwa risasi ndani ya nyumba hio hio ya mama daniani na hata chopa kuja kumchukua mzungu huyo , watu hawakulala kila mtu alikuwa akiongea hili na lile ilimradi tu ni jambo la kuongea , lakini pia kuna baadhi ya watu walikuwa kwenye majonzi makubwa ya kupoteza uhai kwa mama damiani tena kwa kifo cha kikatiri sana , watu walilaani vikali kwa kilicho tokea .
Damini alikuja kupata fahamu lisaa limoja mbeleni akijikuta yupo ndani ya zahanati akiwa amelazwa , ni kama akili zake hazikiwa sawa wakati wa kuzinduka na hata nesi na daktari walimuona wakati wa kuzinduka huku kila mtu akiwa kwenye uso wa majonzi na kumuonea huruma kijana huyo , kwani waliona ni mambo makubwa na magumu ambayo anakwenda kupambana nayo katika maisha yake .
Ni kama mkanda wa filmu ulikuwa ukipita ndani ya kichwa cha kijana damiani , picha ya kumuona mama yake akiwa amelala kwenye dimbwi la damu zilianza kupita .
Alijikuta akitoa ukulele uliowafanya dokta amsogeleee haraka haraka na kumtuliza, hawakua na jinsi ilibidi wamchome tena sindano ya usingizi ambayo ilikuwa makali ya kuisha siku nyingine .
Ilikuwa muda wa asubuhi ambao habari za majambazi kumuaa mama damiani na mzungu zilisambaa lushoto nzima na kwenye vyombo vya habari.
Jeshi la polisi lilithibtisha kuwa wahusika wa mauaji hayo walikuwaa ni majambazi yaliokuwa na makazi yao katika msitu wa mlola huku wakihusisha swala hilo na tukio lililotokea miaka ya nyuma la kuvamiwa kwa chuo kikuu cha SEBATIANI KOROA MEMORIAL UNIVERSITY (SEKOMU) miaka iliopita huku wakiahidi uchunguzi unaendelea mpaka kuwatia hatiani majambazi hayo .
Upande wa damiani alifumbua macho asubuhi akiwa na akili zake zote , roho yake ilimuuma mno pale alipokumbuka duniani amebaki kuwa yatima , alijilaumu kwa kumsaidia mzungu yule kwani aliona kama angemuacha tu kule kule huenda yote hayo yasingemkuta mama yake , alijilaumu sana na kuhuzunika na moyo wake , lakini hakuwa na lakufanya kwa wakati huo , ilibidi aruhusiwe ili akashuhudie maziko ya mama yake , watu walimuonea huruma sana na kumpa pole , alizipokea huku akijitahidi kujikaza kiume .
Taratibu zote mazishi zilikuwa zimekwisha kufanywa na serikali , akiwemu mkuu wa wilaya aliehudhuria mazishi hayo.
Basi padri alifanya sala fupi na kuruhusu watu waage mwili akiwemo damiani alielia sana baada ya kumuona mama yake akiwa kwenye jeneza , alitolewa na watu wengine walipewa nafasi na hatimae mwili ulipelekwa makaburini
“SARAH RABAN AMEZALIWA MWAKA 1979 AKAFARIKI MWAKA 2019 AKIWA NA MIAKA 40 AMEACHA MTOTO MMOJA “ wosia mfupi ulisomwa na hapo mwili ukapumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.
Damini hakuamini kama mama yake hakuwa nae tena duniani , watu walimhurumia sana , lakini ndio la kutokea lishatokea
*******
Maisha mapya ya kijana damiani yalianza , yalikuwa ni maisha ya huzuni kwani alikuwa amemzoea mama yake sana na sasa hakuwa nae tena duniani , kwake aliona kama ndoto na asubuhi ataamka na kumkuta mama yake , lakini haikuwa ndoto tena ulikuwa uhalisia na mama yake hakuwpo tena duniani , kila akikumbuka ahadi alizojiwekea juu ya kumtoa mama yake katika umasikini alijikuta akihuzunika sana .
Wiki moja ilipita na siku hio ilikuwa ni asubuhi ni siku ambayo aliamka na mawazo mapya na aliona kabisa yakutokea yamekwisha kutokea na sasa anatakiwa kujikaza kama mwanaume na kuruhusu mambo megnine yaendelee . lakini siku hio pia alikumbuka tukio la yule mzungu kumpa bahasha flani iliojaradiwa na plastic alifikicha kichwa chake na hapo hapo alikumbuka sehemu aliokuwa ameificha , ilikuwa ni nje kwenye banda la mbuzi kwenye paa la nyasi kwani anakumbuka ndipo sehemu alio ichomeka siku ile kabla ya kwenda kumuita mzee kivinje , alitoka nje na kisha alisogelea banda lile na kisha aliingiza mkono sehemu alipo amini ndio alipoweka , lakini hakuiona alijaribu tena lakini hakuona , alijikuta akitafuta mpaka akikata tamaa , alilalia kibanda hicho akiwa anaangalia chini na kujiona kuwa na mkosi lakini ni kama kuna kitu alikuwa amekiona kwenye kinyesi cha mbuzi wale aliona plastc kama ile ile , alikurupuka na kukimbilia upande wa nyuma ya banda lile na kushika ile plastic na kuivuta na kweli ilikuwa ni yenyewe alijikuta akitabasamu na kuifuta uchafu ule na bahati nzuri ni kwamba ilikuwa imehifadhiwa kwenye plastic bag kwa hio ilichafuka juu tu .
Alisogea mpaka ndani kwao na kisha aliitoa kwa utaratibu bahasha ile na kutoa karatasi nne alizitoa haraka haraka na kuanza kupitia moja “: BRUNO LAMBERK BORN 1947 hapo alitambua kuwa mzungu yule alikuwa akiitwa kwa jina la bruno lamberk
“ owned properties ( mali anazomiliki )
Chini ilikuwa ni orodha mjumuisho iliokuwa na maelezo ya mali anazomiliki bwana Bruno ilikuwa ni mali nyingi bwana huyu ambazo alikuwa akimiliki kulikuwa n mashamba nyumba na namba account ya bank ya uswisi na card yake benki ambayo damiani hakuitambua “
Alipitia karatasi nyingine ilikuwa ni ramani ya Tanzania lakini ndani yake kulikuwa na sehemu zimechorwa kwa alama nyekundu ni kama zilikuwa zikionesha eneo husika hakutaka kuangalia sana hio karatasi alipitia ya pili yake ilikuwa na akaunti za benki ya CRDB na card yake lakini jina halikuwa la Bruno bali limeandika seline amber aliweka pembeni na ya mwisho ilikuwa na majina mengi karibia tisini , ila hakutaka kujihaingaisha nayo , alifungua kimkebe kilichokuwa ndani ya hio bahasha na ndani yake kulikuwa na vitu viwili moja ilikuwa ni flash disk , pili ilikuwa cheni yenye kidani kilichokaa kwa muundo wa msalaba lakini kina utofuti kidogo , aliachana na ile cheni na kisha akahamia kwenye ile flash , alijua kuna kitu kilikuwa ndani ya hio flash , alikumbuka alikuwa na laptop , alifuata kwenye begi lake na kisha aliitoa na ikawaka alisubiria window iload na ikakubali na hapo hapo hakutaka kuchelewa aliingiza password na kisha akchomeka ile flash.
CONTINUARA......
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO CHAKE
MWANDISHI: SINGANOJR
GENRE: FICTION (KUBUNI )
........................….........................................
UTANGULIZI
.....................................................
Damiani mhitimu wa chuo kikuu cha uhasibu , anahitimu masomo yake na kurudi kijijini kwao kwa ajili ya kusubiria upepo wa ajira lakini katika hali ya kutokutegemea mama yake kipenzi anapigwa risasi mbili za kifuani na kufa hapo hapo na hio inatokana na kumpatia msaada mwanaume ambae hamfahamu mwenye asili ya ulaya (mzungu ) ambae na yeye alikuwa kwenye hatua ya mwisho ya kupoteza uhai wake kwani alikuwa na jeraha la risasi tumboni ,lakini mzungu huyo kabla ya kupoteza maisha anamkabidhi damiani nyaraka bila kumpa maelekezo ya aina yoyote ile .
Damiani anajikuta anajenga chuki na kisasi kwa watu waliohusika na mauaji ya mama yake , anajiapiza kuwatafuta mahali popote pale na kulipiza kisasi , katika harakati za kuwatafuta wabaya wake anajikuta akifahamu siri nzito iliokuwa nyuma ya kifo cha ghafla cha raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania , anapata waraka ulioachwa na raisi huyo uliopewa jina la KAULI YA MWISHO YA RAIS KABLA YA KIFO CHAKE .
JE UNAFIKIRI ATAFANIKIWA KULIPIZA KISASI CHAKE ?
JE NI KAULI GANI YA MWISHO ALIO ACHA MHESHIMIWA RAISII KABLA YA KIFO CHAKE ?.
.
SEHEMU YA KWANZA>>≥>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Damiani ni kijana wa miaka ishirini na mbili mhitimu wa chuo kikuu cha TANZANIA INSTITUTE OF ACCOUNTANCY (TIA) akiwa amechukua kozi ya Finance and accounting in public sector(kozi inayohusu maswala ya uhasibu) , mara baada ya damiani kumaliza masomo yake hakutaka kubaki ndani ya jiji la dar es salaam , kwani hakuwa na kazi maalumu ambayo ingemuwezesha kujiingizia kipato ndani ya jiji hilo , pia maisha ndani ya jiji hilo yalikuwa ni ghali sana na yalikuwa yakihitaji pesa ili kuweza kuishi .
Hivyo mara baada tu ya kumaliza masomo yake aliamua kurudi nyumbni kwao kijijini mkoani Tanga kwa ajili ya kusikilizia upepo wa ajira kwani mwaka ambao alikuwa amemaliza haikuwa kama miaka ya nyuma kwamba ukimaliza tu unasubiria matokeo na kupata ajira , kinyume chake ni kwamba utasubiria matokeo yatoke na kuomba ajira kwa makampuni ambayo yatakuwa na uhitaji ama serikari pale itakapo tangaza nafasi za ajira na kuomba , na kwakuwa kipindi hicho kulikuwa na wimbi kubwa la vijana ambao walikuwa ni wahitimu na hawakuwa na ajira mtaani hivyo ilikuwa ni ngumu sana kupata ajira , ilikuwa ni kama kubahatisha tu pale nafasi zinapo toka kwani wengi waombaji wana sifa zinazofanana .
Mkuzi ndio kijijini kwa kijana damiani , kijiji hiki kilikuwa ndani ya wilaya lushoto kilomita kadhaa kutoka lushoto mjini , yaani kama utasafiri kwa gari ni muda wa dakika therathini mpaka arobaimi kufika ndani ya kijiji hichi , ni moja ya vijiji ambavyo vilikuwa vimezungukwa na misitu na kuwa na mazingira ya kuvutia sana , na yalikuwa ni moja ya mazingira ambayo watalii wengi wa mataifa ya nje na hata watalii wa ndani pia walikuwa wakipenda kutembelea na hio yote ni kutokana na hali yake ya hewa ilivyokuwa safi na ya kuvutia .
Basi kijana damiani ndani ya kijiji cha mkuzi ndio alikulia na kujipatia elimu yake ya msingi na sekondary .
Damiani alikuwa ni kijana mpole mcheshi mrefu maji ya kunde mwenye sura yake ya kuchongoka lakini ilioumbwa vizuri , alikuwa ni moja ya vijana walio kuwa na miili mikubwa ya wastani , Damiani alikuwa akiishi na mama yake tu kwani baba yake alikuwa amekwisha kufariki miaka mingi nyuma kipindi akiwa tu na umri wa miaka kumi .
Kurudi kwa damiani kijijini baada ya kumaliza masomo ilikuwa ni moja ya furaha kubwa sana kwa mama yake kumuona mwanae kurudi ndani ya kijiji hicho , kwani mama huyo alikuwa akimpenda sana mwanae .
" karibu sana mwanangu " mama alifurahia sana kwa mwanae kumaliza masomo yake ya ngazi ya juu , na kujihisi kuwa mwanamke aliefanikiwa kulea kwani watoto wengi ndani ya kijiji hicho hawakufanikiwa kufika ngazi ya juu ya kielimu kama ilivyokuwa kwa damiani .
" Asante mama , hatimae nimemaliza chuo na nimerudi rasmi " aliongea damiani huku akiachia tabasamu huku nje watoto wengi walikuwa wakimwangalia na kumshangaa , hio ilikuwa ni kawaida sana kwa vijiji kushangaa watu walio tokea mjini na hata kwa wageni pia .
Basi damiani alikaribishwa vizuri na mama yake katika nyumba yao hio ya vyumba vitatu ilio ezekwa kwa samora , na kwakuwa damiani alikuwa na chumba chake tokea akiwa shuleni ndiko mama yake alipeleka begi lake na kukifanyia usafi .
Maisha ya kijana damiani yanaanza rasmi ndani ya kijiji cha mkuzi , licha ya damiani kuwepo ndani ya kijiji hicho lakini alikuwa na mipango mikubwa sana ya maisha yake hapo mbeleni , kwani alihitaji kuja kuwa mfanya biashara mkubwa sana katika maisha yake na hio ilikuwa ndio moja ya ndoto yake kubwa, japo alikuwa amesoma na alikuwa akitarajia kuwajiriwa lakini ajira kwake haikuwa kipaumbele , ila kipaumbele kwake ikikuwa nikupata mtaji utakoa mwezesha kuanzisha biashara , hakika alikuwa na safari ndefu sana na hata kwa yeye pia alilijua hilo na hivyo kwa umri aliokuwa nao hakuwa na sababu ya kukatishwa tamaa na mazingira aliokuwemo na aliokulia , kwani alichokuwa akikiamiani katika maisha yake ni juu ya uchapaji kazi kwa bidiii na kutokukata tamaa na kuwa na malengo ndio nguzo kubwa sana ya kuja kufanikiwa , hakutaka kabisa kukatishwa tamaa na hali ya maisha yao ya umasikini yaliopo hapo nyumbani , ila aliamini katika mawazo chanya tu .
Basi hatimae wiki ,mwezi na hata miezi ilikatika na matokeo yake yalikuwa yamekwisha kutoka na akiwa amefaulu kwa ufaulu wa daraja la kwanza , kwake na kwa mama yake ilikuwa ni furaha na faraja kubwa sana , kwani aliamini kupitia ufaululu mkubwa basi angeweza kumrahisishia kupata kazi kwa wepesi zaidi .
Hakutaka kusafiri mpaka dar es salaam kwa ajili ya kuomba kazi ilihali kulikuwa na njia rahisi , alichokifanya yeye ni kutuma maombi kwa kila kampuni ambayo iljkuwa ikitangaza nafasi za ajira kwa njia ya mtandao .
Mwezi wa kwanza uliisha kijana damiani akiwa amekosa kabisa uelekeo wa ajira kwani ni makampuni zaidi ya matatu ambayo alikuwa ameomba kwa ajili ya kupata ajira lakini amekosa hata wito wa interview( mahojiano ya kiufanisi ) , zikiwa zimepita siku kadhaa za kijana damiani kukata tamaa hatimae kwenye moja ya kampuni ambayo haikuwa imetoa majibu ilirudisha jibu kwa kijana damiani kwa ajili ya kuhudhuria interview .
ilikuwa ji moja ya kampuni ilio kuwa ikipatikana ndani ya jiji la dar es salaam ,kampuni moja ya usafirishaji iliokuwa na makao yake makuu ndani ya posta , kwake damiani alifurahia kwani aliona tumaini la kupata ajira linaridhisha zaidi , alimwambia mama yake juu ya taarifa hio na mama yake pia alifurahia na kumpa baraka zote mwanae kwa ajili ya kuhudhuria interview hio.
Ilikuwa ni siku ya jumatatu ndio siku ambayo kijana damiani alikuwa ndani ya basi akielekea jijini dar kwa ajili ya kuhudhiria interview ,alifanya maombi juu ya safari yake hio na kusudio lake analoliendea kulifanyia kazi.
Kutoka lushoto mpaka ndani ya jiji la dar ni umbali wa masaa sita mpaka saba , hivyo damiani alikuja kufika ndani ya jiji hilo kwenye muda wa saa nane kamili mchana ,siku hio alipanga akifika ndani ya jiji hilo kwakuwa hakuwa na ndugu wa kufikia , alipanga kwenda kwa rafiki yake mmoja aliekuwa amemuacha ndani ya chuo akiendelea na masomo kwa ajili ya kumuhifadhi mpaka siku inayofuata afanye interview na kisha ageuze kurudi nyumbani .
Basi baada tu ya kushuka ndani ya basi akijisogeza mpaka kwenye daladala zinazoelekea mbagala na kisha alipanda huku malengo yake aje ashukie mtongani kwa azizi ally kwani hapo ndio rafiki yake huyo alipokuwa akipatikana kwa kuishi , barabara haikuwa na foleni sana hivyo hawakuchukua masaa mengi kufika sehemu aliokuwa amekusudia .
Mara baada tu ya kushushwa hatimae alinyoosha moja kwa moja upande wa kushoto wa barabara , huku akipita vichochoro viwili vitatu na kuja kutokelezea mbele ya nyumba moja kubwa iliokuwa na ukuta, Hatimae alisimama nje ya geti la nyumba hio huku nikama ni mtu aliekuwa akijishauri agonge ama asigonge , ila kwakuwa kilichomleta hapo ni kuonana na rafiki yake na rafiki yake alikuwa akiishi ndani ya nyumba hio basi hakuwa na budi ya kugonga geti hilo.
Haikuchukua muda mrefu hatimae alikuwa amefunguliwa na msichana mmoja aliekuwa amejifunga khanga moja , na alionekana alikuwa akifua kwani alikuwa na mapovu mikononi .
" Karibu " sauti hio nyororo ilimkaribisha ndani huku.dada huyo akitangulia mbele na kumuacha kijana damiani kumsanifu mdada huyo kwa nyuma , alikuwa ni mlimbwende kweli aliekuwa amejaliwa umbo zuri haswa la kumvutia kila mwanaume atakae mtia machoni , alikuwa mrefu wa wastani mwenye rangi yake ya chocolate , alibarikiwa uso wa duara na kwa tathimini za haraka haraka mdada huyo alionekana umri wake haukuwa si chini ya miaka ishirini kwenda juu.
" nimemkuta elvisi ??"
" katoka sema anakuja muda si mrefu , wewe ndio Damiani ??"
" Ndio ni mimi "
" " Okey ! Alinipa maelekezo yako kwamba ukifika nikukaribishe ndani " aliongea msichana huyo huku akimkaribisha damiani ndani kwani muda wote huo alikuwa amesimama , Damiani alijua lazima huyo bidada atakuwa hawara(mwanamke anaeishi na mwanaume pasipo kuolewa au mpenzi ) wake elvis maana alimjua mngoni huyo songea kwa kupenda warembo hakuwa nyuma na ndio maana kabla ya kutoka nyumbani alimtaarifu kuwa atakuja kulala kwake .
Basi bidada huyo alimuongoza damiani ndani ya nyumba hio iliokuwa imepakwa rangi nyeupe mpaka kwenye chumba cha katikati upande kushoto na kisha alimkaribisha ndani , kilikuwa ni chumba kimoja kikubwa saizi ya kati kilichokuwa kimejaa makorokocho mengi , Damiani alikuwa akikijua chumba hichi sana kwani hata kwa baadhi ya vitu hivyo villkuwa vyake na ni baada ya yeye kumaliza masomo alimuuzia rafiki yake huyo .
Basi baada ya kukaribishwa dada yule alitoka nje na kuendelea na shughuri yake ya ufuaji huku akimwacha damiani akimsubiri rafiki yake , na haikuchukuwa hata dakika isbirini rafiki yake elvisi aliingia ndani ya nyumba hio , elvisi alifurahia sana kumuona damiani na hata kwa damiani ilikuwa ni hivyo hivyo , wote walifurahia kuonana kwa mara nyingine .
" karibu sana HB asietaka warembo " aliongea elvis akionesha kumtania mwenzie na kwa damiani kwakuwa alikuwa ashamzoea rafiki yake huyo kwa matani basi na yeye alicheka .
" mzee wa totozi , naona shemeji yangu wa awamu hii ni shida "
" Yaani acha tu mzee toto la toto na isitoshe limedata na ndio limenifanya nihangaike siku ya leo "
" Unahangaishwa na nini sasa?? "
" hahaha lazima kuhangaika , unajua jana ulivyonicheki unakuja ilikuwa ghafra sana na sikutaka kukwambia naishi na mtoto wa kike, kwa hio unavyoniona hapa kuna msela nimetoka kumpanga ili ukale mbonji kwake ukamilishe mambo yako maana hapa sikuwa na jinsi "
" Daah ! hapo ndio maana nakukubali mshikaji wangu "
" hahaha .. usijali mzee si unajua hata wewe umenisaidia mara kibao , hata mavitu haya ni kama ulinipa tu kutokana na bei ile "
Basi damiani walichukuana na rafiki yake na kutoka eneo hilo kuelekea barabarani na kupanda magari ya kuelekea Rangi tatu , walivyo fika mbagala zakhemu walishuka na kuchukua upande wa kushoto barabara , umbali wa mita kadhaa hatimae waliingia chochoro ambayo walikuja kuibukia mbele mtaa mwingine , na wakaja kutokea mbele ya kanisa la KKKT na hapo walipinda kushoto tena na kukuta nyumba moja kubwa iliokuwa na geti na kwa nje ilisomeka kwa maandishi ya lodge , elvis alisukuma mlango na kisha aliingia ndani , kwa damiani yeye alikuwa akifatisha tu kuona mwisho wake kwani kuna hisia zilizokuwa zikimwambia kaletwa lodge
" Oya mshikaji anakaa hapa , sio lodge hapa tena japo ilikuwa lodge , mwenye nyumba kaamua kuifanya nyumba ya kupangisha " aliongea elvis na kumfanya Damiani aelewe , walipita kwenye vyumba kadhaa na hatimae walisimama nje ya mlango na elvisi aligonga na nusu dakika mlango ilifunguliwa na jamaa mmoja wa makamo mfupi mwenye mwili mkubwa wa kibonge .
" Karibuni "
Waliingia ndani ya chumba hicho , kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri sana , na pia hata kitanda na samani(furniture) zilizokuwemo humo ndani zilionesha jamaa anaeishi humo ndani hakuwa mnyonge kipesa .
" oyaa huyu ni joshua rafiki yangu sana mwaka wa kwanza hivyo ndio utachili hapa kwake mpaka utakapo kamilisha mambo yako " aliongea elvis na joshua alimkaribisha Damiani na elvisi aliaga akaondoka .
Basi siku nyingine iliingia ambayo ni siku Damiani alikuwa akielekea mtaa wa posta kwa ajili ya kufanya interview , alikuwa amevaa akapendeza maana kwenye nguo alikuwa nazo na mkopo ulimsaidia sana kipindi akiwa chuo .
Alijisogeza mpaka barabarani ili kusubiria gari ya kwenda stesheni posta apande , ila mara baada ya kufika tu kwenye barabara nje kabisa ya supermarkert iliosomeka kwa jina la Kivoni , ilisimama gari moja aina ya vanguard nyeusi na kioo kilishushwa na akaonekana bwana mmoja wa makamo , makadirio ya miaka 30 kuendelea mweusi alivalia shati jeupe na koti akiwa na miwani , Damiani wakati huo gari hio ikisimama alikuwa akiiangalia na hata jamaa huyo alivyoshusha kioo alikuwa pia akimwangalia , Damiani alijikuta akijishtukia na hio ni mara baada ya jamaa huyo kumuonesha ishara ya kumuita , alijihakikishia kama ndio yeye aliekuwa akiitwa na hapo ndipo alipo piga hatua kulisogelea gari hilo
INAENDELEA HIVI PUNDE ........
SEHEMU YA 02.
INAENDELEA
“Vipi wapi unaelekea ?”. aliuliza mwanaume yule
" Naelekea posta "
" Okey ingia twende , naelekea upande huo , nina baadhi ya maswal nataka nikuulize " aliongea jamaa yule na kumfanya hata damiani ashangae inakuwaje mtu asie mjua awe na maswali ya kuulizwa na yeye ,jambo hilo lilimpa mashaka mengi juu ya mtu huyo .
" fanya haraka , ingia acha uoga asubuhi yote hii unawaza mambo mabaya " aliongea yule jamaa na ni kama alijua ni kitu gani alikuwa akimaanisha na Damiani kwa mashaka mengi alijiingiza kwenye gari hilo na kisha likawashwa na kuondoshwa eneo hilo .
" Unaenda kufanya interview ?" aliuliza yule bwana na kumfanya damiani ashangae Zaidi ni kivipi kajua anaenda kufanya interview .
" usiwe na wasiwasi mimi nimeishi miaka mingi na najua hulka ya vijana wengi hasa wanaoenda kuomba kazi na wewe kwa uvaaji wako unaonekana kabisa unaenda kufanya interview kama sio kuomba kazi .”
" Yeah! naenda kufanya interview " alijibu
" umesomea kozi gani na elimu yako ni kiwango gani ?? "
" Degree of finance and accounting in public sector"
" okey safi na hongera , unapaswa kujiamini tu na maswali ya kawaida sana wanauliza , unaweza ulizwa elfu kumi ina mnyama gani na ukakuta swali lina maksi nyingi "
Aliongea yule bwana huku akiongeza umakini katika barabara hio iliokuwa na magari mengi asubuhi hio .
Hawakuchukua muda mrefu walikuwa posta , na gari ilisimamishwa kwenye jengo la waterfront na Damiani akashuka , huku bado akiwa na dukuduku la maswali mengi kichwani mwake kwa jamaa yule kwa jinsi alivyomwambia wakati wa kumpandisha kwenye gari kwamba alikuwa na maswali ya kumuuliza , lakini cha kushangaza hata hayo maswali yenyewe hakuulizwa , ila hakutaka kufikiria sana na aliona ni labda jamaa huyo hakuwa na nia ya kumuuliza maswali ila alikuwa akitaka tu kumsaidia kwa kumpa lift na kama alivyosema alijua kuwa alikuwa akielekea kwenye interview .
Basi wakati akiwa anatembnea kuelekea upande wa samora alijikuta akikumbuka yale maneno ya kwamba anaweza kuulizwa maswali ya kawaida sana hata elfu kumi ina mnyama gani , na hapo ni kama amekumbuka kitu , alianza kujiuliza elfu kumi ina mnyama gani lakini hakuweza kabisa kupatia alijaribu kuchekescha akili yake ili kupata jibu la elfu kumi ina mnyama gani lakini alijikuta akikosa jibu kabisa , aliinua mkono wake wenye saa na kuona bado alikuwa na muda wa kutosha kabla ya interview kuanza .
Basi kijana damiani alijiamulia kusogelea duka moja lililokuwa na tigo pesa kwa ajili ya kutoa kiasi kidogo cha pesa ambacho kitamsaidia katika mahitaji yake ya siku hio na pia kilichokuwa kingebaki angefanya nauli ya kurudi nyumbani kwao lushoto.
“ kumbe tembo daah ! upuuzi kabisa yaani siku zote naishika hii hela nimeshindwa kujua kuwa mnyama ni tembo haha .. “ aliongea huku akivuka barabara na kutembea hatua chache tu aliona jengo alilokuwa akilitafuta mita kadhaa kwani ndipo kampuni ya usafirishaji aliokuwa akiitafuta na kwenda kufanya interview ndio ilikuwa ikipatikana katika eneo hilo .
Alijikuta akipigwa na mshangao mara baada ya kufika ndani ya eneo hilo maana kulikuwa na watu kibao waliokuwepo ndani ya eneo hilo na wote hao walionekana walikuwa wameitwa kwa jili ya kufanya interview .
“ hapa kweli kuna kupata ajira kweli?? “ alijiongelesha huku akiingia ndani kabisa ya jengo hilo na kwenda mpaka eneo la mapokezi na aliambiwa kuwa utaratibu ni kusubiri kwani interview itaanza muda sio mrefu .
Basi alijiunga na wenzie kwa ajili ya kusubiri na hakutaka kukata tamaa kirahisi kwani alikuwa amejiandaa vya kutosha na siku zote aliamini kwamba kwenye nafasi ya watu kuchaguliwa na wakawa na nafasi sawa basi hakuna kukata tamaa na hata yeye anayo nafassi ya kushinda na kupata ajira hivyo alizidi kujipa moyo na kujiandaa na interview , ni baada ya kama dakika arobaini hivi ndio watu wote waliitwa kwa kuanza interview, ilikuwa ni written interview(mahojiano ya kuandika ) katika nafasi ya finance manager( msimamizi wa fedha ) .
Basi mameneja rasilimali watu waliokuwa wakisimamia interview hio walitoa taratibu na maelekzo ya kila namna na hatimae interview ilianza , ajabu kwa damiani ni kwamba jambo lile aliloambiwa kule na yule mtu aliempa lift likuwa ni vile vile na hata yeye alijikuta akishangaa sana ilikuwaje jamaa yule akajua kwamba ataulizwa swali la kwamba elfu kumi ilikuwa na mnyama gani ilikuwa ajabu ilio jaa bahati .
Basi interview ile ilienda vizuri kwa upande wake huku akiamini kabisa amefanya vizuri na kilichofata hapo ilikuwa ni matokeo tu ya interview hio , japo mtu yule wa asubuhi alikuwa na mashaka nae ila alijikuta akiona kwamba mtu yuke alikuwa kama malaika kwake alietumwa na mungu . .
*****
Upande mwingine ndani ya jengo la LPPF tower lililokuwa likipatioana ndani ya mikocheni sayansi kuna gari moja nyeusi aina ya range rover sport ilisimama asubuhi hio ndani ya eneo la kupark magari na alishuka mwanaume mmoja mwenye umri kati ya miaka hamsini hivi aliekuwa amevalia suti yake nadhifu kabisa iliomkaa vizuri , alikuwa na mwili mkubwa kidogo na alionesha hali yake ya kiafya sio mbaya , alikuwa ametangulizana na bwana mmoja hivi aliekuwa amevalia miwani na bila shaka alikuwa ni mlinzi wake kama sio msaidizi .
Basi alitembea kuingia ndani ya jengo hilo huku mkononi alikiwa ameshikilia miwani yake ya jua na yule msaidizi wake akiwa ameshikilia briefcase nyeusi ,walifatana mpaka kwenye lift na kisha walibofya kitufe cha namba kumi na sita kuashiria ndio floor waliokuwa wakielekea , haikuwachukua muda mrefu walikuwa ndani ya korido ndefu kidogo iliokuwa na mandhari ya kuvutia huku kwa mbele kabisa kulikuwa na maandishi yameandikwa KIMBONA INTERNATIONAL LINK AND COMPANY (KILAC)
Mzee huyo alitembea kwa mwendo wake wa taratibu lakini wenye afya na kufika eneo la mapokezi na alikutana na dada .mmoja alievalia nadhifu kabisa eneo la mapokezi na baada ya kumuona mzee huyo alisimama haraka na kusalimia, alikuwa ni secretary .
" shikamoo boss ,karibu kazini " aliongea dada huyo kwa heshima kubwa sana na mzee huyo aliitika huku akiwa sio mwenye kujali sana na akapita kuelekea ofisi moja iliokuwa ikisomeka jina la mkurugenzi , aliingia ofisini humo na kisha yule mlinzi aliweka ile briefcase juu ya meza
Ni moja ya ofisi iliokuwa ikivutia sana iliokuwa imenakishiwa vyema huku samani zilizokuwemo humo ndani zilionesha kuwa zillikuwa ni za bei ya juu sana lakini bei hio iliendana na ofisi kwani ziliipendezesha kwa ujumla wake .
"okey derick tutaonana baadae na hakikisha unafatilia lile.swala kwa umakini mkubwa maana baadae nina kikao na nataka kuwa kwenye nafasi nzuri kwemye kikao hicho "
" Sawa boss " aliongea kijana huyo kwa sauti ya kikakamavu kabisa na kisha aligeuka na kutoka ndani ya ofisi hio .
Hazikupita dakika kumi simu ilipigwa na ilitoka kwa sekretary na alimjulisha bossi wake huyo kuwa kuna mgeni wake na bwana huyo aliruhusu mgeni huyo kuingia .
" mister kimbona!. "
" Samueli! hahha ..Umefika lini Tanzania? " aliongea mister kimbona kwa bashasha sana huku akimlaki mwanaume huyo aliekuwepo mbele yake , alikuwa ni mwanaume wa saizi yake sio mrefu sana umri ulikuwa ni miaka arobaini hivi kupanda kimakadirio, akiwa amevalia suti yake ya gharama ya rangi ya blue .
" Nimefika juzi mara baada tu ya kupata taarifa za kunifurahisha moyo wangu ".
" hahaha karibu sana , unipe hizo taarifa , huenda na kwangu pia zikawa zakufurahisha .
" wewe ushazisikia sana na kama ni zakufurahisha basi zishakufurahisha mpaka zikachuja .
" hahahahaha... hahahaha... ni kweli kabisa usemayo na najua ni kipi una maanisha hahhaha.. , karibu sana Tanzania kwa mara nyingine kwenye nchi yako .
Basi walionekana kuwa maswahiba wakubwa sana hawa watu kwani walionesha furaha sana kwenye nyuso zao na walionekana kufurahia jambo .
" Nimekuja Tanzania kwa kazi maalumu , naamini unaelewa biashara zetu hizi zilivyoyumba ndani ya utawala wa mwendazake , sasa baada ya kusikia taarifa ya kwamba keshatutangulia mbele za haki , kwangu ilikuwa njema sana na niliona ni wakati mwingine tena wa kufufua biashara zetu .
" ni kweli usemayo , lakini sidhani kama itakuwa ni rahisi na jambo la kufanyika haraka haraka maana linahitaji connection na unajua nchi yetu imeimarika ki ulinzi kwa sasa .
" Ndio hilo nalifahamu fika , na ndio maana nikasema nimekuja kwa kazi hio na mtu ambae naamini atanisaidia kwenye mpango huo ni wewe , we have to establish our destroyed system once again."
"Nimekusikia na ninaelewa shauku na mipango yako , lakini mimi nakusaidiaje katika hilo ?."
" Nafikiri unaelewa mister bruno ndio alikuwa chanzo kwa sysytrm yetu kufa hapa nchini mara baada ya mwendazake kuchukua madaraka "
" Ndio nalielewa fika swala hilo "
"Sasa hapo ndio pa kuanzia "
" Kivipi sam??? "
" come on! Kimbona usiniambie siku hizi umekuwa mlokole kiasi cha kupelekea akili yako kushindwa kung'amua swala dogo kama hilo ."
" haha….you meaan to kill him?? "
" correct , na naamini hilo ni swala unalo liweza sana na lipo ndani ya uwezo wako , naujua upande wako mwingine , na ukiutumia vyema tutafanikiwa katika hili , na nakwambia mtu wa kwanza kupata faida sio mimi tu ni wewe pia maana utakuwa pia kwenye system " aliongea mwanaume huyu anaejulikana kwa jina la samueli kwa lugha yake iliojaa tamathali za nchi za nje .
Bwana kimbona alijikuta akiwaza na kukuna kichwa na akainua uso wake akamwangalia sam usoni na kisha aliachia tabasamu .
"Assume its dome from now on , We are back my friend " aliongea huku akimfanya sam kufurahia sana na kisha walipeana mikono na kutakiana siku njema na kisha wkaagana huku sam akimsisitizia kuwa swala hilo lifanyike mapema .
*******
Katika watu waliotoka na sura zilizojaa tabasamu alikuwa ni kijana Damiani , huku wenzake wengi wakitoka na nyuso za kuonesha kukata tamaa kwa kile walichokutana nacho .
" Daah ! nakutumia kwangu kote pesa eti leo nimeshindwa kung'amua elfu kumi ina mnyama gani , hata hawa HR wenyewe wanazingua " aliongea kijana mmoja aliekuwa na marafiki zake hapo akionesha kulalamika kwa kukutana na swali kama lile kwani lilikuwa ni swali ambalo halikuwa la kawaida na la kutegemea hasa kwa nafasi kama hio ya finance manager (usimamizi wa pesa ).,hakuwa kijana mmoja tu aliekuwa akilalamika ila wengi walionyesha kuchukizwa na aina hio ya swali na kilichowakasirisha ni kwamba maswali yale magumu yaliwekewa maksi chache . .
" Mambo ! " Ilisikika sauti moja nyororo sana ya kuamsha hisia kwenye ngoma za masikio ya Damiani na kumfanya ainuke kwani wakati huo alikuwa ameegamia uzio kuangalia upande wa barabarani magari yaliokuwa yakipita na watu waliokuwa kwenye hekaheka za siku hio .
Alikuwa ni msichana mrembo kweli kweli , alikuwa mrefu saizi ya kati , aliekuwa na rangi flani hivi ambayo kwa haraka haraka ungejua kabisa mlimbwende huyu alikuwa ni mchanganyiko wa mataifa mawili ,kama sio wa muhindi basi ni mzungu na mwafrika , huku baba yake akiwa ni mzungu kamili ama mhindi , alikuwa anavutia kwakweli na hasa tabasamu alilokuwa ameachia usoni mwake lilimfanya vishimo vyake kwenye mashavu vizidi kuupamba uso wake na kumfanya kijana damiani abung'ae .
" poa mambo " alijikuta akiitikia ki uoga uoga
" Naitwa merina wewe je ??"
" Damiani " .
" Ohoo ! Na wewe upo kwenye interview?! "
" Ndio " .
" Hata mimi pia , nafrah kukufahamu Damiani " Aliongea msichana huyo na alionekana kuwa mchangamfu kwani ndio aliekuwa ametawala maongezi hayo .
" by the way how is written ?" aliongea mwanadada huyo kumuuliza swali hilo na kumfanya Damiani atabasamu kidogo na kisha alijibu .
" Nashukuru mungu , ilikuwa safi , and you ??? "
" Me pia " jibu hilo lilimfanya Damiani awaze na kuona kati ya watu waliokuwa wamefanikiwa kujua elfu kumi ina mnyama gani basi hata huyo mlimbwende atakuwa amepatia , sasa swala hilo kidogo lilimnyima raha maana aliona kuwa nafasi yake inakuwa ndogo ya kuchaguliwa ila hakutaka kuonyesha hilo na kukata tamaa ,
" Umetokea chuo gani?"
" Harvard " jibu hilo lilimfanya Damiani ashangae kwani alijua duniani chuo kinachotamkika kwa jina hilo kilikuwa ni chuo kikubwa duniani na kilikuwa hakipo tanzania bali kilikuwepo ndani ya nchi kubwa duniani yaani Marekani .
" You mean USA ??"
" Yeah !." Hapo Damiani ndio alipochoka maana alijua kama mwanadada huyo alikuwa amepatia maswali yote ya written basi hata kama yeye atapita na kwenda oral interview basi asingefua dafu mbele ya bidada huyo man a kwanza chuo tu kingembeba .
" congratulation (hongera ) "
"Thanks!, And you? "
" TIA "
" ooh! Kipo wapi? "
" Tanzania institute of accountancy kipo njia ya mbagala " aliongea Damiani huku akionekana hata mood ya kuongea na mwanamke huyo ikipotea ghafra kwani aliamini kwa nafasi hio moja iliokuwa ikipiganiwa na mamia ya wahitimu asingepata kitu kabisa , kiufupi alinyong'onyea .
Basi damiani aliachana na mlimbwende yule na hio ni mara baada ya kutangaziwa kuwa majibu yatatoka kesho na kwa wale ambao wamepita kwa hatua inayofata basi watajulishwa na ukiona wewe mpaka saa nne asubuhi hujapata ujumbe wowote ama simu kutoka kwetu basi jua hujapita na tunakushukuru sana kwa kushiriki .
Kwa damiani alikosa Tumaini kabisa na aliona ni kama alipoteza hela zake tu za kuja jijini dar ,alitamani kuondoka siku hio hio kurudi lushoto kwao lakini hakutaka kuondoka siku hio hio , aliona ngoja asubiri akapambane na mwanadada yule , kwani aliamini pia kumaliza kwenye chuo kikubwa sio tija, tija ni kuwa competent(uwezo) kwa kile unachokijua .
Alirudi zake mbagala huku akiwasiliana na mama yake juu ya siku yake ilivyo enda , huku mama yake akiendelea kumpa nguvu ya kutokata tamaa bali azidi kujipanga , alirudi mpaka zakhem mbagala bahati nzuri au mbaya hakumkuta yule joshua ila kwakua alikuwa amepewa ufunguo aliingia na kujipumzisha huku akianza kufikiria matukio yote ya siku hio ,kuanzia asubuhi mpaka muda huo , alijikuta akitabasamu na kuna jambo lilimpa nguvu zaidi na kuona kama mungu alikuwa na makusudi ya kupata ajira kwa wiki hio atapata kwa hio hakutaka kukata tamaa , kwani alivyokumbuka mtu yule wa asubuhi alivyomuambia kuhusu elfu kumi ina mnyama gani na kweli swali hilo likawepo kwenye interview basi aliona ni mungu ndie aliemua kujidhihilisha kwake kupitia mtu yule , kwa hio hakuona kuna haja ya kukata tamaa .
Siku nyingine iliwadia na kwa damiani alikuwa na furaha sana kwani alikuwa tayari amekwisha kupokea ujumbe kuwa amepita kwenda kwenye oral interview , kwake ilikuwa jambo la baraka sana na alimshukuru mungu na alijipanga haswa kwa ajili ya lililoko mbele yake .
Aliagana na joshua huku akimtakia mafanikio mema na pia alimpigia mama yake kipenzi kwa hatua alio fikia na mama yake alimuambia anamuombea , alifika barabarani na alibahatika kupata gari baada ya kufika tu lililokuwa likielekea stesheni na alipanda , ndani ya madakika machache alikuwa chini ya jengo la kampuni hio .
Alitembea kwenye ukingo wa barabara na kisha alikunja kushoto na kuingia eneo hilo na wakati huo huo anaingia gari aina ya Audi new model rangi nyeupe ilisimama na alishuka yule dada wajana Merina na alionyesha alikuwa akiendesha yeye mwenyewe , alimuoa a Damiani na mdada ndio wa kwanza kuita jina la damiani kwani Damiani wala hakuwa hata na habari nae .
" Mambo "
" Poa , za toka jana?. "
" Safi , hongera " aliongea merina na kutabasamu huku akionekana hakuwa na wasiwasi wowote kabisa hali iliomfanya Damiani kuamini kwamba mdada huyo alikiwa na uhakika wa kupata nafasi hio .
Waliongozana na kupewa utaratibu na muda kidogo alianza merina ,siku hio walikuwa wa nne ndani hapo , aliingia merina na ndani ya dakika kumi na tano alitoka , na aliingia mwingine na kisha aliingja Damiani , aliulizwa maswali kadhaa na akajibu ki ufasaha kwa kadri anavyojua na kisha alimaliza interview yake.
UNAFIKIRI NI BIASHARA GANI ,
.................SEHEMU YA TATU..............
.
ILIPOISHIA
Siku nyingine iliwadia na kwa damiani alikuwa na furaha sana kwani alikuwa tayari amekwisha kupokea ujumbe kuwa amepita kwenda kwenye oral interview , kwake ilikuwa jambo la baraka sana na alimshukuru mungu na alijipanga haswa kwa ajili ya lililoko mbele yake .
Aliagana na joshua huku akimtakia mafanikio mema na pia alimpigia mama yake kipenzi kwa hatua alio fikia na mama yake alimuambia anamuombea , alifika barabarani na alibahatika kupata gari baada ya kufika tu lililokuwa likielekea stesheni na alipanda , ndani ya madakika machache alikuwa chini ya jengo la kampuni hio .
Alitembea kwenye ukingo wa barabara na kisha alikunja kushoto na kuingia eneo hilo na wakati huo huo anaingia gari aina ya Audi new model rangi nyeupe ilisimama na alishuka yule dada wajana Merina na alionyesha alikuwa akiendesha yeye mwenyewe , alimuoa a Damiani na mdada ndio wa kwanza kuita jina la damiani kwani Damiani wala hakuwa hata na habari nae .
" Mambo "
" Poa , za toka jana?. "
" Safi , hongera " aliongea merina na kutabasamu huku akionekana hakuwa na wasiwasi wowote kabisa hali iliomfanya Damiani kuamini kwamba mdada huyo alikiwa na uhakika wa kupata nafasi hio .
Waliongozana na kupewa utaratibu na muda kidogo alianza merina ,siku hio walikuwa wa nne ndani hapo , aliingia merina na ndani ya dakika kumi na tano alitoka , na aliingia mwingine na kisha aliingja Damiani , aliulizwa maswali kadhaa na akajibu ki ufasaha kwa kadri anavyojua na kisha alimaliza interview yake
INAENDELEA ……….
Basi baada ya damiani kumaliza interview ,alitoka huku akiwa amepewa maelekezo kwamba majibu yatatoka siku kumi zijazo kama amepata kazi au hajapata . .
Alitoka na moja kwa moja na kuondoka eneo hilo na alipanga siku hio hio kuondoka kuelekea Tanga maana muda ulikuwa ukirihusu .
Saa sita kamili alikuwa ndani ya basi la mining nice akielekea lushoto , alikuwa na nusu tumaini la kupata ajira , kwani kila akikumbuka bidada yule aliona kabisa kumshinda mtu alietoka katika moja ya chuo kikubwa duniani ni vigumu na ndio maana alikuwa na nusu tumaini na hilo lilikuwa ni kutokana na kwamba alikuwa amejibu vyema maswali alioulizwa , lakini alijua mfumo wa Tanzania ulikuwa ukiangalia sana nani katoka chuo gani .
Basi saa moja kamili ndio muda aliokuwa akiingia lushoto mjini , alishuka na nakisha alisogelea mpaka moja ya noah zilizokuwa zikielekea kijijini kwao na kisha bahati nzuri zilikuwepo , alipanda na kisha alisubiria baadhi ya abiria wajae na hatimae walifanikiwa kuondoka eneo hilo kuelekea kijijini kwao mkuzi .
Japo alikuwa na mawazo ila picha ya yule mwanadada ilikuwa muda mwingine ilikuwa ikimjia , kuna muda alijisema kama ingekuwa ni rafiki yake elvis mpenda warembo basi hata interview asingejali na angejali kumtongoza yule mwanamke , maana kila akimkumbuka aliishia kutabsamu na kukiri kwamba alikuwa mrembo haswa ambae hakuwa level yake .
Alikuja kushituka kwenye mawazo mara baada ya kufika mkuzi na konda kumshitua, aliangalia nje kama ndio sehemu aliokuwa akishukia , ila aliona anashukia kituo cha mbele yake kwa hio alimtaaarfiu kabisa konda na mara baada ya kufika eneo husika alishushwa na kuanza kuporomoka kwenye kijimlima kuelekea kijijini kwao , kijiji cha mkuzi kilikuwa na umeme kila kona , na pia kilikuwa kimechangamka na hata baada tu ya yeye kushuka alionekana na baadhi ya watu waliuokuwa wakimfahamu na walimsalimia na watoto walimpokea na kupeleka mizigo kwao .
********
Ilikuwa ni siku kadhaa tokea raisi wa tanzania apoteze maisha , raia wengi wa tanziania walikuwa kwenye maombolezo ya siku ishirini na moja , japo kiongozi huyo alikuwa amezikwa lakini watanziania wengi waliokuwa wakimpenda walikuwa wakimlilia na hio ni kutokana na raisi huyo kupendwa sana , .
Naam ! bendera onyango ni raisi wa awamu ya nane ndani ya taifa la Tanzania , ni moja ya maraisi waliokuwa na msimamo sana katika uongozi wake , na kupita hilo alitokea kupendwa sana na kundi kubwa la watanzania huku kundi lingine likuwa halimpendi na hio nikawaida sana katika siasa , licha ya raisi huyu kutopendwa na kundi dogo la watu ni raisi aliekuwa akijitahidi sana kutekeleza majukumu yake ya kazi , hususani yale ambayo alikuwa ameyaahidi katika kampeni zake , huku chini yake akiwa na makamu wake bwana henri mushi .
Hakika bwana onyango alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana katika kuhakikisha yale yote aliyo yaahidi kuyatimiza na hayo ni hususani katika maswala ya miundombinu , msimamo wake katika kusimamia kodi za raia ulimpa wafuasi wengi sana , lakini hata hivyo kuna waliokuwa hawampendi kwasababu zao ama ziwe za msingi ama sio za kimsingi ilihali binadamu hakuwa amekamilika na alikuwa na madhaifu yake basi hawezi kuwa sawa katika kila Nyanja za kiuongozi na hivyo hata bwana bendera alikuwa moja ya binadamu hao ambao hawakuwa wamekamilika .
Katika mambo ambayo bwana onyango alifanikiwa kuyakomesha ndani ya utawala wake moja wapo lilikuwa ni swala la madawa ya kulevya nchini , kwani alijitahidi kwa kushirikiana na wasaidizi wake na polisi kuhakikisha anaziba njia zote za uingizwaji wa madawa ya kulevya hapa nchini, na vile vile madawa kupitishwa nchini, na kwa asilimia kubwa hilo lilifanikiwa , lakini mwanzo wa kufanikiwa kwa jambo hilo ndio mwanzo wa kutengeneza maadui na wafanya biashara hao wa madawa , lakini kwakuwa kazi hio hakuwa akifanya mwenyewe, bali alikuwa akishirikiana na watu wengine na hao walikuwa ni mawaziri na wafanya biashara hao hao wa madawa ya kulevya , na moja ya wafanya biashara hao alikuwa ni bwana Bruno lamberk , huyu bwana alikuwa ni mzungu na alikuwa ndani ya nchi ya Tanzania kwa muda wa miaka ishirini na alikuwa ni moja ya wawekezaji wakongwe ndani ya tafia la Tanzania , bwana huyu alikuwa ni nmoja ya matajiri wakubwa sana waliotajirika wakiwa ndani ya taifa hili , lakini licha ya biashara zake za halali , pia alikuwa ni muuza ngada ndani ya ukanda wa afrika mashariki na kwa kifupi yeye ndie aliekuwa doni ndani ya ukanda wa afrika mashariki yote ,.
Bwana huyu haikujulikana kama alikuwa na familia au lah , kwani kwenye maisha yake hakuwahi kuishi na mwanamke zaidi ya wale wanawake wa kuja kufanya starehe na kuondoka , basi bwana huyu mara baada ya raisi bendera kuingia madarakani , haikujulikana raisi huyo alitumia mbinu gani kumnasa bwana huyo mpaka kupelekea bwana Bruno kutoa ushirikiano na kuwasaliti wauza madawa wenzake, na kupelekea biashara hio kwa Tanzania kufungiwa kabisa na haikuweza kufanyika ,na wauza madawa maarufu kukimbilia nje ya nchi , na moja ya watu waliokuwa wamekimbilia nje ya nchi alikuwa ni bwana Samuel saitoto(rich sam) , huyu alikuwa ni muuza madawa mkubwa sana ndani ya mtandao wa bwana bruno na baada ya kusalitiwa na rafiki yake ndipo alipo amua kukimbilia mexico pamoja na familia yake
Basi habari ya kifo cha raisi bendera kwa bwana Bruno ilikuwa ni pigo kubwa sana , kwani raisi huyo ndie aliekuwa akimpa ulinzi mkubwa sana zidi ya maadui zake , ni siku ya ishirini sasa tokea kuzikwa kwa raisi bendera ndani ya nchi ya Tanzania, bwana Bruno alikuwa amejificha ndani ya jiji la Tanga wilayani lushoto.
“ mkuu nimefanikiwa kuongea nae , anaoneakna ni kijana shupavu kama atakuwa na mafunzo maalumu atafaa kabisa “ aliongea bwana mmoja ambae tulimuona ndani ya jiji la dar es salaam , aliempa lift kijana Damiani . na siku hio bwana huyo alikuwa ndani ya wilaya hio na walioneakana walikuwa na mambo kadha wa kadha walikuwa wakiuongea .
“ Good nimempenda yule kijana na piga ua piga chini lazima tumuingize kwenye system , kwa hio endelea kumwangalia , maana muda si mrefu tutaexcute the plan , my enemies are looking for me , bendera is dead , no one can protect me now “ aliongea huku akiamaanisha kwamba muda mchache ujao wataendelea na mpango wao kwani bendera amekufa na hakuna mtu yoyte anaeweza kumlinda .
“Inabidi uondoke ndani ya nchi hii “
“ siwezi danny nitafia hapa hapa Tanzania “
“ but its too dangerous “{ lakini ni hatari sana )
“ najua na ndio maana nakwambia endelea kumtrack Damiani we need to prepare him ( akimaanisha aendelee kumchunguza damiani kwani wanatakiwa kumuandaa mapema .
*******
Kimbona kama alivyokuwa ameahidiana na samu juu ya kumtafuta bruno na kumpotezea mbali mzungu huyo , hakutaka kabisa swala hilo lifeli , na alikuwa na mood kweli ya kulifanya swala hilo , hasa kila alipokuwa akikumbuka ni kiasi gani alikipoteza mara baada ya Bruno lamberk kuwasaliti kwenye mtandao wao , kilimuuma sana , hela zake zilimpa nguvu ya kukamilisha mauaji hayo .
Haikumuia vigumu ,kwani ni kama alikuwa amepumzika katika biashara hio, kwani watu wake (gang) walikuwepo ndani ya nchi hio na alikuwa akiwalipa kisiri siri kwani alikuwa akiamini siku moja atarudi ulingoni na kuendelea na biashara hio, kwake baada ya kifo cha ghafra cha raisi bendera aliiona hio kama fursa nyingine ya kurudi kwa kishindo katika biashara hio ya uuzaji wa madawa ya kulevya .
“ Derick hakikisha unawapanga vijana mkao wa kazi , taarifa zilizopo kwa sasa kutoka kwa shushu wetu ndani ya TISS ni kwamba bwana Bruno kajificha ndani ya wilaya ya lushoto mambo view hotel.
“sawa mkuu vijana kwa sasa wako tayari na wanasubiria maelekezo yako tu “
“ basi safi , pumzika kwa leo na kesho nitakuambia nini cha kufanya , hakikisha swala hili linafanyika kwa weledi mkubwa , hakuna kufeli “
“ sawa boss “ huku akitoka
“ hahahahaha… hahaha… hii ni fursa nyingine kabisa kwangu naenda kurudi ulingoni muda si mrefu , Bruno …. Brunooooo …. Ama zako ama zangu “ aliongea tajiri kimbona kwa kicheko cha kifedhuli huku akigugumia wine yake aina ya black and white .
Siku ilio fuata derick alipokea simu kutoka kwa boss wake na kumtaarifu kufika kwenye kampuni yake ndani ya jengo la LAPF tower , kampuni iliokuwa ikjjulikna kwa jina la KILAC (KIMBONA INTERNATIONAL LINK AND COMPANIES }.
Derick haikumchukua muda mrefu kufika ndani ya jengo hilo la LAPF, alifika moja kwa moja na aliripoti kwa secretary na aliruhusiwa kuingia moja kwa moja na alisalimiana na boss wake huyo na kisha alipewa ramani nzima ya kufanya tukio hilo .
“ kuweni makini na Danny huyu ni jasusi wa kimataifa na ana mbinu nyingi za kuwazidi , lakini na nyie pia mna mbinu nyingi za kumzidi akili , narudia swala hili halina kufeli hakikisheni mnalimaliza baada ya siku kumi zijazo.
“ sawa boss “
Derick alitoka ofisini hapo na kisha hakutaka kuchelewa aliwashitua genge lake la kimafia na kuwapa ramani wapi wakutane kuelekea lushoto .
********
Ni baada ya siku kumi kupita kijana damiani bila kupokea ujumbe wowote kutoka kwa kampuni ambayo amekwisha kufanya interview , japo mama yake alimtia moyo wa kutokata tamaa ila kwake yeye ukiunganisha na yale anayo yajua mwenyewe hakuona nafasi kabisa ya kushinda kazi ile , alimwangalia mama yake aliekuwa amevaa nguo zilizoochanika na zisizokuwa zikivutia , alimuonea hruma sana , alitamani amtoe mama yake katika lindi hilo la umasikini kadri ya uwezo wake , kiufupi alikuwa akimpenda mama yake sana , kila akikumbuka misoto mama yake aliopitia kwa ajili ya kuhakikisha anasoma ,ilizidi kuumia mno aliilaumu serikali sana kwa kutokuwa na mfumo mzuri wa kutoa ajira kwa wanafunzi , kwani wahitimu walikuwa wakijitahidi kusoma sana kwa bidiii na pia wazazi wanawasomesha watoto wao kwa juhudi zote, lakini mwisho wa siku wanamaliza hakuna ajira , ilikuwa ni swala la kukatisha tamaa sana wazazi pia na wahtimu wenyewe .
Siku hio damiani aliamua kushinda na mama yake tu nyumbani hawakwenda popote , maana hata mama yake siku hio alikuwa kichwa kinamsumbua hivyo hakuweza kabisa kwenda kwenye vibarua vyake ambavyo vilikuwa vikimuwezesha kuleta nyumbani na kupata chochote tumboni .
Basi siku hio damiani alikuwa akitengeneza banda lao la mbuzi hapo uwani huku muda mwingi aliangalia emaili yake ama simu ikiita , kwani alikuwa na shauku kubwa ya kujua kama amepita ama hajapita , lisaa la kwanza likapita , la pili nalo likapita , la tatu hatimae la nne , mpaka saa kumi na moja hakukuwa na jumbe wala simu yoyote , aliweka simu chini huku akiona kabisa hakukuwa na tumaini lingine lililobaki la kupata ajira , hakuona sababu ya kukaa nyumbani hapo alimuaga mama yake kwa kumwabia anarudi muda si mrefu anaenda kwenye shanba lao la miti kwa ajili ya kuchukua miti kidogo aje amalizie banda lao la mbuzi , maana hakupenda kabisa kulala na mbuzi hao nyumba moja kwani mikojo yao ilikuwa na harufu kali .
Alitembea kwa muda wa kama nusu saa na hatimae alipita kijijini kwao , siku hio watu wengi walionekana kuwa barabarani kwani siku hio kulikuwa na sherehe iliokuwa ikifanyika kwenye kanisa moja la roman kwa hio watoto watoto alikuwepo huko na hata baadhi ya wamama pia , ni mama yake pekeee na baadhi ya wanakijiji waliokuwa wapo majumbani hasa wale wazee waliokuwa hawawezi kutembea , alitembea huku akiwa anakula apple kwani kijiji chao hicho kilikuwa na kilimo cha matunda aina ya apple , matunda damu na peasi na hata mananasi.
Basi baada ya dakika kama arobaini na tano hivi ndio muda alioingia kwenye shamba lao kubwa la miti ya biashara , hakutaka kuchelewa maana baada ya kufika tu alianza kazi ya kutafuta mikalitusi ilio nyooka na kisha kuikata , lakini wakati akiendelea na kazi hio simu yake ilitoa mlio kwamba kuna ujumbe umeingia , aliendelea kukata miti kwanza kama ishirini na aliridhika kwamba hio inatosha , ndipo alipo toa simu yake kuangalia ni ujumbe gani umeingia .
“ HONGERA BWANA DAMIANI RABANI UMEFANIKIWA KUPITA KWENYE INTERVIEW YAKO ULIO FANYA TAHEHE HIO , UNAPASWA KURIPOTI KAZINI MAPEMA KABLA YA TAREHE HIO”
Ulikuwa ni ujumbe uliomtoa machozi bwana damiani , yes yalikuwa ni machozi ya furaha alijikjuta akiruka ruka kwa furaha sana , hata ile kazi ya kukata miti iliishia hapo na jambo alilolifikiria kwa kwakati huo ni kurudi nyumbani na kwenda kumuonesha mama yake ili wafurahie pamoja , muda ulikuwa umeenda na kagiza kameanza kuingia alifunga miti yake haraka haraka huku akipiga mluzi wa furaha hata haikueleweka ni wimbo gani ulikuwa ukiimbwa .
Lakini wakati hayo yakiendelea mara alisikia kitu kilicho mfanya kunyanyuka haraka na kuangalia upande wa kushoto kwani kilikuwa ni kishindo kikubwa cha kitu kudondoka , lahaula ! ilikuwa mtu bwana kadondoka tena mwenye ngozi nyeupe huku akioneakana kuvuja damu nyingi usoni na ubavuni , damiani alipatwa na woga na akili yake yote iliwaza kukimbia kwa wakti huo , lakini alishuhudia mtu yule akimpungia mkono kwa shida kama anaomba msaada , ilibidi damiani aangalie kulia na kushoto kuona kama kuna mtu anakuja , maana akili yake ilicheza na kufanya kazi kama mashine kwa wakati huo na alijua mtu yule lazima atakuwa anawindwa kama sio kukimbizwa , alimsogelea kwa tahadhari .
“ help me to get out here wataniuu ..wa tafadhari nisaidie “ aliongea na kweli alikuwa mzungu kama damiani hisia zake zilivyokuwa zikimwambia , hakutaka sana kujishauri maana kweli aliona mtu huyo alikuwa akihitaji msaada , lakini alifikiria ni msaada gani anatakiwa kumpa , alichokifanya ni kurudi pale alpoacha miti yake na kisha aliichukua na kuisukumizia kichakani na haikueleka alikuwa na maana gani , kisha alimrudia yule mtu na kumuweka begani huku mzungu yule akiinua uso wake.
“shika hii just in case tusipofanikiwa , kimbia uniache.” Ilikuwa ni bahasha iliojaradiwa kwa mfuko wa plastic.
Damiani alivipokea huku akiwa hajui mzee yule alikuwa akimaanisha nini , ila kwakuwa wakati huo alichokuwa akiamini ni kumuokoa tu basi alijitahidi kadri ya uwezo wake kumtoa msituni hapo na kumfikisha nyumbani kwao kwani aliamini ndio ingekuwa sehemu salama , na angejua angefanya nini baada ya hapo
Uzuri ni kwamba giza lilikuwa limetamalaki hivyo kwa kupitia njia za vichaka aliweza kupita bila kuonekana kwa urahisi lakini pia kwakuwa watu walikuwa kwenye sherehe , alitembea na kufanikiwa kutoka kwenye msitu na hatimae aliingia ndani ya kijiji chao, alionekana na mbibi mmoja tu aliekuewa hawezi kutembea vizuri na kuongea pia kwani alikuwa amepinda mdomo , na kwa fununu ni kwamba ni adhabu alio pata katika shughuli ya ulozi wake .
Alimpitisha mpaka kwao na mama yake alipigwa na mshangao nusu apige kelele, lakini damiani alimzuia na kumwambia huyo mtu anataka msaada kamuokota huko msituni , mama yake alifungua mlango na walimpitisha kisha walimlaza kwenye kipande cha mketa , na wakati huo mzungu huyo hakuwa na fahamu , nadhani ni kutokana na kupoteza damu nyingi .
“ mama inabidi tumuite mzee kivinje anaweza kumsaidia nikifanya taratibu za kupata usafiri wa kumpeka hospitalini “( mzee kivinje alikuwa ni mganga kutumia mitishamba )
“ kwanini usimpeleke moja kwa moja akitufia hapa si itakuwa kesi “
“ hapana mama hali yake hio inaonesha anawindwa na inatupasa kumsaidia kwanza na kufanya mambo kwa umakini “ aliongea damiani kwa ujasiri mkubwa sana na kisha alitoka na kwenda kwa kivinje daktri wa mitishanmba lakini pia alikuwa mganga wa kienyeji .
Hapakuwa mbali sana , kutokana na mwendo wake alifanikiwa na bahati nzuri aliweza kumkuta bwana kivinje akiwa nje kashikiria kikombe na alionekana alikuwa akinywa maziwa ya mbuzi , damiani alieleza shida yake na kumstua sana kivinje na hakutaka kupoteza muda aliingia ndani na kutoka na dhana zake za kazi na kuongozana na damiani .
Haikuwchukua muda , walifika na kivinje alihitaji damiani amuoneshe mgonjwa alipo lakini hapo ndipo damiani aliposhuhudia kitu ambacho hakukitarajia kabisa .
Alimuona mama yake akiwa kwenye dimbwi la damu , huku mwili wa yule mzungu na wenyewe ukiwa kwenye dimbwi la damu , aliishia kutamka neno mama lakini sauti haikutoka.
INAENDELEA
INAENDELEA SEHEMU YA NNE
Damiani alijikuta akijikaza na kumkimbilia mama yake pale alipo na wala hakujali zile damu maana alimuinua mama yake huku akilia
“ mamaaa, mamama , amka mama nini kimetokea mama yangu … mamaaaa… mama amka “ mama yake damiani alikuwa akitapatapa na aliishia kunyosha mkono kuelekea mlangoni na hapo hapo akakata roho , ilikuwa ni huzuni kwake kwani alilia na kuutingisha mwili wa mama yake japo aamke , lakini haikuwezekana kabisa na kivinje ndio alimsogelea na kumshikilia asiendelee kufanya anacho kifanya
“ mama mama wee ,, mama amka mimi mwanao unaniacha na nani , mama yangu , bado sijapata nafasi ya kukutoa kwenye umasikini mama yangu wee …. Amka mamama nimefanikiwa kupata ajira sijakuambia bado mma amka mama weeee…..” ilikuwa ni huzuni na kama haukuwa na moyo basi ungelia ,maana mama yake alikuwa ameuwawa kikatili sana , watu tayari walikuw wamejaa kwani walisikia vilio hivyo , kila alieambiwa na kivinje kwamba mama damiani kafariki ilikuwa ni kilio kikubwa mno kwa kila aliekuwa akimjua mama huyo .
Watu waliendelea kulia ,damiani alikuwa amezimia wakati huo ,chopa ilisikika ikitua eneo la karibu ndani ya kijiji hicho na mwili wa yule Bruno ukichukuliwa na kupelekwa upande chopa ilipokuwepo , huku polisi nao wakiwa eneo la tukio , ilikuwa ni tukio la kusikitisha na kila mtu alikuwa akiongea lake , na wakati huo hayo yanaendelea vijana wa kimbona walionekana hapo na derick mwenyewe akiwa wamesimama upande wa juu hivi kuepuka watu kuwaona na mara baada ya kuona mwili wa Bruno ukitolewa na wao waliondoka eneo hilo .
*******
“Hahaha… hahahah…. Safi sana derick , kazi nzuri vijana wangu “ aliongea kimbona huku akionekana kuwa katika uso uliojawa na furaha ya ushindi baada ya kusikia kuwa bruno kazichapwa risasi na amekwisha kufa.
Hakutaka kuchelewa aliinua mkonga wake na kumpigia sam na kumpa tarifa hizo ambazo kwa sam alizipokea kwa furaha kubwa mno , na kumshukuru sana kimbona huku akimualika kuwa siku hio aende serena hoteli kuna watu anataka kuwakutanisha nao muda was aa nne usiku .
Na bila hiyana mzee huyo aliitikia wito huo kama atakuwepo eneo hilo bila kukosa , ilikuwa ni furaha sana kwa kimbona katika moja ya hatua ya kurudi kwenye biashara yake aliiona kabisa kwa mafanikio makubwa inakwenda kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana .
Ilivyofika muda wa saa nne usiku kimbona alimuaga mkewe na familia yake kwa ujumla na kisha alitoka na mlinzi wake kuelekea kwenye miadi yake kama alivyokuwa ameelekezwa na Samuel , kwakuwa ni usiku gari haikukawia kufika ndani ya hoteli hio ya hadhi ya juu sana ndani ya jiji la dar es salaam .
Alifika mpaka mapokezi na kujitambulisha hapo na kisha ni kama ujio wake ulikuwa umetegemewa kwani aliongozwa mpaka kwenye lift na mdada mmoja mrembo sana aliefika eneo hilo kumchukua , lift ilipanda mpaka kwenye floor ambayo ilikuwa na vyumba vya VVIP yaani kwamba hapo walikuwa wakiingia watu wa hadhi ya juu sana ndani ya jiji hilo , alitabasamu maana ilikuwa ni muda kidogo kuingia sehemu zilizokuwa zina ulinzi mkali kama aliouona ndani hapo .
Mdada yule mrefu mrembo alievalia suti yake ya zambarau na viatu vya high heels alitembea mpaka kufika kwenye moja ya chumba na kisha alifungua mlango na kumkaribisha bwana kimbona , kimbona alijikuta akiwa kwenye mshangao kwani watu waliokuwepo hapo ndani hakuwatarajia kabisa .
“ mheshimiwa , alijikuta kimbona akiongea kwa kupaniki kwani aliekuwa mbele yake alikuwa ni rais mstaafu wa awamu ya saba bwana Athumani ndalu , upande wa kulia alikuwepo waziri wa mambo ya ndani bwana musiba , mbele yake alikuwepo samueli , kulikuwa na jumla ya watu wanne ukimjulisha na yeye pia lakini kuna kiti kilionekana hakikuwa na mtu ..
“ hongeera sana bwana kimbona kwa ushindi wa leo “ aliongea raisi mstaafu .
“ asante sana mheshimiwa , unajua ni mara yangu ya kwanza kuonana na wewe laivu , ni heshima kubwa sana “
“ hahahaha.. kimbona huu ni mwanzo tu , na sasa unakwenda kukutana na mtu mkubwa Zaidi na penginepo wakubwa Zaidi karibu kwenye U-97( UNITY 97) aliongea sam kwa sauti ya majisifu
“U-97?” aliongea kimbona akimwangalia sam lakini hapo hapo mlango ulifunguliwa na hapo ndipo bwana kimbona aliposhangaa zidi kwani mtu aliekuwepo mahali hapo hakumtegemea kabisa.
“ Mheshimiwa raisi!!!”””” alijikuta akijisemea moyoni kwa mshangao
*******
Watu walikuwa wakizungumza hili na lile ndani ya kijiji hicho na habari zilitapakaa kila kona , kila mtu alikuwa akiongelea swala la mama damiani kupigwa risasi na watu wasiojulikana , pia mzungu kupigwa risasi ndani ya nyumba hio hio ya mama daniani na hata chopa kuja kumchukua mzungu huyo , watu hawakulala kila mtu alikuwa akiongea hili na lile ilimradi tu ni jambo la kuongea , lakini pia kuna baadhi ya watu walikuwa kwenye majonzi makubwa ya kupoteza uhai kwa mama damiani tena kwa kifo cha kikatiri sana , watu walilaani vikali kwa kilicho tokea .
Damini alikuja kupata fahamu lisaa limoja mbeleni akijikuta yupo ndani ya zahanati akiwa amelazwa , ni kama akili zake hazikiwa sawa wakati wa kuzinduka na hata nesi na daktari walimuona wakati wa kuzinduka huku kila mtu akiwa kwenye uso wa majonzi na kumuonea huruma kijana huyo , kwani waliona ni mambo makubwa na magumu ambayo anakwenda kupambana nayo katika maisha yake .
Ni kama mkanda wa filmu ulikuwa ukipita ndani ya kichwa cha kijana damiani , picha ya kumuona mama yake akiwa amelala kwenye dimbwi la damu zilianza kupita .
Alijikuta akitoa ukulele uliowafanya dokta amsogeleee haraka haraka na kumtuliza, hawakua na jinsi ilibidi wamchome tena sindano ya usingizi ambayo ilikuwa makali ya kuisha siku nyingine .
Ilikuwa muda wa asubuhi ambao habari za majambazi kumuaa mama damiani na mzungu zilisambaa lushoto nzima na kwenye vyombo vya habari.
Jeshi la polisi lilithibtisha kuwa wahusika wa mauaji hayo walikuwaa ni majambazi yaliokuwa na makazi yao katika msitu wa mlola huku wakihusisha swala hilo na tukio lililotokea miaka ya nyuma la kuvamiwa kwa chuo kikuu cha SEBATIANI KOROA MEMORIAL UNIVERSITY (SEKOMU) miaka iliopita huku wakiahidi uchunguzi unaendelea mpaka kuwatia hatiani majambazi hayo .
Upande wa damiani alifumbua macho asubuhi akiwa na akili zake zote , roho yake ilimuuma mno pale alipokumbuka duniani amebaki kuwa yatima , alijilaumu kwa kumsaidia mzungu yule kwani aliona kama angemuacha tu kule kule huenda yote hayo yasingemkuta mama yake , alijilaumu sana na kuhuzunika na moyo wake , lakini hakuwa na lakufanya kwa wakati huo , ilibidi aruhusiwe ili akashuhudie maziko ya mama yake , watu walimuonea huruma sana na kumpa pole , alizipokea huku akijitahidi kujikaza kiume .
Taratibu zote mazishi zilikuwa zimekwisha kufanywa na serikali , akiwemu mkuu wa wilaya aliehudhuria mazishi hayo.
Basi padri alifanya sala fupi na kuruhusu watu waage mwili akiwemo damiani alielia sana baada ya kumuona mama yake akiwa kwenye jeneza , alitolewa na watu wengine walipewa nafasi na hatimae mwili ulipelekwa makaburini
“SARAH RABAN AMEZALIWA MWAKA 1979 AKAFARIKI MWAKA 2019 AKIWA NA MIAKA 40 AMEACHA MTOTO MMOJA “ wosia mfupi ulisomwa na hapo mwili ukapumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.
Damini hakuamini kama mama yake hakuwa nae tena duniani , watu walimhurumia sana , lakini ndio la kutokea lishatokea
*******
Maisha mapya ya kijana damiani yalianza , yalikuwa ni maisha ya huzuni kwani alikuwa amemzoea mama yake sana na sasa hakuwa nae tena duniani , kwake aliona kama ndoto na asubuhi ataamka na kumkuta mama yake , lakini haikuwa ndoto tena ulikuwa uhalisia na mama yake hakuwpo tena duniani , kila akikumbuka ahadi alizojiwekea juu ya kumtoa mama yake katika umasikini alijikuta akihuzunika sana .
Wiki moja ilipita na siku hio ilikuwa ni asubuhi ni siku ambayo aliamka na mawazo mapya na aliona kabisa yakutokea yamekwisha kutokea na sasa anatakiwa kujikaza kama mwanaume na kuruhusu mambo megnine yaendelee . lakini siku hio pia alikumbuka tukio la yule mzungu kumpa bahasha flani iliojaradiwa na plastic alifikicha kichwa chake na hapo hapo alikumbuka sehemu aliokuwa ameificha , ilikuwa ni nje kwenye banda la mbuzi kwenye paa la nyasi kwani anakumbuka ndipo sehemu alio ichomeka siku ile kabla ya kwenda kumuita mzee kivinje , alitoka nje na kisha alisogelea banda lile na kisha aliingiza mkono sehemu alipo amini ndio alipoweka , lakini hakuiona alijaribu tena lakini hakuona , alijikuta akitafuta mpaka akikata tamaa , alilalia kibanda hicho akiwa anaangalia chini na kujiona kuwa na mkosi lakini ni kama kuna kitu alikuwa amekiona kwenye kinyesi cha mbuzi wale aliona plastc kama ile ile , alikurupuka na kukimbilia upande wa nyuma ya banda lile na kushika ile plastic na kuivuta na kweli ilikuwa ni yenyewe alijikuta akitabasamu na kuifuta uchafu ule na bahati nzuri ni kwamba ilikuwa imehifadhiwa kwenye plastic bag kwa hio ilichafuka juu tu .
Alisogea mpaka ndani kwao na kisha aliitoa kwa utaratibu bahasha ile na kutoa karatasi nne alizitoa haraka haraka na kuanza kupitia moja “: BRUNO LAMBERK BORN 1947 hapo alitambua kuwa mzungu yule alikuwa akiitwa kwa jina la bruno lamberk
“ owned properties ( mali anazomiliki )
Chini ilikuwa ni orodha mjumuisho iliokuwa na maelezo ya mali anazomiliki bwana Bruno ilikuwa ni mali nyingi bwana huyu ambazo alikuwa akimiliki kulikuwa n mashamba nyumba na namba account ya bank ya uswisi na card yake benki ambayo damiani hakuitambua “
Alipitia karatasi nyingine ilikuwa ni ramani ya Tanzania lakini ndani yake kulikuwa na sehemu zimechorwa kwa alama nyekundu ni kama zilikuwa zikionesha eneo husika hakutaka kuangalia sana hio karatasi alipitia ya pili yake ilikuwa na akaunti za benki ya CRDB na card yake lakini jina halikuwa la Bruno bali limeandika seline amber aliweka pembeni na ya mwisho ilikuwa na majina mengi karibia tisini , ila hakutaka kujihaingaisha nayo , alifungua kimkebe kilichokuwa ndani ya hio bahasha na ndani yake kulikuwa na vitu viwili moja ilikuwa ni flash disk , pili ilikuwa cheni yenye kidani kilichokaa kwa muundo wa msalaba lakini kina utofuti kidogo , aliachana na ile cheni na kisha akahamia kwenye ile flash , alijua kuna kitu kilikuwa ndani ya hio flash , alikumbuka alikuwa na laptop , alifuata kwenye begi lake na kisha aliitoa na ikawaka alisubiria window iload na ikakubali na hapo hapo hakutaka kuchelewa aliingiza password na kisha akchomeka ile flash.
CONTINUARA......