Trainee
JF-Expert Member
- Sep 22, 2018
- 2,226
- 2,842
Salaam alaykum...
Wengi wamekuwa wakipotosha watu kuhusu uislamu mpaka watu hao (wapotoshwaji) wamekuwa wakiona uislamu ni kitu kisichofaa katika jamii. Haijaisha hapo tu bali hata waliofuata huo uislamu wamepotoshwa baadhi ya mambo mpaka kufikia kuona dini yao ni chungu na ngumu kutekeleza
Tuongelee pande zote mbili yaani ugumu uliowekwa kwa mtu kuingia uislamu na ugumu uliowekwa kwa waislamu wenyewe
Tukianza na upotoshaji unaomkimbiza asiye muislamu
1. Ugaidi
Matendo yote ya ugaidi na yasiyoendana na ubinadamu mfano uhaini, uuaji bila hatia, ubakaji, ni miongoni mwa mambo yanayopingana vita sana na uislamu. Hoja wanazozisema wengi kuhusu uislamu kuwa ni ugaidi zinajibika kirahisi tu kwa mwenye kutaka kuelewa anaelewa. Aya za quran zote wanazocopy na kupaste wakisema zinasapoti kuua ukiangalia zinaongelea/zinaamrisha kuua baada ya kuwa adui amekusudia kukuua hivyo kupigana vita/kuua kunakuwa ni kwa sababu ya kujihami, kujitetea au kupambania kuondosha fitina iliyokithiri ili haki itendeke kwa wanajamii.
Tena hata kuua huko kuna masharti yake kadha wa kadha siyo kuua kwa mtu atakavyo. Mfano wale wanaoambiwa wanajitoa mhanga, wanaoteka mabinti na kuwanyanyasa (kama ni kweli) basi hiyo ni kwa matakwa yao wenyewe tu lakini uislamu unatetea kila mtu. Ushauri; hizo aya zote wanazosema humu watu na kuzipaste hebu ukiipata usiishie hapo tu bali soma kifungu chote (karaa) au sura kabisa halafu baada ya hapo utarudi. Kwa tafsiri ya ugaidi na maana zake hakuna aya wala hadithi hata moja utakayopata ikisapoti hiyo kitu!
2.Ubaguzi
Kuna mambo mengi ya kiibada ambayo muislamu akifanya kwa kuzingatia dini yake anaonekana kama anafanya ubaguzi kumbe siyo hata. Maswala kama ya ndoa muislamu haruhusiwi kufanya ibada hii ya kufunga ndoa na asiye muislamu, kuchinja muislamu haruhusiwi kula kilichochinjwa na asiyekuwa muislamu, muislamu haruhusiwi kushiriki ibada za wasiokuwa waislamu. Hayo yote siyo ubaguzi bali ni utaratibu wa dini kama ilivyo kwa dini zingine kuwa na mambo ambayo yanawahusu wao wenyewe tu na mengine yakawahusu watu wote na ndiyo maana hata kwa waislamu wakaruhusiwa kushirikiana na wasio waislamu kwa maswala yasiyokuwa ya ibada mahsusi mfano kula pamoja, kupiga stori, kufanya kazi, nk
3.Kuhusu Muhammed
Wapo waliomzushia mtume mambo mengi sana lakini majibu yote yametolewa kwenye quran sitaki nirudie rudie. Bali nitajikita kwenye uzushi mmoja tu kwamba Muhammed alikuwa anapenda sana ngono hasa na vitoto ndomaana alimwoa Aisha katoto. Watu wanaoelewa Historia vizuri wanacheka tu wakiona huu uzushi maana Muhammed amekuwa akiaminiwa tangu utoto mpaka ujana wake mpaka utu uzima wake hata kabla hajapewa utume watu wote walimpenda kwa ubora wa tabia aliyokuwa nayo haya huo uzinzi umetoka wapi. Pia huyu mtu ujana wake wala hakuufaidi ukitaka ukweli maana ana miaka 25 ndo akapata mke wake wa kwanza tena mwanamke akiwa na miaka 40! Mapungufu yote anayosingiziwa Mtume huyapati kwenye hadithi sahihi wala quran
4.Kuhusu Allah, Quran na shetani
Wengi wanaaminisha watu kwamba Allah ndiye shetani mara hivi mara vile. Jamani hebu tusome kwa uelewa vitu siyo kwa kumezeshwa. Kuna aya hapa wanapenda kuipaste kwamba eti shetani ndiye kateremsha kuran kumbe masikini ni shida ya kuelewa maandishi tu wala mola hakumaanisha kuwa ni shetani bali malaika jibril. Soma aya zote zinazotaja vitatu hivyo Allah, Quran na Iblis halafu utajionea mwenyewe
5.Kwamba ukiritadi unauawa. Hoja hii wanaipenda sana masikini lakini wanashindwa kusoma andiko lote lililoko pale. Kama ingekuwa ni kweli hicho wanachosema uislamu ndo ulivyo basi tungeona au hata kusikia huko watu wkiuawa kwa
Twende upotoshwaji kwa waislamu wenyewe
1.Ukiingiwa na najisi ya nguruwe usiswali siku 7 (wengine wakasema siku 40) eti baada ya hapo ndiyo unatwaharika. Ukishajitwaharisha vizuri kwa kufuata taratibu zote zinazokubalika basi wewe ni kazi kazi tu wala hakuna sheria hiyo ya kukaa bila kuswali
2.Janaba la zinaa linaisha kwa siku 40 eti ukizini na mwana wa watu hata kama utaoga usiingie msikitini siku 40 zipite ndipo utakuwa umetwaharika. Huu ni ujinga wa kiwango kikubwa sana, kalamu inasimama kwa mtoto mdogo, aliyepoteza fahamu/akili na aliyelala sasa sijui huyu wa siku 40 haswali anajinasulia wapi kwenye kuulizwa swala 200 atakazoziacha
3. Mama akijifungua anaogeshwa na shekhe. Hii ndo inauma sana aisee wazee wa zamani eti anaitwa akamuogeshe mmama wa watu yaani ni ushetani juu ya ushetani. Hadathi zote kama ilivyo najisi mtu anajitwaharisha mwenyewe tu sijui mashekhe wa zamani walikuwa na mpango gani na wadada wa watu
4. Mtu akichinja inabidi apewe shingo (ya mnyama aliyechinjwa). Hii mpaka sasa hivi huku nilipo bado wanayo yaani nyama ikiiva tu atatafutwa apewe shingo yake na kama mchinjaji akiifuata yeye mwenyewe akakuta imeliwa anadai hela. Hiyo kitu haipo wewe chinja uondoke ukipewa baadae ni swadaqa tu usipopewa isiwe deni wala mtoaji asifanye ni lazima akuchagulie shingo ndo akupe huo ni uzushi. Hela analipwa yule ambaye hiyo ni kazi yake mfano mchinjaji buchani, hotelini nk
5. Biashara inatakiwa kuuza faida isizidi robo yake (wengine nusu yake) yaani kama kitu umenunua sh.100 maana yake usiuze kwa bei ya itakayozidi 125 (robo) au 150 (nusu). Huu ni uongo mwingine wa mchana kweupe. kilichokatazwa kwenye biashara ni uongo na ulaghai tu lakini kama kitu umeamua kuuza laki na wewe ulinunua mia na mteja akakipenda akaridhia kununua bila kumchomekezea maneno ya kumpambisha na kumlaghai basi kitu hicho unaruhusiwa kumuuzia tu bila shida
6. Lailatul qadr ni nyota ing'aayo sana na ukipata bahati kuiona (ikikutokea hiyo nyota) basi unaomba chochote na hapaohapo unapata. Huu ni uongo ambao wengi bado wanao na tatizo ni darsa watu hawasomi madrasa wakaelewa. Usiku wa cheo, lailatul qadr ni usiku ndiyo lakini hauna alama yoyote kwamba mtu atasema ameupata bali tunahimizwa kufanya yaliyo mema zaidi ndani ya usiku huo (mfano kuswali, kusoma quran, kumsifu mola, kutoa sadaka nk) ili uwe umefanya jambo jema kwenye usiku bora kabisa. Haihusiani na nyota fulani wala jeneza wala kaburi wala...
7. Matendo mema ni kukusanya watu kufanya dua, kusoma maulidi, kuzuru na kusafishia makaburi, kuwafanyia dua ya kumbukumbu ya watu waliokufa, kusoma barzanji mara kwa mara, dhikri ya kidarueshi (ya kukohoa). Hapo kuna mambo mengi sana ambayo watu wamekuwa wakikomaa nayo huku wakiacha matendo mema kabisa kuliko yote ambayo ni kuswali, kusoma quran, kutoa zaka na sadaka, kufunga, kuelimisha watu, kukumbusha watu wadumu na matendo mema na kuzuia watu wasifanye maasi, kuwatii wazazi, nk
Mambo ni mengi sana ila yote kwa yote ni kwamba uislamu mola hatutakii magumu yenye uzito bali anatutakia yaliyo mepesi tu. huo ugumu na uzito wanaweka watu wenyewe! Ingia uislamu ujionee usisikilize propaganda za wasioutakia heri uislamu
Wengi wamekuwa wakipotosha watu kuhusu uislamu mpaka watu hao (wapotoshwaji) wamekuwa wakiona uislamu ni kitu kisichofaa katika jamii. Haijaisha hapo tu bali hata waliofuata huo uislamu wamepotoshwa baadhi ya mambo mpaka kufikia kuona dini yao ni chungu na ngumu kutekeleza
Tuongelee pande zote mbili yaani ugumu uliowekwa kwa mtu kuingia uislamu na ugumu uliowekwa kwa waislamu wenyewe
Tukianza na upotoshaji unaomkimbiza asiye muislamu
1. Ugaidi
Matendo yote ya ugaidi na yasiyoendana na ubinadamu mfano uhaini, uuaji bila hatia, ubakaji, ni miongoni mwa mambo yanayopingana vita sana na uislamu. Hoja wanazozisema wengi kuhusu uislamu kuwa ni ugaidi zinajibika kirahisi tu kwa mwenye kutaka kuelewa anaelewa. Aya za quran zote wanazocopy na kupaste wakisema zinasapoti kuua ukiangalia zinaongelea/zinaamrisha kuua baada ya kuwa adui amekusudia kukuua hivyo kupigana vita/kuua kunakuwa ni kwa sababu ya kujihami, kujitetea au kupambania kuondosha fitina iliyokithiri ili haki itendeke kwa wanajamii.
Tena hata kuua huko kuna masharti yake kadha wa kadha siyo kuua kwa mtu atakavyo. Mfano wale wanaoambiwa wanajitoa mhanga, wanaoteka mabinti na kuwanyanyasa (kama ni kweli) basi hiyo ni kwa matakwa yao wenyewe tu lakini uislamu unatetea kila mtu. Ushauri; hizo aya zote wanazosema humu watu na kuzipaste hebu ukiipata usiishie hapo tu bali soma kifungu chote (karaa) au sura kabisa halafu baada ya hapo utarudi. Kwa tafsiri ya ugaidi na maana zake hakuna aya wala hadithi hata moja utakayopata ikisapoti hiyo kitu!
2.Ubaguzi
Kuna mambo mengi ya kiibada ambayo muislamu akifanya kwa kuzingatia dini yake anaonekana kama anafanya ubaguzi kumbe siyo hata. Maswala kama ya ndoa muislamu haruhusiwi kufanya ibada hii ya kufunga ndoa na asiye muislamu, kuchinja muislamu haruhusiwi kula kilichochinjwa na asiyekuwa muislamu, muislamu haruhusiwi kushiriki ibada za wasiokuwa waislamu. Hayo yote siyo ubaguzi bali ni utaratibu wa dini kama ilivyo kwa dini zingine kuwa na mambo ambayo yanawahusu wao wenyewe tu na mengine yakawahusu watu wote na ndiyo maana hata kwa waislamu wakaruhusiwa kushirikiana na wasio waislamu kwa maswala yasiyokuwa ya ibada mahsusi mfano kula pamoja, kupiga stori, kufanya kazi, nk
3.Kuhusu Muhammed
Wapo waliomzushia mtume mambo mengi sana lakini majibu yote yametolewa kwenye quran sitaki nirudie rudie. Bali nitajikita kwenye uzushi mmoja tu kwamba Muhammed alikuwa anapenda sana ngono hasa na vitoto ndomaana alimwoa Aisha katoto. Watu wanaoelewa Historia vizuri wanacheka tu wakiona huu uzushi maana Muhammed amekuwa akiaminiwa tangu utoto mpaka ujana wake mpaka utu uzima wake hata kabla hajapewa utume watu wote walimpenda kwa ubora wa tabia aliyokuwa nayo haya huo uzinzi umetoka wapi. Pia huyu mtu ujana wake wala hakuufaidi ukitaka ukweli maana ana miaka 25 ndo akapata mke wake wa kwanza tena mwanamke akiwa na miaka 40! Mapungufu yote anayosingiziwa Mtume huyapati kwenye hadithi sahihi wala quran
4.Kuhusu Allah, Quran na shetani
Wengi wanaaminisha watu kwamba Allah ndiye shetani mara hivi mara vile. Jamani hebu tusome kwa uelewa vitu siyo kwa kumezeshwa. Kuna aya hapa wanapenda kuipaste kwamba eti shetani ndiye kateremsha kuran kumbe masikini ni shida ya kuelewa maandishi tu wala mola hakumaanisha kuwa ni shetani bali malaika jibril. Soma aya zote zinazotaja vitatu hivyo Allah, Quran na Iblis halafu utajionea mwenyewe
5.Kwamba ukiritadi unauawa. Hoja hii wanaipenda sana masikini lakini wanashindwa kusoma andiko lote lililoko pale. Kama ingekuwa ni kweli hicho wanachosema uislamu ndo ulivyo basi tungeona au hata kusikia huko watu wkiuawa kwa
Twende upotoshwaji kwa waislamu wenyewe
1.Ukiingiwa na najisi ya nguruwe usiswali siku 7 (wengine wakasema siku 40) eti baada ya hapo ndiyo unatwaharika. Ukishajitwaharisha vizuri kwa kufuata taratibu zote zinazokubalika basi wewe ni kazi kazi tu wala hakuna sheria hiyo ya kukaa bila kuswali
2.Janaba la zinaa linaisha kwa siku 40 eti ukizini na mwana wa watu hata kama utaoga usiingie msikitini siku 40 zipite ndipo utakuwa umetwaharika. Huu ni ujinga wa kiwango kikubwa sana, kalamu inasimama kwa mtoto mdogo, aliyepoteza fahamu/akili na aliyelala sasa sijui huyu wa siku 40 haswali anajinasulia wapi kwenye kuulizwa swala 200 atakazoziacha
3. Mama akijifungua anaogeshwa na shekhe. Hii ndo inauma sana aisee wazee wa zamani eti anaitwa akamuogeshe mmama wa watu yaani ni ushetani juu ya ushetani. Hadathi zote kama ilivyo najisi mtu anajitwaharisha mwenyewe tu sijui mashekhe wa zamani walikuwa na mpango gani na wadada wa watu
4. Mtu akichinja inabidi apewe shingo (ya mnyama aliyechinjwa). Hii mpaka sasa hivi huku nilipo bado wanayo yaani nyama ikiiva tu atatafutwa apewe shingo yake na kama mchinjaji akiifuata yeye mwenyewe akakuta imeliwa anadai hela. Hiyo kitu haipo wewe chinja uondoke ukipewa baadae ni swadaqa tu usipopewa isiwe deni wala mtoaji asifanye ni lazima akuchagulie shingo ndo akupe huo ni uzushi. Hela analipwa yule ambaye hiyo ni kazi yake mfano mchinjaji buchani, hotelini nk
5. Biashara inatakiwa kuuza faida isizidi robo yake (wengine nusu yake) yaani kama kitu umenunua sh.100 maana yake usiuze kwa bei ya itakayozidi 125 (robo) au 150 (nusu). Huu ni uongo mwingine wa mchana kweupe. kilichokatazwa kwenye biashara ni uongo na ulaghai tu lakini kama kitu umeamua kuuza laki na wewe ulinunua mia na mteja akakipenda akaridhia kununua bila kumchomekezea maneno ya kumpambisha na kumlaghai basi kitu hicho unaruhusiwa kumuuzia tu bila shida
6. Lailatul qadr ni nyota ing'aayo sana na ukipata bahati kuiona (ikikutokea hiyo nyota) basi unaomba chochote na hapaohapo unapata. Huu ni uongo ambao wengi bado wanao na tatizo ni darsa watu hawasomi madrasa wakaelewa. Usiku wa cheo, lailatul qadr ni usiku ndiyo lakini hauna alama yoyote kwamba mtu atasema ameupata bali tunahimizwa kufanya yaliyo mema zaidi ndani ya usiku huo (mfano kuswali, kusoma quran, kumsifu mola, kutoa sadaka nk) ili uwe umefanya jambo jema kwenye usiku bora kabisa. Haihusiani na nyota fulani wala jeneza wala kaburi wala...
7. Matendo mema ni kukusanya watu kufanya dua, kusoma maulidi, kuzuru na kusafishia makaburi, kuwafanyia dua ya kumbukumbu ya watu waliokufa, kusoma barzanji mara kwa mara, dhikri ya kidarueshi (ya kukohoa). Hapo kuna mambo mengi sana ambayo watu wamekuwa wakikomaa nayo huku wakiacha matendo mema kabisa kuliko yote ambayo ni kuswali, kusoma quran, kutoa zaka na sadaka, kufunga, kuelimisha watu, kukumbusha watu wadumu na matendo mema na kuzuia watu wasifanye maasi, kuwatii wazazi, nk
Mambo ni mengi sana ila yote kwa yote ni kwamba uislamu mola hatutakii magumu yenye uzito bali anatutakia yaliyo mepesi tu. huo ugumu na uzito wanaweka watu wenyewe! Ingia uislamu ujionee usisikilize propaganda za wasioutakia heri uislamu