Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Katika Siasa za Tanzania lazima ufanye hivyo na pia itachukua muda kwa ajili CCM kuendesha siasa za kistarabu kuliko kuwa sasa hivi, Hivyo Chadema ni sawa kabisa kujibu na kuwatuhumu CCM na ndio siasa hizo na pia itakuwa vizuri sana kama nao wakiwa wanakura sahani moja na CCMCHADEMA kwanza wanatakiwa kuacha kuiga ''siasa'' za CCM. CCM imeundwa kwa misingi tofauti na CHADEMA na kuiiga CCM inakuwa ni sawa na jinsi Afrika inavyoendelea kuwa masikini kwa sababu ya kuhangaika kuiiga Ulaya ( ambayo historia yake imeiweka hapa ilipo).
CHADEMA wanapaswa kufocus kwenye kuwadhihirishia wananchi kuwa CHADEMA ni waaminifu. Imani ya watanzania kwa vyama vya siasa, NGOs, Serikali na Viongozi haipo tena. Ukweli ndio huu. Mtu, watu au chama kitakachoweza kurudisha imani kwa wananchi watakuwa na mafanikio makubwa kisiasa.
CHADEMA sasa hivi nayo inajiingiza kwa kasi kubwa sana kwenye siasa za hila, vurugu, malumbano etc. Hii inafanya CHADEMA ionekane haina tofauti na CCM. Ukienda Dodoma leo hii, huwezi kuona tofauti kati ya mbunge wa CHADEMA na yule wa CCM. Unadhani wananchi wataamini vipi kwamba CHADEMA ni tofauti iwapo wote wanatafuna kwa mtindo huohuo?
CHADEMA pia wanatakiwa kuwa na mipango ya muda mrefu. Siasa za uchuuzi hazina manufaa yoyote. Mfano, Mbowe alipata ubunge. Kulikuwa na kila sababu ya Mbowe kutokuliachia lile jimbo lirudi kwa CCM. Sasa hivi tunaona Zitto naye anasurrender jimbo. Hii inadhihirisha kuwa CHADEMA kila mtu ana agenda yake na hakuna agenda ya chama. Kwa mtindo kama huu watakuwa wananusa na kuachia na hawatafika popote.Urais ni rahisi kuutamka lakini kama huna wabunge usitegemee kupata uraiskwa jinsi siasa za Tanzania zilivyo.
CHADEMA inapaswa kuonyesha usafi wa hali ya juu ili iaminiwe. Chaguzi zao za ndani tu zimejawa na mizengwe. Matumizi ya ruzuku yamejawa na mizengwe. Katika hali kama hii hata ukipiga makelele vipi unaonekana another mlaji tu.