Ubunge Arumeru Mashariki utakuwa mgumu sana

Wakuu,

Ni wazi sasa baada ya kumpumzisha mwenzetu-(R.I.P) jimbo litakuwa wazi.
Ninaomba niwaambie wazi wenzetu wa CDM kwamba wananchi wana imani kubwa na aliyekuwa mgombea wenu Joshua Nassary. Msije mkajidanganya mkamteua mtu mwingine.Ni wazi kwa nguvu ya CDM sasa wenye pesa watajipenyeza kugombea ili waukwae ubunge.

Nawaambia wazi kamati kuu ya CDM mkimchakachua Joshua Nassary tutakuja huko makao makuu na mabango na tutawafungia ndani ya ofisi kwa kufuli.

Dr Slaa najua uko huku jamvini.Hakikisha wajanja hawatapenyeza pesa kwa ajili ya kumtosa kijana wetu Nassary.Tuna imani kubwa na huyu kijana.Kamati kuu hakikisheni mnamtendea haki huyu kijana.

Huyu kijana ni machachari mfano wa Lema, Mnyika, Zitto nk.
Hayo ni mawazo yangu kwenu kamati kuu.Tupeni chaguo tunalolitaka.
 
Chadema mgombea anapatika baada ya primary hayo mengine ni majungu tu. Pia kumbukwa unaweza kuwa kipenzi cha wanachadema lakini si cha wanajimbo wote!
Nleta mada tupe unayeona anafaa
 
Nawaza hali itakavokuwa kwa jimbo la Arumeru Mashariki wakati wa uchaguzi baada ya kuondokewa na Mheshimiwa Sumari. CCM watataka wajitahidi kwa nguvu zai zote kuliko ilivokuwa Igunga ili kulinda heshima yao. CDM nao watataka wahakikishe kuwa wanalichukua ili kuimarisaha ukanda wa kaskazini tokea Mbulu, Karatu, Arusha mjini, Hai, Moshi Mjini na Rombo. rangi za kijani na magwanda kazi kwenu.

Acha watu wazike kwanza wewe; mbona una haraka hivyo; kwa nini hujadili mchakato wa kumtafuta mrithi wa mtema
 
Uchakachuzi ilikuwa majimbo yote sio lake tu na hukohuko aidha cdm ilitoa upinzani mkali au ilishinda e.g regia ailizidiwa kura 4000, mchange 4000, khalfani kwa serukamba kigoma mjini hata 200 hazikufika iweje yeye akiwa peke yake akazidiwe kura elf 15 zote?

Mkuu una uhakika Regia alizidiwa kura 4000?
 
oki mie nataenda kwenye kampeni ili nikomae zaidi kisiasa. Yote inabidi tumutegemee Mungu
 
Mmeshaanza chokochoko kumtoa huyo kijana, kura 19 elfu alizopata unaziona ndogo, je kama magamba waliiba. acheni kampeni uchwara. subirini wakati ufike
 
Kujitokeza ni ujasiri mkubwa sana na mie nampa heshima yake. Lakini chama chaweza kumjenga akaimalika na kuwa tegemeo letu kesho kwa nafasi nyingine
 
kijana anafaa sana kupeperusha bendera ya chama, mimi binafsi namuunga mkono.
Naamini Chadema ina watu makini na wenye busara na nawaamini kwa maamuzi makini.

Nawapa pole wafiwa wa Mh. Sumari.
 
Ndugu wana jf

Joshua Nasary ndie aliyepeperusha bendera ya chama chetu mwa 2010 kwa nafasi ya ubunge ktk jimbo hilo na mwishoni hakufanikiwa kushinda.
Marehemu Jeremia sumari alikuwa mgonjwa kipindi chote cha kampeni na hakuhutubia mkutano hata mmoja bali wana-ccm wenzake ndio waliompigia kampeni na kuibuka mshindi.

Mimi binafsi nina mashaka na uwezo wa huyo kijana wetu juu ya kuweza kulichukua jimbo hili wakati wa uchaguzi mdogo, Km ktk kipindi cha kampeni alikuwa peke yake ila ameshndwa, je atawezaje kushinda ktk kipindi ambacho ccm nao watakuwa na mgombea ambae atajipigia kampeni?

Chadema km chama kinatakiwa kusimamisha mgombea ambae tuna asilimia nyingi za kushinda na sio kuridhishana eti kwa kuwa yy aligombea 2010 basi na sasa awe huyo huyo.

ulitegemea ccm wakubali waziri ashindwe hivihivi? Hakuna sababu ya cdm kubadili mtu. Kwa mgombea huyohuyo cdm wajipange vyema watachukua jimbo. Cha kuangalia pia ni mpishano wa kura
 
Hoja yako ni nzuri,kwani inatupa nafasi ya kujadili suala muhimu.wasiwasi ni kwamba kama mgombea hakufanya kampeni na alishinda. Basi hiyo ilikuwa chakacxhua ya magamba system

Kwani lazima kuchakachua kura. Hamjui tu kwamba wana uwezo wa kuchakachua wagombea pia.
 
Kwa maoni yangu Nassary apewe tena nafasi kuchukua jimbo,tayari wananchi wanamfahamu,walishamuona majukwaani last campaigns,kuliko kuweka figure yingine mpya,besides competency alizokuwa nazo 2010 naamini still anazo na obvious zimeongezeka zaidi
 
Heshima kwako Gwota.

Mkuu wangu,
Bwana Nassary ni kati ya vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kuitetea kwa busara kubwa hana papara hapendi kukurupuka.Binafsi nimewahi kukutana na Bwana Nassary ni msomi mzuri anajua anachoongea anaufahamu mkubwa katika masuala mbali mbali (Siasa,Uchumi,Sheria na uhusiano wa Kimataifa) anajua matatizo ya jamii yake hasa suala la ardhi.Meru ni sehemu yenye msongamano mkubwa wa watu per sq km unaweza kulinganisha Meru na Mkoa wa Kilimanjaro au Wilaya ya Ukerewe.Pamoja na tatizo la ukosefu wa ardhi ya kutosha utashangaa viongozi wengi wa chama na serekali wamenyakua ardhi kubwa iliyoachwa na wazungu badala ya kuigawa kwa wananchi maskini wa Meru.Wapo wageni wengi(Wazungu) toka Zimbabwe,South Afrika na Uholanzi wamepewa ardhi Meru huku wananchi wakiachwa bila ardhi katika nchi yao!.Nisingependa kutaja majina ya viongozi wakubwa walionyakua ardhi Meru wakati wanajua shida ya ardhi Meru.Tanzania ina ardhi kubwa lakini pia kuna baadhi ya maeneo kama Meru na Kilimanjaro yenye uhaba mkubwa ardhi najiuliza ni kwanini Viongozi wetu wasijigawiye ardhi maneo ya Mtwara,Tanga,Morogoro,Dodoma maeneo yenye msongamano mdogo wa watu ?.

 
Kiukweli mie wazazi wangu wanaishi arumeru mashariki katika kijiji kiiywacho nkoanrua, na pia ni mdau wa cdm, kuanzia kipindi chote chote cha uchaguzi hadi Leo hii sijawahi kukutana na hata bendera ya cdm! So kwa maoni yangu tatizo sio kwa nassary Bali chama kutofanya uhamasishaji na upanuzi, kwa kifupi wamepasahau japo wananchi wanatambua uwepo wa cdm thru media.
Kwa hili si vema kumlaumu nassary ila cdm ni vyema kuanza kuinvest kila political resources walizonazo kwani wengi wakazi wa hapo home hawana upenzi wa chama chochote cha siasa
nawasilisha
 
lolote laweza kutokea ktk huo uchaguzi mdogo mwacheni kijana ajaribu bahati yake kwa mara nyingine tena.
 
Sumari aliugua sana Mkuu watu watakao lia labda ni wachache, hasa waliokuwa wanapata pensheni/posho kwa uwepo wake. binafsi nasema apunzike kwa amani aliteseka sana.
Wanasiasa kaeni attention! Jimbo nje nje! jamaa kafa kikweli kweli!

kwani kuna kufa kiuongo uongo?
 
Heshima kwako Gwota.

Mkuu wangu,
Bwana Nassary ni kati ya vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kuitetea kwa busara kubwa hana papara hapendi kukurupuka.Binafsi nimewahi kukutana na Bwana Nassary ni msomi mzuri anajua anachoongea anaufahamu mkubwa katika masuala mbali mbali (Siasa,Uchumi,Sheria na uhusiano wa Kimataifa) anajua matatizo ya jamii yake hasa suala la ardhi.Meru ni sehemu yenye msongamano mkubwa wa watu per sq km unaweza kulinganisha Meru na Mkoa wa Kilimanjaro au Wilaya ya Ukerewe.Pamoja na tatizo la ukosefu wa ardhi ya kutosha utashangaa viongozi wengi wa chama na serekali wamenyakua ardhi kubwa iliyoachwa na wazungu badala ya kuigawa kwa wananchi maskini wa Meru.Wapo wageni wengi(Wazungu) toka Zimbabwe,South Afrika na Uholanzi wamepewa ardhi Meru huku wananchi wakiachwa bila ardhi katika nchi yao!.Nisingependa kutaja majina ya viongozi wakubwa walionyakua ardhi Meru wakati wanajua shida ya ardhi Meru.Tanzania ina ardhi kubwa lakini pia kuna baadhi ya maeneo kama Meru na Kilimanjaro yenye uhaba mkubwa ardhi najiuliza ni kwanini Viongozi wetu wasijigawiye ardhi maneo ya Mtwara,Tanga,Morogoro,Dodoma maeneo yenye msongamano mdogo wa watu ?.


Mkuu Ngongo,
Asante sana kwa hili bandiko lako.Umewapa jibu lao.waambie watafute mbinu nyingine ya kumkwamisha huyu kijana.Penye ukweli lazima tuseme
 
Back
Top Bottom