Tofauti ya kura ni 15, 438. Mimi nakubali kuwa ccm watakuwa walichakachua lkn hyo haitoshi coz hawajachakachua jimboni kwake tu, tazama watu km wenje, kiwia, nyerere, mnyika,mdee pamoja na hila za ccm ila walishinda. pia hata ukitizama watu ambao hawakushinda ktk majimbo yao na wagombea wa ccm walikuwepo ila walitoa ushindani mkubwa na walizidiwa kidogo mfano mchange wa kibaha, marehemu regia, shelembi wa shy, khalfan wa kigoma, mpendazoe na wengine wengi tu.
Tatizo langu kwa kijana wetu huyu ni kwamba kwanza hakuwa na mpinzani ila akapata kura chache sana je km angekuwa na mpinzani ungetegemea apate ngapi? hapa wanachadema tunatakiwa kufanya analysis vzr kwa manufaa ya chama na sio kufurahishina binafsi
Mkuu inaonekana una chuki kubwa na kijana Nassary.Ama unataka kumchafua ili ugombee wewe.Ama umetumwa na mafisadi.
Ingawa huyu dogo simjui vema lakini ni vigumu kumsuta sasa hivi. Hawa wau wa ccm ni wezi na wabababe inawezekana kabisa waliiba kura kama wlivyofanya kwenye majimbo mengine. Pia hiyu Sumari alitumia saana msuri wa fedha kuraghai na kuhonga wapiga kurana kumbuka kipindi hicho alikuwa waziri mdg wa fedha. Tusimkatishe tamaa wacha apambane nina imani this time atashinda
Yatakuwa kama yale ya Igunga kwa CUF,mtaji wa kura 11elfu badala yake wakaambulia kura elfu 2!kuweni makini cdm!Napendekeza Dr W.P.Slaa akagombee!lazima atakomba zaidi ya 80+% za kura.
Yatakuwa kama yale ya Igunga kwa CUF,mtaji wa kura 11elfu badala yake wakaambulia kura elfu 2!kuweni makini cdm!Napendekeza Dr W.P.Slaa akagombee!lazima atakomba zaidi ya 80+% za kura.
usilete majungu kaka, niambie ni wapi niliposema uongo ambapo nipo namchafua? tusiwe watumwa wa mawazo eti ukimwa ukweli basi mtu katumwa
Hadhi ya Slaa sio ya ubunge acha kumdhalilisha
Hili wazo ni zuri sana na nilikuwa sijaliwaza, kwani arumeru mashariki hadi karatu vimepishana kwa umbali gani? tena itatusaidia sana 2015 wakati anagombea urais.hata mrema 1996 alirudi bungeni kupitia jimbo la temeke
Mshawishini Anael Nkya agombee kwa ticket ya CHADEMA kama ni mwanachama wa CDM, huyo anaweza kulibeba jimbo hilo!!!!!!!!!!Ndugu wana jf
Joshua Nasary ndie aliyepeperusha bendera ya chama chetu mwa 2010 kwa nafasi ya ubunge ktk jimbo hilo na mwishoni hakufanikiwa kushinda.
Marehemu Jeremia sumari alikuwa mgonjwa kipindi chote cha kampeni na hakuhutubia mkutano hata mmoja bali wana-ccm wenzake ndio waliompigia kampeni na kuibuka mshindi.
Mimi binafsi nina mashaka na uwezo wa huyo kijana wetu juu ya kuweza kulichukua jimbo hili wakati wa uchaguzi mdogo, Km ktk kipindi cha kampeni alikuwa peke yake ila ameshndwa, je atawezaje kushinda ktk kipindi ambacho ccm nao watakuwa na mgombea ambae atajipigia kampeni?
Chadema km chama kinatakiwa kusimamisha mgombea ambae tuna asilimia nyingi za kushinda na sio kuridhishana eti kwa kuwa yy aligombea 2010 basi na sasa awe huyo huyo.
Kwa taarifa nilizo nazo Kijana Joshua alishinda tena kwa mbaali akafatiwa na Marehemu ila kama mjuavyo walichakachua kubwa ni watu kutokulinda kura zao baada ya kupiga,mimi nashauri dogo apewe mikoba ila makamanda wakatoe shule mapema najua kura za Arumeru mashariki hazitawezekana hata kuzichakachua safari hii hata CCM wanajua napata wasiwasi na aliye post thread hii kama ni Gamba coz CCM wanajua ukweli na dogo wanaujua moto wake!
Hamasisha vijana wajiandikishe kupiga kura huko ARUMERU MASHARIKI wafundishe waelewe umuhimu wamkupiga kura!!!!!!!!!!!!!kinachotokea ni kilekile vijana wengi wa hapa hatuna kadi za kupigia kura kitajirudia kilekile
Kama ni hivyo dogo apewe tafu arudi ulingoni mgoma ni yake safari hii, naomba wakuu kazi ianze mapema baada tuu ya mazishi!!!!!!!! Bila shaka watu wote wa Arumeru wanajua kinachofuata sasa!!!!Waeleze mkuu.