Tuulize chochote kuhusu mbao na changamoto zake

Mbao za mikaratusi zina changamoto ya kupinda na kuliwa na mchwa. Pia wakati wa mvua zinavimba hivyo milango haifungi
Ndio maana hazipendekezwi sana japo zinafaa. Ni chache zilizopandwa vizuri tangu zikiwa mbegu ndio zinaweza kutoa matokeo chanya.
 
Heri ya mwezi mpya,

Sisi ni wataalamu wa mbao za aina mbalimbali zinazozalishwa nchini Tanzania. Tupo Dar es Salaam. Tunao ujuzi na uzoefu wa miaka mingi.

Kama inavyofahamika, shughuli za ujenzi wa majengo na baadhi ya miundombinu hapa kwetu kwa kiasi kikubwa bado hutegemea mbao kama mojawapo ya nyenzo muhimu.

Je, unawezaje kutambua mbao nzuri, imara na zinazofaa kwa mradi anuai?

Tumekuja JamiiForums kujuzana na kuepusha hasara ambayo wadau wa ujenzi hukumbana nazo, yakiwemo makampuni na watu binafsi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha.

Tutajibu maswali yote tutakayoyamudu kwa wakati.

Karibuni sana.
Nin ddawa ya mdudu anayekuka mbao na kuacha unga unga?
 
Je, naweza kuezeka Nyumba yangu kwa kutumia mbao za Mninga?
Bila kujali gharama ya mninga, mbao ngumu (hardwood) hazitumiki kuezekea kwa sababu mbili kubwa:
1. Ni fupi (ni ngumu kupata mninga ulionyooka kwa zaidi futi 12, hivyo hufanya mbao zake nyingi kukatwa kwenye vipimo vya futi 8 au zaidi kidogo tu)
2. Ni nzito (inafanya paa liwe zito sana, utahitaji ujenge kuta/nguzo imara zaidi ili kuhimili uzito wa paa)
 
Ni kutokana na asili yake.

Ndiyo sababu ni nadra mikaratusi kutumika kutengenezea milango, makabati na samani na badala yake hutumika kama mistimu ya umeme, fremu na baadhi ya kingo/viambata vya madaraja n.k.

Bado mninga ndiyo mbao nzuri na bora kwa utengenezaji wa samani kuliko aina nyingine yoyote.
Uzuri wake ni upi zaidi ya mkongo?
 
Nin ddawa ya mdudu anayekuka mbao na kuacha unga unga?
Ni kupulizia au kupaka dawa mbao husika. Kuna aina mbalimbali za dawa ambazo unaweza kutumia.

Aidha tunashauri wakati mwingine utumie mbao zilizochemshwa na dawa kama tulizonazo.
 
Ni kupulizia au kupaka dawa mbao husika. Kuna aina mbalimbali za dawa ambazo unaweza kutumia.

Aidha tunashauri wakati mwingine utumie mbao zilizochemshwa na dawa kama tulizonazo.
Kuna wengine niliona wanatumia machine ya vacuum ili kupenyeza dawa kwenye mbao.
Zinakaa saa 24
 
Utajuaje ile dawa ya kutreat mbao ni fake ama sio fake..ile ya kijan..maana naskia mchezo huo upo sana bugurun pale
 
Mkuu wangu Mbao Tanzania tafadhali nipe elimu kuhusu mbao ya Mkangazi, je inafaa kwenye furniture za kitanda? Maana nataka nichukue kitanda cha mkangazi nimeambiwa ni kizuri na mbao yake ni bei ghari
 
Back
Top Bottom