Tundu Lissu: Waliofaulu kidato cha nne 2011 ni asilimia 9.98

Moja shule ambazo matokeo ya kidato cha nne yalikuwa mabaya sana ni Yusuf Makamba Secondary School iliyopo jijini Dar Es Salaam. Shule hii bado inaendelea kushikilia rekodi ya kuwa na matokeo mabaya ya kidato cha nne. Katika matokeo ya mwaka 2010, kati ya wanafunzi 452 waliofanya mitihani, wanafunzi 414 walipata Division 0. Wanafunzi waliobakia walipata kati ya Division I na IV na wengine.

Matokea ya mwaka huu yanatia aibu zaidi. Ikiwa imewekwa kwenye kundi la shule zenye watahiniwa 40 au zaidi, shule hii ya Yusuf Makamba imekuwa ya 1,481 kati ya shule 3,108 ikiwa na mwanafunzi mmoja tuu aliyepata Division I, saba Division II, kumi na nane Division III, 139 Division IV na 185 Division 0.

Kama alivyose Lissu kuwa Division IV ni failure kwa mahesabu ya haraka haraka haraka ni asimilia ngapi waliofaulu kwenye hii shule?
Mkuu wangu unajua mnatia hasira sana mnapoanza kutafuta mchawi.. Matokeo ya kidato cha nne mwaka huu yanadhihirisha wazi ELIMU nchini ni mbovu.. Huwezi kupata asilimia 9 ya wanafunzi walioshinda mtihani halafu mkaendelea kutafuta sababu. Nimesema sana na nitaendelea kusema tena na tena kwamba MFUMO wa ELIMU nchini ni mbovu.. Hamuwezi kuiga mfumo wa Ulaya mkauleta hapa hata kidogo na tutaendelea kushindwa kwa sababu wanafunzi wetu wengi hukariri masom na majibu kwa sababu wanasoma tu lakini hawaelemiki.. Tunafundisha elimu feki kama tunavyotumia madawa na mali feki za kichina na India..
 
Tatizo wanasoma maswali na majibu ya Nyambale Nyangwine wa CCM badala ya kusoma vitabu wapate uelewa wa kupambana na changamoto za kidunia. Mtu aliyesomea mtihani kwa miaka mi4 akifeli ujue kwishnei, either aolewe au ataishia kuwa kibaka tu. Kawambwa anaangalia tu... Au kwa kuwa Mwanaasha naye ana 4 then tubadili standards na 4 iwe ufaulu kumfuata FIRST STUDENT

LIKE! Nyambali Nyangwine
 
Mkuu wangu unajua mnatia hasira sana mnapoanza kutafuta mchawi.. Matokeo ya kidato cha nne mwaka huu yanadhihirisha wazi ELIMU nchini ni mbovu.. Huwezi kupata asilimia 9 ya wanafunzi walioshinda mtihani halafu mkaendelea kutafuta sababu. Nimesema sana na nitaendelea kusema tena na tena kwamba MFUMO wa ELIMU nchini ni mbovu.. Hamuwezi kuiga mfumo wa Ulaya mkauleta hapa hata kidogo na tutaendelea kushindwa kwa sababu wanafunzi wetu wengi hunukuu majibu kwa sababu wanasoma lakini hawaelemiki.. Tunafundisha elimu feki kama tunavyotumia madawa na mali feki za kichina na India..

Mkuu ukweli unauma lakini sasa tuufiche? Tena shule ya Yusuf Makamba ni afadhali kama ukilinganisha Ali Hassan Mwinyi Islamic Secondary School iliyoko mkoani Tabora. Katika matokeo ya mwaka huu, shule hii ilichukua nafasi ya 1,655. Kati watahiniwa 129, hakuna Division I wala II. Watahiniwa watatu tuu ndio waliofanikiwa kupata Division III, wakati 60 wamepata Division IV. Watahiniwa 60 wamepata Division 0 wengine 6 sijui wamefuiwa matokeo.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...jina-ya-wanasiasa-na-matokeo-ya-mitihani.html
 
Jamani pamoja na kwamba kuna matatizo ya kisekta watoto wetu hawasomi. Wameaminishwa/ kujiaminisha kuwa maisha ni rahisi sana. Vijana wanatumia muda wa kusoma vibaya sana. Cha kusikitisha wanapenda sana anasa za muda mfupi. Wamekuwa hedonists (Piga starehe kesho itajipa yenyewe). Hawatafaulu kwa staili hii na wanapaswa walaumiwe. Kwanza wafundishwe kuwa maisha ni magumu then wakitambua hilo watasoma.
Unaenda shule ya sekondari, unakutana na walimu wawili tu, na hao hawafundishi, wakijitahidi sana wanawapa wanafunzi nakilishi (notes), hakuna mihutasali, kama ipo walimu hao hawajawahi kuitumia. Shule ina vitabu vingi sana vya sayansi yaani physics, bilogy, chimistry na hesabu, lakini walimu wa masomo hayo hawapo. Tangu shule ifunguliwe wanafunzi hao hawajawahi kuona kifaa chochote cha maabala wala maabala yenyewe. Mwishowe wanafika kidato cha nne na kuambiwa wafanye mtihani wa taifa wa baraza la mtihani. Hawana cha kuandika, wanaamua kuandika matusi ya nguoni kwani ndio waliojifunza wakiwa bila walimu. Katibu mtendaji anawafutia matokeo na kutafuta namna ya kuwafikisha mahakamani. Wewe unakuja hapa na kuwalaumu vijana wale ati wanapenda starehe na hawataki kusoma, ati wanaamini maisha ni rahisi........lo huna huruma wewe...........hujaenda ukawaona watoto wale..........unadhani Tanzania ni D'salaam tu.
 
Kaishiwa hoja huyo!siyo kila four ni zero,manake kuna div four nyingi ambazo zinaweza kwenda A-level.Kwa mfano mtu mwenye C-3 na D-6 nae hyu utasema amefeli.

mtu akiwa na alama hizo ulizotaja tayari hana div. IV bali III, isitoshe huwa ni haiwezekani mtu kupata div. IV kisha akawa na sifa za kwenda A level...
 
Mkuu kama umesoma hiyo post vizuri nimesema pamoja na matatizo mengine. Wazazi tuna nafasi kubwa sana ya kwanza kuwafanya hawa vijana kujua kuwa hatma ya maisha yao ipo mikononi mwao. Kuna katabia kameibuka hawa vijana muda mwingi ni wa kucheza na simu, mitandao, na mengine mengi ambayo sio ya kishule. Mkuu usije ukafikiri kuwa wanaofaulu kwenye maseminari ni watoto tofauti au walimu wao ni tofauti sana. La hasha, ni nidhamu tu. Bila mtoto kujua kuwa kazi yake kuu ni kusoma hakuna kitu hapo. Nakubaliana na wewe kuwa kuna shida ya kimfumo japo naamini kuwa uzembe wa wanafunzi ni mkubwa zaidi
Nakusoma! Ila hawa 90% wote wazazi wao ni wazembe? wote 90% hawana nidhamu? Daima shule sio nidhamu peke yake, japo nayo ina nafasi katika ustawi wa wanafunzi. Kusema tu kuwa wanafunzi hawana nidhamu, wakati mazingira ya kusoma hayapo na kumtegemea mwanafunzi afaulu ni njozi vile. Wanafunzi wengi, wanasikia tu bansen burner, beaker n.k lakini hawajawahi kuziona. Lakini cha kusikitisha wengi wala hawajawahi kuzisikia kwani hawakuwahi kuona vitabu (kwani vinauzwa wapi huko uyole?), hawajawahi kumuona mwalimu wa masomo kadhaa, Halafu wewe unaongelea nidhamu! Ningeshangaa kama watoto wangekosa hata fursa ya kupevuka (kwani shule siku hizi zimegeuzwa sehemu za kwenda kukulia na kujifunzia mapenzi).

Wewe umeona wanachuo waliokuwa wakimpigia magoti mkuu wa mkoa, ukadhani nidhamu ndio inayowasukuma? wangekuwa na nidhamu wasingempigia magoti mkuu wa mkoa, bali wangemweleza yale wanayofikiri kuwa ni ya msingi walioshiriki katika ujenzi wa taifa lao. Mwanachuo wa ualimu, hakufundishwa somo, akagoma akafukuzwa, huyo wa msingi itakuwa je, kulinganisha na picha ya mwalimu wake mtarajiwa kupiga goti?
 
kwanza haya yakirudi mambo yataenda sawa.
1.Bakora
2.Mchakamchaka
3.Kuhesabu namba asubuhi
4.Ukaguzi wa meno ,unifomu,kucha,kuoga na nywere
5.Walimu wakimaliza mafunzo wapite JKT ndo waje mashuleni
 
Mkuu ukweli unauma lakini sasa tuufiche? Tena shule ya Yusuf Makamba ni afadhali kama ukilinganisha Ali Hassan Mwinyi Islamic Secondary School iliyoko mkoani Tabora. Katika matokeo ya mwaka huu, shule hii ilichukua nafasi ya 1,655. Kati watahiniwa 129, hakuna Division I wala II. Watahiniwa watatu tuu ndio waliofanikiwa kupata Division III, wakati 60 wamepata Division IV. Watahiniwa 60 wamepata Division 0 wengine 6 sijui wamefuiwa matokeo.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...jina-ya-wanasiasa-na-matokeo-ya-mitihani.html
Mimi sijali matokeo ya shule moja ama mbili sababu ni zile zile tu.. Haya nipe matukeo mazuri basi ambayo wewe umeyaona yanatupa sifa ktk elimu nchini maana hapa mtoto wangu anaposoma asilimia 98 wamekwenda sekondary nambie shule hata moja iliyofikia asilimia nzuri unayoiona wewe..
 
Kaishiwa hoja huyo!siyo kila four ni zero,manake kuna div four nyingi ambazo zinaweza kwenda A-level.Kwa mfano mtu mwenye C-3 na D-6 nae hyu utasema amefeli.
Acheni kusifia kila ***** anaongea Lissu.
A=vizuri sana, B=vizuri, C=wastani, D=dhaifu, F=mbaya sana. Kwa hiyo C 3 na D 4 ni sawa sawa na D ( by finding average). Hivyo huyu mtu bado ni dhaifu kwa maana halisi hajafaulu.
 
Ni kweli!
Halafu ndio unakuta wanahangaika kutafuta vyuo vya ualimu ili wakafundishe watoto wetu!...kipofu anamuongoza kiwete!...huh!

Kimbilio La Waliofeli ni Ualimu Na Upolisi... Waitin for comments frm teachers& Police.
 
Nakusoma! Ila hawa 90% wote wazazi wao ni wazembe? wote 90% hawana nidhamu? Daima shule sio nidhamu peke yake, japo nayo ina nafasi katika ustawi wa wanafunzi. Kusema tu kuwa wanafunzi hawana nidhamu, wakati mazingira ya kusoma hayapo na kumtegemea mwanafunzi afaulu ni njozi vile. Wanafunzi wengi, wanasikia tu bansen burner, beaker n.k lakini hawajawahi kuziona. Lakini cha kusikitisha wengi wala hawajawahi kuzisikia kwani hawakuwahi kuona vitabu (kwani vinauzwa wapi huko uyole?), hawajawahi kumuona mwalimu wa masomo kadhaa, Halafu wewe unaongelea nidhamu! Ningeshangaa kama watoto wangekosa hata fursa ya kupevuka (kwani shule siku hizi zimegeuzwa sehemu za kwenda kukulia na kujifunzia mapenzi).

Wewe umeona wanachuo waliokuwa wakimpigia magoti mkuu wa mkoa, ukadhani nidhamu ndio inayowasukuma? wangekuwa na nidhamu wasingempigia magoti mkuu wa mkoa, bali wangemweleza yale wanayofikiri kuwa ni ya msingi walioshiriki katika ujenzi wa taifa lao. Mwanachuo wa ualimu, hakufundishwa somo, akagoma akafukuzwa, huyo wa msingi itakuwa je, kulinganisha na picha ya mwalimu wake mtarajiwa kupiga goti?

Mkuu nilimaanisha nidhamu ya shule. Ni kweli mazingira ni magumu ila kwa kweli mkuu inabidi pia (ambalo ni kubwa) wanafunzi ni nini maana ya kuwa mwanafunzi. Nakubaliana na wewe kimsingi na ukosefu wa vifaa mkuu. Angalia zile shule walizoia specia schools kama ashira na kwingine; hali sio nzuri. Ni lazima wazazi tuanze na lile lililo ndani ya uwezo wetu huku tukidai mazingira mazuri. Kumbuka shule bila nidhamu ya uanafunzi si shule, japo pia shule bila vifaa ni majengo
 
MGOMO BARIDI WA WAALIMU KOTE NCHINI SASA YATUJALIA KAMA TAIFA 90.02 % VIJANA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE KUJIUNGA RASMI NA SEKTA NYETI ZA UJAMBAZI NA UCHANGUDOA NCHINI - NI ZIGO LA TAIFA HILO

Ni nani huyo asiyejua kwamba MGOMO BARIDI wa Walimu kwa nchi nzima unahatari nzito kwa taifa kwa kipindi kirefu baadaye kuliko hata robo ya hatari iliosababishwa na Mgomo wa Madaktari kote nchini?

Sasa ni dhahiri kwamba kwa ufinyu wa viongozi wetu kuona mbali juu ya madai ya walimu nchini hivi sasa kada hii ya watumishi wetu serikalini wameamua KWA HASIRA KULITWISHA TAIFA ZIGO NENE la 90.02 % ya vijana waliofeli kote nchini.

wenye akili ni sharti tukajiulize kwamba hali itakuaje katika kipindi cha mia 10 ijayo kwa taifa kudondoshewa zigo zito na hatarishi kama hilo kwa hisani ya mgomo baridi wa waalimu kwa kutokusikilizwa kero zao na kutimiziwa miadi zote?

KHakika ni vema taifa tukaanza kujianda kikamilifu jinsi gani TUTAKAVYOWEZA KUUBEBA HUO MZIGO WA ASILIMIA 90.02 % pindi watakapojiunga na sekta rasmi ya UCHANGUDOA na UKIMWI kupaishwa kama ndege ya Rais Kikwete.

Ndio, wengi wao wanategemewa kujiunga na sekta ile nyeti ya UJAMBAZI kote na sekta hiyo kujaliwa nguvukazi mpya, na kwenda huko vijiweni pato la taifa kuendelea kuanguka kutokana na idadi ndogo ya watenda kazi kulea taifa la wavivu wengi na watu waliokata tamaa.

Hayo yote kwa serikali hii ya CCM, ni matatizo tu ya kujitakia!!


"Maana halisi ya mtu aliyefaulu ni yule aliyepata daraja la kwanza mpaka la tatu, chini ya hapo amefeli. Kwa maana hii basi waliofaulu katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2011 ni asilimia 9.98 pekee.

Wanafunzi 10 kati ya 100! Hao ndio waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza mpaka la tatu. Vijana wetu hawajifunzi tena. Hawa asilimia 90 wanaelekea wapi?"

Nawasilisha
 
Kaishiwa hoja huyo!siyo kila four ni zero,manake kuna div four nyingi ambazo zinaweza kwenda A-level.Kwa mfano mtu mwenye C-3 na D-6 nae hyu utasema amefeli.
Acheni kusifia kila ***** anaongea Lissu.

Nakusahihisha kidogo mkuu, mwanafunzi aliepata C-3 na D-6 anapata division three ya points 25 na sio division four. Ukitaka kuthibitisha chukua masomo saba aliyofanya vizuri halafu piga hesabu.ZINGATIA! C=points 3 na D=points 4.
 
Tatizo la kufeli kwa wanafunzi wetu siku hizi limeanzia mbali sana,na wala si suala la kudhani ni kitu cha leo tu,ni tatizo la kimfumo,hivyo limebeba mambo mengi ndani yake,ni tatizo la kijamii pia hasa kwa upande wa wazazi na mfumo wa maisha katika kaya zetu.

Katika sekta ya elimu kuanzia shule za msingi walimu wanaoandaliwa leo ni wale waliofaulu kwa kiwango cha chini,wakimaliza chuo cha ualimu ambao ni grade A wakija kusfundisha tayari wanakuwa walisha kata tamaa na kazi maana wanakuta mazingira ya kufundishia ni mabovu ni mabaya yasiyo na kifani,maisha yake binafsi nayo ni mashaka,mshahar ni kuduchu,vitabu hakuna madawati hakuna,yaani ni matatizo matupu.
Ukigeukia Secondary nako ni yale yale,shule hazina walimu,mfano kuna shule moja huko Shinyanga inaitwa Shingita secondary ni shule ya kata,mpaka mwezi wa sita kabla ya kufanya mtihani wa Form 4 kulikuwa na headmaster tu na hakuna mwalimu mwingine ,hakuna vitabu,hakuna maabara na mambo kama hayo je unategemea hapo kutakuwa na ufaulu?ni jambo kubwa mtambuka.
 
Taifa lisiloamini na kuthamini watumishi wake katika sekta ya ELIMU KWA UMMA wake huelemewa na kundi kubwa la vijan Machangudoa, Machinga, na Majambazi kil kona ya nchi!!

Naam, hakika CHADEMA hili swala ni zito na nyeti mno taifa letu kutwishwa zigo la vijana damu changa 90.02 % waliofeli mtihani wa kidato cha nne 2011.

Jambo hili lisipozungumzwa leo tena kwa kina na tahadhri zote kuchukuliwa mapema, Kamanda Saed Mwema peke yake hatoweza tena ni wazi Watanzania tutakua tunamuonea sana huyu bab kudhibiti matokeo mabaya ya kusinzia kwetu kwa mambo nyeti kama hii kwa ustawi mzuri wa taifa letu.

Tafuteni ilani ya CDM muone inasema nini kuhusu elimu
 
Kwamtazamo wa haraka mfumo wa elimu unashuka siku hadi siku walimu hawana moyo tena, Serikali inaendelea kufilisika na sasa sio pesa tu lakini hakuna wabunifu. Watu wana PHDs lakini wanaondoa mitihani na kurudisha nashuri waliohusika kuondoa mitihani ya drs la 4 na kdato cha 2 wapunguziwe Educational title mfano Kikwete anyang'anywe PHD yake yakichina.
 
Hawasomi, jibu ndio hilo, wanahangaika na mitandao.

Namshukuru Mungu binti yangu kapata
B mbili C tatu D moja na F moja. Alikuwa day ya government, kwa kweli alikuwa anasoma
karibia usiku kucha ndo kaambulia hivyo.

Ninachoomba sasa Mungu ajalie apangiwe shule.
 
Back
Top Bottom