"SHEREHE za kusimikwa kwa Kamanda mpya wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UV-CC), Bw. Deo Filikunjombe zilitikisa mji wa Ludewa mkoani Iringa baada ya wana CCM kutoka kata zote 22 za wilaya hiyo kushiriki huku wakiwa na furaha kubwa. Shamrashamra hizo zilipambwa na wanaCCM waliokuwa wamevaa fulana zenye maandishi yanayosomeka Tunampenda Deo Filikunjombe, baadaye, Bw.Filikunjombe alikabidhi msaada wa gari la wagonjwa katika Kituo cha afya Manda kwani ilielezwa kuwa wagonjwa walikuwa wakipata shida kubwa kutokana na kukosa huduma hiyo."
Mwaka huu kazi ipo ndani na nje ya chama.
Mwaka huu kazi ipo ndani na nje ya chama.