Raynavero
JF-Expert Member
- Apr 29, 2014
- 38,413
- 55,989
Chanel 5Walikuwa wanarusha channel gani vile
Chanel 5Walikuwa wanarusha channel gani vile
Walikuwa wanaanza kuzionyesha kuanzia saa tisa mchana huboreki yani CTN ilikuwa moto sana enzi hizo mkuu
Daah mkuu unakumbuka hadi mpangilio wa vipindi aisee upo juu sana mkuu yaani wangeweza wangetupatia hata marudio ya vipindi vyoteeeJumamosi itv walikuwa na hekaya za journey to the west a.k.a brother monkey sun wukong, zhu bajie nguruwe na master shifo hsuan tsan. Pia katuni za kina john quest, silver hawks na popeye the dreamer.
Nakumbuka pia tangazo la michael power na katili hekta dekta kama movie flani hivi ya kuitangaza bia ya guiness
Kule ctn na ndugu yake cen katuni network kila saa kumi jioni. Tangazo la tritel watu wamebeba bonge la simu.
Dtv tulikuwa tunaona ligi ya uingereza kila wiki mchambuzi dakta leakey stori nyingi. Pia kulikuwa na vitimbi vya mzee majuto, mwanachia, mangushi na gladys zipompapompa
Je unalikumbuka tangazo la seven up la fidodido lilikuwa poa piaSijawahi kutazama telenovela za ukweli kama Camila na La muje de Lorenzo,tangu hapo sijaangalia tena,kwa matangazo la jambo lotion lilitisha...na wewe je? Mimi naitwa jambo doogoo
kaka utakuwa unakaribia kustaafu.....hahaaha....mi nilivyo hv najiona mzee na kipindi hiko ndo kwaanza nipo la tatu.....wakati ITV inaanza kuna kifaa kilikuwa lazima ununue kiwekwe kwenye TV ili uangalie mpira.....kulikuwa na jamaa mmoja wa kipemba nadhani alikuwa akiitwa Abdi saleh ktk kipindi cha muziki.Nakumbuka ITV walipozindua tu wakaanza na World Cup 1994 USA. nilikuwa nakesha sitting room peke yangu hadi alfajiri, wakati huo nikiwa kidato cha nne.
Sanaaa tulikuwa tunakumbuka sana tuuKipindi hicho tulikua tunakariri nyimbo zotw za matangazo kama sigara Sm sigara sweetmenthol ni maarufu tanzania yoteee nimesahau maneno,taifa letu tanzania,gazeti letu tanzania mnakumbuka?revolaaa aaa revolaaaa,ule wimbo w chai jaba pia
Wow mi pia revola ndio maana hata id yangu nimeiweka hovyo coz hadi Leo natamani IPP media warudie aisee yule Dada alikuwa na sauti nyororo snKatika matangazo nilokuwa nayapenda moja wapo la revola.
'Tueleze siri ya mafanikio,
Sio siri, ni revola,
Revola pekeyake?
Ndio, kwani marashi yake ni tulivu na huniweka fresh mchana kutwaa.
Yalikuwa kama matatu tofauti, ila me nilikuwa nalipenda la yule mdada alokuwa anafanya mazoezi, ile lafudhi yake ilikuwa tamu na mbwembww zake.
Jengine la maji ya kilimanjaro.
'Maji safi kilimanjaroooo'
Tangazo la colgate la watoto, na tangazo la fanta la watoto pia.
Tamthilia nilokuwa naipenda ni Acapulco bay.