Tukumbushane Nyimbo za Bongo Flava Zilizotamba enzi za 2000-2008

nilikuwa muumini mzuri sana wa bwana sugu na sijawahi kukosa tape yake yoyote...nakumbuka wimbo wake ndani ya bongo alisema maneno haya...maisha ni kujirusha unataka kuleta zako zipi,maisha yenyewe ni mafupi,ndani ya bongo...hii ilikuwa korasi.kuna kipande anasema...kwako maisha ni matamu,kwangu ni magumu ndo maana nilaumu.iweje mi nirudi kijijini wakati mbunge wangu yupo mjini,anatanua na shangingi.mi nina akili nyingi toka msingi mpaka sekondariila naona hatari kwenda chuo kikuu,FFU wasijenivunja miguu nitakapogoma kusoma.mi nasema msije sema mi sikusema..Funika ilikuwa wimbo wa ndoto ambapo huwa nahisi aliota atakuja kuwa mbunge...mistari yake inasema....usiku naota ndoto napigana na shetani....mchana naota ndoto natoa hotuba bungeni..mwaka 2000 rais ni nani,ni ndoto.
Niliupenda ule wimbo wa sugu wa "MIKONONI MWA POLISI", Jamaa alichana haswa, c unajua tena harakati toka kitambo enzi za "Muziki & Maisha" teh!
 
kuna ule wimbo unaimbwa hivi, wanasema nimedata sina hata lakusema tena x2 ooooh no! aliimba mad ice bana ile ilikuwa bonge la pini dully sikes aliimba julieta, salome na nyambizi baasi sijaona tena wimbo mzuri wake. ila daz nundaz na nipe tano kile kilikuwa kiwango cha juu ndo maana baada ya hapo wakasambaratika
Mkuu ule wimbo ulikua unaitwa Rose, daz nundaz niliwapenda ule wimbo wa barua!
 
Huuu wimbo unatukubusha ipo siku tutakuwa no more. Kifo sio kizuri but huu wimbo i like it Kamanda- Daz Nundaz Nipe TanoAlafu kuna hawa jamaa wa mandojo na domo kaya.Aisee nilikuwa nawafagilia sana na nyimb zao kama wanock nockBila kumsahau Afande sele darubini
Safi sana mkuu! Unaukumbuka ule wimbo wa Maji ya shingo wa daz na ule wa NIKUPE NINI wa kina domo na dojo?
 
Last edited by a moderator:
Jinsi kijana- Juma Natureilikuwa inakonga moyo sana, Lizzy sio kila thread uchangie na wewe sio mod tafadhari
Yeah! Ule wimbo ulikua poa mkuu, siku hzi realy sioni kipya kwenye bongo flava. Kwanza beats zimepungua uzito, sio km enzi za Majani.
 
Kina Bush Baby enzi hizo duh! John Dillinga etc

Dah huyo John Dillinga my crew alikuwa Mkali sana yaani ni kati ya maDJ wakali sana Bongo hivi sasa hivi yuko wapi, nakumbuka kuna disco lilikuwa pale by then mambo Club walikuwa wanajiita the powerfull 4 DJ JD, DJ RICO wawili siwakumbuki) aisee jamaa walikuwa wanatandika hizo ngoma ile mbaya, DJ JD anacheza na turn table hadi aibu!!!
 
Album - ukweli mtupu, 'songi' liliotingisha Tanga kunani - Dr john & Mkololoni pata huu mstari wanakwambia "promise zao ni nyingi ila haziambiiki sijui wametutenda ni mabahau au ni visiki"
Nakumbuka kazi ya mwisho Complex kuprodyuze ilikua ni NYETI YA WAGOSI pale Backyard Records! Rest in Peace Complex and Vivian tilya!
 
deiwaka ya sugu, balozi bado nipo ya dola so, nawaza ya chindo man wa kijenge, ngangari ya gangwe mob, kipi halali kipi haramu-xplasters...
 
deiwaka ya sugu, balozi bado nipo ya dola so, nawaza ya chindo man wa kijenge, ngangari ya gangwe mob, kipi halali kipi haramu-xplasters...
Toka Ras Nelly wa x plastaz afariki, hawa washikaji wamepotea kweli duh!
 
mi nilikua naupenda sana ule wa Sos B unaitwa Kukuru kakara zako zitakuponza....pamoja na ule wa Kwanza unit wa Mimi Msafiri......pia kuna ule wa x Plasters na machalii wa arusha unaitwa wachaga piga Chata....dah hapo nakuwa burdaaani.......pia kuna ule wa big dog posse unaitwa kumwambia...
 
.....Yo, yo ndani ya bongo mambo supa hapana uongo,
ingawa sometimes bongo chungu kama sifongo,
nafanya makaratee kama machinga mtaa wa kongo,
na kimtindo mtindo nakata ngebe kimtima nyongo,

hapana matata kitu roho inapenda mtapata,
bongo dar es salaam ni mpeto wa kutakata,

pitia pitia viwanja vya bongo ustaajabu,
napita slip way, blue palm a mambo club,
kama hujazoea unaweza ukavunja shingo,
mambo isidingo, na watu mkononi nokia ringo,

huwezi kujua yupi mtoto wa geti yupi changu,
wote wanameremeta kama mamtoni mwanangu,

rudi mwananyamala ooh mateja kibao,
katiza saa moja moja uone roba za mbao,........!!!
 
Nyumba ya urithi...''ndugu zangu wamenitenda ooh,kitendo kibaya wamenitendeaaaa,sikujua napokwenda mi,ila mungu bado ananipenda;''...hope mnaukumbuka...ni jamaa anaitwa 'kijiwe'
 
kambuzi mememe kakolo mwamwamwa kabru kate chabo pwiyaa usiende resi masela tumetaitiwa!saa saba mchana mbuzi anakula jani!plasmod fella kompayalii.......manzewse crew sijui lugha gani walitumiakatika hii verse katika wimbo wao kula kona!!!!!.........................
 
nilikuwa muumini mzuri sana wa bwana sugu na sijawahi kukosa tape yake yoyote...nakumbuka wimbo wake ndani ya bongo alisema maneno haya...maisha ni kujirusha unataka kuleta zako zipi,maisha yenyewe ni mafupi,ndani ya bongo...hii ilikuwa korasi.kuna kipande anasema...kwako maisha ni matamu,kwangu ni magumu ndo maana nilaumu.iweje mi nirudi kijijini wakati mbunge wangu yupo mjini,anatanua na shangingi.mi nina akili nyingi toka msingi mpaka sekondariila naona hatari kwenda chuo kikuu,FFU wasijenivunja miguu nitakapogoma kusoma.mi nasema msije sema mi sikusema..Funika ilikuwa wimbo wa ndoto ambapo huwa nahisi aliota atakuja kuwa mbunge...mistari yake inasema....usiku naota ndoto napigana na shetani....mchana naota ndoto natoa hotuba bungeni..mwaka 2000 rais ni nani,ni ndoto.
Doctore mzee vp unazo tape za Sugu, nimezimis sana zile za kuanzia 1995 kipindi anaanza game!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom