True Story: Sikufaidi first love

Attelan

JF-Expert Member
Oct 12, 2023
433
696
Habari kwa wana JamiiForums!

Naomba niende kwenye simulizi moja kwa moja, hii ilinikuta miaka kadhaa iliyopita. Mambo yalikuwa hivi:-

Wakati ninaanza kidato cha kwanza katika shule moja ya Serikali mkoani Mbeya kama ilivyo kwa wazazi wengi baba yangu alinipa maneno haya "soma kwa bidii, shuleni ufuate Elimu tu!", Maneno haya yalinijaa vyema kichwani mwangu, si kwamba yalinikaa kwakuwa nilikuwa msikivu ila ni kwakuwa katika familia yetu kaka yetu mkubwa ambaye ndiye mzaliwa wa kwanza kwetu alimsumbua sana mzee wetu.

Kichwani nilitaka nibadilishe imani ambayo ilianza kujengeka kwa mzee wetu kwamba "watoto wa kiume kwake tulikuwa kama mzigo", kutokana na kutoka kwenye shule za Serikali ambazo msingi wake katika somo la Kiingereza sio mzuri hata mimi nilipatwa na tatizo linalowakumba wanafunzi wengi kutoka shule za Serikali (Darasa la saba) "Ung'eng'e" uliniyumbisha sana.

Katika mkondo wetu (mkondo B) tulikuwa na wanafunzi wawili ambao walitoka shule za English Medium. Hali ya kuwa na uchu wa kujua lugha ya Kiingereza ilikuwa kubwa ila iliambatana na uoga wa kuuliza kwa mara ya kwanza. Ki-haiba nilikuwa mpole na sio kobe kobe ila upole wangu ulinifanyaa nionekane mtulivu lakini kwa bahati mbaya mtulivu ambaye hata darasani matokeo yangu yalikuwa ya kawaida tu.

Baada ya mwalimu wa English kuanza kufundisha (baada ya kozi ya miezi mitatu ya Kiingereza inayotolewa shuleni kuisha) hapa ndipo nilipoanza kupata mwangaza wa lugha ya Kiingereza. Nakumbuka mtihani wa kwanza wa Kiingereza nilioufanya tulitakiwa kuandika barua iliyokuwa ikihusu 'Pocket Money' yaani pesa ya Matumizi. Nilikuwa sijui maana ya neno "Pocket Money" na ninakumbuka niliandika ya kwamba nilisahau "Pocket Money" katika ile barua nikijiweka kwenye 'neutral ground' hapa nilikuwa nabahatisha tu 😂😂

Katika hiyo barua nilichokiandika nikikikumbuka huwa nacheka tu, hata sanduku la Posta niliandika S.L.P badala ya neno P.O BOX. Nashukuru Mungu mwalimu aliamua kukata na kuniandikia P.O BOX. Baada ya mwalimu wetu huyo kuanza kutufundisha angalau nilianza kuuona mwanga.

Siku zilisonga lakini kwa bahati mbaya licha ya kwamba shule yetu ya ilikuwa katikati ya jiji haikuwa na walimu wa Masomo ya Fizikia, Kemia, Baiolojia na Hesabu. Kwa jitihada za mkuu wa shule tulipata walimu wa ziada ambao nao walikuwa wakiondoka baada ya malipo yao kusuasua. Muda ulienda na hatimaye tukaingia kidato cha Pili, hapa mambo yalianza kuwa ya ajabu ajabu kidogo.

Sikuwa na utaratibu wa kujisomea vitu ambavyo sikufundishwa na hapa ndipo nilipopigwa na pigo la kwanza. Tulipoingia katika mtihani wa Mock wa kidato cha Pili, katika somo la Hesabu tulikuwa tumesoma mada tatu tu (Exponent and Radical, Algebra na Logarithms), mtihani ulipokuja ulitubamiza vibaya na shule yetu ilikuwa miongoni mwa shule za mwisho katika matokeo ya mtihani wa Mock, tulifanikiwa kuishinda shule moja tu na sisi tuliibuka kwenye nafasi ya pili kutoka mwisho.

Hesabu iliniangusha ila nilifaulu Fizikia, Kemia na Baiolojia katika masomo ya Sayansi (kwa marks kuanzia 55% na Kemia ndilo somo nililopata 72%) kwangu niliona ulikuwa ushindi mkubwa na nikaamua kuongea na mzazi anilipie pesa ya Masomo ya ziada ili nijifunze somo la Hesabu.

Baada ya kuanza masomo ya ziada kwa moja kati ya ma'brother' wa mtaani kwetu ambaye alikuwa mwanafunzi aliyekuwa anaendelea na Masomo ya ngazi ya juu kutoka chuo kikuu cha Dar Es Salaam--UDSM hapo angalau Hesabu zikaanza kuingia kichwani. Tulianza na mada ya 'Similarity and Congruence' hapa nilianza kuona kwamba Hesabu haikuwa ngumu kama mwanafunzi anaweza kupata mwalimu mzuri. Nilikuwa nafurahia namna ambavyo nilivyokuwa nikifundishwa na yule "brother" ambaye katika mtaa alikuwa miongoni mwa 'vipanga' ambao walikuwa wa mwanzo kufaulia shule za vipaji wakati wa kujiunga na kidato cha Kwanza.

Wakati pindi linaendelea nilianza kujinoa taratibu katika usomaji na hatimaye ikawa ni tabia yangu kusoma na hapa ikawa msuli na mimi, nakumbuka sikuwahi kuwa na timu ninayoishabikia nilikuwa na ule ushabiki wa juu wa mpira ilikuwa ni kwamba akishinda Manchester na nikapata habari basi nitakenua na kuendelea na mambo mengine. Nilikuwa napenda kusoma hadithi za Kiingereza kupata maneno mapya ili kukuza idadi ya misamiati ambayo kuna muda niliishia kuikariri tu kwani sikupata mahali pakuitumia.

Baada ya matokeo ya Kidato cha Pili kutoka na mimi nilikuwako katika idadi ya wale watu ambao walifanya vizuri ingawa sikupewa zawadi kwakuwa ufaulu watu ulionekana wa kawaida mbele ya "vipanga" wa darasa sikukata tamaa nikaona niendelee na pindi tu, mtafutaji hachoki na mimi nilikuwa nikijiapiza.

Katika ukuaji kuna baadhi ya marafiki niliowapata hapo hapo shuleni waliokuwa wakifanya ngono na kuja kutupa stori wakati wa break na wangejisifia sana, ninachoshukuru Mungu ni kwamba nilikuwa muoga muoga na nisingeweza kuongea na msichana ana kwa ana na hiyo ilinisaidia kuepukana na kutafunana kimazoea na wale warembo wa darasani. Nilikuwa nikisikia kwamba fulani alikuwa akinitaka ila sikuwa na muda nao kabisa.

Baada ya kuona shule inaendelea kukosa walimu nikaamua kumuomba mama kwa kuikandia shule niliyokuwa nikisoma na kumwambia hali halisi kwamba haikuwahi kutokea waliofaulu kuingia kidato cha Tano kufika 15 tangu shule ilipoanza hivyo nikaomba uhamisho na kuhama kabisa.

ITAENDELEA
UPDATES
Sehemu ya Pili
 
PART TWO

Baada ya kufanikisha kupata uhamisho hatimaye nikaamia kwenye shule nyingine mpya kabisa. Kwanza niliyapenda mazingira ya shule, unajua unapofika sehemu ambayo kweli inafuata taratibu za uendeshaji na sheria za kila siku inafurahisha sana. Ugeni katika shule hii mpya ulikuwa ukichachafya kiasi.

Baada ya kufika shuleni na kupelekwa kwenye mkondo niliopangiwa masomo yalianza. Hapo awali macho ya kila mtu yalikuwa kwangu, ilikuwa kama nilikuwa mbele ya maafisa ambao walikuwa wakiniangalia kila dakika wakijaribu kuyatazama matendo yangu. Baada ya kukaa kwa siku kama tatu nilifanikiwa kumpata rafiki mpya, huyu rafiki nilimpata baada ya yeye kiniletea swali la Hesabu ambalo hapo awali nililifanya kwa haraka na hivyo akaweka imani yake kwangu.


Sikuwahi kuwa kwenye mazingira ambayo yalikuwa na wanafunzi wengi kama nilipoanza kusoma katika shule hii mpya. Kulikuwa na watu wa kila aina hapa, nilikutana na wale vituko wa darasani ambao wao kila siku ilikuwa no vituko. Kiufupi ni kwamba darasa lilikuwa limekamilika kila idara kama yalivyo madarasa mengine.


Baada ya siku ya dini kufika nilifuatwa na mwanafunzi mmoja wa kike ambaye hapo awali nilimuona darasani akiwa muda wote ameegamia dawati akiwa anasoma. Baada ya mwanafunzi yule kunifikia alinisalimu kiheshima "Habari!", baada ya kumjibu aliniambia yeye alikuwa kiongozi wa dini na alikuwa akiniuliza kama nilikuwa mtu wa CASFETA, TYCS, MUISLAMU au shahidi wa Yehova. Baada ya kumjibu nilimshuhudia akianza kukenua meno. Ilikuwa kana kwamba nijibu alilolitegemea.

"Nifuate tuelekee kwenye chumba cha dini" aliniambia yule mwanafunzi na baada ya hapo nilipoingia nilifanikiwa kimuona yule rafiki ambaye alinipatia swali la Hesabu nikamfuata. Kiukweli huyu jamaa alikuwa mjanjamjanja na alikuwa anaweza kuwaita hata watu akiwaambia nilikuwa nawasalimu wakati wala haikuwa hivyo.


Baada ya dini kuisha yalitangazwa maombi ya majira ya jioni na mimi nikashauriwa sana na kiongozi wa dini "Baki kwenye maombi, unaonekana ni mtulivu sana" aliongea yule kiongozi na baada ya kukubali kweli nilibaki kwenye maombi. Tukiwa bado kwenye maombi alikuja binti mmoja ambaye tulikuwa tukisoma naye darasa moja na kukaa kwenye dawati la mbele yangu.


Baada ya kukaa kwenye kiti baada ya dakika kadhaa chache tu aliinama chini na kubetua kiuno, nguo ya ndani ya yule binti ilikuwa ikionekana. Macho yangu yakawa yakibishana na ubongo ambao tayari ulianza kuwaza ngono. Rangi nyeupe ya yule binti ilikuwa ikiniharibu na kunidukua kabisa, akili ilikuwa ikiwaza ingekuwaje kama ningefanikiwa kumshika sehemu ya mgongoni hata maungoni mwake ila ndo hivyo isingewezekana kwa muda huo.

Msichana mwingine alivuta sweta la yule mwanafunzi aliyejilaza mbele yangu na kufanya ule mgongo wake ufunikwe. Tukio hili la ghafla lilinifanya nijione kama mtu aliyekamatwa akiiba mali ya mtu kwani kwa takribani dakika nilishindwa kuyatoa macho yangu kwenye mgongo wa yule msichana ambao muda huu ulikuwa umefunikwa na sweta tena vizuri.



Siku zikasonga na hapa nikaanza kupata mazoea na baadhi ya watu, kama mwanaume ambaye tayari balehe ilikwishanikaribisha kwenye urijali miaka kadhaa nyuma nilianza kuwatamani wasichana kadhaa ambao nilikuwa nikiwapenda mno. Kuna baadhi ya muda ningesimama hata mbali wasichana hao walivyokuwa wakipita. Kuna huyu mmoja alifanikiwa kuushika moyo wangu sehemu mbaya sana kiasi cha kushindwa kufurukuta. Huyu tumuite Jane ambalo si jina lake halisi.



Baada ya kufanya uchunguzi wangu butu niligundua Jane alikuwa na boyfriend wake wa humo humo darasani kwetu, na uhusiano wao ulikuwa ukifahamika na watu wengi tu na kama ningetamani kumfuata na kumfungukia kuhusu mapenzi yangu kwake uwenda wale mashushu wangefikisha taarifa kwa huyo boyfriend wake ambaye naye hakuwa makini sana kimasomo ila alimakinikia wasichana (siwezi kumlaumu isipokuwa pale alipozidisha) na ubabe.



Siku zilisonga nikiwa naumia na nilichokuwa nikitamani kukiwasilisha kwa Jane ila malengo yangu yaliishia njiani baada ya siku moja msako kufanyika ukiongozwa na mwalimu wa nidhamu. Mwalimu huyu alikuwa ni wale walimu wenye mioyo ya kina Firauni yani msamaha kwake haukuwa miongoni mwa misamiati ambayo ilikuwepo kichwani mwake.

Yaani mambo yalianza taratibu walimu waliingia darasani na kutoa maelezo kwamba kama tuliifuata Elimu basi tuendelee kusoma na kuachana na mapenzi na mara nyingi walikuwa wakitolea mfano wa Ngoswe ambaye aliishia kupoteza taarifa za sensa, mara nyingi kazi hii walipewa walimu wa kike ambao baada ya kuongea aliingia mwalimu wa nidhamu na hapo tukapewa kazi ndogo tu.

"Andika majina ya watu wenye mahusiano" alitoa amri Mwalimu wa Nidhamu na baada ya hapa kila mtu alijiinamia na kuandika jina kwenye karatasi ndogo tuliyogawiwa na kuandika majina, baada ya kukusanya yale majina majibu yalirejea na vinara ambao walionekana wana ma-girfriend na ma-boyfriend wengi waliitwa na huko hakukuwa na maelezo walikuwa wakichapwa tu.


Huko walioitwa wakataja na wengine na fimbo zikaanza kushuka kwa nguvu. Moyo uliniuma baada ya kumuona Jane akirejea akiwa anatokwa na machozi akiwa anashika mikono yake akiwa anaiweka katikati ya sketi yake akiwa anatembea kwa taratibu. Muda huu nilifanikiwa kuuona ukuu wa Mungu katika uumbaji wake, umbo la Jane lilikuwa la kibantu aswaa, hips pana, rangi nzuri, ngozi nyororo, sauti tamu na hata usafi. Ilikuwa ukipita karibu yake unaisikia harufu nzuri ya Perfume ambayo mpaka sasa bado sijaisahau, huwa nikikutana na harufu hiyo huwa mapigo ya moyo yananienda mbio mno.



ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom