The Bottom line ya sanaa ya kutongoza

katika umri wangu wa miaka 26 nimetongozwa na hata kutongoza sana. Na kwa kweli napenda sana kutongoza na kutongozwa. Kwangu mimi kutongoza/kutongozwa ni njia ya kupanua mawasiliano miongoni mwa watu mbalimbali katika jamii. Hii ndiyo silaha ama nyenzo kuu inayosaidia kuanzisha mahusiano ya kimapenzi kati ya waume kwa wake ingawa siku hizi kutokana na mporomoko wa maadili, unaweza kukuta mahusiano ya jinsia moja.

Hapa najaribu kuweka wazi uzoefu wangu katika sanaa hii ambayo wengi wetu tumepitia. kama una chochote cha kuongeza basi kitafaa sana. Pia Nataka kuweka wazi mapema kuwa wanyama wote majike kwa madume hutongoza, ila hapa nitazingatia zaidi wanadamu.

Kutongozaa ni sanaa. kama zilivyo sanaa nyingine zote kuna wanaoimudu zaidi yaw engine kutokana na utofauti wa vipaji mbalimnali. By definition naweza kuiita kuwa ni sanaa ambayo kwayo mtu anajaribu kupenya “ngome ya gereza” ambamo moyo wa mtu Fulani umewekwa mahabusu. Hapa nataka wote tuchukule kuwa moyo ama nafsi ya mtu inayotakiwa kuridhia mapenzi ni sawa na mahabusu aliyefichwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali na kuingia humo lazima hatua zote za usalama zichukuliwe ili kujiridhisha kuwa haitakuwepo hatari yoyote. Hatua hizi ni pamoja na kukaguliwa na kupekuliwa nk. kwa hali ya juu sana na ikiwapo dalili ya wasiwasi wowote, basi anayetaka kuingia hurudishwa nyuma au kukataliwa kabisa. Sasa hapo ndipo kuna sanaa mbalimbali hutumika kuwahadaa walinzi walio kwenye mlango wa hilo gereza na wakati mwingine hujikuta wameruhusu hata watu hatari kuingia humo gerezani na wakati mwingine kuutesa huo moyo humohumo gerezani ulimofungiwa.

Mbinu za mwanaume
Imezoeleka kuwa mwanumme ndiye anayetongoza zaidi na mara nyingi hutumia mbinu mbalimbali kama mazungumzo, nyimbo, miluzi, barua/email/sms, zawadi kama pesa, outgoings za shopping, dinner, lunch nk., maua, nguo, picha, uturi nk na hata ishara za mwili mfano kukonyeza, kutikisa kichwa, shingo, kuumua na kukamua uso/mashavu, kufanya baadi ya mtindo kama ya nywele na ndevu, kukitakita miguu chini kujitekenya mwenyewe ama kumtenkenya mwenzie, kujieleza ama kujisifu, kulalamika, kulia ama kuomboleza kwa lengo la kuvuta hisia na huruma ya mwenzie,kuomba msamaha kujenga hisia za uadilifu, kutoa msaada kama kumbebea vitu kama ndoo za maji, mikoba, mizigo mbalimbali nk, kujiweka karibu kimawasiliano na hata kutoa msaada kwenye familia ya msichana, kuonyesha vituko, utundu au ufundi na uhodari katika mambo fulanifulani kama michezo mbalimbali kama riadha, kucheza ngma,muziki, mpira, kuimba hata games kama karata, bao, draft nk, kuonyesha uhodari mfano kwenye kilimo, biashara, uvuvi nk. Yoote hayo kwa lengo la kupenya ngome iliyohifadhi moyo wa msichana.

Mbinu za mwanamke
Wengi huamini kuwa mwanamke hutongoza mara chache, lakini hii si kweli. Wanwake hutongoza mara nyingi sana na huenda mara yingi zaidi ya mwanaume. Tofauti ni kuwa mwanaume yuko active zaidi na mwanamke hutongoza akiwa passive zaidi. Hata wanaume wengi (kadiri ya 47%)hutongoza wasichana ambao tayari walishaanza kuwatongoza wao. Hii hutokea pale amabapo mvulana alikuwa hajiamini au amejaa woga wa kumuanza msichana kwa kuamini kuwa huenda akakataliwa au hisia kuwa msichana matawi ya juu. Sasa kama binti kampenda atamuanza yeye kwa kujiweka karibu yake na soon mwanume atapata confidence na kurusha ndoano ambayohata isipokuwa na chambo itadakwa na binti na mwanume atakuwa akiamini kuwa altongoza na kufanikiwa kupata kiulaini, kumbe hali halisi ni kuwa yeye ndiye aliyetongozwa na kunaswa kiulaini!

Tena wanawake hufanikiwa kunasa mara nyingi zaidi ukilinganisha na wanaume. Inakadiriwa kuwa zaidi ya 92% ya wanawake wanaotongoza hufankiwa huku wanaume wanaofanikiwa wakiwa 67% pekee. Ni wazi wahenga hawakukosea waliposema kuwa simba mwenda pole ndiye mla nyama!

Wanawake hutumia mbinu kama be the first to call strategy, kukuomba no. ya simu, email nk, hukuomba msaada hata pale ambapo hana shida kabisa na huo msaada mfano, vocha au misaada ya kimasomo anaweza kukuomba umsaidie swali Fulani hata kama hilo swali analijua vizuri pengine zaidi yako. Katika nchi zingine msichana anaweza kukushika kiuno mnapotembea barabarani, hapa kwetu anaweza kukushika mkono huku akikutekenya kiganja cha mkono wako, au anaweza kuzungumza nawe huku akikutazama au hata kukuchorachora kwa vidole vyake kifuani au mkononi, anaweza kuvaa nguo fulanifulani mfano za rangi ya zambarau au nyekundu hutumiwa sana, kukutembelea chumbani au nyumbani kwenu bila taarifa (japo wakati mwingine kwa taarifa) zawadi mbalimbali (kama mwanaume hapo juu), mzungumzo, nyimbo nk (ingawa si active kama alivyo mwanaume)

Naona niishie hapa na naamini licha ya kuwachosha kwa maelezo marefu, kwa kiasi fulani nimeshare nanyi kauzoefu kangu kadogo katika masuala haya.

Stay blessed & Good day
Judy

KIPAJI YA KUZALIWA HIYO...HAIFUNDISHWI...:wink2:
 
Ndio tatizo la watanzania wengi, hasa viongozi wetu wa nchi ndio maana tunaletewa mpaka wamachinga wa kichina na wapaka rangi wazungu. Sitaki niongee sana, lakin ukifanya kitu kizuri, ni ngumu sana mtanzania mwenzako akuamini

Hapo umenena mkuu, na tukiendelea hivi tutaletewa hadi wachanganya zege wa kigeni
 
mmmhhhh umetoa siri zangu Miss Judith,sasa mimi ninamtongozaje CPU? thanks,good analysis!!
 
what you have written can be 8 paragraphs but the content weights more than 8000 paragraphs
 
sijatilia mashaka uwezo wake SMU, yawezekana anao uwezolakini kwa nature ya kazi inaonesha kabisa kuwa vingi si vya calture zetu! tumeshuudia watu wengi wakipata umaarufu kutafsiri kazi za wenzao, mfano ni E. Shigongo!

Duh! Mbona unatilia shaka uwezo wake?
 
Mi nilienda Mango kwa Twanga pepeta. Nikawa najichezea zangu pale mbele pamoja na wadau wengine. Mnapafahamu Mango siku ya Jmosi usiku. Katika kucheza wakawepo mabinti wawili wazuri tu nadhani wanatoka chuo fulani. Wakatoka huko nyuma na kuja mbele yangu na mmoja (beautiful) akawa anacheza nami na mara ananipa mgongo n.k. Zikawa kama zinatembea ishara fulani kati yao. Mwisho wa siku mziki uliisha tukaenda kukaa. Inawezeka ni njia ya kutongoza? Unfortunately sikuchukua hatua yoyote maana walikuwa ni wageni kwangu ila roho ilinisuta. Niambieni ili next time nisifanye tena blunders

(kwenye red)hadithi yako nzuri sana mkubwa!(btn ze linez!!)
 
thanks kwa ujumbe bomba,watanikoma kitaa sasa.
katika umri wangu wa miaka 26 nimetongozwa na hata kutongoza sana. Na kwa kweli napenda sana kutongoza na kutongozwa. Kwangu mimi kutongoza/kutongozwa ni njia ya kupanua mawasiliano miongoni mwa watu mbalimbali katika jamii. Hii ndiyo silaha ama nyenzo kuu inayosaidia kuanzisha mahusiano ya kimapenzi kati ya waume kwa wake ingawa siku hizi kutokana na mporomoko wa maadili, unaweza kukuta mahusiano ya jinsia moja.

Hapa najaribu kuweka wazi uzoefu wangu katika sanaa hii ambayo wengi wetu tumepitia. kama una chochote cha kuongeza basi kitafaa sana. Pia Nataka kuweka wazi mapema kuwa wanyama wote majike kwa madume hutongoza, ila hapa nitazingatia zaidi wanadamu.

Kutongozaa ni sanaa. kama zilivyo sanaa nyingine zote kuna wanaoimudu zaidi yaw engine kutokana na utofauti wa vipaji mbalimnali. By definition naweza kuiita kuwa ni sanaa ambayo kwayo mtu anajaribu kupenya “ngome ya gereza” ambamo moyo wa mtu Fulani umewekwa mahabusu. Hapa nataka wote tuchukule kuwa moyo ama nafsi ya mtu inayotakiwa kuridhia mapenzi ni sawa na mahabusu aliyefichwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali na kuingia humo lazima hatua zote za usalama zichukuliwe ili kujiridhisha kuwa haitakuwepo hatari yoyote. Hatua hizi ni pamoja na kukaguliwa na kupekuliwa nk. kwa hali ya juu sana na ikiwapo dalili ya wasiwasi wowote, basi anayetaka kuingia hurudishwa nyuma au kukataliwa kabisa. Sasa hapo ndipo kuna sanaa mbalimbali hutumika kuwahadaa walinzi walio kwenye mlango wa hilo gereza na wakati mwingine hujikuta wameruhusu hata watu hatari kuingia humo gerezani na wakati mwingine kuutesa huo moyo humohumo gerezani ulimofungiwa.

Mbinu za mwanaume
Imezoeleka kuwa mwanumme ndiye anayetongoza zaidi na mara nyingi hutumia mbinu mbalimbali kama mazungumzo, nyimbo, miluzi, barua/email/sms, zawadi kama pesa, outgoings za shopping, dinner, lunch nk., maua, nguo, picha, uturi nk na hata ishara za mwili mfano kukonyeza, kutikisa kichwa, shingo, kuumua na kukamua uso/mashavu, kufanya baadi ya mtindo kama ya nywele na ndevu, kukitakita miguu chini kujitekenya mwenyewe ama kumtenkenya mwenzie, kujieleza ama kujisifu, kulalamika, kulia ama kuomboleza kwa lengo la kuvuta hisia na huruma ya mwenzie,kuomba msamaha kujenga hisia za uadilifu, kutoa msaada kama kumbebea vitu kama ndoo za maji, mikoba, mizigo mbalimbali nk, kujiweka karibu kimawasiliano na hata kutoa msaada kwenye familia ya msichana, kuonyesha vituko, utundu au ufundi na uhodari katika mambo fulanifulani kama michezo mbalimbali kama riadha, kucheza ngma,muziki, mpira, kuimba hata games kama karata, bao, draft nk, kuonyesha uhodari mfano kwenye kilimo, biashara, uvuvi nk. Yoote hayo kwa lengo la kupenya ngome iliyohifadhi moyo wa msichana.

Mbinu za mwanamke
Wengi huamini kuwa mwanamke hutongoza mara chache, lakini hii si kweli. Wanwake hutongoza mara nyingi sana na huenda mara yingi zaidi ya mwanaume. Tofauti ni kuwa mwanaume yuko active zaidi na mwanamke hutongoza akiwa passive zaidi. Hata wanaume wengi (kadiri ya 47%)hutongoza wasichana ambao tayari walishaanza kuwatongoza wao. Hii hutokea pale amabapo mvulana alikuwa hajiamini au amejaa woga wa kumuanza msichana kwa kuamini kuwa huenda akakataliwa au hisia kuwa msichana matawi ya juu. Sasa kama binti kampenda atamuanza yeye kwa kujiweka karibu yake na soon mwanume atapata confidence na kurusha ndoano ambayohata isipokuwa na chambo itadakwa na binti na mwanume atakuwa akiamini kuwa altongoza na kufanikiwa kupata kiulaini, kumbe hali halisi ni kuwa yeye ndiye aliyetongozwa na kunaswa kiulaini!

Tena wanawake hufanikiwa kunasa mara nyingi zaidi ukilinganisha na wanaume. Inakadiriwa kuwa zaidi ya 92% ya wanawake wanaotongoza hufankiwa huku wanaume wanaofanikiwa wakiwa 67% pekee. Ni wazi wahenga hawakukosea waliposema kuwa simba mwenda pole ndiye mla nyama!

Wanawake hutumia mbinu kama be the first to call strategy, kukuomba no. ya simu, email nk, hukuomba msaada hata pale ambapo hana shida kabisa na huo msaada mfano, vocha au misaada ya kimasomo anaweza kukuomba umsaidie swali Fulani hata kama hilo swali analijua vizuri pengine zaidi yako. Katika nchi zingine msichana anaweza kukushika kiuno mnapotembea barabarani, hapa kwetu anaweza kukushika mkono huku akikutekenya kiganja cha mkono wako, au anaweza kuzungumza nawe huku akikutazama au hata kukuchorachora kwa vidole vyake kifuani au mkononi, anaweza kuvaa nguo fulanifulani mfano za rangi ya zambarau au nyekundu hutumiwa sana, kukutembelea chumbani au nyumbani kwenu bila taarifa (japo wakati mwingine kwa taarifa) zawadi mbalimbali (kama mwanaume hapo juu), mzungumzo, nyimbo nk (ingawa si active kama alivyo mwanaume)

Naona niishie hapa na naamini licha ya kuwachosha kwa maelezo marefu, kwa kiasi fulani nimeshare nanyi kauzoefu kangu kadogo katika masuala haya.

Stay blessed & Good day
Judy
 
Nakubaliana na mwandishi wa thread lakini mbinu za kutongoza zinatofautiana kulingana na ulinzi wa hilo gereza. Magereza mengine yana walinzi wenye silaha kali lakini wakisomeshwa kidogo tu, wanalainika na kuruhusu wezi kuingia gerezani. Kwa mfano ukienda kwa wa wahaya hakikisha una akiba ya senene mfukoni ili unapo-sign-off unamwachia bibie anakula wakati anatafakari 'paper' uliyopresent.
 
KAMA KUTAKUWA NA UFISADI WA AINA HII NI MZURI SANA NA HATA JINA LA UFISADI LITAPOTEA, MAANA AMEFICHUA SIRI NZITO,
mimi nilkuwa najua sana maana nimeshatongozwa mara nyingi bila ya kujua. Hongera Judy kwa kutupa mambo
JUDY article yako ni nzuri sana na ya kuvutia, hongera sana! ILA NINA MASHAKA KUWA HIYO KAZI SIYO YAKO, EBU JARIBU KU ACKNOWLEDGE ORIGINAL SOURCE YA HIYO KAZI! KUTOKUFANYA HIVO NI WIZI MKUBWA SAWA NA UFISADI NDANI YA UAKADEMIA!
 
Hiyo nayo sawa lakini kumbinya kiganya si kwa mtu humjui kabisaaa, inakkuwa ni mtu ambaye unamjua ila yeye haoneshi kama anakupenda, ivo wewe unamuwahi kumwambia ili asiende kwa wengine.
I see Judy ni ngumu kumbinya binya kiganja mwanaume ambaye hujamzoea na unajua ukifanya hivyo ni msg sent.....
Labda sometimez macho yanaongea kama umempenda mtu ukimtizama usoni utajitahidi kukwepesha macho fasta ili asisome hisia zako lakini kama utaendelea kumtizama anaweza kugundua unahisia juu yake :hand:
 
Hiyo kutongoza kwa mwanamke nilikuwa naita 'kujilengesha' au 'kutega'. Kumbe twatongozwa sana tu eeh?
 
jamani mnisamehe nilikuwa bize sana nikashindwa kujibu hoja zenu, lakini nashukuru kuwa wengi wenu menielewa na lengo langu lilikuwa ni kushea tu uzoefu wangu na maandoshi yangu haya ni yangu mwenyewe, sijayanakili wala kuyanukuu toka mahali popote.

nakubaliana na aliyesema kuwa japo kuna para 8 tu mambo yaliyomo huenda yangehitaji para zaidi ya 8000. ni kweli kama mtakavyoona hata mbinu zenyewe sikuweza kuzifafanua vizuri moja baada ya nyingine, sasa kama ningefafanua kwa undani, sijui ningeandika kitabu kikubwa kiasi gani!

kutongoza kwaweza kuwa na mitazamo kadha wa kadha ila kutongoza si kitu kibaya na nimekiri kuwa hata mie nilishatongoza mara nyingi. lengo ni kupanua mawasiliano na hata kutaongeza marafiki na pengine wachumba na hata wake/waume watarajiwa. sanaa hii ya kutongoza ikitumiwa vizuri italeta furaha maishani mwa mtu kwani huleta marafiki karibu na kumfanya mtu ajisikie kuwa kati ya jamii na kuondoa upweke. ikitumiwa vibaya, huharibu sifa ya mtu na kumfanya aonekane malaya/mhuni, nk

wanawake na wasichana wanapaswa kutoona haya kutongoza ila wawe makini wasijeonekana vituko kwani jamii yetu bado ina mitazamo isiyo sawa kwa wanawake na wanaume juu ya kutongoza. si lazima msichana akimtongoza mtu basi wamalizie na ngono, wanaweza kupanga hilo baadaye kadiri itakavyoonekana inafaa lakini pia wanaweza kishia kuwa marafiki wa kawaida tu.

nlipokuwwa kidato cha pili nliwahi kumtongoza mvulana fulani na siku moja ya jumamosi ambayo haikuwa siku ya shule (kwa tuliosoma day school) nikamfuata kwao na kumtaka twende tukaongee mambo yetu shuleni manake nilikuwa napenda sana maongezi yake. kwa kweli kuanzia siku iyo alinisumbua sana akitaka tufanye ngono nami nikabaki njia panda. ngono sitaki kufanya na kumuudhi sitaki, nataka aendelee kuwa rafiki yangu. mwishoni hatimaye alinielewa laini alikuwa na huzuni siku zote na hakuwa akinifurahia tena hadi tunaachana baada ya kumaliza form four. so mtaona hatari ya msichana kutongoza.

i hope mtanielewa na nawatakia kila la heri wote wanaotongoza ama kutongozwa.

stay blessed
 
Kwa hizi mbinu za mwanamke, sasa naanza kuamini nimetongozwa zaidi kuliko nilivyotongoza

we acha tu........mimi nilipokuwa chuo kuna mdada alikuwa anapenda sana kunitkea room....tatizo mshkaji wangu alishapita....nikaona nikipita dizaini itakuwa sio fresh.....ila kitu ya haja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom