emmathy
Senior Member
- Sep 22, 2010
- 147
- 25
Leo nimeona tofauti iliyokuwepo kati ya chama tawala na vyama vya upinzani kupitia TBC. Katika taarifa zake za jioni hii ya tarehe 19Febr 2012 wameonyesha katibu wa itikadi na uwenez CCM N.N, akiwa katika moja ya misa akiwaasa vingoz wa dini kukemea mabaya n.k, na vile vile wamemuonyesha katibu wa vijana ccm taifa ndg Shigela akiwa kigoma akiwaasa vijana kutokutumika na viongozi wa juu kufikia malengo yao binafsi.
Huku kwetu Tanga yupo Naibu katibu mkuu CHADEMA ZITO, mkurugenzi wa habari CHADEMA MNYIKA, pamoja na Mwenyekiti wa vijana taifa CHADEMA bwana HECHE , ambao kimtazmo uzito wao na sawa na viongozi hao wa CCM niliowataja kama sikuwazidi. Hakuna taarifa ya CHADEMA iliyoripotiwa juu yakile wanachokifanya kama vile ambavyo wameripoti kwa CCM.
Je TBC ambayo ni television ya Taifa, inatumia vigezo gani kutangaza habari katika television ambayo wananchi wote tunaichangia ktk uendeshaji wake kupitia kodi zetu? Ni mtazamo tu, tutafakari.
Huku kwetu Tanga yupo Naibu katibu mkuu CHADEMA ZITO, mkurugenzi wa habari CHADEMA MNYIKA, pamoja na Mwenyekiti wa vijana taifa CHADEMA bwana HECHE , ambao kimtazmo uzito wao na sawa na viongozi hao wa CCM niliowataja kama sikuwazidi. Hakuna taarifa ya CHADEMA iliyoripotiwa juu yakile wanachokifanya kama vile ambavyo wameripoti kwa CCM.
Je TBC ambayo ni television ya Taifa, inatumia vigezo gani kutangaza habari katika television ambayo wananchi wote tunaichangia ktk uendeshaji wake kupitia kodi zetu? Ni mtazamo tu, tutafakari.