mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Tunapoelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025 ni vyema vyama vyote vya upinzani vitakavyoshiriki vikaanza maandalizi mapema kabla giza halijazama.
Wote tunakumbuka uchafuzi uliofanyika katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 ambapo vyama vya upinzani vilipata pigo moja matata tokea kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Uchaguzi huo ulighubikwa na uonevu mkubwa sana wagombea wengi wa CCM walijikuta wakipita bila kupingwa kutokana na kinachodaiwa wagombea wengine wa vyama vya siasa walishindwa kujaza fomu kwa usahihi.
Tunakumbuka mwaka 2019 wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa jinsi ambavyo wagombea wa upinzani walivyoenguliwa kiubaguzi kwa kasoro ambazo hazikuwa za Kikatiba na ambazo zingeweza kusahihishwa.
Kimsingi Chaguzi za mwaka 2019 na 2020 zilirudisha nyuma mafanikio ya kuratibu chaguzi na matokeo yake.
Maandalizi yaanze mapema sana, vyama hivyo viteue wagombea wenye uwezo, kwanza wajue kusoma na kuandika. Baada ya kupata competent candidates, vyama viwajengee uwezo masuala mazima ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kujaza fomu kwa usahihi.
Ni aibu kubwa mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA kukuta kwenye fomu kajaza CDM badala ya CHADEMA.
Naamini wagombea wakipatikana mapema na kujengewa uwezo, basi mchakato mzima wa uchaguzi utapungua kasoro, vyama vya upinzani vitapata wawakilishi wengi Serikali za Mitaa na kuamsha ari uchaguzi mkuu 2025.
Ni hayo tu.
Wote tunakumbuka uchafuzi uliofanyika katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 ambapo vyama vya upinzani vilipata pigo moja matata tokea kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Uchaguzi huo ulighubikwa na uonevu mkubwa sana wagombea wengi wa CCM walijikuta wakipita bila kupingwa kutokana na kinachodaiwa wagombea wengine wa vyama vya siasa walishindwa kujaza fomu kwa usahihi.
Tunakumbuka mwaka 2019 wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa jinsi ambavyo wagombea wa upinzani walivyoenguliwa kiubaguzi kwa kasoro ambazo hazikuwa za Kikatiba na ambazo zingeweza kusahihishwa.
Kimsingi Chaguzi za mwaka 2019 na 2020 zilirudisha nyuma mafanikio ya kuratibu chaguzi na matokeo yake.
Maandalizi yaanze mapema sana, vyama hivyo viteue wagombea wenye uwezo, kwanza wajue kusoma na kuandika. Baada ya kupata competent candidates, vyama viwajengee uwezo masuala mazima ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kujaza fomu kwa usahihi.
Ni aibu kubwa mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA kukuta kwenye fomu kajaza CDM badala ya CHADEMA.
Naamini wagombea wakipatikana mapema na kujengewa uwezo, basi mchakato mzima wa uchaguzi utapungua kasoro, vyama vya upinzani vitapata wawakilishi wengi Serikali za Mitaa na kuamsha ari uchaguzi mkuu 2025.
Ni hayo tu.