Tanzania: Ni yapi yaliyojiri 1995?

joka kuu naomba utzame facts zako upya

kighoma malima alichukua fomu za uraisi pia.....
hata kama hakufika mbali.but alichukua fomu
Soma taratibu hapo chini...

MwanaFalsafa1,
..kwa kumbukumbu zangu walijitokeza wana CCM kama 15 hivi kutaka ridhaa ya chama chao. Ninaowakumbuka ni kama Balozi.Frederick Rutakyamirwa, Njelu Kasaka,Mark Bomani, Joseph Warioba,Pius Msekwa, Horace Kolimba, Benjamin Mkapa,Horace Kolimba,John Malecela, Cleopa Msuya,Jakaya Kikwete, Edward Lowassa,....
 
The Boss,

..Kighoma Malima stood no chance ya kupewa nafasi na CCM.

..Mabalozi walikuwa wanashinikiza afukuzwe kazi baada ya kuonekana serikali haikusanyi kodi.

mkuu hebu jaribu kuelewa kwanza
hatuzungumzii walio kuwa na nafasi ya kupewa
tunazungumzia waliochukua fomu
hata kama hakuwa na nafasi
alichukua fomu,hilo ndo tunataka lizungumzwe
 
Mkuu JokaKuu, asante sana kwa historia hiyo.

Edward Lowassa na Jakaya Kikwete walikodisha ndege pamoja kwenda Dodoma kuchukua fomu. waliporudi DSM kulikuwa na msisimko mkubwa kutokana na umaarufu aliokuwa nao Lowassa wakati huo. Kikwete yeye alikuwa anasema yuko pale kama kumuunga mkono kijana mwenzake.
Ina maana mkuu JK was not "In it to win it"? Yani alijiunga na kampeni kwa nia ya kumsindikiza Lowassa? Au ilikua kama 2005 walipo ahidiana mmoja atakua raisi na mwingine prime minister.
 
wewe unachanganya watu humu
walikuwepo na wangeweza kugombea ni sawa na kugombea???????/
swali hapa ni waislamu wangapi walichukua fomu za kugombea urais mwaka 1995????/
jibu ni kikwete na malima tu
usilete habari za salim na wazanzibari,wakati mtu hakuchukua fomu
na alijibu ana kazi nyingi,na wewe article umeileta hapa,********???????

The Boss,
Sidhani Mwalimu Nyerere aliangalia ugombeaji wa kiti cha rais katika misingi ya kidini kama unavyotaka kutuaminisha. CCM ingeweza kusimamisha Waislamu wote na kwa Mwalimu lisingekuwa tatizo. Kadhalika CCM ingeweza kusimamisha Wakristo na wapagani wote na hilo kwa Mwalimu lisingekuwa tatizo. Sidhani alikuwa na mtazamo wa kuangalia kuna Waislamu wangapi wanaogombea na kuna Wakristo wangapi. Hii inadhihirishwa na kauli zake mwenyewe, kama alivyotaja Mkandara somewhere in this thread.
 
mkandara unachanganya madawa hapa
sali alizushiwa hayo mambo kwa uchaguzi wa 2005
muanzisha mada anazungumzia uchaguzi wa 1995
na uchaguzi huo salim hakuwepo kabisa katika wagombea,alisema bado ana majukumu oau
ni kweli mwalimu alimtaka achukue fomu,but hakuchukua
Nina kubaliana na The Boss uzushi dhidi ya Salim ulikuwa 2005

Kabla ya uchaguzi 2005 mtandao waliakikisha wanamchafulia mtu yoyote ambaye anaoneka ni tishio kwa Kikwete.Mtikila alitumika kumchafua Sumaye,Magazeti na uzee wa Malecela na Salim kuhusishwa na kifo cha Karume.

1995 magazeti yaliandika mara kwa mara SAS ndio chaguo la Nyerere lakini akaendelea kukaa kimya na bila hata kuonyesha nia.Ndipo Nyerere alipojitokeza hadharani ilikumshinikiza SAS ambaye baadae akaweka wazi hata gombea kwasababu anataka kuendelea na majukumu yake ya OAU.Alipoamua kugombea 2005 Mkapa hakakataa kumuunga mkono SAS na kama sijakosea ndipo mgogoro kati ya taasisi ya Mwl Nyerere na Mkapa ulipoanzia.

 
MwanaFalsafa1,

..let my try my two cents.

..Prof.Malima alikuwa hayuko on the picture. Huyu alikuwa na matatizo makubwa na wafadhili walishashinikiza aondolewe kazini. Aliundiwa tume ya uchunguzi ilyoongozwa na Mohamed Aboud, ambaye alikuwa CAG.

..Salim Salim alikuwa awe mrithi wa Mwalimu tangu mwaka 1985 baada ya kuchukua nafasi ya Edward Sokoine[r.i.p]. Mchezo ulikuwa wawekwe Salim Salim na Mzee Mwinyi ambaye alikuwa ni Raisi wa Zanzibar kuanzia 83/84 baada ya Jumbe kutimuliwa. Inasemekana Seif na Salim walimshawishi Mzee Mwinyi amuachie nafasi hiyo Salim Salim kwa kisingizio kwamba yeye ndiyo kwanza ameshika madaraka makubwa Zanzibar. Mzee Mwinyi aliwageuka wenzake baada ya majina yao kufikishwa mbele ya Kamati Kuu ya CCM. Hiki ni kisa ambacho nadhani kipo ktk kitabu cha maisha ya Seif Sharrif Hamad.

..mwaka 1995 inasemekana Nyerere alimtaka tena Dr.Salim lakini this time akamkatilia kwasababu ilidhani itakuwa vigumu kwa Wazanzibar kushika nafasi ya Raisi wa Muungano kwa vipindi viwili. nadhani baada ya hapo ndiyo Nyerere akaona atupe karata yake kwa Mkapa.

..kwa kumbukumbu zangu walijitokeza wana CCM kama 15 hivi kutaka ridhaa ya chama chao. Ninaowakumbuka ni kama Balozi.Frederick Rutakyamirwa, Njelu Kasaka,Mark Bomani, Joseph Warioba,Pius Msekwa, Horace Kolimba, Benjamin Mkapa,Horace Kolimba,John Malecela, Cleopa Msuya,Jakaya Kikwete, Edward Lowassa,....

..nakumbuka Mkapa alichukua fomu ktk mazingira ambayo ilionekana kama hayuko serious na hana nguvu zozote zile. aliwaita waandishi wa habari ofisini kwake wizara ya sayansi na teknolojia na kwa kweli hata habari zilizoandikwa zilikuwa zinaonyesha kwamba hatafika mbali.

..Cleopa Msuya alichukua fomu nadhani wiki ya mwisho na hakukuwa na taarifa zozote zile. nadhani he did it on a weekend akiwa amekatisha ziara zake za kikazi.

..Edward Lowassa na Jakaya Kikwete walikodisha ndege pamoja kwenda Dodoma kuchukua fomu. waliporudi DSM kulikuwa na msisimko mkubwa kutokana na umaarufu aliokuwa nao Lowassa wakati huo. Kikwete yeye alikuwa anasema yuko pale kama kumuunga mkono kijana mwenzake.

..there are different versions of what transpired in the Kamati Kuu ikiwemo fununu kwamba Nyerere alitishia kurudisha kadi ikiwa Malecela asingeondoa jina lake, na pia kumpiga nyundo Lowassa kwamba alikuwa na utajiri usioeleweka. Nadhani in the end majina matatu ndiyo yalikwenda Halmashauri Kuu kupigiwa kura kupelekwa Mkutano Mkuu.

..kwa kumbukumbu zangu, ktk kura za Halmashauri Kuu, Cleopa Msuya alikuwa mshindi, which was a surprise, akifuatiwa na Jakaya Kikwete which was even a bigger surprise. Benjamin Mkapa alishika nafasi ya tatu. baada ya hapo kukawa na kipindi cha mpito kuelekea wa CCM na ikaonekana Kikwete alikuwa amekosewa. Kuanzia hapo nguvu za Cleopa Msuya zikaanza kufifia.

..katika kipindi cha kuelekea mkutano mkuu upinzani mkubwa, haswa magazetini, ulionekana kuwa kati ya JK na Msuya. magazeti mengi yalielekea kumkubali zaidi JK haswa kutokana na haiba yake ya ujana na kuwa askari mstaafu. Cleopa Msuya alionekana kupingwa zaidi kutokana na kashfa ya kusema "kila mtu atabeba msalaba wake." Msuya pia did not help himself kwasababu alikuwa anahimiza ukusanyaji kodi kipindi hicho akiwa Waziri Mkuu na kuna kipindi alifika Tabora na akalalamika kuhusu wananchi kutokuwa na moyo wa kulipa kodi ambayo yeye alikuwa anaona ni kidogo!! magazeti yalimshambulia sana kwa kauli yake hiyo. Msuya pia alikuwa anaonekana ndiye aliyeshinikiza Augustino Mrema atimuliwe kazi na Raisi Mwinyi.

..kampeni ya Mkapa ilionekana kuibuka kuziba vacuum iliyoachwa na kudorora kwa kampeni ya Msuya. Mkapa alionekana kuungwa mkono na kundi la wana CCM waadilifu waliokuwa wakipiga vita rushwa iliyokuwa imeshamiri wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi. Mkapa alikuwa anapigiwa kampeni kama mtu msafi mwenye nia na uwezo wa kupambana na rushwa.

..sikubahatika kusikia hotuba za wagombea Uraisi wakati wakiomba kura za wajumbe wa mkutano mkuu. nilisikiliza nasaha za Mzee Mwinyi na Mwalimu Nyerere kwa wajumbe wa mkutano mkuu kabla kura hazijapigwa. Mzee Mwinyi alitoa nasaha kwamba wajumbe wafuate kile ambacho wananchi wanataka kwa kumpigia kura mgombea aliyekuwa anasemwa vizuri na wananchi. kwa hotuba ile ilionekana kwamba Mzee Mwinyi alikuwa akimtaka Jakaya Kikwete. Ilipofika zamu ya Mwalimu yeye aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea anayeweza kupiga vita rushwa, ukabila, na udini. Wengi walitafsiri kwamba alikuwa akimtaka Benjamin Mkapa.

..raundi ya kwanza ya kura mshindi alikuwa Jakaya Kikwete, akifuatiwa na Ben Mkapa, na Msuya akashika mkia. Kura ziliporudiwa ilionekana kama kura zote za Msuya zimehamia kwa Mkapa na hivyo akatangazwa mshindi. There is an interesting sub plot baada ya Mkapa kutangazwa mshindi. Inasemekana kuna kundi la mashabiki wa Kikwete waliokuwa wakizomea ushindi wa Mkapa. Mwalimu alionyesha kufurahishwa mno na ushindi wa Mkapa. I dont remember his exact words. Cleopa Msuya alipopewa nafasi ya kutoa concession speech aliwaasa wana CCM waache siasa za "kuchimbana."

jokaKuu,
Hapa ningekuwa mwalimu wako darasani ningekupa 100% tena na plus juu yake.
 
The Boss,
Sidhani Mwalimu Nyerere aliangalia ugombeaji wa kiti cha rais katika misingi ya kidini kama unavyotaka kutuaminisha. CCM ingeweza kusimamisha Waislamu wote na kwa Mwalimu lisingekuwa tatizo. Kadhalika CCM ingeweza kusimamisha Wakristo na wapagani wote na hilo kwa Mwalimu lisingekuwa tatizo. Sidhani alikuwa na mtazamo wa kuangalia kuna Waislamu wangapi wanaogombea na kuna Wakristo wangapi. Hii inadhihirishwa na kauli zake mwenyewe, kama alivyotaja Mkandara somewhere in this thread.


jasusi naona hatukuelewana
ninachoongea mimi ndio hiko hiko unachozungumza wewe

but kuna vitu vingine ni maoni yangu na sio facts kutoka kwa nyerere

mwaka 1995 facts ni kuwa kabla ya kikwete kuchukua fomu,
muislam aliechukua fomu alikuwa kighoma malima peke yake
so hawakutaka chama kionekane kinawabagua waislam
unaweza kupinga udini kwa maamuzi ambayo mwingine anaweza ona ndo udini wenyewe
sisemi nyerere alimwambia kikwete achukue fomu kwa kuwa ni muislam...
 
jasusi naona hatukuelewana
ninachoongea mimi ndio hiko hiko unachozungumza wewe

but kuna vitu vingine ni maoni yangu na sio facts kutoka kwa nyerere

mwaka 1995 facts ni kuwa kabla ya kikwete kuchukua fomu,
muislam aliechukua fomu alikuwa kighoma malima peke yake
so hawakutaka chama kionekane kinawabagua waislam
unaweza kupinga udini kwa maamuzi ambayo mwingine anaweza ona ndo udini wenyewe
sisemi nyerere alimwambia kikwete achukue fomu kwa kuwa ni muislam...
Hapo nimekupata, mkuu.
 
MwanaFalsafa1,

..let my try my two cents.

..Prof.Malima alikuwa hayuko on the picture. Huyu alikuwa na matatizo makubwa na wafadhili walishashinikiza aondolewe kazini. Aliundiwa tume ya uchunguzi ilyoongozwa na Mohamed Aboud, ambaye alikuwa CAG.

..Salim Salim alikuwa awe mrithi wa Mwalimu tangu mwaka 1985 baada ya kuchukua nafasi ya Edward Sokoine[r.i.p]. Mchezo ulikuwa wawekwe Salim Salim na Mzee Mwinyi ambaye alikuwa ni Raisi wa Zanzibar kuanzia 83/84 baada ya Jumbe kutimuliwa. Inasemekana Seif na Salim walimshawishi Mzee Mwinyi amuachie nafasi hiyo Salim Salim kwa kisingizio kwamba yeye ndiyo kwanza ameshika madaraka makubwa Zanzibar. Mzee Mwinyi aliwageuka wenzake baada ya majina yao kufikishwa mbele ya Kamati Kuu ya CCM. Hiki ni kisa ambacho nadhani kipo ktk kitabu cha maisha ya Seif Sharrif Hamad.

..mwaka 1995 inasemekana Nyerere alimtaka tena Dr.Salim lakini this time akamkatilia kwasababu ilidhani itakuwa vigumu kwa Wazanzibar kushika nafasi ya Raisi wa Muungano kwa vipindi viwili. nadhani baada ya hapo ndiyo Nyerere akaona atupe karata yake kwa Mkapa.

..kwa kumbukumbu zangu walijitokeza wana CCM kama 15 hivi kutaka ridhaa ya chama chao. Ninaowakumbuka ni kama Balozi.Frederick Rutakyamirwa, Njelu Kasaka,Mark Bomani, Joseph Warioba,Pius Msekwa, Horace Kolimba, Benjamin Mkapa,Horace Kolimba,John Malecela, Cleopa Msuya,Jakaya Kikwete, Edward Lowassa,....

..nakumbuka Mkapa alichukua fomu ktk mazingira ambayo ilionekana kama hayuko serious na hana nguvu zozote zile. aliwaita waandishi wa habari ofisini kwake wizara ya sayansi na teknolojia na kwa kweli hata habari zilizoandikwa zilikuwa zinaonyesha kwamba hatafika mbali.

..Cleopa Msuya alichukua fomu nadhani wiki ya mwisho na hakukuwa na taarifa zozote zile. nadhani he did it on a weekend akiwa amekatisha ziara zake za kikazi.

..Edward Lowassa na Jakaya Kikwete walikodisha ndege pamoja kwenda Dodoma kuchukua fomu. waliporudi DSM kulikuwa na msisimko mkubwa kutokana na umaarufu aliokuwa nao Lowassa wakati huo. Kikwete yeye alikuwa anasema yuko pale kama kumuunga mkono kijana mwenzake.

..there are different versions of what transpired in the Kamati Kuu ikiwemo fununu kwamba Nyerere alitishia kurudisha kadi ikiwa Malecela asingeondoa jina lake, na pia kumpiga nyundo Lowassa kwamba alikuwa na utajiri usioeleweka. Nadhani in the end majina matatu ndiyo yalikwenda Halmashauri Kuu kupigiwa kura kupelekwa Mkutano Mkuu.

..kwa kumbukumbu zangu, ktk kura za Halmashauri Kuu, Cleopa Msuya alikuwa mshindi, which was a surprise, akifuatiwa na Jakaya Kikwete which was even a bigger surprise. Benjamin Mkapa alishika nafasi ya tatu. baada ya hapo kukawa na kipindi cha mpito kuelekea wa CCM na ikaonekana Kikwete alikuwa amekosewa. Kuanzia hapo nguvu za Cleopa Msuya zikaanza kufifia.

..katika kipindi cha kuelekea mkutano mkuu upinzani mkubwa, haswa magazetini, ulionekana kuwa kati ya JK na Msuya. magazeti mengi yalielekea kumkubali zaidi JK haswa kutokana na haiba yake ya ujana na kuwa askari mstaafu. Cleopa Msuya alionekana kupingwa zaidi kutokana na kashfa ya kusema "kila mtu atabeba msalaba wake." Msuya pia did not help himself kwasababu alikuwa anahimiza ukusanyaji kodi kipindi hicho akiwa Waziri Mkuu na kuna kipindi alifika Tabora na akalalamika kuhusu wananchi kutokuwa na moyo wa kulipa kodi ambayo yeye alikuwa anaona ni kidogo!! magazeti yalimshambulia sana kwa kauli yake hiyo. Msuya pia alikuwa anaonekana ndiye aliyeshinikiza Augustino Mrema atimuliwe kazi na Raisi Mwinyi.

..kampeni ya Mkapa ilionekana kuibuka kuziba vacuum iliyoachwa na kudorora kwa kampeni ya Msuya. Mkapa alionekana kuungwa mkono na kundi la wana CCM waadilifu waliokuwa wakipiga vita rushwa iliyokuwa imeshamiri wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi. Mkapa alikuwa anapigiwa kampeni kama mtu msafi mwenye nia na uwezo wa kupambana na rushwa.

..sikubahatika kusikia hotuba za wagombea Uraisi wakati wakiomba kura za wajumbe wa mkutano mkuu. nilisikiliza nasaha za Mzee Mwinyi na Mwalimu Nyerere kwa wajumbe wa mkutano mkuu kabla kura hazijapigwa. Mzee Mwinyi alitoa nasaha kwamba wajumbe wafuate kile ambacho wananchi wanataka kwa kumpigia kura mgombea aliyekuwa anasemwa vizuri na wananchi. kwa hotuba ile ilionekana kwamba Mzee Mwinyi alikuwa akimtaka Jakaya Kikwete. Ilipofika zamu ya Mwalimu yeye aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea anayeweza kupiga vita rushwa, ukabila, na udini. Wengi walitafsiri kwamba alikuwa akimtaka Benjamin Mkapa.

..raundi ya kwanza ya kura mshindi alikuwa Jakaya Kikwete, akifuatiwa na Ben Mkapa, na Msuya akashika mkia. Kura ziliporudiwa ilionekana kama kura zote za Msuya zimehamia kwa Mkapa na hivyo akatangazwa mshindi. There is an interesting sub plot baada ya Mkapa kutangazwa mshindi. Inasemekana kuna kundi la mashabiki wa Kikwete waliokuwa wakizomea ushindi wa Mkapa. Mwalimu alionyesha kufurahishwa mno na ushindi wa Mkapa. I dont remember his exact words. Cleopa Msuya alipopewa nafasi ya kutoa concession speech aliwaasa wana CCM waache siasa za "kuchimbana."
Hii ya ndege Kikwete na Lowassa walitumia kama njia ya kujingea jina lakini it turned out to be disaster kwa Lowassa.Magazeti ya kaanza kuuliza pesa wamepata wapi,kumbuka 1995 kupanda ndege ya kukodisha ilikuwa ni jambo kubwa.utetezi wa Lowassa ulikuwa ni wamefadhiliwa, ikawa ni last nail to his coffin kwamba wafadhili ndio wanakupeleka ikulu ukifika huko watakuja kudai fadhila zao.
 
Kwa mimi ambae nilikwa kijana mdogo na kwa kufuatilia masimulizi hiyo story ambayo leo ingeniongezea elimu [knowledge] ya mchakato mzima kidogo nimemwelewa Joka Kuu ameonekana kiasi kikubwa kugusa kile nilichokuwa nasikia miaka hiyo.

Na ambalo siwaelewi wengi wenu na kwa kiwango kikubwa naona amjalizingatia ni issue ya Lowasa na Kikwete.
Logical Kikwete katika swala la urais wa 1995 alikuwa ni zaidi ya Lowasa japo wengi wanaona Kikwete ndiye ndiye aliyekuwa Msindikizaji.Kama kuna mambo ya kiutu uzima mmoja alikuwa ndio kusudio na Lowasa alikuwa boya na mapesa yake huku mwezie akijua anafanya nini?

Ukizangatia wengine mmesema Mwalimu alimwambia Kikwete akachukue Form,ni kwanini akamwambie kuchukua form za kugombea urais na aliposhindwa Mwalimu inasemekana alimwambia bado ajakua, kuna mdau kasema unexperienced. Ukizungumzia hoja ya kidini haitakuwa na mashiko kwa kuwa rais aliyekuwa madarakani alikuwa ni Mwislamu basi kama kufuata alipaswa kuwa mkristu kama ingekuwa ni mfumo wa CCM katika uchaguzi.Uchaguzi wa mwaka 1995 hata mimi na udogo wangu nilikuwa fans wa Kikwete.

Hivyo kusema Kikwete ndio alikuwa msindikizaji si kweli,na kwa kuwa mmoja kwa kujua mwezie ni charasmatic na kuwa anakubalika kwa Mwalimu Nyerere akaonekana aegemee kwa faida yake.

Hivi tuhuma za marehemu KM kuwa na Account ya mapesa nje,ilikuwa ni kipindi gani ni kabla ya uchaguzi au ni baada ya uchaguzi naomba msaada kujua hili.Manake nasikia mwalimu alijua uwepo wa mabilion ya pesa ambayo mdau huyo alikuwa amejikusanyia na kujiwekea kwenye account moja uko ulaya.

Uchaguzi wa 1995 Salim Ahmed Salim kama sikosei hakushiriki uchaguzi wa mwaka huo baada ya kuwa bussy zaidi na maswala ya kidiplomasia na kwa mtizamo wangu baada ya zengwe la HIZBU kwa upande wa Zanzabara zaid wakati huo 1985 kumkwaza na kitabia anaonekana Uwanadiplomasia umemkaa.Ni muumini wa stay aside and let nature take it cause.

Uchaguzi wa 2005,hapa ndipo kulifanyika vindumbwe ndumbwe kibao,manake kulikua na kambi kibao,Kuna kusanyiko la kambi nyingi na ambazo zingine ndio wahanga wa toka mwaka 1995. Mteule alisimama baada ya kuwa haikuwa hakuna namna yoyote ile kwa utashi wa Wananchi ambao walikuwa na historia yake toka huko nyuma ya mwaka 1995, ukiunganisha na kuwa charasmatic basi hata wale waliokusudia kumpiga chini ikawawia vigumu manake hofu ya mpasuko kama angeamua kuasi chama ikawa ni vigezo vya uteuzi.
 
Dogo kulikuwa na mtu alikuwa anaitwa Tuntemeke sanga huyu aliishia kwenye 5bora lakn huyu alikuwa na uwezo mkubwa kwani alikuwa anafanya maamuzi mazuri hata akiwa bungeni, lakini alikuwa haivi na nyerere hivyo akatoswa.
umenikumbusha mbali sana historia ya huyu Bwana ktk nchi hii
nakumbuka aliwahi kumwambia SPIKA by then alikuwa MSEKWA kuwa "huko kwenu hakuna wakubwa wa kuwa heshimu" hii ilikuwa pale alipo ambiwa muda wa kuchangia (dk 15) umeisha


huyu Bwana aliwa na degree 7 za masomo tofauti tofauti historia yake ni kubwa
 
Mkuu DSN au mkuu mwingine yoyote yule mnaweza mkatueleza zaidi kuhusu uhusiano wa JK na EL 1995?
 
Kilichojitokeza ni kwamba wale wafuasi wa Msuya walimwunga mkono Che Nkapa na wale Wazenj walikuwa wamepewa maelekezo na Komandoo Salimin (alikuwa bado anakipindi kimoja cha kukaa madarakani) kwamba wasithubutu kumchagua "Play Boy - Kikwete". Kwa hiyo hata Komandoo hakutaka kuwa chini ya Kikwete
 
Kilichojitokeza ni kwamba wale wafuasi wa Msuya walimwunga mkono Che Nkapa na wale Wazenj walikuwa wamepewa maelekezo na Komandoo Salimin (alikuwa bado anakipindi kimoja cha kukaa madarakani) kwamba wasithubutu kumchagua "Play Boy - Kikwete". Kwa hiyo hata Komandoo hakutaka kuwa chini ya Kikwete

Ilikuaje tena hapa mkuu? Maana mdau mwingine alisema kura za Zenji ndizo zilizo mfikisha JK tatu bora kwa sababu alisha wahi kufanya kazi huko kama mwanajeshi. Na kuna sababu zaidi za Salim kutomtaka JK au ni kwa sababu tu alikua "Play Boy".
 
kumbe Warioba hana merits za kuwa Rais,sikujua kuwa naye alishachukua fomu 1995.Kumbe angeweza pata favor ya Nyerere kama angekuwa competent kwa vile alifanya naye kazi kwa karibu,lakini badala yake Mkapa ndiye akaonekana anafaa
 
kinachoendelea leo ni dhambi ya kumnyima uongozi JK nchi isingefika katika hali hii tuliyonayo ss ya watu kujiuzia wao na kusahau ,mamilioni ya wenzao
Nakumbuka baadhi ya mambo licha ya kwamba nilikuwa bwana mdogo.Gari ya Mrema nilisukuma.Wengi tuliamini angeingia ikulu kama si mwalimu.Mwalimu angemchagua JK maybe ingekuwa bora zaidi kwasababu angekuwa chini ya uangalizi wake.Mkapa ni mnafiki mkubwa,mwalimu alifanya kosa hapo.Kama alikjuwa kin EL wanamipesa,basi angemshurutisha Mkapa awawajibishe.Ama angetilia msisitizo kuwa wawajibishwe na si kuwanyima nafasi za kisiasa.Sasa alipotutoka tunaona tatizo bado lipo,na this time mafisadi ndo wenye nguvu because mwalimu was an one army man.
Ntarudi.
 
Back
Top Bottom