MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Kuna wengine wetu tulikua wadogo mwaka 1995 kuweza kufuatilia kinyanganyiro cha uraisi mwaka huo. Ndiyo maana ningependa kujua zaidi nini kilicho jiri ndani ya CCM mpaka kupelekea kumteua raisi mstaafu Benjamin WIilliam Mkapa kuwa mgombea wa CCM kwa mwaka huo.
Machache ninayo jua ni kwamba final three ya CCM ilikua Kikwete, Mkapa na Msuya. Nasikia Kikwete alishinda round ya kwanza ila hakupata zile asilimia 51 zinazo hitajika kupata ushindi wa moja kwa moja. Round ya pili ikawa yeye na Mkapa na Nyerere kwa kutumia ushawishi wake ndani ya chama aka hakikisha ushindi unaenda kwa Mkapa.
Kwa nijuavyo mimi (naweza kusahihishwa) ni kwamba Nyerere hakudhani Kikwete kakomaa kiuongozi kuweza kuwa raisi mpaka akadiriki kusema "hatuendi kutoa posa tunaenda kuchagua raisi. Kama mtu anampenda mtu kwa sababu ya sura akanywe nae chai."
Sasa kwa wanaokumbuka zaidi (najua wapo wengi) naomba mnisaidie kunipa somo la historia hapa ya nchi yetu kwa sababu kinyanganyiro cha 1995 ndicho kilicho toa raisi wa kwanza wa mfumo wa vyama vingi.
Machache ninayo jua ni kwamba final three ya CCM ilikua Kikwete, Mkapa na Msuya. Nasikia Kikwete alishinda round ya kwanza ila hakupata zile asilimia 51 zinazo hitajika kupata ushindi wa moja kwa moja. Round ya pili ikawa yeye na Mkapa na Nyerere kwa kutumia ushawishi wake ndani ya chama aka hakikisha ushindi unaenda kwa Mkapa.
Kwa nijuavyo mimi (naweza kusahihishwa) ni kwamba Nyerere hakudhani Kikwete kakomaa kiuongozi kuweza kuwa raisi mpaka akadiriki kusema "hatuendi kutoa posa tunaenda kuchagua raisi. Kama mtu anampenda mtu kwa sababu ya sura akanywe nae chai."
Sasa kwa wanaokumbuka zaidi (najua wapo wengi) naomba mnisaidie kunipa somo la historia hapa ya nchi yetu kwa sababu kinyanganyiro cha 1995 ndicho kilicho toa raisi wa kwanza wa mfumo wa vyama vingi.