mashatiboyee
Member
- Dec 24, 2022
- 14
- 186
Habari za jioni wanajukwaa wa MMU, ikiwa mmetoka katika mihangaiko akili na mwili vimechoka nawaletea jambo jingine hili tupate kulijadili.
Mimi na mke wangu ni waajiliwa yeye ni mtumishi wa umma na mimi ni mtumishi wa sekta binafsi, ndoa yetu ina miaka mitatu sasa na tuna mtoto mmoja (asante sana MUNGU kwa hili).
Shida iliyonileta kwenu ni kuwa hapa karibuni nimepata matatizo ya kikazi sasa imenibidi niwe nashinda nyumbani kwa sababu mimi siyo mtu wa kukaa nje sana nahisi ndipo matatizo yalipoanzia. Tangu nipatwe na hii hali mke wangu amebadilika tabia sijui kama ni makusudi au lah.
Niwe muwazi kuwa mke wangu amenizidi mshahara lakini pamoja na hayo sijawahi kuona tabia hizi kwake hadi hapo nilipopatwa na hizo shida kazini.
Tabia zipo nyingi ila naleta tatu zilizonishitua;
~ Kwanza amekuwa hataki kushiriki nami tendo.
~ Pili sababu huwa nashinda na mtoto huwa napika kwa ajili yangu na mtoto ambapo ye akirudi anapika kwa ajili ya wote kwani anasema sijui kupika. Sasa hapo juzi kati alinambia itabidi nijifunze kupika kama nataka kuendelea kuwa naye.
~ Tatu ni kuwa tuna machine ya kufulia sasa imeharibika, nikamuomba kuwa nikipata hela tutafanya matengenezo akanijibu kama ni hivyo basi niwee namfulia nguo zikiwemo chupi zake daah.
Mimi nimefikiria uamuzi wa kuachana naye licha ya kuwa na mtoto naye, kwani sina mpango wa kumpiga na hiyo juzi ilibaki kidogo nipige arudi kwao Vunjo Mashariki na ulemavu wa uso alivyosema niwe namfulia.
Nauliza tu wanawake wa humu haya anayofanya mwenzenu ni halali kweli?
Mimi na mke wangu ni waajiliwa yeye ni mtumishi wa umma na mimi ni mtumishi wa sekta binafsi, ndoa yetu ina miaka mitatu sasa na tuna mtoto mmoja (asante sana MUNGU kwa hili).
Shida iliyonileta kwenu ni kuwa hapa karibuni nimepata matatizo ya kikazi sasa imenibidi niwe nashinda nyumbani kwa sababu mimi siyo mtu wa kukaa nje sana nahisi ndipo matatizo yalipoanzia. Tangu nipatwe na hii hali mke wangu amebadilika tabia sijui kama ni makusudi au lah.
Niwe muwazi kuwa mke wangu amenizidi mshahara lakini pamoja na hayo sijawahi kuona tabia hizi kwake hadi hapo nilipopatwa na hizo shida kazini.
Tabia zipo nyingi ila naleta tatu zilizonishitua;
~ Kwanza amekuwa hataki kushiriki nami tendo.
~ Pili sababu huwa nashinda na mtoto huwa napika kwa ajili yangu na mtoto ambapo ye akirudi anapika kwa ajili ya wote kwani anasema sijui kupika. Sasa hapo juzi kati alinambia itabidi nijifunze kupika kama nataka kuendelea kuwa naye.
~ Tatu ni kuwa tuna machine ya kufulia sasa imeharibika, nikamuomba kuwa nikipata hela tutafanya matengenezo akanijibu kama ni hivyo basi niwee namfulia nguo zikiwemo chupi zake daah.
Mimi nimefikiria uamuzi wa kuachana naye licha ya kuwa na mtoto naye, kwani sina mpango wa kumpiga na hiyo juzi ilibaki kidogo nipige arudi kwao Vunjo Mashariki na ulemavu wa uso alivyosema niwe namfulia.
Nauliza tu wanawake wa humu haya anayofanya mwenzenu ni halali kweli?