Tamko la Kamati Kuu ya CCM kuhusu DOWANS na hali ya kisiasa nchini

Sidhani kama huo ndiyo ulikuwa umuhimu wa kikao hiki cha juu kabisa katika CCM, na kikao cha kwanza kwa mwaka mpya 2011.

Mara nyingi umuhimu wa tamko au waraka wo wote, unaonekana kwa kiasi gani muda au nafasi imetumika kujadili hilo suala. Ukiangalia na kuchambua tamko hili la CCM CC, utaona kuwa kwa mpangilio, wametumia:

Maneno 472 kuzungumzia Chadema na u-Meya Arusha
Maneno 193 kuzungumzia Sherehe za CCM
Maneno 171 kuzungumzia vurugu na vifo vya Arusha
Maneno 115 kuzungumzia umoja wa vyama vya ukombozi
Maneno 104 kuzungumzia malipo ya Dowans (bila kutaja tatizo la umeme nchini)
Maneno 100 kuzungumzia semina ya wabunge wa CCM. (Agizo kwa wabunge lilitolewa siku 3 KABLA ya kamati Kuu kukaa)
Maneno 65 kuzungumzia migomo/mitafaruku vyuoni.

Nini ambavyo havikuzungumziwa wala kutajwa hata neno moja:
Utekelezaji wa ahadi za JK na CCM kwa mwaka 2011 na miaka ijayo
Katiba
Uchumi wa nchi
Elimu
Afya
Barabara, Reli, Umeme na Miundombinu yote
Usalama wa Raia na Nchi.

mkuu uchambuzi umetulia
 
Vipi kuhusu Tamko la chadema kuhusu DOWANS?kwanini wanaongelea mjukwaani tu?tuliweke tamko la CDM hapa jamvini ili tulijadili kama hili.
 
Sorry wana jf, Kwenye mistari ya hili tamko sijaona karipio la udini! Au kw CC ya ccm hii antagonism ya viongozi wa dini is not a big deal but an important propagandistic weaponry aspect?

Good point Owenya.

Pili, Mwenyekiti wa kamati ya nidham ni Mh. Vijisenti ambaye pia ni mjumbe wa CC.

Ningeshangaa kama CC ingekuja na majibu tofauti na haya. Wamejaa kiburi na kuwadharau wananchi. Yana mwaisho '' Kuli'' by A.ShAFI.
 
Kwa nini CCM wanafanyia mikutano ya chama chao Ikulu ? Je ikulu ni mali ya CCM? Hivi kweli Obama anaweza kuendesha mkutano wa chama cha Democrat pale white house bila kuraruliwa na raia walipa kodi?

Mkulu
Heshima mbele, siku nyingi hatujaonana hapa jamvini....heri ya mwaka mpya
 
hapa ndipo wametuthibitishia kumbe CC ya CCM ndiyo wamiliki halali wa DOWANS...................................hivi malipo ya wastaafu wa Afrika mashariki ambayo yana sheria ya Bunge mbona majibu mepesi kama ya DOWANS CC ya CCM haiyatoi????????????????????????????????????????????

Jibu ni kuwa wastaafu hao hawana cha kuwahonga............JK na timu yake ya mafisadi...........eti Tanesco walivunja mkataba........................Je waliouvunja mkataba mnawachukulia hatua gani?

Na mkataba upi waliuvunja wakati Richmond iliyorithi mkataba ni kampuni hewa????????????????????????

Only impeachment of Kikwete will end impunity and official graft in this country we all call home.....................

Rutashubanyuma: NAOMBA MAONI YAKO KATIKA HILI LA UMEYA ARUSHA. Naona kama unaruka kimanga.

2. VURUGU KATIKA MANISPAA YA ARUSHA

Kamati Kuu imesikitishwa na tukio la vurugu za kisiasa zilizotokea tarehe 5 Januari, mwaka huu katika Manispaa ya Arusha ambapo watu watatu walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa pamoja na uharibifu mali. Kamati Kuu inawapa pole waliofiwa, waliojeruhiwa na wale ambao mali zao ziliharibiwa. Aidha ni matumaini ya Kamati Kuu kwamba tukio hili halitarudiwa tena hapa nchini kwani lengo letu sote ni kudumisha amani na usalama wa maisha ya wananchi na mali zao. Kuhusu maandamano yaliyozuiwa na Jeshi la Polisi lakini baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakachochea yafanyike na hatimaye kusababisha wananchi kupoteza maisha yao, na wengine kujeruhiwa na uharibifu wa mali, kwa vile suala hili sasa lipo Mahakamani Kamati Kuu haitapenda kulizungumzia kwa undani. Imetoa angalizo kwa viongozi wa siasa wa vyama vyote kuwa wajibu wao wa kwanza ni kulinda amani na utulivu, na kujiepusha kabisa na uchochezi wenye kuleta chuki na ubabe wa kutunishana misuli na vyombo vya dola ambavyo ndiyo muhimili wa ulinzi na usalama wa nchi yetu na wananchi wote na mali zao.

3. UCHAGUZI WA MEYA MANISPAA YA ARUSHA
Kwa kuzingatia kwamba umekuwepo upotoshaji mkubwa kuhusu uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Arusha, na hata kusababisha malalamiko mengi na vurugu, Kamati Kuu inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:-

Kwanza:
· Matokeo ya Udiwani Manispaa ya Arusha yalikuwa ifuatavyo: Madiwani wa Kata: CCM 10, CHADEMA 8 na TLP 1 – Jumla viti 19.
· Madiwani Viti Maalum: CCM 3, CHADEMA 3.
· Wabunge Viti Maalum: CCM 3, CHADEMA 3.

Matokeo ya jumla: CCM – Viti 16, CHADEMA 14 na TLP 1. Jumla Viti 31.

Pili:

Siku ya kupiga kura (tarehe 18/12/2010) Mkutano ulipoanza wajumbe 14 wa CHADEMA hawakuwepo. Waliofika ni wajumbe 16 wa CCM na 1 wa TLP, jumla wajumbe 17 ambao ni zaidi ya nusu ya wajumbe wanaotakiwa ili mkutano uwe halali kwa mujibu wa sheria.

Katika mazingira haya Msimamizi wa Uchaguzi aliendesha uchaguzi ambapo Ndugu Gaudence Vicent Lyimo wa CCM alipata kura 17, hivyo kutangazwa mshindi halali wa kiti cha Umeya na Ndugu Michael Kivuyo wa TLP alipata kura 17 na kutangazwa mshindi halali wa kiti cha Naibu Meya.

Kwa hiyo wanaosema uchaguzi huo haukuwa halali ama hawajui sheria au wanajiingiza tu katika ushabiki wa kisiasa.


Tatu:

CHADEMA wanadai katika wale wajumbe 16 wa CCM, mmoja wao (Mhe. Mary Chatanda) hakuwa mjumbe halali kwa kuwa katika kugombea Ubunge wa Viti Maalum aligombea kupitia Mkoa wa Tanga.

CHADEMA, kupitia Msimamizi wa Uchaguzi waliomba ufafanuzi wa kisheria kutoka Tume ya Uchaguzi, Katibu wa Bunge na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu. Ofisi zote hizo tatu zilitoa jibu kwamba Mhe. Mary Chatanda alikuwa mjumbe halali wa kikao hicho, na kwamba Wabunge Viti Maalum ni Wabunge wa Kitaifa na vyama vyao ndivyo vinawapangia Halmashauri za kufanyia kazi. Mhe. Mary Chatanda anaishi Arusha akifanyakazi kama Katibu wa CCM wa Mkoa huo hivyo CCM ilimpangia hapo hapo Arusha ndipo afanyie kazi za Halmashauri kama Diwani na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa iliarifiwa kuhusu uamuzi huu kama sheria inavyotaka.

Ni ufafanuzi huo huo ndio CHADEMA waliutumia kushinda kiti cha Halmashauri ya Hai baada ya kuwapangia kufanyakazi katika Halmashauri hiyo Wabunge 2 wa Viti Maalum na ambao si wakaazi wa Wilaya hiyo. Kura hizo mbili ndizo ziliwapa CHADEMA ushindi; na CCM tumekubali matokeo kwa kuwa kwa kufanya hivyo CHADEMA hawakuvunja sheria.

Uhalali wa Mhe. Mary Chatanda kupiga kura Manispaa ya Arusha ni sawa sawa na uhalali wa Wabunge wawili wa Viti Maalum wa CHADEMA walivyopiga kura Hai.

Jambo hili CHADEMA wanalijua vizuri lakini wanapotosha umma kwa makusudi wakitumia vyombo vya habari ambavyo bila kufanya utafiti navyo vimekuwa vinashabikia suala hili.

Kwa kifupi Kamati Kuu inasisitiza kwamba Uchaguzi wa Meya wa Arusha ulifuata sheria kwa ukamilifu, na washindi walishinda kihalali na hakuna sababu ya kurudia kufanya uchaguzi mwingine. Iwapo kuna watu hawaridhiki na mchakato wa uchaguzi huo wanayo nafasi ya kupinga katika vyombo vya sheria bila ya kufanya fujo wala kuleta uvunjifu wa amani kama ule uliotokea tarehe 5/1/2011 kule Arusha.


 
Taarifa ya Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi

......

4. HUKUMU YA KUILIPA KAMPUNI YA DOWANS

Kamati Kuu imetafakari kwa makini suala la TANESCO kuilipa kampuni ya DOWANS Shs. 94 bn. na kubaini kuwa huu ni uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Biashara kwamba TANESCO ilivunja mkataba kinyume cha makubaliano na katika hali ya kawaida, kama hakuna njia nyingine ya kujiondoa kwenye kosa, ni busara na ni wajibu kwa muungwana kuheshimu maamuzi ya Mahakama. Hata hivyo, Kamati Kuu imeona kuwa kwa vile wapo Watanzania walioamua kupinga Mahakamani uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa wa TANESCO kuilipa DOWANS fidia ya Sh. bilioni 94, basi ni vema Serikali isubiri uamuzi wa Mahakama Kuu juu ya pingamizi hili.

Katika yote sijaweza kupata picha inayojaribu kutengenezwa hapa, Maswala ya TANESCO shirika la uma kujadiliwa na kutolewa maamuzi na vikao vya chama tawala badala ya baraza la mawaziri. nadhani hii ni move ya kuweka msingi kwa wabunge wa sisiem wasihoji pindi jambo hili likijaribu kuibuka bungeni. kweli hili ni genge la wannyang'anyi ....,
 
Sidhani kama huo ndiyo ulikuwa umuhimu wa kikao hiki cha juu kabisa katika CCM, na kikao cha kwanza kwa mwaka mpya 2011.

Mara nyingi umuhimu wa tamko au waraka wo wote, unaonekana kwa kiasi gani muda au nafasi imetumika kujadili hilo suala. Ukiangalia na kuchambua tamko hili la CCM CC, utaona kuwa kwa mpangilio, wametumia:

Maneno 472 kuzungumzia Chadema na u-Meya Arusha
Maneno 193 kuzungumzia Sherehe za CCM
Maneno 171 kuzungumzia vurugu na vifo vya Arusha
Maneno 115 kuzungumzia umoja wa vyama vya ukombozi
Maneno 104 kuzungumzia malipo ya Dowans (bila kutaja tatizo la umeme nchini)
Maneno 100 kuzungumzia semina ya wabunge wa CCM. (Agizo kwa wabunge lilitolewa siku 3 KABLA ya kamati Kuu kukaa)
Maneno 65 kuzungumzia migomo/mitafaruku vyuoni.

Nini ambavyo havikuzungumziwa wala kutajwa hata neno moja:
Utekelezaji wa ahadi za JK na CCM kwa mwaka 2011 na miaka ijayo
Katiba
Uchumi wa nchi
Elimu
Afya
Barabara, Reli, Umeme na Miundombinu yote
Usalama wa Raia na Nchi.
SALUTE MKUU...............wakati mwingine unaweza kuona anachotaka kuweka wazi mtu kwa kuangalia anaongea sana nini!! tumekusoma.CC na CCM ni mabata wanaoogelea kwenye tope na kupongezana kwamba wamekuwa wasafi sana.
 
Hivi kwa ni vyama vingine haviombi kufanya mikutano yao hapo ikulu? Hawa jamaa wanabuse offisi hii muhimu.
Ikulu ni nyumbani kwa mwenyekiti wa CCM, kwa hiyo huwezi kumchagulia wageni mtu nyumbani kwake. akitaka kufanya party na mabalozi mpaka hasubuhi ruksa, akitaka kuongea na watuumiwa wa ufisadi sawa...... nyinyi vyama vya upinzani mna wivu
JK hadhi yake ni kubwa sana hawezi kufanya mkutano ofisi ya lumumba kwa ajili haina hadhi.
 
"You can not teach an old dog new tricks"..ni neno nililokuwa nawaambia Watanzania..huyu jamaa hatakuja na mabadiliko yoyote katika miaka 5 ijayo sana sana tutarajie hali ngumu zaidi.Nature ya hao waliopo madarakani sasa ni kudeal na vitu vidogo vidogo na mzaha mzaha tu na si mambo serious.
 
Kikwete kutumia ikulu kwa vikao vya ccm ni kosa kubwa kisheria na kimaadili! Ikulu inaendeshwa kwa kodi za raia wote wa Tanzania na siyo za wana ccm tu, na ikulu ni ofisi ya juu ya serikali siyo ya chama! Mkuu wa mkoa au wilaya hawezi kufanya kikao cha chama katika ofisi yake hata siku moja! Pili, tamko la cc ya ccm kuhusu Arusha haliko sawa, wamesema tarehe ya uchaguzi wa meya wajumbe wote wa chadema hawakuwepo! Walikwenda wapi? Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha aliwapa madiwani wa chadema barua ya kuhudhuria kikao kule Olasiti siku tatu kabla na siyo kwenda kwenye ukumbi wa Halmashauri kwa uchaguzi meya, walipofika olasiti mkurugenzi hakufika ndo ikabidi mbunge Lema amfuate ofsni akamkuta ukumbini akiendesha uchaguzi wa meya, Lema alpoingia ukumbini, afande Zuberi ambaye ni kamanda wa polisi wa wilaya ya Arusha akamtoa ukumbini kwa virungu! Na taarifa ya jimbo la HAI imepotoshwa, wajumbe wote wa Hai wamechaguliwa/wameteuliwa Hai na wanaishi Hai!
 
Kwa nini CCM wanafanyia mikutano ya chama chao Ikulu ? Je ikulu ni mali ya CCM? Hivi kweli Obama anaweza kuendesha mkutano wa chama cha Democrat pale white house bila kuraruliwa na raia walipa kodi?
Katiba.... katiba.... katiba.... Katiba ndio mwongozo! Katiba ndio sheria mama. bila katiba hata machinga na wachuuzi watachuuza biashara zao IKULU!
 
Sidhani kama huo ndiyo ulikuwa umuhimu wa kikao hiki cha juu kabisa katika CCM, na kikao cha kwanza kwa mwaka mpya 2011.

Mara nyingi umuhimu wa tamko au waraka wo wote, unaonekana kwa kiasi gani muda au nafasi imetumika kujadili hilo suala. Ukiangalia na kuchambua tamko hili la CCM CC, utaona kuwa kwa mpangilio, wametumia:

Maneno 472 kuzungumzia Chadema na u-Meya Arusha
Maneno 193 kuzungumzia Sherehe za CCM
Maneno 171 kuzungumzia vurugu na vifo vya Arusha
Maneno 115 kuzungumzia umoja wa vyama vya ukombozi
Maneno 104 kuzungumzia malipo ya Dowans (bila kutaja tatizo la umeme nchini)
Maneno 100 kuzungumzia semina ya wabunge wa CCM. (Agizo kwa wabunge lilitolewa siku 3 KABLA ya kamati Kuu kukaa)
Maneno 65 kuzungumzia migomo/mitafaruku vyuoni.

Nini ambavyo havikuzungumziwa wala kutajwa hata neno moja:
Utekelezaji wa ahadi za JK na CCM kwa mwaka 2011 na miaka ijayo
Katiba
Uchumi wa nchi
Elimu
Afya
Barabara, Reli, Umeme na Miundombinu yote
Usalama wa Raia na Nchi.
Hayo si muhimu kwa sasa! Umuhimu wake na kutajwa kwake itakuwa 2015!! Na hapo ndipo itakuwa kipimo cha wazimu wa Watanzania kilipofikia. Maana uchaguzi uliopita ilikuwa ni kipimo cha akili zetu.
 
Ikulu ni nyumbani kwa mwenyekiti wa CCM, kwa hiyo huwezi kumchagulia wageni mtu nyumbani kwake. akitaka kufanya party na mabalozi mpaka hasubuhi ruksa, akitaka kuongea na watuumiwa wa ufisadi sawa...... nyinyi vyama vya upinzani mna wivu
JK hadhi yake ni kubwa sana hawezi kufanya mkutano ofisi ya lumumba kwa ajili haina hadhi.

IKULU NI MAHALI PATAKATIFU.hadhi ya ikulu hairuhusu wahuni kama kina makamba kuwepo eneo hilo.kikao kile ni cha kamati kuu sio cha cabinet,isitoshe pale sio msoga useme kila nduguye mkwere amtembelee.
 
Mmmmmmmmmmmmmmmmmm!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1 Kwakweli ni hatari tujihazari kabla ya hatari. JK alishawahi kutoa msemo kuwa iposiku watoto watakao kuwa wamezaliwa watapiga Makaburi yetu wakisema walikuwa wapi hawa. Lakini sasa kwa staili hii haitakuwa kupigwa makaburi hii itakuwa kavukavu, live live haina kusubir maana mambo yanaonekana mapema watu wazima na watoto uzalendo unwashinda.
 
Kikwete kutumia ikulu kwa vikao vya ccm ni kosa kubwa kisheria na kimaadili! Ikulu inaendeshwa kwa kodi za raia wote wa Tanzania na siyo za wana ccm tu, na ikulu ni ofisi ya juu ya serikali siyo ya chama! Mkuu wa mkoa au wilaya hawezi kufanya kikao cha chama katika ofisi yake hata siku moja! Pili, tamko la cc ya ccm kuhusu Arusha haliko sawa, wamesema tarehe ya uchaguzi wa meya wajumbe wote wa chadema hawakuwepo! Walikwenda wapi? Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha aliwapa madiwani wa chadema barua ya kuhudhuria kikao kule Olasiti siku tatu kabla na siyo kwenda kwenye ukumbi wa Halmashauri kwa uchaguzi meya, walipofika olasiti mkurugenzi hakufika ndo ikabidi mbunge Lema amfuate ofsni akamkuta ukumbini akiendesha uchaguzi wa meya, Lema alpoingia ukumbini, afande Zuberi ambaye ni kamanda wa polisi wa wilaya ya Arusha akamtoa ukumbini kwa virungu! Na taarifa ya jimbo la HAI imepotoshwa, wajumbe wote wa Hai wamechaguliwa/wameteuliwa Hai na wanaishi Hai!

Nashukuru kwa ufafanuzi wa hoja. Lakini CCM kama wao wana madiwani wengi kwa nini waliamua kuwakimbia Chadema? Au kwanini wasingewaruhusu tu chadema wawepo na wao wangeshinda bila hata Mary Chitanda kupiga kura kwa sababu idadi yao bado ni kubwa. Hili suala silielewi kabisa au ilikuwa kuonyeshana ubabe tu
 
..kwani kwa mawazo yako wewe serikali ni ya chama gani ili iweze kutofautiana na upuzi wa cc ya ccm?

At least ndani ya ''serikali'' kuna Mawaziri kadhaa hawakubaliani na uamuzi wa kuilipa Dowans. Baadi yao (wenye misimamo thabiti) wameshasema hadharani kwamba DOWANS wasilipwe. Ninajua kuna wengine kadhaa hawataki DOWANS walipwe ila wanaogopa kusema hadharani.

Kama issue ikifikishwa kwenye baraza la Mawaziri, majibu tofauti yanaweza kutoka huko.
 
sijui makamba na kutumia kwake bibilia ana kumbuka maneno aliyo sema Yesu alipowafukuza wacheza kamari nk katika hekalu alisema hii ni nyumba ya baba yangu na sio mahali pa wanyanganyi kufanya mambo yao akimaanisha ni mahali pa kufanyia ibada, sasa ikulu anatakiwa kuelewa ni mahali patakatifu kwa watanzania na sio sehemu ya wanyanganyi kupafanya mahali au gulio za biashara zao, bali pa kulinda na kutetea masilahi ya watanzania na si mafisadi.
Na kichekesho cha kauli ya CC mpaka wakati mwingine unashindwa kuelewa hawa ni majuha, mumiani, wevi etc eti Tanesco ndio walijitoa, je hapo awali tanesco walitaka kuingia huu mkataba? kama sio shinikizo kutoka ofisi kubwa? na aliye kuwa anaongoza shirika si ni mteule wa Serikali? sasa serikali inapo taka kujitenga na huo uamuzi wana maanisha nini?
na Bodi ya tanesco si inateuliwa na viongozi wa serikali? . kweli ikiona mambo yanaenda hivi na suala kupelekwa chamani badala ya kwenye baraza la mawaziri ujue mwizi ndio wetu ni mtu mkubwa kichama ambaye akishughulikiwa nchi yaweza kuyumba.
 
Back
Top Bottom