Tamko la Kamati Kuu ya CCM kuhusu DOWANS na hali ya kisiasa nchini

haya bana,kumbe chadema ndo wagomvi arusha sasa kwa maana hiyo eti eh?
 
Siku ya kupiga kura (tarehe 18/12/2010) Mkutano ulipoanza wajumbe 14 wa CHADEMA hawakuwepo. Waliofika ni wajumbe 16 wa CCM na 1 wa TLP, jumla wajumbe 17 ambao ni zaidi ya nusu ya wajumbe wanaotakiwa ili mkutano uwe halali kwa mujibu wa sheria.

Katika mazingira haya Msimamizi wa Uchaguzi aliendesha uchaguzi ambapo Ndugu Gaudence Vicent Lyimo wa CCM alipata kura 17, hivyo kutangazwa mshindi halali wa kiti cha Umeya na Ndugu Michael Kivuyo wa TLP alipata kura 17 na kutangazwa mshindi halali wa kiti cha Naibu Meya.

Kwa hiyo wanaosema uchaguzi huo haukuwa halali ama hawajui sheria au wanajiingiza tu katika ushabiki wa kisiasa.


hii yoote ndio iliyosababisaha vurugu za arusha. ccm wlitakiwa waone hali halisi
 
na katika hali ya kawaida, kama hakuna njia nyingine ya kujiondoa kwenye kosa, ni busara na ni wajibu kwa muungwana kuheshimu maamuzi ya Mahakama.


what a crap comment
 
hivi quoram ya uchaguzi wa meya ni 1/2 au 2/3, kuna mtu mahali alisema ni 2/3, naomba mniweke sawa hapa jamani
 
Hivi kuna aliyetegemea tamko tofauti na haya? Kati ya wajumbe wa CC, wengi wao ni wale wanaotuhumiwa hapa jamvini, RA, EL, Vijisenti, etc. na ukiweka list nzima, kati ya 36 zaidi 50% ni wachakachuaji!
 
Wameshaambiwa kuwa fedha walizokuwa wakitumia katika kampeni ni hizo ambazo mwenyewe RA anazitaka. Hawana jinsi yaani serikali nzima inakuwa chini ya mtu mmoja tena fisadi! Kweli CCM wamechoka na wameshindwa kabisa kusoma alama za nyakati. Licha ya kelele zote lakini hizi lakini wao hawakosi usingizi.
 
yaani very easy & simple answers, majibu mepesi kwa mambo makubwa kama migomo,
Dowans, etc, imani yangu kwa hawa is -ve 100% i feel nausea each time, is like
they don't think at all, wapo wapo tu, eeh Mungu, & why kikao cha chama
kifanyike Ikulu? Is Ikulu a CCM Office? since when? kumbe na wao wanandamana
nchi nzima, ngoja wapinzani pia wanadamane then tuone kama watanyimwa?
i hate them
 
Hivi kwa ni vyama vingine haviombi kufanya mikutano yao hapo ikulu? Hawa jamaa wanabuse offisi hii muhimu.
 
Nchi imeuzwa-natangaza rasmi leo.
CC ya ccm ni vichwangumu na ni watu wanaoishi kwenye dunia ya tofauti na hii yetu.
Ishu ya dowans siamini kama hayo ndiyo majibu-iam baffled!
Hivi Tanesco wanakubali kutwishwa gunia hilo la MISUMARI na kuwa MBUZI WA SADAKA, wakati tunajua kabisa kwmb walishinikizwa kwa amri za mkubwa?
This is NO MANs COUNTRY!,..HUH!
 
Wameanguka na pua sasa wanajizoazoa.. Kama hao kwenye picha ni kweli kamati kuu ya ccm na ndiyo iliyotoa hilo tamko basi hakuna kiongozi hata mmoja serekalini mwenye kufaa kuchaguliwa au kuwepo kwenye serikali makini.. Hivi ukiangalia hii inamaana gani???

1. Wazee wa eac wanadai malipo yao hadi leo hawajalipwa.. Je hayo siyo ya ulazimaa?????
2. Walimu wanadai malimbikizo ya malipo yao kwa zaidi ya miaka 5 sasa.. Hayo je siyo ya lazima???
3. Walimu wa vyuo malimbikizo kibao... Hayo je??
4. Walimu wa sekondari hawana ajira kisa serikali haina hela.. Hapo je???

Deni la imf & world bank zaidi ya usd$200 bilion je hilo halina haraka??

Hivi ccm wanapeleka wapi hii nchi..

Niliona jk, makamba, chenge, karamagi, rostam, manji, msabaha ndiyo wajinga tu na wezi wa kutupa.. Kumbe kuna wajinga wengine ambao wamevua utu wao kwa ajili ya kukumbatia ajira kwani wangezikataa hizo ajira ingekuaje?? Mfano pinda, makufuli, tibaijuka, sitta na mwakyembe.. Watoke huko haraka kabla ule msemo wa samaki mmoja akioza wote wameoza...

Siku tukiwa na serikali makini.. Sijui hawa wataenda wapi..
 
.[/FONT]

3. UCHAGUZI WA MEYA MANISPAA YA ARUSHA
Kwa kuzingatia kwamba umekuwepo upotoshaji mkubwa kuhusu uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Arusha, na hata kusababisha malalamiko mengi na vurugu, Kamati Kuu inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:-

Kwanza:
· Matokeo ya Udiwani Manispaa ya Arusha yalikuwa ifuatavyo: Madiwani wa Kata: CCM 10, CHADEMA 8 na TLP 1 – Jumla viti 19.
· Madiwani Viti Maalum: CCM 3, CHADEMA 3.
· Wabunge Viti Maalum: CCM 3, CHADEMA 3.

Matokeo ya jumla: CCM – Viti 16, CHADEMA 14 na TLP 1. Jumla Viti 31.

Pili:

Siku ya kupiga kura (tarehe 18/12/2010) Mkutano ulipoanza wajumbe 14 wa CHADEMA hawakuwepo. Waliofika ni wajumbe 16 wa CCM na 1 wa TLP, jumla wajumbe 17 ambao ni zaidi ya nusu ya wajumbe wanaotakiwa ili mkutano uwe halali kwa mujibu wa sheria.

Katika mazingira haya Msimamizi wa Uchaguzi aliendesha uchaguzi ambapo Ndugu Gaudence Vicent Lyimo wa CCM alipata kura 17, hivyo kutangazwa mshindi halali wa kiti cha Umeya na Ndugu Michael Kivuyo wa TLP alipata kura 17 na kutangazwa mshindi halali wa kiti cha Naibu Meya.

Kwa hiyo wanaosema uchaguzi huo haukuwa halali ama hawajui sheria au wanajiingiza tu katika ushabiki wa kisiasa.


Tatu:

CHADEMA wanadai katika wale wajumbe 16 wa CCM, mmoja wao (Mhe. Mary Chatanda) hakuwa mjumbe halali kwa kuwa katika kugombea Ubunge wa Viti Maalum aligombea kupitia Mkoa wa Tanga.

CHADEMA, kupitia Msimamizi wa Uchaguzi waliomba ufafanuzi wa kisheria kutoka Tume ya Uchaguzi, Katibu wa Bunge na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu. Ofisi zote hizo tatu zilitoa jibu kwamba Mhe. Mary Chatanda alikuwa mjumbe halali wa kikao hicho, na kwamba Wabunge Viti Maalum ni Wabunge wa Kitaifa na vyama vyao ndivyo vinawapangia Halmashauri za kufanyia kazi. Mhe. Mary Chatanda anaishi Arusha akifanyakazi kama Katibu wa CCM wa Mkoa huo hivyo CCM ilimpangia hapo hapo Arusha ndipo afanyie kazi za Halmashauri kama Diwani na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa iliarifiwa kuhusu uamuzi huu kama sheria inavyotaka.

Ni ufafanuzi huo huo ndio CHADEMA waliutumia kushinda kiti cha Halmashauri ya Hai baada ya kuwapangia kufanyakazi katika Halmashauri hiyo Wabunge 2 wa Viti Maalum na ambao si wakaazi wa Wilaya hiyo. Kura hizo mbili ndizo ziliwapa CHADEMA ushindi; na CCM tumekubali matokeo kwa kuwa kwa kufanya hivyo CHADEMA hawakuvunja sheria.

Uhalali wa Mhe. Mary Chatanda kupiga kura Manispaa ya Arusha ni sawa sawa na uhalali wa Wabunge wawili wa Viti Maalum wa CHADEMA walivyopiga kura Hai.

Jambo hili CHADEMA wanalijua vizuri lakini wanapotosha umma kwa makusudi wakitumia vyombo vya habari ambavyo bila kufanya utafiti navyo vimekuwa vinashabikia suala hili.

Kwa kifupi Kamati Kuu inasisitiza kwamba Uchaguzi wa Meya wa Arusha ulifuata sheria kwa ukamilifu, na washindi walishinda kihalali na hakuna sababu ya kurudia kufanya uchaguzi mwingine. Iwapo kuna watu hawaridhiki na mchakato wa uchaguzi huo wanayo nafasi ya kupinga katika vyombo vya sheria bila ya kufanya fujo wala kuleta uvunjifu wa amani kama ule uliotokea tarehe 5/1/2011 kule Arusha.


Huu ni mtihani kwa Chadema kudhibitisha kuwa ni chama chenye vision, makini na kisichokurupuka katika mipango na maamuzi yake,

Endapo hakitachukua action yoyote itakayowawezesha kufanikisha lengo la maandamano ya January 5 na hivyo Meya wa CCM kuendelea na madaraka hayo au kuamua sasa kwenda mahakamani kitaonyesha udhaifu mkubwa wa fikra kama chama kinachopaswa kuwa tayari kuongoza taifa hili.
 
yani CCM ktk matatizo ya nchi walichoona cha maana ni DOWANS peke yake au kwakua inagusa maslahi yao?mfumuko wa bei wao wanaona sii tatizo?kukosekana kwa umeme na nishati zingine si tatizo?hali mbaya za huduma za afya na maji sasa si tatizo?ubadhirifu na ufisadi ktk miradi mbali mbali ya serikali eg pesa wa hisani wa sweden wanazotaka warejeshewe ktk wizara ya misitu.badala ya kutueleza bei ya dhahabu kupanda soko la dunia watanzania tunafaida gani ktk kipato?yapo mengi sana inatia uchungu kwa kweli
 
JF Great thinkers vipi tena? CC ya CCM wamekuja na hoja na utetezi mzito wenye nguvu! nyinyi mnabaki kuponda picha zao na ukumbi waliofanyia kikao chao! sasa huu sio uungwana! kama mna hoja tofauti na wao toeni hapa tuzione wacheni kutuyumbisha na kupost upuuzi kila wakati! mnatupotezea muda hapa kuzisoma post za kipuuzi zisizo na source wala logic!
 
Mbona hawakujadili jinsi watakavyotekeleza zile ahadi za JK wakati wa kampeni? Katiba? Hali ya uchumi wa nchi? Huduma za jamii zilizodorora?

Hicho kikao utadhani cha Democratic Party, yaani chama kisicho madarakani na kilichofutika kwenye ramani ya siasa.
 
Bila bias kidogo wamejieleza kwa busara na kufafanua mambo bila jazba....Wale vijana wa ccm jana waliniudhi sana.
Utadhani walitoka chooni!!!!

Ila hii kamati kuu bado hawajaonyesha nia ya kuwakomboa wananchi na mzigo wa umeme uliopo....
Hawa tatizo kubwa wanakosa washauri wa kuwaambia wananchi wanataka nini!!!!
Kama wangemaliza tatizo la mgawo wa umeme na ku maintain garama za umeme na gas nadhani wananchi wasingelalamika wala kuona tatizo la kuheshimu hukumu ya mahakama ya kimataifa ya biashara..
Sasa kuna haja gani ya kutumia hela zetu kulipa wezi ambao mpaka sasa umeme hatuna na garama zinapanda kila siku??
Hili ndilo litakalosababisha maandamano nchi nzima.
 
UVCCM na CC, hawapingani! They are all singing the same language only differring in dialect and sentence formation!
 
kwani ccm ndio waamuzi wa kura zirudiwe au la? Wao ni ccm na ni wapinzani wa Cdm . Ngoja tuone huyo Meya atafanyaje kazi
 
Kwa maamuzi haya ya CCM kujilipa bilioni 94 tupende tusipende, kama walivyojitangazia nia yao, inatosha!!!!!!
 
Bila bias kidogo wamejieleza kwa busara na kufafanua mambo bila jazba....Wale vijana wa ccm jana waliniudhi sana.
Utadhani walitoka chooni!!!!

Ila hii kamati kuu bado hawajaonyesha nia ya kuwakomboa wananchi na mzigo wa umeme uliopo....
Hawa tatizo kubwa wanakosa washauri wa kuwaambia wananchi wanataka nini!!!!
Kama wangemaliza tatizo la mgawo wa umeme na ku maintain garama za umeme na gas nadhani wananchi wasingelalamika wala kuona tatizo la kuheshimu hukumu ya mahakama ya kimataifa ya biashara..
Sasa kuna haja gani ya kutumia hela zetu kulipa wezi ambao mpaka sasa umeme hatuna na garama zinapanda kila siku??
Hili ndilo litakalosababisha maandamano nchi nzima.

Ukiangalia umri wa wajumbe wa CC utagundua kwamba hawajui JF wala hata FB. Wanategemea zaidi taarifa eanazopewa na wasaidizi wao. Kutokana na umri na kwamba wao hawana shida, hawawezi kuelewa. Hivyo usishangae, hicho walichoweza kujadili nakuambia wametumia akili na nguvu zao zote. Ukidai zaidi, unawaonea!
 
Back
Top Bottom