Tamko la Kamati Kuu ya CCM kuhusu DOWANS na hali ya kisiasa nchini

Sorry wana jf, Kwenye mistari ya hili tamko sijaona karipio la udini! Au kw CC ya ccm hii antagonism ya viongozi wa dini is not a big deal but an important propagandistic weaponry aspect?
 
hili la kufanyia mikutano ya chama ikulu ni sawa na matumizi ya magari ya serikali wakati wa kampeni yaliyokemewa na msajili wa vyama vya siasa. nadhani sasa ni wakai mzuri wa kumwomba mh. tendwa akemee na hili pia.

halafu nimeona wameitisha maandamano ya mshikamano na mikutano ya hadhara nchi nzima kuwashukuru wanachi kwa kukipigia kura chama. mikutano ya namna hiyo na maandamanano ya vyama vya upinzani yamepigwa marufuku mara kadhaa na jeshi la polisi likiwamo tukio la arusha la hivi karibuni kutokana na taarifa za kiintelijensia kuwa kuna dalili za uvunjifu wa amani. hivi haya ya ccm hakuna taarifa za kiintelijensia kama hizo? afande mwema yuko wapi afafanue hapa please.

ama kweli kutawala wanachi wapole kama watanzania raha sana!

nilitegemea kabisa kukutana na haya mambo yao, na cha ajabu ni wenyewe kujipangia maandamano, sasa nione jeshi hili la tz-ccm, tuone kama litawazuia. niliwahi kuandika hapa JF kwamba maandamano ya ccm yanaruhusiwa na kuonekana mazuri lakini ya wapinzani wanayaona ya kuhatarisha amani na mali zao, yani wana boa hawaaaaa
 
Mwakyembe na Sitta, mnaisemeaje hiyo CC yenu? Mlikuwepo kwny mkutano huo?
Mtaonekana serious only kama mtachukua hatua baada ya tamko hilo! Nyie ni watu wazima, najua mtatumia vizuri busaRa zenu...na Tanzania itawaelewa vizuri zaidi hoja zenu, MTAKUWA MASHUJAA.
Tofauti na hivyo, i will have to revisit my outlook on you brodas!
 
JF Great thinkers vipi tena? CC ya CCM wamekuja na hoja na utetezi mzito wenye nguvu! nyinyi mnabaki kuponda picha zao na ukumbi waliofanyia kikao chao! sasa huu sio uungwana! kama mna hoja tofauti na wao toeni hapa tuzione wacheni kutuyumbisha na kupost upuuzi kila wakati! mnatupotezea muda hapa kuzisoma post za kipuuzi zisizo na source wala logic!

Wamebariki malipo kwa Dowans tayari. Je, mle ndani ya Dowans, Watanzania tunamlipa nani na kwa TIJA GANI TULIOPATA WAKATI HADI SASA TUKO GIZANI?

Ndugu Tanzania Kwanza, tunamlipa nani na kwa maslahi yepi. Maslahi ya Taifa (Umma wa Tanzani) kwanza, bila hivyo hakuna kutaniana zaidi.
 
Sorry wana jf, Kwenye mistari ya hili tamko sijaona karipio la udini! Au kw CC ya ccm hii antagonism ya viongozi wa dini is not a big deal but an important propagandistic weaponry aspect?

inashangaza hata mwenyekiti wa chama hakuwakumbusha hili.
 
Aliyeandika hiyo taarifa amesahau jambo: CC imelaani jitihada za dr Slaa kufanya hii nchi isitawalike!
 
Ipo hadithi ninayoipenda kusoma kwa kuirudia rudia sana ndani ya biblia,ambayo ilihusu watoto wawili wa Isaka, yaani Esau na Jacob.Esau aliiuza Ile baraka ya mzaliwa wa kwanza kwa mdogo wake Jacob kwa bakuli la dengu. Na jinsi maneno yanavyoumba, wakati baba mtu anataka kutoa baraka ile ambayo alimuandalia Esau, Jacob aliiba kitu kilichomuuzi sana Esau mpaka akafikia hatua ya kutaka kumuua mdogo wake Jacob.
Pamoja na mema yote ambayo CCM imefanya kwa miongo kadhaa, miaka michache iliyopita, kwa ridhaa yao wenyewe, kama alivyofanya Esau, wameamua kuuza mbaraka wa mzaliwa wa kwanza kwa bakuli la dengu. Chonde chonde msije kukurupuka na kutafuta mchawi na kusahau kuwa mmeamua kuiuza baraka kwa tamaa ya mali na madaraka bila kujari matakwa ya wananchi.
 
Sorry wana jf, Kwenye mistari ya hili tamko sijaona karipio la udini! Au kw CC ya ccm hii antagonism ya viongozi wa dini is not a big deal but an important propagandistic weaponry aspect?

inashangaza hata mwenyekiti wa chama hakuwakumbusha hili.
 
Ipo hadithi ninayoipenda kusoma kwa kuirudia rudia sana ndani ya biblia,ambayo ilihusu watoto wawili wa Isaka, yaani Esau na Jacob.

Esau aliiuza Ile baraka ya mzaliwa wa kwanza kwa mdogo wake Jacob kwa bakuli la dengu. Na jinsi maneno yanavyoumba, wakati baba mtu anataka kutoa baraka ile ambayo alimuandalia Esau, Jacob aliiba kitu kilichomuuzi sana Esau mpaka akafikia hatua ya kutaka kumuua mdogo wake Jacob.

Pamoja na mema yote ambayo CCM imefanya kwa miongo kadhaa, miaka michache iliyopita, kwa ridhaa yao wenyewe, kama alivyofanya Esau, wameamua kuuza mbaraka wa mzaliwa wa kwanza kwa bakuli la dengu.

Chonde chonde msije kukurupuka na kutafuta mchawi na kusahau kuwa mmeamua kuiuza baraka kwa tamaa ya mali na madaraka bila kujari matakwa ya wananchi.
Mle ndani watakaokuwa wamekuelewa mle japo kidogo ni Mzee Makamba peke yake ambaye ndio mara moja moja hugusa Biblia na kuchagua japo kimstari panapo haja.
 
JF Great thinkers vipi tena? CC ya CCM wamekuja na hoja na utetezi mzito wenye nguvu! nyinyi mnabaki kuponda picha zao na ukumbi waliofanyia kikao chao! sasa huu sio uungwana! kama mna hoja tofauti na wao toeni hapa tuzione wacheni kutuyumbisha na kupost upuuzi kila wakati! mnatupotezea muda hapa kuzisoma post za kipuuzi zisizo na source wala logic!
Kuona jambo ambalo limekiukwa na kulinyamazia ndiko kunakopelekea mambo mengi yaende shaghalabagala nchini mwetu. Kuanzia kwenye ukiukaji wa sheria mabarabarani, ujenzi holela wa makazi na viwanda, na hata kuingia mikataba kama hii ya Dowans kwa kutokuwa makini kwa yale yaliyoandikwa kwenye mikataba hiyo.

Wewe unafikiri Clinton asingetomasana na Lewinsky ndani ya White house kesi ingelikuwa kubwa kiasi hicho?! Leo CC ya CCM ndani ya Ikulu, kesho tafrija ya CC ya CUF, na miaka 6 ijayo tunajikuta Dr. Slaa au Zitto wakifanya birthday zao kwenye ukumbi huo. Tusipokemea haya leo, polepole maadili yanazidi kutoweka au mpaka wapinzani waingie Ikulu?!

Heshima ni heshima tu, majumbani na hata maofisini. Huwezi kumruhu mtoto wako wa kiume akamleta demu wake na kufanya mapenzi kwenye kitanda chako hata kama una afiki mahusiano baina yao. Lakini kama huzingatii maadili ya kifamilia na pahala pa kazi, hili laweza lisiwe na maana kwako, everything goes, anywhere any time!! Shaghalabagala!!
 
CCM kuona ni BORA kututangazia kubariki kulapa kampuni ya KITAPELI Dowans kuliko KUKEMEA UDINI NCHINI sasa ni kithibitisho tosha kwamba ni hii ni sera rasmi ya chama hiki.

Hata chombo chao cha UVCCM nao hawakuliona kabisa hili. Tunasema ujanja wa kutugawa kwa misingi ya kidini ili ndio CCM na Rostam Aziz wakajilipe mgongoni mwetu, haikubaliki!!!
 
Mbona hawakujadili jinsi watakavyotekeleza zile ahadi za JK wakati wa kampeni? Katiba? Hali ya uchumi wa nchi? Huduma za jamii zilizodorora?

Hicho kikao utadhani cha Democratic Party, yaani chama kisicho madarakani na kilichofutika kwenye ramani ya siasa.

Sidhani kama huo ndiyo ulikuwa umuhimu wa kikao hiki cha juu kabisa katika CCM, na kikao cha kwanza kwa mwaka mpya 2011.

Mara nyingi umuhimu wa tamko au waraka wo wote, unaonekana kwa kiasi gani muda au nafasi imetumika kujadili hilo suala. Ukiangalia na kuchambua tamko hili la CCM CC, utaona kuwa kwa mpangilio, wametumia:

Maneno 472 kuzungumzia Chadema na u-Meya Arusha
Maneno 193 kuzungumzia Sherehe za CCM
Maneno 171 kuzungumzia vurugu na vifo vya Arusha
Maneno 115 kuzungumzia umoja wa vyama vya ukombozi
Maneno 104 kuzungumzia malipo ya Dowans (bila kutaja tatizo la umeme nchini)
Maneno 100 kuzungumzia semina ya wabunge wa CCM. (Agizo kwa wabunge lilitolewa siku 3 KABLA ya kamati Kuu kukaa)
Maneno 65 kuzungumzia migomo/mitafaruku vyuoni.

Nini ambavyo havikuzungumziwa wala kutajwa hata neno moja:
Utekelezaji wa ahadi za JK na CCM kwa mwaka 2011 na miaka ijayo
Katiba
Uchumi wa nchi
Elimu
Afya
Barabara, Reli, Umeme na Miundombinu yote
Usalama wa Raia na Nchi.
 
Hawa jamaa wanafikiria vizuri kweli? Tanesco ni shirika la umma na serikali ndio inalisimamia.Haya mambo ya kusema ni makosa ya Tanesco yametokea wapi? Nani aliwachagua Rex attorneys kuwawakilisha Tanesco kama mawakili? Usanii mwingine bwana.
 
Kitendo cha kamati kuu ya chama tawala kuacha kutoa maelekezo ya kuwajibisha wale wote waliosababisha taifa liingie hasara hiyo ni ushahidi tosha kuwa sakata hilo lina mkono wa chama hicho; maana haingii akilini mtu anavyoweza kuvuja mkataba miezi mitatu tu kabla ya mkataba husika haujamaliza mda wake, na kitendo hicho kikasababisha harara ya mamia ya bilioni ya fedha, lakina mamlaka husika ikakaa kimya.
 
Inaonekana CCM wana kiburi sana, hizi taarifa wapeane kwenye chama chao. Wananchi wa Tanzania wanategemea Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa tamko kuhusu Vurugu za Arusha , malipo kwa Dowans nk. mambo yao ya kichama wapeane huko huko kwao. Serikali inafanya makosa kwa kutegemea Wanaharakati kufanya kazi ambayo wametumwa na wananchi, hivi wanafahamu maana ya Serikali kweli au ni kanyaga twende tu?
CCM is a dying horse. There's nothing good that can be expected from these guys and their demise is imminent. Time will tell
 
Kiungani, yaani huo mkutano ni Kama marafiki fulani wamekutana baa bila kuwa walikuwa na mihadi, mazungumzo yakaanza bila muongizo. Am trying to say they did not have anything to deliver.

Au, pengine kilikuwa ni kikao kwa mujibu wa ratiba, yaani wamelazimika kukutana tu ingawa hawakuwa na la maana la kujadili.
 
Back
Top Bottom