Tahadhari: Mbinu mpya wizi wa pesa vijana wanaosajili laini za simu

Candela

JF-Expert Member
Aug 12, 2021
638
1,686
Kama unasoma uzi huu basi u buheri, pole kwa wenye changamoto.

Hawa vijana wanaosajili laini za simu mitaani wamekuja na mbinu mpya kukuibia pesa.

Wanatumia app za kampuni husika, TIGO PESA APP AU MPESA APP n.k. Wanawahadaa wateja kuwaunga 5G wapate intaneti yenye kasi bure kama ofa.

Ukikubali anakwambia utoe laini uweke kwenye smartphone yake aiwezeshe, hapo anaunga namba yako na App kwenye simu yake.(Hizi app huwezi kuunga kama laini haipo kwenye simu).

Atakwambia uweke namba ya siri na anakuwa ameweka namna ya kurekodi screen touches so akitoka hapo namba yako ya siri anaijua.

Akimaliza anakupa laini yako anasepa, so anabaki na App akiwa na uwezo wa ku access akaunti yako ya TIGOPESA ama MPESA n.k.

Wamempiga mtu hapa 46,000 wakakopa na nivushe, ye anashangaa anaona meseji za TIGOPESA tu anakamilisha miamala.

Kuweni makini jamani, pia muelewe 5G ni hardware sio kitu cha kuwekewa kama kifaa chako hakina 5G support usidanganyike. Kama laini yako haina 5G basi nenda kabadilishe laini.

NINI CHA KUFANYA KAMA HILI LIMESHAKUKUTA.
Download App husika kwa mtandao wako(kama tayari ipo ifute u dowload upya), jisajili katika hiyo huduma then ukiwa ndani ya app nenda kwenye sehemu ya Vifaa vyangu(jihudumie/Settings), ukikuta zaidi ya kifaa kimoja futa usichokitambua.

Nawasilisha.
 
Kama unasoma uzi huu basi u buheri, pole kwa wenye changamoto.

Hawa vijana wanaosajili laini za simu mitaani wamekuja na mbinu mpya kukuibia pesa.

Wanatumia app za kampuni husika, TIGO PESA APP AU MPESA APP n.k. Wanawahadaa wateja kuwaunga 5G wapate intaneti yenye kasi bure kama ofa.

Ukikubali anakwambia utoe laini uweke kwenye smartphone yake aiwezeshe, hapo anaunga namba yako na App kwenye simu yake.(Hizi app huwezi kuunga kama laini haipo kwenye simu).

Atakwambia uweke namba ya siri na anakuwa ameweka namna ya kurekodi screen touches so akitoka hapo namba yako ya siri anaijua.

Akimaliza anakupa laini yako anasepa, so anabaki na App akiwa na uwezo wa ku access akaunti yako ya TIGOPESA ama MPESA n.k.

Wamempiga mtu hapa 46,000 wakakopa na nivushe, ye anashangaa anaona meseji za TIGOPESA tu anakamilisha miamala.

Kuweni makini jamani, pia muelewe 5G ni hardware sio kitu cha kuwekewa kama kifaa chako hakina 5G support usidanganyike. Kama laini yako haina 5G basi nenda kabadilishe laini.

NINI CHA KUFANYA KAMA HILI LIMESHAKUKUTA.
Download App husika kwa mtandao wako(kama tayari ipo ifute u dowload upya), jisajili katika hiyo huduma then ukiwa ndani ya app nenda kwenye sehemu ya Vifaa vyangu(jihudumie/Settings), ukikuta zaidi ya kifaa kimoja futa usichokitambua.

Nawasilisha.
Very nice
 
Sema sisi wabishi sana ndio maana tunapigwa, kila siku kampuni za simu na police wanasema kupitia sms kuwa hupaswi kufanya hivi lkn hatuelewi.

Sio wabishi mkuu ni wajinga pia...

Ni jambo la kawaida sana kumsikia mtu akisema, "mimi mambo ya simu huwa sijisumbui hata kuyajua, huwa nawaachi tu wanisaidie kuset"...

Na ndio maana hawakukosea waliosema "mjinga huliwa na mwerevu".
 
Jamaa anaona tu miamala asiyoitambua inakamilika
Yap, ukifanya muamala kwenye App unapokea meseji kawaida, afu jamaa kila mda walikuwa wanaangalia salio maana ana meseji za kuangalia salio kwa App kama zote, anasema alikuwa anashangaa akajua kuna shida kwenye mtandao, kuna mtu akamtumia pesa ndio jamaa wakaanzia hapo kumkomba ndio akaja kutaka kujua hela yake imeendaje.
 
Ajira hakuna maisha magumu na njaa zinauma watu wanajiongeza.
 
Sio wabishi mkuu ni wajinga pia...

Ni jambo la kawaida sana kumsikia mtu akisema, "mimi mambo ya simu huwa sijisumbui hqta kuyajua, huwa nawaachi tu wanisaidie kuset"...

Na ndio maana hawakukosea waliosema "mjinga huliwa na mwerevu".

Watanzania wengi kutafuta maarifa madogo madogo ni wavivu sana..

Mtu ana simu kali ila hajui hata offline mode ni kitu gani?
 
wakuu kubadili laini kuwa 5g yenye kasi namba ya siri inahusikaje hapo?.

yani uyo tapeli anakwambia uweke namba ya siri ili kupata au kuona nini?
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Back
Top Bottom