Taarifa rasmi ya kusitisha mgomo kutoka chama cha madaktari 10/03/2012

Mimi sikuunga mkono mgomo wa kwanza wa madaktari na de facto na huu wa pili sikuunga mkono. Ila kuna kitu kimenishangaza zaidi kwenye huu mgomo wa pili: hivi nani aliwashauri madaktari wampe ultimatum mtu ambaye hawajawahi kukaa naye mezani kwenye majidiliano? Mimi nilitegemea madaktari kwanza wangeomba kukutana na Rais wamweleza kumkataa kwao waziri na naibu wake face to face, then kutokana na responce yake ndio wangekuja na reaction. Sasa wao wamereact mahali ambapo hakukuwa na action! Utampaje Rais taarifa ya kutaka atengue uteuzi wake kwa kupitia vyommbo vya habari? Je, viongozi wa mgomo walimuandikia Rais barua ya kumtaka afukuze kazi mawaziri? Rais hafanyi kazi kwa kutumiaa vyombo vya habari. Mimi nadhani madaktari wakubali tu kuwa hawakupata ushauri unaotosheleza kujenga hoja madhubuti na kwamba utatuzi wa kweli utapatikana iwapo watajikaza "kiume" na kufuatilia madai yao hatua kwa hatua, haya mambo ya ultimatum no no no...
 
Hana lolote jk,naskia madokta wamempa hadi tar 9 april awe amewa_fire mponda na nkya la sivyo wataULIMBOKA tena
 
Mimi sikuunga mkono mgomo wa kwanza wa madaktari na de facto na huu wa pili sikuunga mkono. Ila kuna kitu kimenishangaza zaidi kwenye huu mgomo wa pili: hivi nani aliwashauri madaktari wampe ultimatum mtu ambaye hawajawahi kukaa naye mezani kwenye majidiliano? Mimi nilitegemea madaktari kwanza wangeomba kukutana na Rais wamweleza kumkataa kwao waziri na naibu wake face to face, then kutokana na responce yake ndio wangekuja na reaction. Sasa wao wamereact mahali ambapo hakukuwa na action! Utampaje Rais taarifa ya kutaka atengue uteuzi wake kwa kupitia vyommbo vya habari? Je, viongozi wa mgomo walimuandikia Rais barua ya kumtaka afukuze kazi mawaziri? Rais hafanyi kazi kwa kutumiaa vyombo vya habari. Mim
i nadhani madaktari wakubali tu kuwa hawakupata ushauri unaotosheleza kujenga hoja madhubuti na kwamba utatuzi wa kweli utapatikana iwapo watajikaza "kiume" na kufuatilia madai yao hatua kwa hatua, haya mambo ya ultimatum no no no...

Ina maana hamna mawasiliano kati wa waziri mkuu na rais? Je Pinda alivyosema kuwa atamshauri rais ina maana alidanganya na huenda hawa watu hawaongei na wana mabifu kati yao ( tumeshuhudia huyu akisema hivi, mwingine anakanusha).
 
Tanzania ni taifa la ahadi na si taifa la mfumo. Ukweli wa maslahi ya madaktari hauwezi kupatikana katika kauli za JK wala Pinda utapatikana pale tu tutakapokuwa na taasisi huru ya kupanga mishahara ya watumishi na si vile waziri na watu wake wanavyoamua wizarani na kupanga maslahi kidogo kwa watu muhimu kama madaktari. Jambo moja juu ya mishahara linalotufanya nchi zetu zisiendelee ni kwa vile mishahara haipangwi kwa haki. Duniani kote mishahara ni 'function' ya muda mtu aliokaa darasani, hatari ya kazi anayoifanya, umuhimu wa kazi na masaa ya kazi. Lakini kwetu eti ni 'function' ya wanasiasa!!! Afrika tubadilike tusitafute mchawi wa maendeleo mahala pengine ila tukubali ukweli wa tafiti za kisayansi tutaweza kuendelea, la sivyo hakuna lolote ni udwanzi mtupu hata ahadi ya JK kwa madaktari inaweza kuisha na JK hiyo 2015 kama atafika maana anaonekana kuchoka kimawanzo na uso wake kupauka pauka.
 
sasa hapo ndo mmekosea, next time mkisema mmegoma hakuna mtu atakaye wasupport,

With or without support, they will strike if need be.
Be it legal or illegal, it's the least of their worries.
 
Pamoja na obovu wote wa JK
Lakini JK anakitu kimoja very unique....... ushawishi mnapokutana naye uso kwa uso.
He never failed in this

Hongera JK hongera Drs

Ila weakness yake kubwa ni kuogopa kukutana na watu uso kwa uso na kukimbilia kutumia wazee wa CCM wa Dar ili kufikisha mipasho. Kama JK kweli anataka kupata heshima kama rais aliyewahi kuitawala Tanzania kwa umahili basi washauri wake wa sasa awabadili. Maana wanamletea habari za uongo na yeye kujikuta anapata jazba ya kukimbilia mipasho na vitisho. Alicho kifanya kwa madaktari ndicho hasa ambacho Rais wa nchi katika wakati huu anatakiwa kukifanya kwa hili ninampongeza rais wa nchi yangu.

Suala la madaktari lilikuwa ni suala sensitive sana kama angekuwa na washauri bora tokea mwanzo. Maana afya ni national security issue. Ukiwalazimisha kurudi kwa vitisho wanaweza kwenye kuchoma watu sindano za maambukizi badala ya za kutibu (Japo ninaamini madaktari ni wazalendo na hawawezi kufikia hatua hivyo labda wawe provoked na kupoteza reasoning-kitu ambacho hasa kingetokea kama wangeburuzwa kwa nguvu za dola na mipasho na vitisho kurudi kazini).

Uongozi ni ushawishi na JK anao ila anashindwa kuutumia kwa manufaa yake kwa kuhofia kuonekana weak-president kwa mujibu wa washauri wake. Ikulu ikibadilishwa kuwa nyumba iliyo wazi kwa watanzania wenye malalamiko yao ya msingi badala ya ile dhana iliyozoeleka kuwa Ikulu ni sehemu ya kutembelewa na wateule wachache na kufanya hivyo kwa watu wengine ni 'KUTAFUTA PHOTO OPPORTUNITY NA RAIS' - BY MKAPA BENJAMINI, ni dhana potovu kabisa.
 
Yetu macho na masikio kuona na kusikia huo utekelezaji maana demand zenu ziko open. Hongera kwa kufikia maelewano na huduma kuanza kutolewa tena kwenye hospitals zetu
 
RIPOTI KWA VYOMBO VYA HABARI.

UTANGULIZI
Baada ya kikao cha madaktari kilichofanyika leo tarehe 10/3/2012. Madaktari nchini kupitia chama cha madaktari Tanzania (MAT), tunapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:

... 1. Jamii ielewe kuwa daktari kama binadamu mwingine anayefanya kazi Tanzania ana mahitaji muhimu (basic needs) na mahitaji ya kijamii (social responsibility) na hivyo si chombo cha kufanyia kazi (Machine).

2. Pia Daktari ana haki ya kupata ujira unaomfaa kutokana na kazi anayofanya na ana haki ya kuacha kazi muda wowote iwapo ataona kazi hiyo ya udaktari haimpi ujira wa kutosha na heshima ya kuendesha maisha yake.

3. Pia jamii itambue kuwa daktari anaweza kulazimishwa kurudi kazini lakini hawezi kulazimishwa kufanya kazi. Matokeo ya kulazimishwa yanaweza yasiwe mazuri kwa wale watakao hudumiwa.

4. Jamii itambue kuwa madai na hoja kuu za madaktari ni kwa ajili ya faida ya Watanzania wote,yakiwemo mazingira bora ya kufanya kazi mjini na vijijini, na kuboresha afya za watanzania kwa ujumla. Pia vifaa na dawa ziwepo mahospitalini zinakohitajika.

5. Pia tunawashukuru madaktari wote kwa mshikamano wetu tulioonyesha na tunaomba mshikamano huu uendelee daima.

TAMKO LETU:

JANA TAREHE 9/3/2012, TULIKUTANA NA MH. RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE. TULIMWELEZA HOJA ZETU, AMBAZO ALIZIELEWA NA ALIAHIDI KUZISHUGHULIKIA KIKAMILIFU. TUNA IMANI SANA NA MH. RAIS KWAMBA HATATUANGUSHA.

KUTOKANA NA HILO, TUNAPENDA KUUTANGAZIA UMMA WA WATANZANIA KUWA TUNARUDI KAZINI RASMI KUANZIA LEO TAREHE 10/3/2012, WAKATI MHESHIMIWA RAIS AKISHUGHULIKIA MADAI YETU.

PIA WAKATI MADAI YETU YAKISHUGHUKLIKIWA TUNAPENDA KUSEMA KUWA HATUNA IMANI NA WAZIRI WA AFYA MH. DR. HAJI MPONDA NA MH. DR. LUCY NKYA, NA KUWA TUNAMSIMAMISHA RASMI UANACHAMA WA MAT MH. DR. LUCY NKYA.

MADAKTARI TUNATAMKA WAZI KUWA WAZIRI WA AFYA DR. HAJI MPONDA NA NAIBU WAKE DR. LUCY NKYA NI MAADUI WA MADAKTARI NA SEKTA YA AFYA KWA UJUMLA HAPA NCHINI NA TUNAAHIDI KUTOKUWAPA USHIRIKIANAO WA AINA YOYOTE WA KIBINAFSI AU WA KIUTENDAJI.

SOLIDARITY FOREVER.
RAIS(MAT)

nAONGEZEA KIDOGO HAPA (NI MTAZAMO WANGU)

  1. PIA MADAKTARI KAMA WATAALAM WALIOSOMEA FANI ZINGINE MFANO ENGINEERS,WANASHERIA WALIMU NK WAMESOMESHWA NA SERIKALI KWA RUZUKU KWANI MADAKTARI PIA NAO NI WADAIWA WA LOAN BOARD KAMA WALIVYO HAWA WATALAAM WA FANI ZINGINE TENA UKIFUATILIA UTAGUNDUA KUWA MADENI YA MADR NI MAKUBWA ZAIDI YA HATA HAWA WA FANI ZINGINE HIVYO SERIKALI NA JAMII HUSIKA WAACHE UPOTOSHAJI USIOKUWA NA MSINGI
  2. WITO WA KWENYE FANI YA AFYA SI WA MADR TU HATA KIAPO CHA MADR KINAONESHA HILI KUWA SERIKALI NA WANANCHI PIA WANAHUSIKA KATIKA KUDUMISHA KIAPO HICHO, HIVYO UPANDE MMOJA UKIVUNJA KIAPO BASI KINAVUNJIKA RASMI KWA PANDE ZOTE KWANI UDUMISHAJI WAKE UNATEGEMEA PANDE HIZO MUHIMU.
  3. MADAKTARI WALILAZIMISHWA KUGOMA NA SERIKALI KWA SERIKALI KUTAKA KUWAACHIA JUKUMU LA KUTOA HUDUMA YA AFYA BILA YA "KUWEZESHWA " ILI HALI SERIKALI NDIO YENYE JUKUMU LA KUTOA HUDUMA YA AFYA KWA WANANCHI KIKATIBA...
    HIVYO MADAKTARI WANARUDI KAZINI,LAKINI WANANCHI WAELEWE KUWA VITU VINGI MUHIMU VILIVYOKUWA VIKIDAIWA BADO HAVIJATIMIZWA ,ILA NI KWA IMANI KUWA SERIKALI ITAYAPA UZITO STAHILI HAYA MATATIZO NA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA KADIRI IWEZEKANAVYO KWA NIA YA DHATI KWANI MAZINGIRA YA KAZI BADO YATAKUWA NI MAGUMU NA HATARISHI KWA WATUMISHI WA AFYA PIA WAGONJWA WENYEWE.
 
Nakubaliana na wewe ila JK hakuhitaji washauri kuweza kuona "sensitivity" ya issue hii. Mtu yeyote anaweza kuliona hili bila kuambiwa na watu wengine.

nIMEWWAELEZA WENGI SANA HILI AMBAO WALIKUWA WAKIAMINI KUWA ETI JK ALIKUWA ANAPOTOSHWA NA WASAIDIZI WAKE JAMBO AMBALO LINA UKWELI KABISA KWANI HAWA WAPAMBE HAWA WAO KAZI YAO NI KUANDIKA MAZURI TU HII NDIO FALSAFA YA UONGOZI WA BONGO UKIONA KIONGOZI ANAKUJA KWNYE ENEO LAKO LA KAZI KWA ZIARA BASI SIKU HIYO KILA KITU KINAANDALIWA VIZURI ILI JAMAA AKIJA AONE HALI NI NZURI, KAMA NI HOSPITALI HAPO YATATANDIKWA MASHUKA MAPYA
"NASIKIA WAKATI CLINTON ANAKUJA TZ KWA MARA YA KWANZA ARUSHA WALISAFISHA BARABARA NA SABUNI "

LAKINI KWA HILI NAKUBALIANA KUWA-"JK hakuhitaji washauri kuweza kuona "sensitivity" ya issue"


sTORY Ya ukweli
kuna wakati mh mmoja alikuwa anatembelea hospitali flani basi siku hiyo yakatandikwa mashuka mapya toka stoo meupee
sasa manesi walipotandika mashuka wakashangaa wagonjwa wengi hawakulala vitandani mwao
wakawaambia, mbona hamlali vitandani mwenu
wagonjwa wakajibu kuwa, wanaogopa kuyachafua mashuka
manesi wakawajibu kuwa, msijali laleni tu,
alipokuja Mh kutembelea wodi hizo bado kuna mgonjwa mmoja akakutwa amelala chini kisa anaogopa kuchafua mashuka
nafikiri unapata picha jinsi watz walivyonyanyasika hadi wanaona kulalia mashuka masafi hospitalini si haki yao...............
 
Kama ni kudharirika nadhani Pinda anadharirika vya kutosha!, pole sana waziri mkuu, seriously nakuonea huruma, umenyang'anywa uwaziri mkuu ukabakishiwa mshahara tu!
 
Kama ni kudharirika nadhani Pinda anadharirika vya kutosha!, pole sana waziri mkuu, seriously nakuonea huruma, umenyang'anywa uwaziri mkuu ukabakishiwa mshahara tu!

"Kudhalilika" na sio kama ulivyoandika hapo juu.
 
Sun, Mar 11th, 2012




Tanzania |Sun,March 11th 2012


Namala-Mkopi.jpg


MAT president, Dr. Namala Mkopi


Medical doctors on Saturday announced an end to the strike they had called nationwide, one day after an order by the Labour Division of the High Court to do so, which also instructed them to publish the announcement in the national media.

However, the President of the Medical Association of Tanzania (MAT), which called the strike, Dr Namala Mkopi, claimed that the announcement was not in response to the court order but that it resulted from reassuring talks with President Jakaya Kikwete on Friday.

"We have decided to resume work immediately following President Kikwete's reassurance that he is committed to addressing our demands," he maintained.A source in the Attorney General's chambers, whose application to declare the strike illegal and order it ended was granted by High Court Judge Regina Rweyemamu on Thursday, said they are monitoring compliance by the doctors.

"We expect the doctors to comply with the order by Monday, failure of which we would go back to court for further action," said the source.The doctors' announcement on Saturday, which followed a meeting of MAT members at Don Bosco hall in
Dar es Salaam, was unconditional. The doctors had called the strike in order to press for the resignation or sacking of Health Minister, Dr Hadji Mponda and his deputy, Dr Lucy Nkya, a demand that was rejected by the government.


Details of the talks between the doctors and President Kikwete at the State House on Friday were not revealed. But Dr Mkopi confirmed that no conditions or deadlines are attached to their resolve to call off the strike.MAT Secretary General Dr Rodrick Kabangila said that the objective of the strike was not to endanger the lives of Tanzanians but to improve working environment for medical workers.


He maintained that the medics were not ready to work with Dr Mponda and his deputy. The Labour Court has declared the doctors strike illegal and ordered them back to work immediately.The application for the order was filed to the Commission for Mediation and Arbitration (CMA) by the Attorney General, Judge Frederick Werema, in
Dar es Salaam, under a certificate of urgency.


Meanwhile, the Health Ministry said on Saturday that it would monitor service delivery in hospitals following the doctors' decision to return to work. "We are informed that doctors have agreed to resume work, but we will keep a close eye on them countrywide so as to monitor their activities," The Acting Chief Medical Officer (CMO) Dr Donnan Mmbando told the Sunday News.


Earlier, Dr Mmbando said they had arranged for emergency referrals that could not be handled by the Muhimbili National Hospital to be transferred to the Aga Khan, Hindu Mandal , TMJ, CCBRT, IMMTU private hospitals and Lugalo Military Hospital.He said that 67 senior doctors working at the Health Ministry headquarters had been deployed to hospitals to mitigate the impact of the doctors' strike.


By ROSE ATHUMANI, Tanzania Daily News


 
Back
Top Bottom