ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,019
- 7,223
Mimi sikuunga mkono mgomo wa kwanza wa madaktari na de facto na huu wa pili sikuunga mkono. Ila kuna kitu kimenishangaza zaidi kwenye huu mgomo wa pili: hivi nani aliwashauri madaktari wampe ultimatum mtu ambaye hawajawahi kukaa naye mezani kwenye majidiliano? Mimi nilitegemea madaktari kwanza wangeomba kukutana na Rais wamweleza kumkataa kwao waziri na naibu wake face to face, then kutokana na responce yake ndio wangekuja na reaction. Sasa wao wamereact mahali ambapo hakukuwa na action! Utampaje Rais taarifa ya kutaka atengue uteuzi wake kwa kupitia vyommbo vya habari? Je, viongozi wa mgomo walimuandikia Rais barua ya kumtaka afukuze kazi mawaziri? Rais hafanyi kazi kwa kutumiaa vyombo vya habari. Mimi nadhani madaktari wakubali tu kuwa hawakupata ushauri unaotosheleza kujenga hoja madhubuti na kwamba utatuzi wa kweli utapatikana iwapo watajikaza "kiume" na kufuatilia madai yao hatua kwa hatua, haya mambo ya ultimatum no no no...