Pfizer
JF-Expert Member
- Mar 25, 2021
- 304
- 518
Mheshimiwa Rais,
Amani iwe nawe daima.
Mheshimiwa Rais, Awali ya yote tunakupa pole kwa kazi zako za kila siku za kuhudumia Watanzania, huku tukiamini Mwenyezi Mungu anaendelea kukujalia afya tele na tunatambua pia una majukumu mengi kwa ajili ya ustawi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Rais, hii ni sauti ya Umoja wa Madaktari wahitimu watarajali ambao tunaleta kwako waraka huu kwa lengo la kukufikishia ujumbe kutokana na vikwazo vinavyotukabili ambavyo vimetufanya kugeuka ombaomba mtaani licha kwamba sisi ni wasomi madaktari ambao tumeshindwa kujiajiri, kuajirika kutokana na kizingiti kinachoitwa leseni.
Mheshimiwa Rais, tumeamua kuleta waraka huu kwako baada ya juhudi zetu za kupeleka changamoto zetu na hata kuonana na baadhi ya viongozi wa Wizara ya Afya kugonga mwamba.
Mheshimiwa Rais, Tumekuwa kwenye mazoezi ya vitendo (internship) katika hospitali kubwa za rufaa nchini, huko kazi zote na za aina zote tumekuwa tukizifanya sisi na kusimamiwa na madaktari bingwa nchini.Huko tumeokoa maisha ya Watanzania wenzetu wengi, tumejipatia umahiri wa kuhudumia wagonjwa kwa uwezo wa elimu tuliyonayo.
Mheshimiwa Rais, Sisi madaktari wa utarajali tunashangazwa na kuumizwa na utaratibu wa Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) pamoja na Wizara ya Afya, kwa kadhia kubwa wanayotusababishia.
Sisi madaktari watarajali tunaamini Serikali ilikuwa na nia njema ilipoamua kutunga Sheria No.11 ya Mwaka 2017 ambayo ilipitishwa na Bunge letu Tukufu ikitaka kila Mhitimu wa fani ya Udaktari sharti apewe leseni baada ya kufanya mtihani wa MCT.
Mbali na nia hiyo njema ya Serikali, bahati mbaya chombo hiki hakijaweza kujua kifanye kazi ipi na kwa wakati upi ili kiweze kulisaidia taifa lipate madaktari bora na sio bora madaktari.
Mheshimiwa Rais, hatuipingi sheria hiyo isipokuwa utaratibu au kanuni zinazotumika, hususan kuanzishwa kwa mtihani wa ‘pre na post internship. Baraza hili (MCT) limekuwa likiendesha mitihani hiyo kwa hasara, uonevu, ukatili na hujuma kwa madaktari watarajali.
Ikumbukwe kwamba sisi madaktari Watarajali hatupingi kuwapo kwa mitihani hiyo ikizingatiwa tumemaliza vyuo pamoja na kufanya mazoezi kwa vitendo (internship) na kupata ufaulu usiotiliwa shaka.
Tunachokipinga na ambacho kimetufanya kuandika waraka huu kwako Mheshimwa Rais ni haya yafuatayo:
1. Mtihani wa baada ya utarajali (post internship) uliofanyika 22/03/2023 kumekuwa na massive failure kiasi ambacho hadi imesababisha Baraza kutokutoa takwim za waliofeli na waliofaulu ingawa mpaka sasa tupo madaktari zaidi ya 300 ambao matokeo hayakutoka vizuri hivyo kushindwa kupatiwa leseni, hivyo tunaomba mtihani huu usahihishwe upya na matokeo yafanyiwe standardization, na usahihishwe na wasimamizi wa nje ya MCT (external examiners) ili kuondoa hii massive failure kama ilivyotokea matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 mitihani ilisahihishwa upya na ufaulu ukapatikana
2. MCT kutokuzingatia uhalisia wa namna ya kumpata daktari bora
3. MCT kutumia mtihani kwa lengo la kuondosha changamoto za ulevi uliopitiliza kwa baadhi ya madaktari, kuchelewa kazini au kutokufika kazini pamoja na uzembe kazini
4.MCT kutokuzingatia muda wa daktari kumaliza mazoezi kwa vitendo (internship) na kwenda kufanya kazi ili kulihudumia taifa.
5. MCT kutokuzingatia namna sahihi ya kumpima daktari kulingana na huduma zinazotolewa katika hospitali tunazofanyia internship
6. MCT kutokujali na kuheshimu muda jambo linalopelekea daktari kutaka hatari ya kupoteza taaluma yake kwa kusubiri mtihani kwa muda mrefu wakati mwingine kwa miezi takribani 10.
7. MCT kutokuwa wawazi juu ya alama (marks) za ufaulu na uendeshaji mzima wa mtihani na matokeo utakaomfanya mtu ajue amefeli idara ipi hata baada ya kukata rufaa.
8. MCT kutokuheshimu na kuzingatia muda tunaopaswa kumaliza taaluma ya udaktari.
Ushauri na mapendekezo yetu.
1. Yafanyike marekebishio ya sheria ili iweze kuakisi upatiakanaji wa madaktari bora.
2. Wizara ifuatilie mapungufu yaliyopo MCT na itumie dhamana yake kuwawezesha madaktari wapate leseni ili washiriki ujenzi wa taifa lao.
3. Wizara itoe leseni baada ya madaktari kumaliza mazoezi kwa vitendo (internship) na kufaulu vizuri kwa kuzingatia taarifa ya hospitali ambayo daktari amefanya mazoezi kwa vitendo (internship).
4. Tunashauri kusiwepo na mtihani wa leseni, kuwepo na mtihani wa kumpima mwanafunzi kama ana uwezo wa kuwa daktari bora baada ya kumaliza mitihani ya chuo na kabla ya kuapa au kwenda mazoezi kwa vitendo (internship). Hii itapelekea ufaulu mzuri kwa sababu ya mtu kuwa na muda wa kutosha kujiandaa na watakaotakiwa kurudia mtihani warudie kila baada ya miezi miwili katika kituo kimoja ili kuepuka gharama kubwa. Hii itapelekea milango ya hujuma, rushwa, uzalilishaji na uonevu anaoupata daktari wakati wa kusubiri mtihani kutoweka.
5. Mtihani wa kumpima mwanafunzi ili aweze kuwa daktari utungwe kama inavyofanyika vyuoni, mtihami wa kuchagua (multiple choice) wa maswali 100 au 200 pekee hauwezi kuwa kielelezo cha kumpata daktari bora kama ilivyo sasa.
6. Kuwepo na muda rafiki wa kukata rufaa walau kuanzia mwezi mmoja.
7. Kwakuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi wanachama wa Afrika Mashariki (EAC), hivyo tunapendekeza itumie mifumo inayotumiwa pia na nchi wanachama ambapo wahitimu wa udaktari wanapewa mtihani online na kwa muda wowote. Nchi zote wanachama wa EAC zenye utaratibu wa kufanya mitihani ya leseni, mtihani na alama (marks) zake zinajulikana na zipo kwenye website zao isipokuwa Tanzania tu ndiyo alama za ufaulu hazijulikani.
Mheshimiwa Rais, sisi madaktari watarajali tumesoma kuanzia elimu ya msingi hadi vyuo vikuu na kumalizia mwaka mmoja wa mafunzo ya vitendo (internship) na tumefaulu vizuri sana hadi kufikia ngazi ya utabibu, ni nani leo anaweza kusema sisi sio wasomi? Ni nani anayeweza kusema kuwa sisi sio madaktari ili hali tumetibu wagonjwa mwaka mzima na kutunukiwa vyeti vya ufaulu wa alama A ?
Mheshimiwa Rais, ni ukweli kwamba Taifa letu linahitaji madaktari bora, lakini je madaktari bora wanaweza kupatika kupitia maswali 200 ya mtihani wa kuchagua kwa muda wa saa tatu mpaka sita pekee?
Mheshimiwa Rais, kutokana na kadhia ya namna hii huenda Wizara yenye dhamana na afya haiviamini vyuo vyake vilivyopo nchini, hivyo wanaona suluhisho pekee la kupata madaktari bora ni huo mtihani wa saa 3 mpaka sita ambao utaratibu wake umekuwa kikwazo kwa daktari ambaye tayari alikwisha kula kiapo kujiajiri au kuajiriwa katika sekta zote, yaani umma na binafsi.
Mheshimiwa Rais, swali la kujiuliza na lipo kwa Watanzania wengi kama ambavyo walivyoaminishwa na MCT ni hili, Je ni kweli sisi madaktari ni waoga wa mtihani na hatutaki kufanya mtihani wa kujipima wa MCT? Jibu ni hapana!
MCT wanapaswa watoe leseni kwa kila daktari aliyefaulu mazoezi kwa vitendo kwakuwa moja kwa moja ana sifa za kuwa na leseni kwa sababu amekutana na wagonjwa, amewatibu, wamepona na amefanikiwa kuokoa maisha ya watu.
Mheshimiwa Rais, tunasisitiza hatupingi mtihani wa kupata leseni, tunashauri uwepo isipokuwa uende sambamba na mitihani ya kumaliza vyuo na si unaompima daktari baada ya mazoezi kwa vitendo. Utaratibu wa sasa ujulikane ni batili, hivo tunaomba standardization ifanyike na tupatiwe leseni
Mheshimiwa Rais, tunashauri Serikali ipitie upya Sheria ya mitihani ya mwaka 2017 ili kuwepo na utaratibu mzuri usio na malalamiko mengi na kuwepo uwazi wa kutosha.
Aidha tunashauri vyuo vya udakitari viwe chini ya Wizara ya Afya na sio Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) ili waweze kuvisimamia vizuri viweze kutoa wataalam wazuri wa afya.
Tunakushukuru sana.
Kupitia kwako ni matumaini yetu maombi yetu yatapata ufumbuzi wako wewe Rais wetu na Mama yetu mpendwa.
Amani iwe nawe daima.
Mheshimiwa Rais, Awali ya yote tunakupa pole kwa kazi zako za kila siku za kuhudumia Watanzania, huku tukiamini Mwenyezi Mungu anaendelea kukujalia afya tele na tunatambua pia una majukumu mengi kwa ajili ya ustawi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Rais, hii ni sauti ya Umoja wa Madaktari wahitimu watarajali ambao tunaleta kwako waraka huu kwa lengo la kukufikishia ujumbe kutokana na vikwazo vinavyotukabili ambavyo vimetufanya kugeuka ombaomba mtaani licha kwamba sisi ni wasomi madaktari ambao tumeshindwa kujiajiri, kuajirika kutokana na kizingiti kinachoitwa leseni.
Mheshimiwa Rais, tumeamua kuleta waraka huu kwako baada ya juhudi zetu za kupeleka changamoto zetu na hata kuonana na baadhi ya viongozi wa Wizara ya Afya kugonga mwamba.
Mheshimiwa Rais, Tumekuwa kwenye mazoezi ya vitendo (internship) katika hospitali kubwa za rufaa nchini, huko kazi zote na za aina zote tumekuwa tukizifanya sisi na kusimamiwa na madaktari bingwa nchini.Huko tumeokoa maisha ya Watanzania wenzetu wengi, tumejipatia umahiri wa kuhudumia wagonjwa kwa uwezo wa elimu tuliyonayo.
Mheshimiwa Rais, Sisi madaktari wa utarajali tunashangazwa na kuumizwa na utaratibu wa Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT) pamoja na Wizara ya Afya, kwa kadhia kubwa wanayotusababishia.
Sisi madaktari watarajali tunaamini Serikali ilikuwa na nia njema ilipoamua kutunga Sheria No.11 ya Mwaka 2017 ambayo ilipitishwa na Bunge letu Tukufu ikitaka kila Mhitimu wa fani ya Udaktari sharti apewe leseni baada ya kufanya mtihani wa MCT.
Mbali na nia hiyo njema ya Serikali, bahati mbaya chombo hiki hakijaweza kujua kifanye kazi ipi na kwa wakati upi ili kiweze kulisaidia taifa lipate madaktari bora na sio bora madaktari.
Mheshimiwa Rais, hatuipingi sheria hiyo isipokuwa utaratibu au kanuni zinazotumika, hususan kuanzishwa kwa mtihani wa ‘pre na post internship. Baraza hili (MCT) limekuwa likiendesha mitihani hiyo kwa hasara, uonevu, ukatili na hujuma kwa madaktari watarajali.
Ikumbukwe kwamba sisi madaktari Watarajali hatupingi kuwapo kwa mitihani hiyo ikizingatiwa tumemaliza vyuo pamoja na kufanya mazoezi kwa vitendo (internship) na kupata ufaulu usiotiliwa shaka.
Tunachokipinga na ambacho kimetufanya kuandika waraka huu kwako Mheshimwa Rais ni haya yafuatayo:
1. Mtihani wa baada ya utarajali (post internship) uliofanyika 22/03/2023 kumekuwa na massive failure kiasi ambacho hadi imesababisha Baraza kutokutoa takwim za waliofeli na waliofaulu ingawa mpaka sasa tupo madaktari zaidi ya 300 ambao matokeo hayakutoka vizuri hivyo kushindwa kupatiwa leseni, hivyo tunaomba mtihani huu usahihishwe upya na matokeo yafanyiwe standardization, na usahihishwe na wasimamizi wa nje ya MCT (external examiners) ili kuondoa hii massive failure kama ilivyotokea matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 mitihani ilisahihishwa upya na ufaulu ukapatikana
2. MCT kutokuzingatia uhalisia wa namna ya kumpata daktari bora
3. MCT kutumia mtihani kwa lengo la kuondosha changamoto za ulevi uliopitiliza kwa baadhi ya madaktari, kuchelewa kazini au kutokufika kazini pamoja na uzembe kazini
4.MCT kutokuzingatia muda wa daktari kumaliza mazoezi kwa vitendo (internship) na kwenda kufanya kazi ili kulihudumia taifa.
5. MCT kutokuzingatia namna sahihi ya kumpima daktari kulingana na huduma zinazotolewa katika hospitali tunazofanyia internship
6. MCT kutokujali na kuheshimu muda jambo linalopelekea daktari kutaka hatari ya kupoteza taaluma yake kwa kusubiri mtihani kwa muda mrefu wakati mwingine kwa miezi takribani 10.
7. MCT kutokuwa wawazi juu ya alama (marks) za ufaulu na uendeshaji mzima wa mtihani na matokeo utakaomfanya mtu ajue amefeli idara ipi hata baada ya kukata rufaa.
8. MCT kutokuheshimu na kuzingatia muda tunaopaswa kumaliza taaluma ya udaktari.
Ushauri na mapendekezo yetu.
1. Yafanyike marekebishio ya sheria ili iweze kuakisi upatiakanaji wa madaktari bora.
2. Wizara ifuatilie mapungufu yaliyopo MCT na itumie dhamana yake kuwawezesha madaktari wapate leseni ili washiriki ujenzi wa taifa lao.
3. Wizara itoe leseni baada ya madaktari kumaliza mazoezi kwa vitendo (internship) na kufaulu vizuri kwa kuzingatia taarifa ya hospitali ambayo daktari amefanya mazoezi kwa vitendo (internship).
4. Tunashauri kusiwepo na mtihani wa leseni, kuwepo na mtihani wa kumpima mwanafunzi kama ana uwezo wa kuwa daktari bora baada ya kumaliza mitihani ya chuo na kabla ya kuapa au kwenda mazoezi kwa vitendo (internship). Hii itapelekea ufaulu mzuri kwa sababu ya mtu kuwa na muda wa kutosha kujiandaa na watakaotakiwa kurudia mtihani warudie kila baada ya miezi miwili katika kituo kimoja ili kuepuka gharama kubwa. Hii itapelekea milango ya hujuma, rushwa, uzalilishaji na uonevu anaoupata daktari wakati wa kusubiri mtihani kutoweka.
5. Mtihani wa kumpima mwanafunzi ili aweze kuwa daktari utungwe kama inavyofanyika vyuoni, mtihami wa kuchagua (multiple choice) wa maswali 100 au 200 pekee hauwezi kuwa kielelezo cha kumpata daktari bora kama ilivyo sasa.
6. Kuwepo na muda rafiki wa kukata rufaa walau kuanzia mwezi mmoja.
7. Kwakuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi wanachama wa Afrika Mashariki (EAC), hivyo tunapendekeza itumie mifumo inayotumiwa pia na nchi wanachama ambapo wahitimu wa udaktari wanapewa mtihani online na kwa muda wowote. Nchi zote wanachama wa EAC zenye utaratibu wa kufanya mitihani ya leseni, mtihani na alama (marks) zake zinajulikana na zipo kwenye website zao isipokuwa Tanzania tu ndiyo alama za ufaulu hazijulikani.
Mheshimiwa Rais, sisi madaktari watarajali tumesoma kuanzia elimu ya msingi hadi vyuo vikuu na kumalizia mwaka mmoja wa mafunzo ya vitendo (internship) na tumefaulu vizuri sana hadi kufikia ngazi ya utabibu, ni nani leo anaweza kusema sisi sio wasomi? Ni nani anayeweza kusema kuwa sisi sio madaktari ili hali tumetibu wagonjwa mwaka mzima na kutunukiwa vyeti vya ufaulu wa alama A ?
Mheshimiwa Rais, ni ukweli kwamba Taifa letu linahitaji madaktari bora, lakini je madaktari bora wanaweza kupatika kupitia maswali 200 ya mtihani wa kuchagua kwa muda wa saa tatu mpaka sita pekee?
Mheshimiwa Rais, kutokana na kadhia ya namna hii huenda Wizara yenye dhamana na afya haiviamini vyuo vyake vilivyopo nchini, hivyo wanaona suluhisho pekee la kupata madaktari bora ni huo mtihani wa saa 3 mpaka sita ambao utaratibu wake umekuwa kikwazo kwa daktari ambaye tayari alikwisha kula kiapo kujiajiri au kuajiriwa katika sekta zote, yaani umma na binafsi.
Mheshimiwa Rais, swali la kujiuliza na lipo kwa Watanzania wengi kama ambavyo walivyoaminishwa na MCT ni hili, Je ni kweli sisi madaktari ni waoga wa mtihani na hatutaki kufanya mtihani wa kujipima wa MCT? Jibu ni hapana!
MCT wanapaswa watoe leseni kwa kila daktari aliyefaulu mazoezi kwa vitendo kwakuwa moja kwa moja ana sifa za kuwa na leseni kwa sababu amekutana na wagonjwa, amewatibu, wamepona na amefanikiwa kuokoa maisha ya watu.
Mheshimiwa Rais, tunasisitiza hatupingi mtihani wa kupata leseni, tunashauri uwepo isipokuwa uende sambamba na mitihani ya kumaliza vyuo na si unaompima daktari baada ya mazoezi kwa vitendo. Utaratibu wa sasa ujulikane ni batili, hivo tunaomba standardization ifanyike na tupatiwe leseni
Mheshimiwa Rais, tunashauri Serikali ipitie upya Sheria ya mitihani ya mwaka 2017 ili kuwepo na utaratibu mzuri usio na malalamiko mengi na kuwepo uwazi wa kutosha.
Aidha tunashauri vyuo vya udakitari viwe chini ya Wizara ya Afya na sio Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) ili waweze kuvisimamia vizuri viweze kutoa wataalam wazuri wa afya.
Tunakushukuru sana.
Kupitia kwako ni matumaini yetu maombi yetu yatapata ufumbuzi wako wewe Rais wetu na Mama yetu mpendwa.